Huyu mbona anakuja vibaya hivyo??? Anafikiri CCM unajiamulia tu ugombee wapi na unapita kama ilivyo CDM? CCM kuna demokrasia ya kweli, kuna mchakato wa kumpata mgombea, hamna udicteta wa CDM wa Mbowe au Slaa wa kuamua nani agombee wapi!!!!
Hajawajua CCM vizuri, kuna watu ndani ya CCM wanapiga jaramba miaka nenda rudi hata kupewa nafasi ya kugombe uenyekiti wa mtaa hawajapewa sasa yeye kaingia jana tu anajangaza kugombea jimbo la Ubungo? Mbona Nape alishatangaza analitamani hilo jimbo? Na yeye analitaka? Amuulize Hawa Ng'umbi kilichompata hadi sasa hazungumzii tena Ubunge. Sijui au Jay Kaya jana kaonja joto la ka binti? Ndo akakaahidi hiyo chance!
CCM wenyewe hawawezi kumpitisha kwenye kura za maoni
Juliana Shonza aliyetimuliwa Chadema na kujiunga na CCM jana amelalamikia CHADEMA kuwa kuna mfumo dume na kwamba hakuna mwingine anayetoa kauli zaidi ya viongozi wa juu wa chama hicho.
Shonza alitumia fursa hiyo kumtumia salamu Mbunge wa Ubungo John Mnyika (CHADEMA) na kumtaka ajiandae kwa mapambano katika uchaguzi wa mwaka 2015.Shonza amesema mjini Dodoma kwamba mwaka huo ndiyo utaamua kati yake na Mnyika ni nani zaidi Ubungo
Source:Tanzania Daima
Hakuna kilichofanyika kwenye jimbo la Ubungo zaidi ya kumuona mbunge wetu Mnyika akiruka sarakasi zake bungeni ambazo hazitusaidii chochote sisi wananchi.
Juliana Shonza atapata ubunge bila ya wasiwasi.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Huyu mbona anakuja vibaya hivyo??? Anafikiri CCM unajiamulia tu ugombee wapi na unapita kama ilivyo CDM? CCM kuna demokrasia ya kweli, kuna mchakato wa kumpata mgombea, hamna udicteta wa CDM wa Mbowe au Slaa wa kuamua nani agombee wapi!!!!
Juliana Shonza aliyetimuliwa Chadema na kujiunga na CCM jana amelalamikia CHADEMA kuwa kuna mfumo dume na kwamba hakuna mwingine anayetoa kauli zaidi ya viongozi wa juu wa chama hicho.
Shonza alitumia fursa hiyo kumtumia salamu Mbunge wa Ubungo John Mnyika (CHADEMA) na kumtaka ajiandae kwa mapambano katika uchaguzi wa mwaka 2015.Shonza amesema mjini Dodoma kwamba mwaka huo ndiyo utaamua kati yake na Mnyika ni nani zaidi Ubungo
Source:Tanzania Daima
Anachojalibu dada kukifanya ni kutuhadaa tu,lakini bei yake ni ukuu wa wilaya tu!Hata kura za maoni hapenyi
Teh teh teh!kichuguu against mlima kilimanjaro!
Tanzania Daima gazeti la udaku.