Mgombezi
JF-Expert Member
- Mar 23, 2009
- 610
- 178
Ndugu Wana-Jamii
Ni matumaini yangu mnaendelea vyema na shughuli za kila siku, pamoja na changamoto mbalimbali zinazotukabili. Kwa wale tunaofahamiana kwa kukutana ua namna yeyote ile; MALILA, LAT, KANYAGIO, THE FINEST, na wengine ambao nisingeweza kuwataja wote, habari za siku nyingi…..!!!; kwa muda mrefu sikupatikana sana katika jukwaa hili kama MGOMBEZI, hii ilitokana na harakati zangu za kuhamia hapa mjini Dodoma.
Mitandao ya kijamii imetumika katika kutuunganisha, hivyo basi kila wakati ni vyema kuangalia au kutafuta jinsi ambavyo mitandao hii inaweza kutumika katika kuleta maendeleo ya mtu binafsi na jamii kwa jumla; kama inavyotumika JAMII FORUM. Kupitia mtandao wa FACEBOOK ambao vijana wetu wengi wamejikita huko niliamua kuanzisha kundi (Group) linaloitwa WAJASIRIAMALI KWELI, kwa lengo la kushirikishana elimu ya ujasiriamali na kupeana mbinu mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika kuanzisha shughuli za uzalishaji mali. Kwa wale wanaotembelea Facebook watakuwa wanaelewa kwamba kwenye FACEBOOK kuna option ya kuunda kundi na kujitengenezea Page. Nimeona ni vyema kuleta mawazo haya pia kwa "Great Thinkers", ambapo naamini nitapata michango ya kutosha.
WAJASIRIAMAILI KWELI: Log In | Facebook
Dhana ya UJASIRIAMALI katika jamii yetu inaelekea kupoteza mwelekeo au uhalisia. Naamini utaungana nami kwamba mtazamo wa wengi juu ya MJASIRIAMALI, ni pamoja na kununua bidhaa za kichina na kupita nazo mtaani kuuza au hata kama amepanga mahali kuuza. Kwa hiyo basi dhana ya UJASIRIAMALI ni kununua na kuuza (trading), jambo ambalo ninaona kama tunapoteza mwelekeo.
Hiki ni kikundi cha wajasiriamali wakionyesha bidhaa zao; lakini bidhaa nyingi zilizopo ni kutoka china.
MAANA YA UJASIRIAMALI:
Neno ujasiriamali linatokana na maneno mawili ambayo ni UJASIRI na MALI. Hivyo maana ya ujasiriamali ni kuwa na: -
Kwa hiyo mjasiriamali:
Tunaweza kusema hizi ndizo NGUZO kuu tatu (3) za MJASIRIAMALI:
Hivyo basi mtazamo wa WAJASIRIAMALI KWELI ni kujenga uwezo wa kutekeleza nguzo hizi miongoni mwetu, hasa kwa vijana ambao tunawategemea katika shughuli za uzalishaji mali; kama tusemavyo "VIJANA NDIO TAIFA LA KESHO". Tutajengana kwa kupeana elimu ya ujasirimali na mbinu mbalimbali katika kushinda vikwazo mbalimbali.
Msemo tunaotumia…, - "TIMIZA NDOTO ZAKO KWA KUCHANGIWA MTAJI" Je una maana gani?
MTAJI NI NINI?
Mtaji ni uwezo unaoweza kutumika katika kuzalisha mali au kuongeza kipato. Kuna usemi unasema "MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE", kwamba nguzu za mtu zaweza kutumika katika uzalishaji au kuongeza kipato. Katika kuanzisha biashara uwezo huu unaweza kutokana na nguvu alizonazo mtu; kwa maana ya uwezo binafsi juu ya kile anachotaka kufanya, pamoja na rasilimali atakazohitaji.
DHANA YA KUCHANGIWA MTAJI:
Watu wengi wamekuwa na mawazo mazuri katika kuanzisha biashara lakini kikwazo kikubwa ni MTAJI. Katika kutekeleza nguzo namba tatu (3) ya Mjasiriamali; "Uwezo wa kuthubutu kushinda vikwazo vinavyoweza kuzuia utekelezaji wa fursa za biashara". Nimeamua kutumia dhana ya kuchangiana katika kutekeleza wazo la mtu binafsi katika kuanzisha biashara.
Jamii yetu imekuwa na utamaduni wa kuchangiana katika kutimiza lengo la mtu binafsi; hii imekuwa ikitumika katika kufanikisha sherehe mbalimbali za ndugu au jamaa au rafiki zikiwemo za kuzaliwa, ubatizo, kipaimara, maulidi, harusi n.k. Kwamba mtu anakusanya watu wachache ni kuwaeleza haja ya kufanikisha jambo lake na kuwataka ndugu au jamaa au marafiki kumchangia kwa hali na mali katika kufanikisha jambo hilo.
Hivyo basi kutokana na utamaduni huu ambao tumekuwa tukitumia katika kufanikisha sherehe na shughuli nyingine za kijamii, tunaweza kutumia sasa utamaduni huu katika kutekeleza malengo ya mtu binafsi ambaye anataka kuanzisha shughulli za uzalisha mali au biashara kwa kumchangia mtaji.
Mitandao ya kijamii imetumika katika kutuunganisha, hivyo basi muungano huu tunaweza kuutumia vyema katika kuangalia mahitaji ya wengine katika kutimiza ndoto zao.
Mchango tunaoweza kumpatia mtu ni pamoja na mawazo yetu katika kuboresha wazo husika na rasilimali zinazohitajika.
MRADI WA MAJARIBIO (PILOT PROJECT):
Nikiwa kama mwezeshaji wa kujitegemea, nimeamua kutekeleza wazo langu kwa vitendo kwa kuliwakilisha kwenye jamii kwa lengo la kuomba michango yao, kupitia "NIWEZESHE CAMPAIGN".
KILIMO CHA MAPAPAI – STAN'S PAPAYA
Kumekuwa na uhitaji mkubwa wa mapapai katika mji wa Dodoma na hata sehemu nyinginezo za nchi kutokana na utafiti mdogo niliyofanya, Bei ya papai katika maeneo mengi ya nchi inakadiriwa kuwa Tsh. 1000 – 3000, hapa Dodoma ni kati ya Tsh 2000 – 3000. Nikiwa kama mjasiriamali nimeona vyema kutumia uhitaji huu kama fursa ya biashara kwa kuanza kilimo cha mapapai ili kwa sehemu niweze kuchangia uzalishaji wa bidhaa hii, ambapo itasaidia pia kupunguza bei katika soko. Dhamira yangu ni papai kumfikia mlaji kwa bei kati ya Tsh. 500 – 1000. Vile vile nimehamasika kuanzisha kampeni ya matumizi ya mapapai, ikiwa ni pamoja kulitumia kama tunda na bidhaa nyinginezo zitokanazo na papai. Unaweza kutembelea page yangu kupitia mtandao wa FACEBOOK ambapo utapata dondoo za matumizi ya papai na mengineyo. Stan's PaPaYa | Facebook
Ili niweze kuanzisha mradi huu nahitaji kiasi cha fedha Tsh. 5,920,000, ambapo mchango wangu binafsi zitakuwa gharama za uendeshaji zitakazo gharimu kiasi cha Tsh. 950,000/=. Hivyo basi mchango wa fedha ninao hitaji kutoka kwa jamii ni kwa ajili ya gharama za uanzishaji (start-up fund), ambazo ni Tsh. 4,970,000/=. Natafuta watu 1000 kutoka katika jamii watakaoweza kunichangia Ts.4970/= kila mmoja.
Nawatafuta watu hawa kupitia mitandao ya kijamii (JAMII FORUM na FACEBOOK) pamoja na jamaa inayonizunguka.
