Nje ya Bunge hakuna Katiba ya Wananchi

Msimamo wako ni znz yenye mamlaka kamili, serikali 3 au mkataba.

Hivi karibuni umekata kona na kusema'' wznz wameyataka wenyewe'' nikakuuliza, sheikh Mdondoaji kulikoni mbona waniacha pwani bamvua kubwa hili? Ukanijibu umegundua kitu kwa hawa akina Jusa.
Basi niliposikia neno inshallah nikawa kimya nikisubri habari, ndio hadi leo twaonana tena.

Haya, nijaalie kwanza, na ahli, swaumu na kila jema. Tukae kitako unipe habbari, kama waelekea kule tulikokuwa tunakwenda au umekata kona zaidi. Mie sijatoa tuhma yoyote naeleze kilichojiri tu. Lau kuna sintofahamu, huu ndio wakati unieleweshe nikutake radhi niliposhindwa kukuelewa bdio uungwana.


Karibu.


Nguruvi,

Mwanzoni ni kweli nilikuwa pamoja na wale waliotaka Zanzibar huru. Hii ni kwasababu ninawafahamu wazanzibari na mie nimefanya kazi na kuishi Zanzibar muda mrefu. Ila kuna mambo nimeyaona hayajakawa sawa hasa huku kwenye ajenda ya kudai mamlaka kamili. Hoja hii imegubikwa na ubinafsi na kutokujali maslahi ya baadhi ya wazanzibari wenzao hivyo basi kuendeleza lile lile linaloendelea kwa wanayolalamikia.

Pili hakuna mwenye dhamira ya dhati kuwasaidia wazanzibari kimsingi kuna ukungu mzito umetanda katika hii hoja ya Zanzibar yenye mamlaka kamili. Ukitaka kujua angalau wenye kudai mamlaka kamili either wamekosa madaraka? either wamekuwa ni wahanga wa mapinduzi? either wamekuwa wakiharibikiwa biashara zao baada ya mianya ya ukwepaji kodi kuondoka? Either ni watu waliokosa mvuto wa kisiasa baada ya kufa siasa za kindaki ndaki. Hivyo basi wamejiunga katika uwanja wa marriage of convinience kudai madaraka yao kwa msingi wakiwa wachache watadai vizuri zaidi na hivyo pengine wanaweza kufanikiwa wanachokidai. Baada ya kugundua hilo nimejitoa kwani a. Hakuna madai ya dhati yenye lengo la kumsaidia mzanzibari wa kawaida. b. Ule ubinafsi unaolalamikiwa utaendelea hata kama Zanzibar ikiwa huru.

Kimsingi Nguruvi nimeamua kumuunga mkono Mwanakijiji tuwe na Serikali moja au Dola moja. Hizi habari zenginezo tutazitengeneza taratibu .

Swaumu alhamdulilah inakatika taratibu tunamaliza ya 15. Karibu sana halwa ya lozi na kahawa na pia tende zenye sharbati kidogo huku maeneo ya kariakoo. Nasikia mnataka kuandika kitabu wewe na nduguzo vp mmeshakikamilisha?

Nilikuwapo!!!
 
Nguruvi,

Mwanzoni ni kweli nilikuwa pamoja na wale waliotaka Zanzibar huru. Hii ni kwasababu ninawafahamu wazanzibari na mie nimefanya kazi na kuishi Zanzibar muda mrefu. Ila kuna mambo nimeyaona hayajakawa sawa hasa huku kwenye ajenda ya kudai mamlaka kamili. Hoja hii imegubikwa na ubinafsi na kutokujali maslahi ya baadhi ya wazanzibari wenzao hivyo basi kuendeleza lile lile linaloendelea kwa wanayolalamikia.

Pili hakuna mwenye dhamira ya dhati kuwasaidia wazanzibari kimsingi kuna ukungu mzito umetanda katika hii hoja ya Zanzibar yenye mamlaka kamili. Ukitaka kujua angalau wenye kudai mamlaka kamili either wamekosa madaraka? either wamekuwa ni wahanga wa mapinduzi? either wamekuwa wakiharibikiwa biashara zao baada ya mianya ya ukwepaji kodi kuondoka? Either ni watu waliokosa mvuto wa kisiasa baada ya kufa siasa za kindaki ndaki. Hivyo basi wamejiunga katika uwanja wa marriage of convinience kudai madaraka yao kwa msingi wakiwa wachache watadai vizuri zaidi na hivyo pengine wanaweza kufanikiwa wanachokidai. Baada ya kugundua hilo nimejitoa kwani a. Hakuna madai ya dhati yenye lengo la kumsaidia mzanzibari wa kawaida. b. Ule ubinafsi unaolalamikiwa utaendelea hata kama Zanzibar ikiwa huru.

Kimsingi Nguruvi nimeamua kumuunga mkono Mwanakijiji tuwe na Serikali moja au Dola moja. Hizi habari zenginezo tutazitengeneza taratibu .

Swaumu alhamdulilah inakatika taratibu tunamaliza ya 15. Karibu sana halwa ya lozi na kahawa na pia tende zenye sharbati kidogo huku maeneo ya kariakoo. Nasikia mnataka kuandika kitabu wewe na nduguzo vp mmeshakikamilisha?

Nilikuwapo!!!
Mashallah ,hapa Muheza twasema chungu cha 15, bwana wee umesahau kibandameno ndugu yangu. Kikiwekwa nazi na chai ya rangi iliyokoza na mchachai ah nikuwambie nini, kahawa saa nne. Acha tu.

Sasa Mdondoji pamoja na kumuunga mkono Mwanakijiji, bado umetuacha kizani.
Hivi una maana kuwa huu muungano wa ''lanatullah Nyerere kama wanavyosema wznz'' una faida kwa znz au hauna faida?

Pili, kwanini tusiwe na mambo 7 ya kushirikiana mengine kila mtu akawa na lake. Huoni hiyo ni njema kwasababu inapunguza gubu na zogo sheikh!

Tatu, kwani sheikh kuna ulazima wa kuungana, tukiamua kuvunja jahazi kutakuwa na tatizo gani? Znz wana nchi yao, na ilikuwa nchi tena nzuri kweli kweli tunaambiwa kabla ya mapinduzi na muungano. Vipi tuwe na serikali moja na tusirudi kule kwenye znz yenye neema miaka hiyo ya 1963 kurudi nyuma, 1950 na hata 1930?

Nisaidie hapa sheikh
 
Mkuu Nguruvi3, asante kwa hiyo heshima unayonipa ambayo nina hakika kwa asilimia 100% kwamba, kama binadamu, inanipwaya; siwezi kufikia kiwango hicho. Tatizo langu kubwa ni moja...sisiti hata siku moja kuliita koleo kwa jina lake...in a nutshell, sina uvumilivu na mawazo ninayoamini ni ya kinafiki. Kama ninaishi sehemu yenye unyevu unyevu halafu najikuta nikiathirika kiafya, nahama...tofauti na Mkuu Mkandara atakayetetea kubaki hapo hapo kwa sababu tu kajikuta hapo, ni msimamo wa ajabu kweli kweli. Safari ni ndefu; huku simba na huku mbwa mwitu wote wakiwa na njaa kali, laiti angejua...!

Si uungwana kumjadili mtu na najua kwa posti hii wapo watu watashindwa kunielewa, kwao natanguliza samahani...ni upungufu tu wa kibinadamu. Mkandara nimekuja kumuelewa labda zaidi ya ambavyo ningekusudia hivyo najitahidi sana kutojibu nyingi katika michango yake. Mara nyingi, kama walivyo wasomi wetu wengi, anajikuta between a rock and a hard place kama wasemavyo waongea ung'eng'e, tabia ambayo ni rutuba kubwa ya unafiki. Hali hiyo imewafanya wasomi wetu wengi washindwe kupata jawabu la swali, wangependa wakumbukwe kwa lipi siku za baadaye katika historia ya taifa hili kwani huku wataka na kule wataka!

Nakumbuka kuna wakati kwenye mnakasha kuhusu historia ya Tanganyika na wazee wa Gerezani, Mkandara alivyokimbizwa kwa mashambulizi alipotaka kuonesha kuwa naye ni mtoto wa mjini...naam alikutana na saizi yake wanaoongea lugha moja (ya Saigoni?), hakurudi tena kwenye mjadala na badala yake sisi wakuja ndio tukaachiwaa usukani, kuwatetea wazee wetu waliolipigania nchi yetu bila kujali tofauti zao kikabila wala kidini; nachelea kusema, kutokana na msimamo wetu huo na mwelekeo wa mnakasha Mkandara alichukulia kwamba wengi wetu tumepitia ubatizo! Laiti angejua...!

Kusema kweli wengu humu hatufahamiani; wengine shule zetu ni za kuunga unga lakini pamoja na will and desire to fight for change, we happen to have the courage kwa sababu bila vyote vitatu kinachobakia ni usanii! Unafiki at its best!Unafiki wa kukataa serikali tatu kwa madai ya kuvunja Muungano wakati ni wazi mabadiliko ni lazima ili tuweze kupiga hatua kutoka point A na kufikia poin B.Wazo la serikali moja ni la kufikirika na kwa sasa kila moja wetu anajua haliwezekani labda kwa mtutu wa bunduki, kitu kisichowezekana katika karne hii na kulivalia njuga ndio usanii wenyewe! Laiti angejua...!
Mkuu unayoyazungumza hayaingii akili kabisa kwa sababu unavyonifikiria miye sivyo kabisa! Na labda niweke record clear ya kwamba sijawahi kuondoka hapa kijiweni kwa sababu ya watu wa Mujini wala hakuna mada ambayo mimi nimepelekana na watu hao ktk maswala ya Historia ya Tanganyika nikashusha gloves - HAKUNA. Na nachelea kusema hakuna mtu alokwenda pound for pound na Mdai mkuu bw. Mohammed Said hapa JF kama mimi juu ya uongozi wa AbdulWakil Sykes na viongozi wengine wa TANU. Juu ya Nyerere vs waislaam na kadhalika. Kumbukumbu zipo wala sii kidogo wee tafuta mada za Mohammed Said kanisome upya.

Yeye ndiye alonikimbia mara kibao asirudi kujibu hoja zangu baada ya kumuonyesha kwamba waasisi wa TANU hawakuweka uislaam wala Ukristu mbele ama malengo ya kujenga Uislaam. Na alijaribu kumtumia mtoto wa marehemu mzee Ally Sykes (Abdul Sykes) nikamwambia sio tu mimi nawafahamu watu hao, nimewahi kuzungumza nao kwa kina juu ya Uhuru wa Tanganyika, Familia ya marehemu AbdulWakil Sykes sio tu tunafahamiana bali ni ndugu na marafiki zangu kwa ukaribu sana, yeye akaingia mitini.

Nakushangaa sana unapokuja na utunzi huu kinyume wakati ushahidi umo humu humu JF, maana ukweli ni kwamba niliondoka hapa kutokana na tabia mbaya ya wanaChadema/CCM kushabikia Udini wakishindana kwa lugha chafu, na kuanza kunipa picha tofauti kabisa na jinsi nilivyolelewa ama ustaarabu wetu. Udini ndio uliniondoa kijiweni na sii mambo ya mujini hata kidogo maana hakuna kitu hicho, miye mwenyewe wa kuja!

Mkuu nashindwa kuwaeleza kwa makini zaidi ili mpate kunielewa japo nyie tayari mmeisha weka ushabiki wenu wa vyama mbele ya hoja zangu. Labda nikwambie kwa kifupi sana, Hoja yetu wananchi na sii UKAWA wala CCM ni ipi haswa? -bila shaka ni kuitaka - KATIBA MPYA. Nadhani tatizo ni kwamba Uandishi sio maji yangu nashindwa kujieleza vizuri mkaweza kutenganisha mifano na nasimama wapi.

Sasa ikiwa ni katiba mpya, Je ni katiba gani ya serikali ya muungano inayoweza kutengua kwanza muundo wa serikali zake? Je kuna katiba yoyote ya Taifa lolote ilitenganisha serikali zake ama muundo wa serikali hizo hutangulia kuandikwa kwa katiba ya nchi hizo? Hapa tena tunakuta lazima muundo wa serikali utangulie kuwepo kabla ya kuandikwa kwa katiba na muundo tulonao ni serikali 2. Na katiba yoyote inayoandikwa ni kuanisha Uhuru wa serikali hizo kuwa na mamlaka yao kamili kwa mapana ya muungano wao. Kwetu sisi swali limeongezeka ya kuwa muundo wa hizi serikali zilizopo (serikali 2) inasemekana Wananchi pia hawautaki - Swadakta!

Sasa, tuseme keli wananchi hawautaki muundo wa serikali 2. Je unapotaka muundo mpya wa serikali ni njia zipi zinazotakiwa kufanywa? bila shaka ni Referendum na hatua hii haihusiani kabisa na uandishi wa katiba mpya, huu ni wwanzo mpya wala siii ukurasa mpya! Maana Pengine wananchi wanataka sio tu serikali 3 pengine wanataka serikali za Majimbo, wanataka madaraka mikoani, wanataka serikali 1 na kadhalika. Maswala ya hati na uhalali wa muungano ungezungumziwa kwa wale wanaotaka kuvunja muungano ama kutafuta Uhalali wa ndoa hii japo hawaulizi hati na uhalali wa hati za wazazi walowazaa!

Hili la muundo wa serikali sii jambo dogo la kuunganishwa na jambo jingine lolote kama tunavyotaka kuunganisha na uandishi wa katiba mpya, Haya ni makosa makubwa na napingana na utaratibu huu, hivyo ikiwa kweli hoja ni Muungano, basi nimewahi kuandika mengi sana juu ya kudai Refendum huko nyuma na hasa kwa Wazanizbr ambao walikuwa hawataki tena Muungano uliopo kwa sababu Tanganyika imevaa koti la Muungano. Na sio hivyo tu niliwahi kuwambia hata Maalim Seif kwa nini hawapendekezi bungeni Refendum ifanyike ikiwa kweli wao hawautaki Muungano?..Sijui kama unanifuatilia? Hivyo kuvunja muungano na muunda serikali ndani ya Muungano ni hoja mbili tofauti pia, huwezi kuziweka pamoja pia.

Hivyo, hekima yangu inavyonituma ktk swala hili ni kwamba taratibu na mchakato mzima tulokuwa nao mezani leo ni - Uandishi wa Katiba mpya! hatuwezi kuchanganya na Muundo wa serikali maana haikuwahusu wananchi. Kama toka mwanzo wananchi tungeanza kudai Muundo MPYA wa serikali zetu, basi utaratibu wake usingekuwa huu hata kidogo. Utaratibu wake ungefuatwa kwanza kwa kupata kura za maoni ya wananchi wote juu ya swala hilo moja ili kutoa suluhu ya Jambo hilo na hakika ningekuja na msimamo wangu ktk kura yangu. Lakini haikuwa hivyo sii kwa wananchi, Ukawa wala CCM kuomba kupitia Bungeni wala mahakamani tuwe na Muundo wa serikali mpya ila imepachikwa ktk uandishi wa katiba mpya. Hapa nimetenganisha maswala haya mawili na siyaweki meza moja kama mnavyotaka, hivyo hoja zangu zote hapa zinahusu katiba mpya ya JMT pinzani na kujumuisha muundo wa serikali ndio maana nabakia na serikali 2 maana kinyume chake haihusu.

Maadam mjadala mzima hapa JF umejikita katika muundo wa serikali, mimi sikubaliani na lolote nje ya sheria na taratibu za kuunda serikali maana huu ni uamuzi wa wananchi wenyewe na haihusiani na Katiba ya wananchi wanatodai. Utaratibu wake upo lakini haukufuatwa kwa sababu lengo na nia likuwa kuipata katiba Mpya na sio kubadilisha muundo wa serikali. Kufanya hivi (kuua ndege wawili kwa jiwe moja) ni makosa na pia imesababisha mtafaruku huu mkubwa baina ya wanasiasa wenyewe ilihali wananchi hawajashirikishwa. Na ndio maana wamepanga toka mwanzo kuwa Wananchi watashirikishwa mwishoni baada ya uandikaji wa Katiba Mpya ili kuikubali ama kuikataa.

Na sababu nyingine kubwa ambazo mimi sikukubaliana na waraka wa Warioba kuhusiana na serikali 3 ni swala la Mambo yasokuwa ya Muungano. Na nimefanya hivyo kutokana na experiance yangu ya kwamba serikali kuu ya Muungano lazima itegemee serikali zake. pato la serikali kuu hutoka serikali ndogo kwa kila nchi yenye kuunda Muungano wa aina hii. Na nimeeleza kwa undani zaidi juu ya hili na hata kumkosoa JK alipopendekeza zaidi kuwepo kwa mambo yasokuwa ya Muungano nikielewa MAMBO hayo ni wizara za serikali. Hivyo ikiwa Mambo yote yatakuwa ya Muungano na serikali 3 zikaundwa ningeunga mkono ikiwa utaratibu wa kuwashirikisha wananchi kwanza kuamua muundo huu nje ya uandishi wa katiba.

Na zaidi ya hapo nikasema, mapungufu yaloleta kero zote hizi ni mfumo mbaya wa Utawala ambao umeweka Mambo mengi yasokuwaya Muungano kutokana na siasa za wakati ule wa Ujamaa jambo ambalo leo hii hatuhitaji kulihofia tena. Na nikatumia sana mifano ya ndoa ya kwamba tunapofikia kusema kwamba wanandoa wamewekeana mipaka ndani ya nyumba na kwamba kuna Mambo ya Mume na ya Mke basi ndoa hiyo itakuja pata matatizo makubwa mbeleni maana jiko sii la mke wala Mume ila shughuli za jikoni zinaweza kuwa za mke na chakula kikipikwa huilisha familia nzima, hakuna jokofu la Mume wala la mke ama firigisi ni za bwana, paja la mama na vipapatio ndio vya watoto. Kufikira kuunda nyumba hii kama ndio suluhisho la matatizo ya ndani ya nyumba ni kutafuta kuivunja ndoa.

Hapa ndipo niliposimama mimi na naitaka Katiba mpya kwanza maana hii ndiyo wananchi wameidai na tuliahidiwa kupewa kabla ya mwaka 2015. Kama tungelitaka muundo wa serikali ubadilishwe hili ni swala pekee linalotaka mjadala wake peke yake na usiunganishwe kabisa na uandishi wa Katiba mpya.

Haya maswala ya Udini kuhusu Ubatizo ni lugha yangu tu huitumia na mara nyingi humtumia hata Yesu ktk mifano bora na sio ile inayotutengenisha isipokuwa kwa kutofahamu kwenu na fikra zenu mnachukulia iweje Mkandara Muislaam azungumzie ya ubatizo na Yesu au Ukristu kama sio Udini? kumbe nachokifanya ni kutumia mifano bora ambayo nina hakika wengi wanaweza kuitazama kwa sura wanayoijua kwa umakini zaidi kuelewa jambo nalosisitiza. Kumbe ni kosa, kwa sababu Udini bado upo akilini mwenu na neno Ubatizo wa wakirstu halina maana sawa na Kusilimu kwa waislaam! Muislaam ni lazima atumiye neno kusilimu na sio kubatiza - Sikuyajua hayo!

Well, labda nikubali miye kushindwa na kesho mhadithie tena kwamba Mkandara alikimbia hapa wakati nimejaribu sana kuwafahamisha lakini hamtaki kuelewa kama nilivyoshindwa huko Chadema ktk maswala ya uanachama na uongozi nimeshavikwa Usaliti kwa kutoa maoni yangu tu juu ya makosa waloyafanya. Mwisho wa yote haya nawaambieni Katiba Mpya haitapatikana leo wala kesho ikiwa swala la muundo wa serikali litajumuishwa na Katiba mpya. Tulioliwa ni sisi wananchi na kwa ubishi usokuwa na maana kabisa.. Maasalaam..
 
Mashallah ,hapa Muheza twasema chungu cha 15, bwana wee umesahau kibandameno ndugu yangu. Kikiwekwa nazi na chai ya rangi iliyokoza na mchachai ah nikuwambie nini, kahawa saa nne. Acha tu.

Sasa Mdondoji pamoja na kumuunga mkono Mwanakijiji, bado umetuacha kizani.
Hivi una maana kuwa huu muungano wa ''lanatullah Nyerere kama wanavyosema wznz'' una faida kwa znz au hauna faida?

Pili, kwanini tusiwe na mambo 7 ya kushirikiana mengine kila mtu akawa na lake. Huoni hiyo ni njema kwasababu inapunguza gubu na zogo sheikh!

Tatu, kwani sheikh kuna ulazima wa kuungana, tukiamua kuvunja jahazi kutakuwa na tatizo gani? Znz wana nchi yao, na ilikuwa nchi tena nzuri kweli kweli tunaambiwa kabla ya mapinduzi na muungano. Vipi tuwe na serikali moja na tusirudi kule kwenye znz yenye neema miaka hiyo ya 1963 kurudi nyuma, 1950 na hata 1930?

Nisaidie hapa sheikh


Nguruvi,

Kuna mambo Nyerere ameyafanya na sio mazuri ila pia yana makovu ambayo hayawezi kuzibika ila kwa ajili ya kulipeleka taifa mbele sio msingi wa kuendelea kungangania makovu yaliyopita.

Muungano huu unafaida na hasara kwa wazanzibari ila faida hizo zinaweza kuonekana kama jambo la mazoea na sio tunu kwa taifa. Pia zipo hasara hatukatai ikiwemo kutoheshimiwa kwa taifa la zanzibar, sintofahamu kwenye mapato ya zanzibar na mchango wa zanzibar katika benki kuu. Vyote ni vitu vinahitaji kujadiliana na kuondoshwa ila sio msingi wa kuuvunja umoja uliodumu muda mrefu.

Tatu muungano wa Tanzania ni wa kindugu na kiukoo, Zanzibar kuna koo asili yake zimetokea Tabora wakati wa utumwa na biashara ya mazao na vito Afrika ya kati na Asia. Pia koo zengine ni koo asili yake wamakonde hasa wapemba ambao walipelekwa Pemba kwenye kilimo cha karafuu. Na wengine ni wasambaa walioishi pemba muda mrefu. Hivyo kwa namna moja au nyengine asilimia kubwa ya wazanzibari wana ndugu zao Tanganyika na kuanzisha utengano sidhani ni jambo la busara.

Nne Zanzibar kuna matabaka yanayohasimiana muda mrefu tangia kipindi cha usultani , mapinduzi hadi sasa haya matabaka hayaaminiani hadi kesho na mfano halisi ni pale Bunge la Katiba lilipoanza watu wakaanza kuitana majina ya kibaguzi sasa imagine wakiwa huru watakuwa vipi?

Solution ya wazanzibari ni kuwa na Serikali moja tu au Dola Moja. Serikali moja inaweza kuja sasa au hata baadae baada ya muungano kuvunjika kwani thamani ya muungano itajulikana baadae. Kwani wazanzibari wakienda kuanzisha nchi yao na matatizo watakayokumbana nayo ndio watafahamu muungano una faida au hasara. Vile vile Tanganyika wakiwa wamepakana na nchi isiyotulivu na wakakumbana na migogoro mbali mbali watatambua thamani ya kuungana na Zanzibar.

Kwa ufupi hatujui thamani ya mambo tuliyo nayo hadi tuyakose. Ila Zanzibar huru sidhani kama ni busara wala serikali 3 kwani tukiyamaliza ya serikali mbili tutayaanza ya serikali tatu na kumbuka Serikali ya muungano wakati huo haitakuwa na mamlaka kama iliyonayo sasa.
 
Mdondoaji , kwanza nikupongeze kwa kuwa mkweli na mwaminifu. Kubadili mtazamo si jambo baya na wala haliwi. Kusimamia unachokiona ni sahihi kwa hoja ni ukomavu.

Na kuzungumza bila innuendos au insinuation za ukabila na udini ili ku-justify tu hoja ni jambo zuri.
Mitazamo tofauti si upungufu, kwa kingledha 'difference does'nt mean deficiency''
Ujerumani kutwaa Kombe. Nimefurahi sana. Imewachukua miaka zaidi 15 kutengeneza timu kwa euro million 9.

Watoto wa Argentina wanalia kwa kukosa ushindi, hawajazoea na wanajiuliza kwanini.
Watoto wa Tanzania wanawashangaa wa Argentina nini kinawaliza! Anyways nizirejee hoja zako kwa mafungu
Mdondoaji;10055579]Nguruvi,Nyerere ameyafanya na sio mazuri ila pia yana makovu ambayo hayawezi kuzibika...sio msingi wa kuendelea kungangania makovu yaliyopita
Alikuwa mwanadamu kama wengine.

Nilidhani muhimu ni kuwafundisha jamii mazuri aliyoyafanya na kumsamehe kwa makosa.
Kinyume chake jamii inafundishwa ubaya wa mazuri ya Nyerere.

Leo ukisema Nyerere znz unaambiwa 'laanatullah' hata wanaota meno.
Watu wamefundishwa kumchukia tu bila sababu, na wala hawaelezwi kuwa umoja wao una mchango wa Nyerere, na aliwapendelea zaidi ya watu wake, nashashangaa laantullah watu hao hao wanataka muungano wa laanatulah Nyerere.
Muungano unafaida na hasara kwa wazanzibari ila faida hizo zinaweza kuonekana kama jambo la mazoea na sio tunu kwa taifa. Pia zipo hasara hatukatai ikiwemo kutoheshimiwa kwa taifa la zanzibar, sintofahamu kwenye mapato ya zanzibar na mchango wa zanzibar katika benki kuu. Vyote vinahitaji kujadiliana na kuondoshwa,sio msingi wa kuuvunja umoja uliodumu muda mrefu.
Ni kwa msingi huu wengine tunataka taifa hilo liheshimiwe. Lipewe hadhi ya mambo kama kukopa, misaada, uwezo wa kupanga mipango yao bila kuingiliwa na kuondoka katika mambo 22 hadi 7 ili znz iwe na hadhi zaidi.

Hii ni pamoja na kupewa fungu lao la Benki kuu tofauti na sasa kupata aslimia 4.5(7%) pato la Tanganyika.
Mapato ya znz hakuna maana ni bilioni 400 tu, tunataka wapewe access za IMF ili tusituhumiane kuiba kischokuwepo. Mdondoaji, hivi unajiasikiaje ninikutuhumu umemuiba Matonya(marhum).Tunaotaka Tanganyika tunawatakia heshima
Tatu muungano wa Tanzania ni wa kindugu na kiukoo, Zanzibar kuna koo asili yake zimetokea Tabora wakati wa utumwa na biashara, zengine ni koo asili ya wamakonde hasa wapemba..... Hivyo asilimia kubwa ya wazanzibari wana ndugu zao Tanganyika na kuanzisha utengano sidhani ni jambo la busara.
Hii ni hoja dhaifu sana. Mwaka 1927 kulikuwa na uhusiano wa kisiasa bila muungano.

Uhusiano na msumbiji ni wa ndugu wa kimakonde, kiyao n.k. Pale Songea kuna watu wa Mbamba bay na Blantyre kwa Pande zote. Kigoma kuna watu wa Kalenzi n.k. Rwanda na Uganda, kuna watu wa pande zote, Mara, Arusha, Tanga-Mombasa kuna watu wa karibu wa undugu wa damu si kuoeleana. Kote huko hautuna muungano nako.
Naweza kusema Mombasa kwangu mimi pale mjasani nina ndugu zaidi ya Znz, lakini hatuna muungano.

Kuna watu wameoa America, Norway, Arhentina n.k. Kote huko hakuna muungano.
Ninachotaka uelewe hapa ni kuwa muungano si kwasababu ya undugu wa Damu na znz, kama unajenga hoja hiyo lazima uisimamishe kwa miguu kwa kuangalia factors nyingine na si hiyo unayosema.

