Niwezeshe kutimiza ndoto yangu

Nimeipenda. Nzuri sana hangaika dunia hii inahitaji juhudi binafsi. Nitachangia kesho mchana.

John Kennedy wa USA aliwahi sema "Don't ask what the USA has done for you,but rather ask yourself what have you done for USA"
 
Nimeipenda. Nzuri sana hangaika dunia hii inahitaji juhudi binafsi. Nitachangia kesho mchana.

John Kennedy wa USA aliwahi sema "Don't ask what the USA has done for you,but rather ask yourself what have you done for USA"

Natanguliza shukrani Mkuu KITOKOTA.....!!!
 
Kaka yangu nishakukaribisha(Facebook) uje kuchukua hope itatosha!

Nashukuru KIBANGA AMPIGA MKOLONI, naamini utakuwa umesoma kwa makini maelezo ya awali na utakuwa umeelewa dhamira yangu. Ningependa kufahamu, umenialika katika kundi gani la kuweza kupata hope?, japokuwa na mchango wako wa NIWEZESHE nauhitaji pia.
 
Nimepokea kiasi cha Tsh 96,000/= kutoka kwa wachangiaji 10; bado ninahitaji kiasi cha Tsh 4,874,000/= ili niweze kuanza mradi huu. Nimekuwa nikitafuta watu 1000 kutoka kwenye jamii watakaoweza kunichangia Tsh 4970/= kila mmoja ili niweze kupata Tsh 4,970,000/= ninazohitaji katika kuanzisha mradi huu. Kutoka na michango ya watu 10 niliyopokea ni sawa na watu 19 kama kila mmoja angetoa kiasi cha Tsh. 4970/=, hivyo basi ninahitaji watu 981 kunichangia kiasi cha Tsh 4970. Nawashukuru wale wote walioguswa na hitaji hili na kunichangia, hasa wale waliotoa kwa kiwango cha juu na kuweza kufidia watu 9 zaidi. Bado ninahitaji mchango wako....NIWEZESHE....!!!
 
Kaka mie mchango wangu ntatoa mwisho mwa wiki hii,


Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD
 
Juzi nilikuahidi kuwa nitakurushia cho chote ingawaje siioni message yangu. Hapana shaka ahadi ni deni, pokea mchango wangu. Elfu kumi tu.Asante.
 
Juzi nilikuahidi kuwa nitakurushia cho chote ingawaje siioni message yangu. Hapana shaka ahadi ni deni, pokea mchango wangu. Elfu kumi tu.Asante.

Nashukuru Mkuu KITOKOTA, nimepokea mchango wako.
 
Kaka nishatuma mchango wangu, na muwakilishi wangu kanambia umempigia, je ni kweli ? Mwisho wa mwezi ntatoa nyingine inshaAllah tukiwa hai na panapo uzima


Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD
 
Tupo pamoja mkuu, ila tu labda ungesogeza deadline ili kwa wale wenye nia ya kukuchangia na kwa sasa wanasubiri mwisho wa mwezi waweze kukuunga mkono wakati unapofika wa mishiko. kisha Baada ya hapo ni ushauri wangu kuwa uwezekano ni mkubwa kuwa pesa zitakuwa hazijakamilika,

Lakini kile ambacho utakuwa umejaaliwa kukikusanya mpaka wakati huo wewe anza tu mchakato wa mambo madogo madogo. na kadri unavyowahakikishia wana Jf hatua ulizofikia na kuwathibitishia lazima watajitokeza wafadhili zaidi na hata hao waliokwisha toa huenda wakaingiwa moyo wa kutoa zaidi.
Kila La kheri.
Mkulima mwenzio,
Kitope
 
Tupo pamoja mkuu, ila tu labda ungesogeza deadline ili kwa wale wenye nia ya kukuchangia na kwa sasa wanasubiri mwisho wa mwezi waweze kukuunga mkono wakati unapofika wa mishiko. kisha Baada ya hapo ni ushauri wangu kuwa uwezekano ni mkubwa kuwa pesa zitakuwa hazijakamilika, lakini kile ambacho utakuwa umejaaliwa kukikusanya mpaka wakati huo wewe anza tu mchakato wa mambo madogo madogo. na kadri unavyowahakikishia wana Jf hatua ulizofikia na kuwathibitishia lazima watajitokeza wafadhili zaidi na hata hao waliokwisha toa huenda wakaingiwa moyo wa kutoa zaidi.
Kila La kheri.
Mkulima mwenzio,
Kitope

Nashukuru KITOPE kwa ushauri wako, nimeupokea vyema; kweli niliweka malengo ya kuendesha kampeni hii ndani ya mwezi mmoja yaani mwezi huu JUNE. Umuhimu wa kuongeza deadline unaonekana kwani mpaka sasa nimefikia lengo kwa asilimia 2.6%. Naamini wengi watajitokeza kunichangia katika kipindi hiki cha mwisho wa mwezi na kuniwezesha kupata kiasi cha Tsh. 2,000,0000; na kuniwezesha kuanza hatua za utekelezaji katika mwezi ujao wa JULY 2012.
 
Kaka nishatuma mchango wangu, na muwakilishi wangu kanambia umempigia, je ni kweli ? Mwisho wa mwezi ntatoa nyingine inshaAllah tukiwa hai na panapo uzima


Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD

Nashukuru Mkuu ASRASMA, nimepokea mchango wako; natanguliza shukrani kwa ahadi yako.
 
Ifikapo JAN-2013, Niwezeshe kutimiza ndoto yangu kwa kunichangia kiasi cha Tsh 4970 tu, nahitaji wachangiaji 974 ili kukamilisha kiasi ninachohitaji ili kufanikisha kuanza kwa mradi huu.
farm02.gif
 
Muhimu kufanya upembuzi yakinifu katika kutafuta eneo la shamba ; hivyo basi kwa sasa nimepata maeneo mawili (2) tofauti ambapo nitatakiwa kufanya maamuzi wakati wa kununua; nimepeta shamba katika kijiji cha Michese na Nala hapa Dodoma. Niwezeshe Kutimiza ndoto yangu kwa mchango wako.

Shamba lililopo katika kijiji cha MICHESE ambo lina takribani heka 3 na nusu

Farm Layout.png

Shamba lililopo katika kijiji cha MICHESE ambo lina takribani heka 2

NALA-Proposed Area for Farm.png


 
UPDATES: 28 June 2012 - MALIPO YA AWALI KWA AJILI YA SHAMBA LILILOPO KATIKA KIJIJI CHA NALA:

Shamba nililopata katika kijiji cha Nala lina ukubwa wa heka mbili (2) na litagharimu kiasi cha Tsh. 1,500,000/=. Leo nimelipa malipo ya awali kiasi cha Tsh. 700,000/=, bado Tsh. 800,000/=. Malipo haya ya awali yametokana na mchango binafsi wa Tsh. 100,000/= kutokana na michango niliyopokea kutoka kwa jamii na kiasi cha Tsh. 600,000/= ni mchango binafsi.

DSC04209.JPG

Mkono wa Kulia; Mimi, Kutoka kushoto; Mzee Mosha akiandaa makubaliano ya kuuza shamba na kupokea malipo ya awali. Walioketi kwenye matofali; aliyevaa shati jeupe na kuwekewa mkono begani na bwana aliyesimama huyu ndiye mwenye shamba, Mzee Cheni na wengine ni viongozi wa Mtaa wa Nala.

DSC04212.JPG

Kulia; Bwana Mwinyi akipokea malipo ya awali kwa niaba ya mwenye Shamba Mzee Cheni (Hayupo katika picha hii)

NB: Katika mchanganuo wa mradi gharama za shamba nilikadiria kiasi cha Tsh.1,000,000/= kwa heka, lakini hapa nimepata heka 2 kwa Tsh. 1,500,000/=; niliamua kuchukua heka mbili kutokana na maoni ya wadau niliokuwa nakutana nao, kwani walishauri ni vyema kuchukua heka zaidi ya moja ili kuwe na eneo la ziada kidogo.

Nawashukuru wale wote waliotoa michango yao mpaka sasa na kuniwezesha kuchukua hatua za awali za utekelezaji, lakini bado naomba mchango wako ili niweze kutimiza ndoto hii.

Msaada: Kwa anayefahamu jinsi ya kukuza picha niomba anielekeze au kufanya hivyo; ningependa picha hizi kuonekana vyema.
 
Mkuu Mgombezi,
naona jina langu kwenye list ya waliochangia umelikosea.
Ni Muhinda sio Milinda.
nakutakia kila la kheri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom