Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Ninaweza kuwa nakosea, lakini kwa nafsi yangu nipo sahihi.
Nimefurahishwa sana kwa kitendo cha serikali kumshikilia Dr Slaa. Nimefurahi sana anapohenyeka. Binafsi naungana na msimamo wa wale wanaotaka mkataba wa DP World uangaliwe upya na maboresho yafanyike. Hapo namuunga mkono Dr Slaa na wakosoaji wengine. Ila kwa kukamatwa kwa Dr Slaa, nimefurahi sana, haijalishi kuwa ni kweli alipanga uhaini au lah.. hilo halinihusu.
Nilikuwa nampenda sana na kumuamini mno Dr Slaa. Ila Kwa kitendo chake cha kuwasaliti, kuwaponda Chadema na kuisaidia CCM mwaka 2015 nilimtoa kabisa thamani. Mwaka 2015 baada ya kuitosa CDM nilimpigia simu (nashukuru aliipokea) nikamuomba kwa heshima kubwa kuwa, kama hajaridhishwa na ujio wa Lowassa Chadema, basi akae kimya bila kujiingiza kuivuruga Chadema na UKAWA kwa ujumla. Alinisikiliza na akajibu, nimekuelewa. Lakini baada ya hapo akaanza kutoa matamko, kupitia mikutano na waandishi wa habari.
Hayo yakapita, akaenda Canada na baadae akateuliwa kuwa Balozi huko ughaibuni.
Baada ya muda, mkataba wake wa Ubalozi ukaisha. Karudi nyumbani. Mwenyekiti wake wa Chama wa zamani Freeman Mbowe yupo matatizoni kwa kesi ya Ugaidi. Watu wanapaza sauti kuwa, Mbowe sio Gaidi aachiwe huru. Dr Slaa anaibuka kutoka katika makazi yake na kusema, ANASIKITISHWA SANA NA WATU WANAOSEMA MBOWE SIO GAIDI. ANASHAURI WATU HAO WAKAE KIMYA WAKISUBIRI SERIKALI NA MAHAKAMA VIFANYE KAZI YAO. Mungu jaalia, Mbowe ametoka na yupo huru. Kibao kimegeuka.
Acha nae asote. Nimefurahi sana
Nimefurahishwa sana kwa kitendo cha serikali kumshikilia Dr Slaa. Nimefurahi sana anapohenyeka. Binafsi naungana na msimamo wa wale wanaotaka mkataba wa DP World uangaliwe upya na maboresho yafanyike. Hapo namuunga mkono Dr Slaa na wakosoaji wengine. Ila kwa kukamatwa kwa Dr Slaa, nimefurahi sana, haijalishi kuwa ni kweli alipanga uhaini au lah.. hilo halinihusu.
Nilikuwa nampenda sana na kumuamini mno Dr Slaa. Ila Kwa kitendo chake cha kuwasaliti, kuwaponda Chadema na kuisaidia CCM mwaka 2015 nilimtoa kabisa thamani. Mwaka 2015 baada ya kuitosa CDM nilimpigia simu (nashukuru aliipokea) nikamuomba kwa heshima kubwa kuwa, kama hajaridhishwa na ujio wa Lowassa Chadema, basi akae kimya bila kujiingiza kuivuruga Chadema na UKAWA kwa ujumla. Alinisikiliza na akajibu, nimekuelewa. Lakini baada ya hapo akaanza kutoa matamko, kupitia mikutano na waandishi wa habari.
Hayo yakapita, akaenda Canada na baadae akateuliwa kuwa Balozi huko ughaibuni.
Baada ya muda, mkataba wake wa Ubalozi ukaisha. Karudi nyumbani. Mwenyekiti wake wa Chama wa zamani Freeman Mbowe yupo matatizoni kwa kesi ya Ugaidi. Watu wanapaza sauti kuwa, Mbowe sio Gaidi aachiwe huru. Dr Slaa anaibuka kutoka katika makazi yake na kusema, ANASIKITISHWA SANA NA WATU WANAOSEMA MBOWE SIO GAIDI. ANASHAURI WATU HAO WAKAE KIMYA WAKISUBIRI SERIKALI NA MAHAKAMA VIFANYE KAZI YAO. Mungu jaalia, Mbowe ametoka na yupo huru. Kibao kimegeuka.
Acha nae asote. Nimefurahi sana