wewe ni mume wa mke na watoto 2. unaish nje ya nchi, mkeo yupo tanzania sasa mkeo kapata safari ya kikaz kwenda nje ya nchi je utakubali aende ama utakataa? nchi anayokwenda ni tofauti na uliyoko wewe.
yeye anakwenda kikazi na wewe uko huko kikazi. wewe kazi yako ni contract ya muda mrefu yeye ni safari ya muda mfupi. nyumban watoto ni wadogo sana ambao kubaki peke yao pasi usimamizi wa mzazi ni ngumu utafanyeje?
je wewe mama ama wewe baba mtafanyaje?
je unafikiri hela mnazotafuta wewe baba na mama watoto wanazifaidi kwa stail hii ya maisha?
Katika dunia hii ....maisha swala ni kujipanga.... mlipooana ulikuta mkeo kaenda shule kasomeshwa na wazazi wake, kifupi ana elimu yake, na wewe ulijua hivyo na pengine ulivutiwa na hilo sasa,..... mpe uhuru wa kwenda masomoni kujiendeleza au kikazi ... hamuwezi kukosa ndugu wa kuwaachia watoto kwa pande zote mbili ... kuna wadada house girls maalumu wanapatikana kwa kazi hiyo... wapeleke kwa ndugu nenda kwa wanaosajili house girl maalum ingia nao mkataba kwa kipindi chote mtakachokuwa mko majuu, dunia ya leo mama analeta na baba analeta .... hakuna kulala.....