Njia panda ya mapenzi

Kipepeo wa chuma1

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2021
Posts
387
Reaction score
558
Habari za mchana wadau.
Ni hivi ni takriban miezi sita Niko kwenye mahusiano na mume wa mtu,tunapendana Sana na tumespend Sana kipindi cha miez mitano iliyopita bila mkewe kujua.

Nikapata Safari mkoa flan,tukawa tunawasiliana kwenye simu almost every day and night.Sasa mhusika akawa hafuti zile simu na meseji tunazoandikiana.Akabadilika na tabia kwani kila usiku ilikuwa lazima tuzungumze hata hadi saa 8 za usiku.Mkewe akamchunguza simu yake akagundua Hilo, akachukua na namba yangu.

Sikumoja akanipigia simu usiku wa manane akanionya kuhusu kutoka na mumewe,akanambia ananipa taarifa kistaarabu ,nikamjibu nimemwelewa na nitaacha.Mchana akanipigia mumewe kunijulia hali,nikamweleza hali halisi ya mkewe kugundua penzi letu na mkwara alionipiga,nikamsihi aache kunipigia simu hasa usiku.Akanambia sawa.

Baada ya sikumbili wamekaa sehemu na mkewe usiku,akatoka pembeni kunipigia simu,mkewe akamwona,alivyorudi walipokuwa wameketi,mkewe akachukua simu ya mumewe kuangalia jamaa alikuwa anaongea na Nani,akakuta ni Mimi.Basi ukazuka ugomvi mkubwa Hadi kuvunjiana simu na mwanamke kuondoka nyumbani.

Asubuhi jamaa akanipigia simu kunielezea kisa kile,nikamshauri amfate mkewe ambembeleze arudi nyumbani.Kweli akafanya hivyo.Tatizo jamaa amegoma kutonipigia simu,anapiga hadi usiku.Wasiwasi wangu nakaribia kurudi toka Safari,halafu tunaishi majiran,je akinivamia?manake alishanionya nikamwelewa Ila tatizo mumewe kawa king'ang'anizi kwangu.
Wadau nifanyeje kwenye scenario hii?
 
Mhh! Mbona hatari hiyo na kuwa makini maana ukijaribu kuuvaa uhusika ingekuwa ndo wewe unachukuliwa mmeo ingekuweje?

Huyo mwanamke mwenzio hapo alipo anahisi maumivu+hasira so kuwa makini usijemwagiwa hata maji ya moto,, huyo mshikaji atakuletea balaaa we mblock tu na Game over,, unamuumiza mwanamke mwenzio.
 
Tafuta Mume wako , Achana na waume za watu.

Kama mkewake ameshakufahamu na nijirani yako nenda moja kwa moja kwa mke wake mweleze ukweli wote na usirudie tena .
 
Jamaa alinambia ye muislam anaruhusiwa kuongeza mke so nisihofu.
 
Kwani wewe ni mtumwa wake huyo mwanaume, unachokitaka utakipata la sivyo chukua hatua stahiki haraka sana. Achana naye awe ameafiki au lah. Tofauti na hapo unajipunguzia muda wa kuishi kwa kujitakia.
 
Shetani siyo lazima awe na mapembe, hata kuvuruga ndoa za watu ni ushetani vile vile
 
Kwa nini unafanya hivy huoni mbele za Mungu wako anakuna kila siku ni vibaya unatenda dhambi itakayo haribu kizazi chako wewe acha na utubu na Mungu atakupa wa kwako.
 
Jamaa alinambia ye muislam anaruhusiwa kuongeza mke so nisihofu.
Usifarijike na maneno haya,, sisi wanaume tukiwa tunamhitaji mwanamke tutampa maneno yoyote ili tutimize lengo letu,japo si wote lakini asilimia kubwa atakwambia anakupenda kumbe anataka akutumie na kukuacha.

Tambua huyo ni mme wa mtu na wewe ni ex wake so jaribu kuwaza kwa herufi kubwa.
 
Naogopa hata kurudi home,na aliongea kwa msisitizo nikae mbali na mumewe tusijeonana wabaya.

Ubaya ushautafuta we jiandae tu hujui atakufanyia nini ili akukomeshe maana alikuomba kiustarabu kabisa hukutaka kuchukua hatua ngoja ugeuzwe kuku .
 
Ongea na mke mpange akuachie, mambie mke hukujua ameoa ila mume bado anakazania.. Huyo mke kuna majamboz mumee kayachoka kwao wawili.. kwa anajiona kama ndio kapata wa milele. kipindi cha mpito.. mkewe mwambie ampe furaha na amani.
 
No ilitokea tu tunapendana,na nilivyojua Ana mke nikajitahidi isijulikane, that's y kwa miezi mi5 yote hakuwahi jua,amejua baada ya Mimi kuwa mbali na jamaa kuzidisha mawasiliano.
Sawa. Itafika zamu yako na wewe kama utabahatika kuolewa. Mume wako nae itatokea tu, na kibinti cha hapo mtaani kwenu. Ila na wewe uwe mvumilivu tu.
 
Jamaa alinambia ye muislam anaruhusiwa kuongeza mke so nisihofu.
Mimi hapa ndipo ninapopata kizunguzungu....Kiimani (Islamic) mume anaruhusiwa kuongeza mke wa pili mpaka hata wa nne...... Wakati akiwa kwenye hii process je huyo mwanamke wa nyongeza (wa pili, tatu au nne) huwa haihesabiki kama anakuwa na mahusiano na mume wa mtu? Au Kiislamu kuwa na mahusiano na mume wa mtu sio dhambi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…