Unaweza kuwakilisha Mchango wako kupitia:
Taarifa za kupokelewa kwa michango na utekelezaji wa mradi hatua kwa hatua zitawakilishwa kupitia:
JAMII FORUM - Business & Economic Forum, Katika post hii
FACEBOOK - Stan,s PaPaYa Stan's PaPaYa | Facebook
WAJASIRIAMALI KWELI Log In | Facebook
NB: Ikiwa upo ndani ya Mji wa Dodoma, unaweza kutoa order ya Mapapai na kufanya malipo ya awali. Kiwango cha chini ni mapapai kumi (10) na kila papai utalipia Tsh.500/=
Naomba kuwasilisha..............!!!, Natanguliza Shukrani.......!!!
MAHITAJI YA MRADI:
A: UWEKEZAJI
I: RASILIMALI
NB: KILIMO CHA UMWAGILIAJI:
Kilimo cha umwagiliagi kwa njia ya matone (Drip Irrigation System), ambapo mabomba (mipira) itapita kataka kila shina la mche na kudondosha matone ya maji yanapohitajika.
II: UPANDAJI
III: UENDESHAJI
NB: Kutokana na mbegu itakayotumika Mche wa papai utachukua Miezi sita (6) mpaka kuanza uzalishaji.
JUMLA YA MTAJI = Tsh. 5,920,000/=
B: JINSI YA KUPATA MTAJI:
Mtaji nategemea kupata kwa kuchangiwa na wana-jamii kama ifuatavyo:
Hivyo Basi Wana-Jamii = 1000
Kila mmoja anaweza kunichangia = Tsh. 4,970/=
***********************************UPDATES***********************************
A: HATUA ZA UTEKELEZAJI:
31/May/2012 - Upatikanaji wa eneo/shamba huko Michese, bado halijalipiwa.
B: MICHANGO KUTOKA KWA JAMII:
Ni matumaini yangu mnaendelea vyema na shughuli za kila siku, pamoja na changamoto mbalimbali zinazotukabili. Kwa wale tunaofahamiana kwa kukutana ua namna yeyote ile; MALILA, LAT, KANYAGIO, THE FINEST, na wengine ambao nisingeweza kuwataja wote, habari za siku nyingi…..!!!; kwa muda mrefu sikupatikana sana katika jukwaa hili kama MGOMBEZI, hii ilitokana na harakati zangu za kuhamia hapa mjini Dodoma.
Mitandao ya kijamii imetumika katika kutuunganisha, hivyo basi kila wakati ni vyema kuangalia au kutafuta jinsi ambavyo mitandao hii inaweza kutumika katika kuleta maendeleo ya mtu binafsi na jamii kwa jumla; kama inavyotumika JAMII FORUM. Kupitia mtandao wa FACEBOOK ambao vijana wetu wengi wamejikita huko niliamua kuanzisha kundi (Group) linaloitwa WAJASIRIAMALI KWELI, kwa lengo la kushirikishana elimu ya ujasiriamali na kupeana mbinu mbalimbali za kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika kuanzisha shughuli za uzalishaji mali. Kwa wale wanaotembelea Facebook watakuwa wanaelewa kwamba kwenye FACEBOOK kuna option ya kuunda kundi na kujitengenezea Page. Nimeona ni vyema kuleta mawazo haya pia kwa "Great Thinkers", ambapo naamini nitapata michango ya kutosha.
WAJASIRIAMAILI KWELI: Log In | Facebook
Dhana ya UJASIRIAMALI katika jamii yetu inaelekea kupoteza mwelekeo au uhalisia. Naamini utaungana nami kwamba mtazamo wa wengi juu ya MJASIRIAMALI, ni pamoja na kununua bidhaa za kichina na kupita nazo mtaani kuuza au hata kama amepanga mahali kuuza. Kwa hiyo basi dhana ya UJASIRIAMALI ni kununua na kuuza (trading), jambo ambalo ninaona kama tunapoteza mwelekeo.
Hiki ni kikundi cha wajasiriamali wakionyesha bidhaa zao; lakini bidhaa nyingi zilizopo ni kutoka china.
