funaku
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 38,535
- 31,199
Ghadaffi aliondolewa na kuuawa kinyama kwa maslahi ya wazungu na hatima ya nchi ya libya imekuwa ni mbaya sana na kupelekea vita visivyoisha na ukimbizi wa aina yake duniani.
leo hii tunashuhudia jaribio la kumuondoa Mugabe kwa mapinduzi baada ya mbinu za kidemokrasia kushindwa.
Kwa mujibu wa BBC wazungu wanaamini kuwa Zimbabwe imekuwa mismanaged kwa miaka zaidi ya 37...msimamo huu unahusianishwa na yeye kuwafukuza matajiri wachache kwa manufaa ya umma.
Leo hii wazungu wanatuaminisha kuwa nchi ya Zimbabwe imeharibika kutokana na kuondoa mazingira ya unyonyaji wa wawekezaji wa kizungu.
Siku zote wazungu wamesisitiza kuhusu kubadilisha utawala kwa njia ya demokrasia...kwa nini wachekelee mapinduzi? Kwa nini hawatumii maguvu yao kuzuia mapinduzi?Je mfumo wa mapinduzi ni sehemu ya njia bora za kubadilisha tawala?
Ni wakati AU kuonesha makucha yake na kukataa double standards katika Demokrasia.Au wanapaswa kupinga kwa kauli na matendo yote dhidi ya mapinduzi haya ya kijeshi.
AU wasipoponga au UN wasipopinga mapinduzi basi tusuwasikie tena kupinga mapinduzi sehemu yoyote duniani.
Inasemekana jeshi la Zimbabwe liliwasiliana na China ili kufanya hayo wanayotaka kufanya...kama hili ni kweli basi AU haina budi kumuonya China na ikiwezekana kumkataa kama muwekezaji kwani naye atakuwa amekubaliana na wazungu kuimaliza Afrika.
AU watakuwa na kikao kinachohusu usalama kesho...tusubiri tuone tamko lao.
leo hii tunashuhudia jaribio la kumuondoa Mugabe kwa mapinduzi baada ya mbinu za kidemokrasia kushindwa.
Kwa mujibu wa BBC wazungu wanaamini kuwa Zimbabwe imekuwa mismanaged kwa miaka zaidi ya 37...msimamo huu unahusianishwa na yeye kuwafukuza matajiri wachache kwa manufaa ya umma.
Leo hii wazungu wanatuaminisha kuwa nchi ya Zimbabwe imeharibika kutokana na kuondoa mazingira ya unyonyaji wa wawekezaji wa kizungu.
Siku zote wazungu wamesisitiza kuhusu kubadilisha utawala kwa njia ya demokrasia...kwa nini wachekelee mapinduzi? Kwa nini hawatumii maguvu yao kuzuia mapinduzi?Je mfumo wa mapinduzi ni sehemu ya njia bora za kubadilisha tawala?
Ni wakati AU kuonesha makucha yake na kukataa double standards katika Demokrasia.Au wanapaswa kupinga kwa kauli na matendo yote dhidi ya mapinduzi haya ya kijeshi.
AU wasipoponga au UN wasipopinga mapinduzi basi tusuwasikie tena kupinga mapinduzi sehemu yoyote duniani.
Inasemekana jeshi la Zimbabwe liliwasiliana na China ili kufanya hayo wanayotaka kufanya...kama hili ni kweli basi AU haina budi kumuonya China na ikiwezekana kumkataa kama muwekezaji kwani naye atakuwa amekubaliana na wazungu kuimaliza Afrika.
AU watakuwa na kikao kinachohusu usalama kesho...tusubiri tuone tamko lao.