Na pia, kuvunjika kwa muungano hakuna maana kuvunja kwa undugu.
Kwani undugu huo si umeanza miaka karne, mbona mwaka 1961 hadi 1964 hatukuwahi kuwakana wznz kama ndugu zetu. In fact tunawatambua watu wa visiwa vya FIJI kama watu warufiji, seuse znz. Hatuna muungano na fiji!!
Nne Zanzibar kuna matabaka yanayohasimiana muda mrefu tangia kipindi cha usultani , mapinduzi hadi sasa haya matabaka hayaaminiani hadi kesho na mfano halisi ni pale Bunge la Katiba lilipoanza watu wakaanza kuitana majina ya kibaguzi sasa imagine wakiwa huru watakuwa vipi?
Hilo ni tatizo lao kwasababu kwasasa adui yao mkubwa ni Tanganyika.

Adui Tanganyika anatakiwa akae pembeni na kuwapa nafasi wa-sort out matatizo yao.
Hii habari ya kutufanya sisi ni matatizo yao wakati hatufaidiki na lolote isipokuwa lawama sasa basi.

Kama wanataka heshima kamunavyosema wajiheshimu kwanza, hatuwezi kuwaheshimu kama hawajiheshimu.
Matatizo yao wayamalize wenyewe hatuna sababu za kutumia resource zetu kuingilia mambo yao.
Solution ya wazanzibari ni kuwa na Serikali moja tu au Dola Moja. Serikali moja inaweza kuja sasa au hata baadae baada ya muungano kuvunjika kwani thamani ya muungano itajulikana baadae. Kwani wazanzibari wakienda kuanzisha nchi yao na matatizo watakayokumbana nayo ndio watafahamu muungano una faida au hasara.

Vile vile Tanganyika wakiwa wamepakana na nchi isiyotulivu na wakakumbana na migogoro mbali mbali watatambua thamani ya kuungana na Zanzibar.
Usinitaje maana unataka 'kifo'.
Serikali moja ni haramu znz, hapo sipo.

Ninakubaliana nawe kuwa kwavile wznz wamekuwa wanafaidika na muungano bila kujua gharama zake, hawajui thamani yake. Huu ni ukweli. Nilidhani tunatakiwa tuwe na miaka 3 ya kutengana ili kila mmoja ajitahmini kama anaweza kuishi peke yake. Of course Tanganyika hahitaji kujitahmini kwasababu hamtegemei znz kwa lolote.
Baada ya miaka 3 wznz wangeweza kutanguliza ada za muungano tofauti na sasa wanapotanguliza favor.

Tanganyika mpaka wake na znz ni mzuri kuliko ule wa Rwanda, Burundi, DRC au Malawi.
Hakuna tatizo lolote wznz watakapokuwa na nchi yao. Hiyo haitatuathiri kwa lolote kwasababu hadi sasa bado tunachukua wznz wengie kuliko taifa lolote duniani.

Mpaka na znz ni mzuri sana, ni mdogo na una buffer zone. Hatutegemei kujuta kwa kuwa na jirani asiye na utulivu.
Ni bora jirani asiye na utulivu kuliko jirani anayeleta uchafuzi na kuharibu utulivu kwako. Tutawaambi wakae pamoja wasuluhishe matatizo yao, lakini hatutegemei kuwa kuwaacha wazungumze wenye kutaharabika jambo.
wa ufupi hatujui thamani ya mambo tuliyo nayo hadi tuyakose.
Ila Zanzibar huru sidhani kama ni busara wala serikali 3 kwani tukiyamaliza ya serikali mbili tutayaanza ya serikali tatu na kumbuka Serikali ya muungano wakati huo haitakuwa na mamlaka kama iliyonayo sasa
Serikali 2 hazina majibu na ndizo zimeifanya znz ikose heshima kwa mujibu wako. Ndizo zinawanyonya utajiri wa znz.

Ni makosa kusema S3 zina matatizo, hatujawahi kuwa na mfumo sheikh, kwanini mnaingia katika unajimu na kupiga ramli? Kwani S2 za ajabu maana hazieleweki, mimi naita 1.5 zilipatikana kwa mwongozo wa kitabu gani?

Sisi tunaotaka Tanganyika tunasababu zinazotjitosheleza
1. Mfumo uliopo unatishia muungano zaidi ya kuimarisha, ni wakati tufikirie mbadala
2. Tunataka fiscal autonomy kwa kila mmoja, Tanganyika isinyonye znz, na wala znz isiwe tegemezi kwa Tanganyika
3. Kuwe na uhuru unaozingatia tamaduni za sehemu ili kutoathiri historia na maisha ya watu
4. Kuleta stability ya nchi baada ya S2 kuleta instability kubwa
5. Kupunguza gharama za muungano kwa kupunguza mambo yanayoleta tabu, na kutoa uhuru wa washirika

6. Kudumisha undugu, ili kuepuka hasira za kuchoma watu.
Tukiwa na S3, wznz watajivunia uznz bila kuminywa au kinyongo.
Na wala Watanganyika hawatakuwa na kinyongo kama wasivyokuwa nacho na majirani wengine.

7. Sisi Watanganyika inatuuma tumebeba mzigo wa muungano wenyewe, mzigo usiothaminiwa na waznz hadi wanapohitaji msaada. Imefika mahali pa kudharau katiba yetu.

Tanganyika tumechoshwa na lawama za kunyonya znz, na tumechoka kutumia resource zetu kuisaidia znz ambayo wamekataa wao si Watanzania na si sehemu yetu ni nchi kamili ya jirani.

Tunahitaji kuamua hatima yetu na kupanga mipango yetu bila kwaingilia wzn wa nchi jirani na wao kutokutuingilia

Tunataka tuepuke mbegu ya ubaguzi inayopandwa kwa uwepo wa znz.
Mfano, WZNZ wakaitaka upendeleo wanatanguliza neno Uzanzibar na si utanzania. Kuanzia masomo hadi ajira na fursa nyingine. Hii mbegu mbaya hatuitaki ichanue, hauwezi kuwa na raia wa nchi jirani wakaja kupanga mipango na taratibu za nchi yetu.

Kibaya zaidi ubaguzi huo unafanywa dhidi ya wananchi wa nchi yetu katika nchi yetu kwa kutumia rasilimali zetu.
Mbegu ya Utanganyika imepandwa na wznz sasa inachanua, lazima wavune walichopanda. Hapa ni 3 tu sheikh.
Wao kwao sisi kwetu, nasema wao kwasababu wamekataa siyo sehemu ya sisi, wao ni waznz.

Kama hatutaweka mpaka wa znz na Tanganyika, wananchi wataweka mpaka, hapo sheikh itakuwa ni hatari kubwa sana!
Na hatari hiyo atalipia mkulima aliyepanda mbegu.
Salama tuwe na mambo machache, mengine kila mtu ajihudumie, sheikh hiyo ndiyo salama.

Watanganyika wameshajitambua!
watu hawataki kusikia ukweli huu, wznz sasa wanaangliwa tofauti kwasababu ya mbegu ya ubaguzi waliyopanda.

Na kwamba mbele ya safari kama hatutaweka mambo yakaeleweka, basi itakuwa ngumu sana kwao.Nasema wazi sina sababu za kuficha ficha. Mdondoaji niambie kama hakuna tension ya uznz na Utanganyika! ipo tena kubwa sana

Watu wanaogopa kusema, sisi tunasema tension iangaliwe, tusijifanye wajinga wa kusema tumeoleana n.k.
 
Nguruvi,

Mwanzoni ni kweli nilikuwa pamoja na wale waliotaka Zanzibar huru. Hii ni kwasababu ninawafahamu wazanzibari na mie nimefanya kazi na kuishi Zanzibar muda mrefu. Ila kuna mambo nimeyaona hayajakawa sawa hasa huku kwenye ajenda ya kudai mamlaka kamili. Hoja hii imegubikwa na ubinafsi na kutokujali maslahi ya baadhi ya wazanzibari wenzao hivyo basi kuendeleza lile lile linaloendelea kwa wanayolalamikia.

Pili hakuna mwenye dhamira ya dhati kuwasaidia wazanzibari kimsingi kuna ukungu mzito umetanda katika hii hoja ya Zanzibar yenye mamlaka kamili. Ukitaka kujua angalau wenye kudai mamlaka kamili either wamekosa madaraka? either wamekuwa ni wahanga wa mapinduzi? either wamekuwa wakiharibikiwa biashara zao baada ya mianya ya ukwepaji kodi kuondoka? Either ni watu waliokosa mvuto wa kisiasa baada ya kufa siasa za kindaki ndaki. Hivyo basi wamejiunga katika uwanja wa marriage of convinience kudai madaraka yao kwa msingi wakiwa wachache watadai vizuri zaidi na hivyo pengine wanaweza kufanikiwa wanachokidai. Baada ya kugundua hilo nimejitoa kwani a. Hakuna madai ya dhati yenye lengo la kumsaidia mzanzibari wa kawaida. b. Ule ubinafsi unaolalamikiwa utaendelea hata kama Zanzibar ikiwa huru.

Kimsingi Nguruvi nimeamua kumuunga mkono Mwanakijiji tuwe na Serikali moja au Dola moja. Hizi habari zenginezo tutazitengeneza taratibu .

Swaumu alhamdulilah inakatika taratibu tunamaliza ya 15. Karibu sana halwa ya lozi na kahawa na pia tende zenye sharbati kidogo huku maeneo ya kariakoo. Nasikia mnataka kuandika kitabu wewe na nduguzo vp mmeshakikamilisha?

Nilikuwapo!!!
Kitabu gani?
 
Back
Top Bottom