Niulize Swali lolote nitakujibu

Niulize Swali lolote nitakujibu

-Kwanini Tanzania ni maskini wakati resource zote za kutuingizia hela tunazo?

-kwanin kuna kufa?

-Mtu akifa huwa anaenda wapi?

-kwanini ulizaliwa?

-kama jf isingekuwepo ungekuwa unafanya nini mda huu?

-Kitu gani kimekusukuma hadi ukaanzisha hii thread?
 
Niambie maana ya ID yako? na kwanini umechagua hiyo?
 
kwanini watu/wasomi. hutoafautiana mawazo katika jamii???? tena katika kutofautiana uko kila mmoja hujiona yuko sahihi zaid ya mwenzake!???? naomba unijibu kitaaluma kwa kutumia majibu ya kisayansi
 
Neno linasema kuwa mungu anatupenda na anaweza kila kitu, hapohapo anasema yeye ndio atupangia kesho yetu.
Sasa iweje mungu aseme kuna watakaoenda motoni?

ndugu yangu, mungu ametupa uhuru wa kuchagua kwa utashi wetu wenyewe. Mungu haingilii maamuzi yetu wala hatupangii kwamba tufanye nini. Motoni ni kwa ajili ya wale ambao ni wakaidi kwa masuala ya mungu
 
Jumamosi hii nimejipanga kujibu swali lolote. Haya, wenye maswali niulizeni kuhusu jambo lolote. Kunihusu, kuhusu siasa, dini, sayansi, teknolojia, mahusiano n.k

niko baa gani hapa??
 
-Kwanini Tanzania ni maskini wakati resource zote za kutuingizia hela tunazo?

-kwanin kuna kufa?

-Mtu akifa huwa anaenda wapi?

-kwanini ulizaliwa?

-kama jf isingekuwepo ungekuwa unafanya nini mda huu?

-Kitu gani kimekusukuma hadi ukaanzisha hii thread?

Tanzania ni maskini kwa sababu ya udhaifu wa rais. Hakuna umakini ktk kusimamia ra7limali zetu. Kama jf isingekuwepo labda ningekuwa kwenye jukwaa jingne.
Mtu akifa anaenda ama mbinguni, motoni au toharani. Mungu anajua kwa n4ni nilizaliwa na m4mi najitahdi kutimiza mapenzi yake. Nimeanzisha hii thrd ili nipime namna gani naweza kujibu hoja za wengne na kujua watu wanawaza nini
 
ndugu yangu, mungu ametupa uhuru wa kuchagua kwa utashi wetu wenyewe. Mungu haingilii maamuzi yetu wala hatupangii kwamba tufanye nini. Motoni ni kwa ajili ya wale ambao ni wakaidi kwa masuala ya mungu

Maandiko yanasema kabla ya kuzaliwa nalikujua na nilijua njia zako zote.
Na pia anasema kuwa yeye hutangaza mwisho kabla ya mwanzo.
Unapaonaje hapo?? Hakuna aijuae kesho isipokuwa yeye.
Nukuulize je? Kuna haja gani ya sisi kujishughulisha wakati yeye ndio mpangaji wa kesho?
Naomba unijibu kama tunajifunza. Iweje mungu aliyemuumba shetani huku akijua tarehe fulani atamuasi lakini akamuumba tu. Kosa la pili ni pale shetani ameshaasi huyohuyo mungu akamuumba tena mwanadamu na huku akijua kabisa tena ikifika muda fulani huyu shetani atamdanganya na atadanganyika. Huyo anakuja anatoa hukumu kwa viumbe wake aliowaumba kwa upendo mkuu japo aliwaambia wasifanye hivi wakafanya vile.
Lakini huyu mungu muumba wa kila kitu, muweza yote, mwenye upendo usio na kipimo anayeona mwanzo kabla ya mwisho na mwisho kabla ya mwanzo aliyaona haya hata kabla ya kutuumba kwanini awe Mkali ivo? Au mateso ya viumbe wake ndio burudani yake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom