njia panda msaada plz...

njia panda msaada plz...

wewe ni mume wa mke na watoto 2. unaish nje ya nchi, mkeo yupo tanzania sasa mkeo kapata safari ya kikaz kwenda nje ya nchi je utakubali aende ama utakataa? nchi anayokwenda ni tofauti na uliyoko wewe.yeye anakwenda kikazi na wewe uko huko kikazi. wewe kazi yako ni contract ya muda mrefu yeye ni safari ya muda mfupi. nyumban watoto ni wadogo sana ambao kubaki peke yao pasi usimamizi wa mzazi ni ngumu utafanyeje?je wewe mama ama wewe baba mtafanyaje?je unafikiri hela mnazotafuta wewe baba na mama watoto wanazifaidi kwa stail hii ya maisha?
Watoto watabaki na bibi au shangazi yao fikiria kama wote hampo duniani watoto watabaki na nani?
 
yaani mpaka naleta uzi huu wamewaza sana juu ya nini kifanyike manake mke ukoo wake ni mdogo sana wajomba na mamma wadogo hana, mume ndo anandugu ila wako makwao. wadogo wa mke wote wako miji tofauti sana. bibi mzaa baba naye anauguza wazazi wakso hawez kuja huku na kipelekewa wajukuu ni kama kumtesa tu mama wa watu.
hapo kwenye red umenikumbusha nikiwa binti nilikuwa natamani sana kuna na mama mdogo ambaye sikuwa naye. sasa nilikuwa namsumbua sana mama, yaani hamna hata ndugu ambaye anaweza akawa mama mdogo wangu?
siku moja akaja ndugu wa mbali sana wa mama, alikuja kutibiwa akafikia kwetu. yaani ni wa ukoo wa mbali sana ila akawa anamwita mama dada, wewe, huyo mgeni mbona alikoma? nilienda naye hadi kijijini kwao....
kiufupi mimi napenda sana ndugu wa vijijini tangu nikiwa mdogo, labda ndo maana sipati shida.
 
Ndio wanawajengea maisha yao, kwani mwanzoni mama alipokuwa anaenda kazini walikuwa wanabaki na nani? cha msingi kabla ya kuondoka kwenda nje kikazi mama anapaswa awaache watoto kwenye mikono salama

mikono salama?ipi na hii dunia yetu sasa hivi?
kuhusu kwenda kazini na kurudi huwezi kulinganisha na kutokuwepo wazazi wote hapo nyumbani!
kuwajengea maisha ni zaidi ya kuwatafutia pesa kwa kweli!
itatufaa nini kutafuta pesa masaa 24 baada ya mwaka ugundue mtoto haekeweki
kuna watu ratiba zao mpka najiuliza hao watoto huko nyumbani ni dah!kuamka saa kumi na moja kurudi saa tano usiku!au kila siku mama na baba wako angani,wanapishana check in point tu!passport mpka wanajaladia kwa jinsi zilivyo busy ukiuliza nini ,natafuta chapaa,mbumba,mkwanja,kisu ,!
haya yote bila usalama wa watoto wangu sidhani kama yana maana kwa kweli!
 
niyumwiki mlongo wangu
mimi kwa kweli tumewekeana kautaratibu na shem wako,mmoja lazima awepo home ,so hata maswala ya kujiendeleza kielimu kwa kweli yanafanyika kwa utaratibu huo.
safi sana.
sisi hatujawahi kwenda shule kwa wakati mmoja. mmoja akiwa shule mwingine nyumbani. ila ikitokea safari ya kikazi kwa yule ambaye hayupo shule haimfungi kukaa nyumbani sababu tu mmoja hayupo
 
Watoto watabaki na bibi au shangazi yao fikiria kama wote hampo duniani watoto watabaki na nani?
dude how's you? were u successfull? BTW did you meet her expectations?
 
Duh! @fb umenigusa sana leo ila nimeshajua kosa lilipo si unajua mwl huwa akigundua kosa fasta anarekebisha? So najua wapi panakosa and patarekebika tu. I love jf bse pple like you and snowhite
 
Last edited by a moderator:
Awaachie ndugu asake mihela ili watoto wanufaike
ishu ni pale unapozisaka wanao wanakosa furaha yao, baadae unakufa bado ni wadogo ndugu wana nyang'anya mpaka viatu na vilemba watoto wanabaki soro si soro kila siku wanafukuzwa na watu wanapokezana kama karata leo kakae kwa huyu kesho kwa huyu so sad aisee.
 
Duh! @fb umenigusa sana leo ila nimeshajua kosa lilipo si unajua mwl huwa akigundua kosa fasta anarekebisha? So najua wapi panakosa and patarekebika tu. I love jf bse pple like you and snowhite
sisi pia tunajifunza mengi toka kwako mwl. usiache kutuweka sawa tunapopinda.......
kiukweli kila mtu anapenda sana kukaa na watoto wake, hasa sisi akina mama. lakini kuna kipindi inabidi kuna mambo pia yaende. hao hao watoto hata kama unawakumbatia sana lakini huwezi kuwapatia vitu wanavyotaka inakuwa shida. mimi huwa najiwekea kila ninapotoka nje ya watoto wangu lazima nikirudi watamani nisafiri tena ili nikirudi wafurahi. kuna siku mtoto wangu aliniuliza kwani mama utasafiri lini? nikamwuliza umenichoka, akasema hapana, nahitaji kitu fulani..... niliishia kucheka tu.
sasa baba akafanya kosa kasafiri akaagizwa kitu, si unajua wababa, ntanunua airport duty free shop, si walipofika hapo ikawa ni mchaka mchaka hakuna cha kupita shop wala nini. kufika home anaulizwa akasema nimeshindwa kununua, akaambiwa tunajua mummy akisafiri atatuletea maana anakoendaga kuna kila kitu, lol
 
sisi pia tunajifunza mengi toka kwako mwl. usiache kutuweka sawa tunapopinda.......
kiukweli kila mtu anapenda sana kukaa na watoto wake, hasa sisi akina mama. lakini kuna kipindi inabidi kuna mambo pia yaende. hao hao watoto hata kama unawakumbatia sana lakini huwezi kuwapatia vitu wanavyotaka inakuwa shida. mimi huwa najiwekea kila ninapotoka nje ya watoto wangu lazima nikirudi watamani nisafiri tena ili nikirudi wafurahi. kuna siku mtoto wangu aliniuliza kwani mama utasafiri lini? nikamwuliza umenichoka, akasema hapana, nahitaji kitu fulani..... niliishia kucheka tu.
sasa baba akafanya kosa kasafiri akaagizwa kitu, si unajua wababa, ntanunua airport duty free shop, si walipofika hapo ikawa ni mchaka mchaka hakuna cha kupita shop wala nini. kufika home anaulizwa akasema nimeshindwa kununua, akaambiwa tunajua mummy akisafiri atatuletea maana anakoendaga kuna kila kitu, lol

hivi unajua watoto ndo kitu pekee ambacho kiukweli kinakupa furaha ya kweli dunian. ila sasa maisha yanabana sana jjiasi kwamba huwez kukaa nao muda wote pasi kuwatenga ili uwatafutie maisha.binafsi mara nyingi sana nimekuwa nasafiri na wanangu sijawah kuwaacha na hata kama naenda nje basi huwaga kinachonipeleka kinanipa nafasi ya kwenda nao ila sasa inapokuja usafiri uwaache ndo siwez kuamua yaani moyo unauma sana.
 
Watoto watabaki na bibi au shangazi yao fikiria kama wote hampo duniani watoto watabaki na nani?

lazima kuna atakayekuwepo kutoa msaada. Kama watoto wako ok kiafya, na unasafiri kwa muda mfupi, mimi sioni tatizo liko wapi. Maana maisha yanaendelea hata kwa "forced eviction" ambayo huwa inafanyika bila ridhaa ya mtu. Remember our lives are in the hands of God...
 
Mbona easy tu unawapeleka kwa mama wakaenjoy na bibi yao,,

Home nimekaa na watoto wa bro for a year, shemeji alikuwa anasoma, na bro yupo nje kikazi watoto wakaletwa kwa bibi yao, yaani mbona tulikoma, bibi na wajukuu kama mayai watoto wakilia tu tunavyofurumushwa ndani kama hatujazaliwa mule, ni katuni tu mda wote... Ukitaka supersport unaambiwa nenda bar

Professional world inachangamoto zake wadau ambazo lazima twende nazo sawa as maji ukiyavulia nguo sharti uyaoge...
 
hivi unajua watoto ndo kitu pekee ambacho kiukweli kinakupa furaha ya kweli dunian. ila sasa maisha yanabana sana jjiasi kwamba huwez kukaa nao muda wote pasi kuwatenga ili uwatafutie maisha.binafsi mara nyingi sana nimekuwa nasafiri na wanangu sijawah kuwaacha na hata kama naenda nje basi huwaga kinachonipeleka kinanipa nafasi ya kwenda nao ila sasa inapokuja usafiri uwaache ndo siwez kuamua yaani moyo unauma sana.
pole sana. utazoea tu ingawa ni ngumu sana
 
lazima kuna atakayekuwepo kutoa msaada. Kama watoto wako ok kiafya, na unasafiri kwa muda mfupi, mimi sioni tatizo liko wapi. Maana maisha yanaendelea hata kwa "forced eviction" ambayo huwa inafanyika bila ridhaa ya mtu. Remember our lives are in the hands of God...

Mbona easy tu unawapeleka kwa mama wakaenjoy na bibi yao,,

Home nimekaa na watoto wa bro for a year, shemeji alikuwa anasoma, na bro yupo nje kikazi watoto wakaletwa kwa bibi yao, yaani mbona tulikoma, bibi na wajukuu kama mayai watoto wakilia tu tunavyofurumushwa ndani kama hatujazaliwa mule, ni katuni tu mda wote... Ukitaka supersport unaambiwa nenda bar

Professional world inachangamoto zake wadau ambazo lazima twende nazo sawa as maji ukiyavulia nguo sharti uyaoge...

brothers yaani sasa naona hivi bora waende kwa bibi yao mzaa baba kwa muda huo ili wawe safe zaid na hapa na buy idea ya @ndahan kwamba hata kwa forced eviction waende tu.
 
Jamani hizi pesa zitatuharibia watoto, bora tu huyo mke asiende. Sio lazima kusafiri,kama mama ana akili, hataenda hiyo safari.
 
Back
Top Bottom