MAANA YA UJASIRIAMALI:
Neno ujasiriamali linatokana na maneno mawili ambayo ni UJASIRI na MALI. Hivyo maana ya ujasiriamali ni kuwa na: -
- Ujasiri au mshawasha wa kutafuta na kupata mali;
- Uwezo wa kutambua fursa za biashara haraka na uthubutu wa kuzitekeleza fursa hizo pindi zinapojitokeza; na
- Uwezo wa kuthubutu kushinda vikwazo vinavyoweza kuzuia utekelezaji wa fursa za biashara.
Kwa hiyo mjasiriamali:
- ni mtu ambaye ana sifa na uwezo wa kutambua mapema fursa za kutengeneza faida na mwenye kuunganisha nguzo kuu za uzalishaji mali (nguvu kazi, mtaji na rasilimali);
- ni mwanzilishi wa wazo na mwenye maono ya mbali ya jinsi ya kufanya biashara, uwezo wa kupanga, kuratibu na kutekeleza wazo lake na kufikia mafanikio;
- pia ni mwenye kujiamini, kujituma kwa muda mrefu, kukubali makosa na kujisahihisha, mbunifu na mwenye kuwa tayari kutumia vizuri uwezo na maarifa ya watu wengine
Tunaweza kusema hizi ndizo NGUZO kuu tatu (3) za MJASIRIAMALI:
- Ujasiri au mshawasha wa kutafuta na kupata mali;
- Uwezo wa kutambua fursa za biashara haraka na uthubutu wa kuzitekeleza fursa hizo pindi zinapojitokeza; na
- Uwezo wa kuthubutu kushinda vikwazo vinavyoweza kuzuia utekelezaji wa fursa za biashara.
Hivyo basi mtazamo wa WAJASIRIAMALI KWELI ni kujenga uwezo wa kutekeleza nguzo hizi miongoni mwetu, hasa kwa vijana ambao tunawategemea katika shughuli za uzalishaji mali; kama tusemavyo "VIJANA NDIO TAIFA LA KESHO". Tutajengana kwa kupeana elimu ya ujasirimali na mbinu mbalimbali katika kushinda vikwazo mbalimbali.
Msemo tunaotumia…, - "TIMIZA NDOTO ZAKO KWA KUCHANGIWA MTAJI" Je una maana gani?
MTAJI NI NINI?
Mtaji ni uwezo unaoweza kutumika katika kuzalisha mali au kuongeza kipato. Kuna usemi unasema "MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE", kwamba nguzu za mtu zaweza kutumika katika uzalishaji au kuongeza kipato. Katika kuanzisha biashara uwezo huu unaweza kutokana na nguvu alizonazo mtu; kwa maana ya uwezo binafsi juu ya kile anachotaka kufanya, pamoja na rasilimali atakazohitaji.
DHANA YA KUCHANGIWA MTAJI:
Watu wengi wamekuwa na mawazo mazuri katika kuanzisha biashara lakini kikwazo kikubwa ni MTAJI. Katika kutekeleza nguzo namba tatu (3) ya Mjasiriamali; "Uwezo wa kuthubutu kushinda vikwazo vinavyoweza kuzuia utekelezaji wa fursa za biashara". Nimeamua kutumia dhana ya kuchangiana katika kutekeleza wazo la mtu binafsi katika kuanzisha biashara.
Jamii yetu imekuwa na utamaduni wa kuchangiana katika kutimiza lengo la mtu binafsi; hii imekuwa ikitumika katika kufanikisha sherehe mbalimbali za ndugu au jamaa au rafiki zikiwemo za kuzaliwa, ubatizo, kipaimara, maulidi, harusi n.k. Kwamba mtu anakusanya watu wachache ni kuwaeleza haja ya kufanikisha jambo lake na kuwataka ndugu au jamaa au marafiki kumchangia kwa hali na mali katika kufanikisha jambo hilo.
Hivyo basi kutokana na utamaduni huu ambao tumekuwa tukitumia katika kufanikisha sherehe na shughuli nyingine za kijamii, tunaweza kutumia sasa utamaduni huu katika kutekeleza malengo ya mtu binafsi ambaye anataka kuanzisha shughulli za uzalisha mali au biashara kwa kumchangia mtaji.
Mitandao ya kijamii imetumika katika kutuunganisha, hivyo basi muungano huu tunaweza kuutumia vyema katika kuangalia mahitaji ya wengine katika kutimiza ndoto zao.
Mchango tunaoweza kumpatia mtu ni pamoja na mawazo yetu katika kuboresha wazo husika na rasilimali zinazohitajika.
MRADI WA MAJARIBIO (PILOT PROJECT):
Nikiwa kama mwezeshaji wa kujitegemea, nimeamua kutekeleza wazo langu kwa vitendo kwa kuliwakilisha kwenye jamii kwa lengo la kuomba michango yao, kupitia "NIWEZESHE CAMPAIGN".
KILIMO CHA MAPAPAI – STAN'S PAPAYA
Kumekuwa na uhitaji mkubwa wa mapapai katika mji wa Dodoma na hata sehemu nyinginezo za nchi kutokana na utafiti mdogo niliyofanya, Bei ya papai katika maeneo mengi ya nchi inakadiriwa kuwa Tsh. 1000 – 3000, hapa Dodoma ni kati ya Tsh 2000 – 3000. Nikiwa kama mjasiriamali nimeona vyema kutumia uhitaji huu kama fursa ya biashara kwa kuanza kilimo cha mapapai ili kwa sehemu niweze kuchangia uzalishaji wa bidhaa hii, ambapo itasaidia pia kupunguza bei katika soko. Dhamira yangu ni papai kumfikia mlaji kwa bei kati ya Tsh. 500 – 1000. Vile vile nimehamasika kuanzisha kampeni ya matumizi ya mapapai, ikiwa ni pamoja kulitumia kama tunda na bidhaa nyinginezo zitokanazo na papai. Unaweza kutembelea page yangu kupitia mtandao wa FACEBOOK ambapo utapata dondoo za matumizi ya papai na mengineyo. Stan's PaPaYa | Facebook
Ili niweze kuanzisha mradi huu nahitaji kiasi cha fedha Tsh. 5,920,000, ambapo mchango wangu binafsi zitakuwa gharama za uendeshaji zitakazo gharimu kiasi cha Tsh. 950,000/=. Hivyo basi mchango wa fedha ninao hitaji kutoka kwa jamii ni kwa ajili ya gharama za uanzishaji (start-up fund), ambazo ni Tsh. 4,970,000/=. Natafuta watu 1000 kutoka katika jamii watakaoweza kunichangia Ts.4970/= kila mmoja.
Nawatafuta watu hawa kupitia mitandao ya kijamii (JAMII FORUM na FACEBOOK) pamoja na jamaa inayonizunguka.
Unaweza kuwakilisha Mchango wako kupitia:
TIGO PESA - 0714 460528 or M - PESA - 0757 941044
(Mwisho ya kupokea michango tarehe 30/06/2012)
(Mwisho ya kupokea michango tarehe 30/06/2012)
Taarifa za kupokelewa kwa michango na utekelezaji wa mradi hatua kwa hatua zitawakilishwa kupitia:
JAMII FORUM - Business & Economic Forum, Katika post hii
FACEBOOK - Stan,s PaPaYa Stan's PaPaYa | Facebook
WAJASIRIAMALI KWELI Log In | Facebook
NB: Ikiwa upo ndani ya Mji wa Dodoma, unaweza kutoa order ya Mapapai na kufanya malipo ya awali. Kiwango cha chini ni mapapai kumi (10) na kila papai utalipia Tsh.500/=
Naomba kuwasilisha..............!!!, Natanguliza Shukrani.......!!!
