Niyonzima atua Simba

Niyonzima atua Simba

Status
Not open for further replies.

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,393
habari nilizozipata punde karibu na uongozi wa Simba zinasema mazungumzo baina simba na niyonzima yako katika hatua ya mwisho kumwaga wino wakati wowote.
Malkia wa nyuki amechukizwa na hatua ya yanga kumsainisha mrisho ngassa na kuongoza msafara ya kulipa kisasa, hii inatokana na yanga kuiona simba kama shamba la bibi kwa kwenda kujivunia wachezaji kama wanavyotaka, sasa ni muda wa kuchukua hatua .
stay tune more to follow....


MEWEKWA MEI 24, 2013 SAA 5:00 ASUBUHI
HATIMAYE kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhili Niyonzima amesaini mkataba wa miaka miwili zaidi kuendelea kuichezea Yanga SC na klabu hiyo asubuhi ya leo imetangaza rasmi kuongeza mkataba na mchezaji huyo wa zamani wa APR na Rayon za kwao.
Kulikuwa kuna mvutano mkubwa kati ya Yanga SC na Haruna juu ya mkataba mpya na kiungo huyo ilikuwa aondoke kesho kurejea kwao, bila kusaini mkataba mpya.
Hata hivyo, kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba Simba SC imemtengea dau la Sh. Milioni 70 na Azam FC pia inamtaka kwa dau nono zaidi, Yanga imekubali kila alichoomba Haruna katika mkataba mpya na wamemalizana.

source: BIN ZUBEIRY


Uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom klabu ya Young Africans leo umekata mzizi wa fitina kwa kiungo mchezeshaji kutoka nchini Rwanda Haruna Niyonzima kuendelea kuitumikia timu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili kufuatia kumalizika kwa mkataba wake awali.
Akiongea na waandishi wa habari makao ya klabu ya Yanga, katibu mkuu Lawrence Mwalusako amesema wameamua kumuongezea mkataba mchezaji huyo kufuatia kuuhitaji mchango wake kwani katika kipindi chake cha miaka miwili ameonyesha kiwango cha hali ya juu na kutoa mchango mkubwa.
Mwalusako amesema kumekua yakiongelewa mengi juu ya mchezaji wetu Niyonzima, baadhi ya vyombo vya habari vimekua vikitoa taarifa za kupotosha juu yake ukweli leo umedhihirika kwamba Niyonzima ni mchezaji wa Yanga na ataendelea kuitumikia kwa miaka miwili.
Haruna Niyonzima alijiunga na Yanga kwa mara ya kwanza Julai 2011 akitokea katika timu ya APR nchini Rwanda ambapo katika miaka yake miwili aliyoichezea timu ya Yanga amefanikiwa kuisadia kupata makombe mawili ya ubingwa wa Ligi Kuu 2012-2013 na Kombe la Kagame 2011-2012.
Naye Niyonzima amesema anawashukuru wanachama, washabiki na wapenzi wa klabu ya Yanga kwa kuwa naye muda wote, Yanga ni nyumbani kwangu kwani najisikia furaha kuichezea timu hii na malengo yangu ni kuisadia ili iweze kufanya vizuri katika upatashindano ya kimataifa.
Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu ya Yanga Abdallah BinKleb amesema palikua na propaganda nyingi juu ya Niyonzima, lakini ukweli ndio huu Niyonzima ataendelea kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili.
"Tunautambua mchango wake alioutoa kwa miaka mwili kwani ameweza kutupatia vikombe viwili vya Ligi Kuu ya Vodacom na Kombe la Kagame hivyo tumemuongezea mkataba wa miaka miwili tena ili aendelee kutoa mchango wake na kuisadia timu katika michezo ya kimataifa" alisema BinKleb

source: NIYONZIMA AONGEZA MIWILI YANGAView attachment 94937View attachment 94937View attachment 94937View attachment 94937
 
habari nilizozipata punde karibu na uongozi wa Simba zinasema mazungumzo baina simba na niyonzima yako katika hatua ya mwisho kumwaga wino wakati wowote.
Malkia wa nyuki amechukizwa na hatua ya yanga kumsainisha mrisho ngassa na kuongoza msafara ya kulipa kisasa, hii inatokana na yanga kuiona simba kama shamba la bibi kwa kwenda kujivunia wachezaji kama wanavyotaka, sasa ni muda wa kuchukua hatua .
stay tune more to follow....

mkuu tuombe iwe kweli pia tumchukue na kiiza na Okwi akirudi itakuwa bomba zaidi....
 
habari nilizozipata punde karibu na uongozi wa Simba zinasema mazungumzo baina simba na niyonzima yako katika hatua ya mwisho kumwaga wino wakati wowote.
Malkia wa nyuki amechukizwa na hatua ya yanga kumsainisha mrisho ngassa na kuongoza msafara ya kulipa kisasa, hii inatokana na yanga kuiona simba kama shamba la bibi kwa kwenda kujivunia wachezaji kama wanavyotaka, sasa ni muda wa kuchukua hatua .
stay tune more to follow....

yule msomali mjanja sana...yule anayeweka bastola kiunoni kipindi cha uchaguzi

yule anayefungua milango ya gari ya malkia wa nyuki

yule aliyefukuzwa chama cha soka tabora( TAREFA)...YULE ANAYEWACHANGISHA WANACHAMA KWENYE MKUTANO M30 kwa ajili ya hati ya kiwanja alichotoa hayati simba wa yuda Mzee kawawa....yule msomali anaendelea kuwadanganya atamchukua niyonzima...
 
Si walisema wao simba wanatengeneza timu ya vijana
 
Huyo Niyonzima mpuuzi tu ndio anaishia....hivyo. .!! Malkia Karibu hayo tunayaweza msije lialia hapa.....stay tuned tooooooo
 
habari nilizozipata punde karibu na uongozi wa Simba zinasema mazungumzo baina simba na niyonzima yako katika hatua ya mwisho kumwaga wino wakati wowote.
Malkia wa nyuki amechukizwa na hatua ya yanga kumsainisha mrisho ngassa na kuongoza msafara ya kulipa kisasa, hii inatokana na yanga kuiona simba kama shamba la bibi kwa kwenda kujivunia wachezaji kama wanavyotaka, sasa ni muda wa kuchukua hatua .
stay tune more to follow....

Yanga bab kubwa mchukueni muone maangamizi..muanze upya ujenzi wakikosi,kwanza sidhani kama atathubutu kucheza tim ambayo msimuujao mashindano yake makubwa ya kimataifa ni kagame hatahuko kwenyewe future is not clear kwasimba
 
yule msomali mjanja sana...yule anayeweka bastola kiunoni kipindi cha uchaguzi

yule anayefungua milango ya gari ya malkia wa nyuki

yule aliyefukuzwa chama cha soka tabora( TAREFA)...YULE ANAYEWACHANGISHA WANACHAMA KWENYE MKUTANO M30 kwa ajili ya hati ya kiwanja alichotoa hayati simba wa yuda Mzee kawawa....yule msomali anaendelea kuwadanganya atamchukua niyonzima...

malizia yule Msomalia alie lizwa mbele ya press na Twite,yulemsomali aliye hukumumiwa akatoka kwa msamaha warais kwa wizi pale FAT...endelea tena
 
Labda kama kuna Niyonzima mwingine unayemzungumzia, ila huyu anayevaa jezi namba 8 wa Yanga SC ataendelea kuchezea Jangwani

Sosi: Mimi mwenyewe
 
Confirmed!
Niyonzima amwaga wino msimbazi.
Ni Niyonzima wa timu ya daraja la 4 ya VIGWAZA FC.......
 
Labda kama kuna Niyonzima mwingine unayemzungumzia, ila huyu anayevaa jezi namba 8 wa Yanga SC ataendelea kuchezea Jangwani

Sosi: Mimi mwenyewe

tomaso, amin ivyo ivyo
 
Oyaa jamani mnajua habari nzito sana hii.. Source pls

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Watani zetu mnataka kuwashawishi wakina Rage na Malkia wa Nyuki kua kisasi kinacho stahili ni kumsainisha Nionzima? hamuwezi hata kidogo maana kufanya hivyo nikutaka vita ambayo hamtaiweza kamwe.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom