Nitapata wapi mkopo wa vitu vya ndani?

Nitapata wapi mkopo wa vitu vya ndani?

Good morning ladies and gents,

Wadau nilipata majanga ya kuibiwa TV, Friji na jiko siku kadhaa nyuma. Mimi ni mwajiriwa na kamshahara sio haba ila nikisema ninunue vitu vyote inakuwa ngumu, wapi naweza kupata mkopo wa kimoja wapo au vyote kati ya TV, Friji au jiko na nilipe kidogo kidogo kwa miezi kadhaa? hata mitatu au minne maximum.
Naweza kujichanga kidogokidogo ila najaribu kuona kama njia hiyo pia inawezekana maana shemeji/wifi yenu anaboreka sana hadi anataka kwenda kupumzika kijijini kwa muda ye na mtoto.
Asanteni
Ushauri usikope kama maingizo yako hayawezi kuulipa huo mkopo kwakujinafasi

Do not get a loan when your cash flow is weak
 
Mkeo anafatilia movie zilizotafsiriwa??
Hapana, wala sio mtu wa TV sana. Tatizo watu wameelewa vibaya, mke ana mtoto mdogo so muda wote anashinda nyumbani, sasa imagine umekaa ndani tu hamna jiko/friji(kupikapika),hamna TV, unaboreka sana ndio maana ameomba aende nyumbani kupoteza muda kidogo maana nimemwambia nataka kununua vyote kwa mara moja. Sasa kila mtu hapa maona anatoa povu kuhusu mke wakati sio lengo kuu la huu uzi.
 
Back
Top Bottom