MAHITAJI YA MRADI:
A: UWEKEZAJI
I: RASILIMALI
MAHITAJI | MAELEZO | KIASI | BEI | JUMLA |
Ununuzi wa Shamba | Heka | 1 | 1,000,0000/= | 1,000,000/= |
Ujenzi wa Nyumba ya Wafanyakazi | Nyumba | 1 | 700,000/= | 700,000/= |
VIFAA VYA UMWAGILIAJI – Umwagiliaji kwa njia ya matone (Drip irrigation systems) | ||||
Bomba – ¾ inch (pvc) | Mita | 1500 | 1000/= | 1,500,000/= |
Tank la Maji | 1000 Lita | 1 | 160,000/= | 160,000/= |
Pump ya kusukuma maji | 1 | 300,000/= | 300,000/= | |
Bomba la kuvuta maji | Mita | 5 | 10,000/= | 50,000/= |
Bomba la kupeleka kwenye Tank | Mita | 20 | 3,000/= | 60,000/= |
Ujenzi wa Mnara wa Tank | 1 | 300,000/= | 300,000/= | |
JUMLA | 4,070,000/= |
NB: KILIMO CHA UMWAGILIAJI:
Kilimo cha umwagiliagi kwa njia ya matone (Drip Irrigation System), ambapo mabomba (mipira) itapita kataka kila shina la mche na kudondosha matone ya maji yanapohitajika.
II: UPANDAJI
MAHITAJI | MAELEZO | KIASI | BEI | JUMLA |
Maandalizi ya Shamba | Heka | 1 | 100,000/= | 100,000/= |
Mbole – Samadi ya Ng'ombe | Tani | 10 | 10,000/= | 100,000/= |
Manunuzi ya Mbegu | 1000 | 500/= | 500,000/= | |
Upandaji wa Mbegu | 1000 | 200/= | 200,000/= | |
JUMLA | 900,000/= |
III: UENDESHAJI
NB: Kutokana na mbegu itakayotumika Mche wa papai utachukua Miezi sita (6) mpaka kuanza uzalishaji.
MAHITAJI | MAELEZO | KIASI | BEI | JUMLA |
Mfanyakazi (miezi 7) | Miezi | 7 | 100,000/= | 700,000/= |
Gharama Nyinginezo | 250,000/= | 250,000/= | ||
JUMLA | 950,000/= |
JUMLA YA MTAJI = Tsh. 5,920,000/=
B: JINSI YA KUPATA MTAJI:
Mtaji nategemea kupata kwa kuchangiwa na wana-jamii kama ifuatavyo:
MCHANGO BINAFSI – Gharama za Uendeshaji | 950,000/= |
MCHANGO WA WANA-JAMII – Rasilimali + Upandaji | 4,970,000/= |
JUMLA | 5,920,000/= |
Hivyo Basi Wana-Jamii = 1000
Kila mmoja anaweza kunichangia = Tsh. 4,970/=
***********************************UPDATES***********************************
A: HATUA ZA UTEKELEZAJI:
31/May/2012 - Upatikanaji wa eneo/shamba huko Michese, bado halijalipiwa.
B: MICHANGO KUTOKA KWA JAMII:
S/NO | ID | AMOUNT | DATE | |
1 | Bakari Kawiza | 5,000 | 29-May-12 | |
2 | Fadhili Chitanda | 5,000 | 29-May-12 | |
3 | Amkawewe | 5,000 | 4-Jun-12 | |
4 | Kaunga | 10,000 | 4-Jun-12 | |
5 | Rose Lusinde | 10,000 | 5-Jun-12 | |
6 | Malila | 10,000 | 7-Jun-12 | |
7 | Miundombinu | 20,000 | 9-Jun-12 | |
8 | Mary Msemwa | 6,000 | 10-Jun-12 | |
9 | Leonard Kisenha | 5,000 | 11-Jun-12 | |
10 | Kibanga Ampiga Mkoloni | 20,000 | 11-Jun-12 | |
11 | Kitokota | 10,000 | 13-Jun-12 | |
12 | Asrams | 5,000 | 17-Jun-12 | |
13 | Jalala | 10,000 | 20-Jun-12 | |
14 | Muhinda | 10,000 | 20-Jun-12 | |
Total contributions as today: |
| |||
Total Amount Requested: | 4,970,000 | |||
Balance: | -4,839,000 |