Majigo
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 5,519
- 1,831
- Thread starter
- #141
57--Swali langu lilimfanya Helena anyamaze kimya na kutazama chini, nililirudia swali langu la awali. Helena mbona hunijibu, kwa hiyo umeacha uchawi? Shija nashindwa nikujibu nini ili unielewe, Helena alinijibu kwa sauti ya upole akiwa bado ameangalia chini.
Helena lolote utakalonieleza nitakuelewa. Nikikueleza kuwa nimeacha uchawi nitakudanganya ila kwa asilimia kubwa sitashiriki kwenye kazi za kichawi, muda wangu mwingi nitautumia kuhakikisha usalama wako japo kwa sasa najua huna tatizo lolote kutokana mzee Manoni kukusimamia.
Najua una kazi nzito ya kuibadili tabia uliyoizoea lakini kila kitu kina mwisho wake, uchukie uchawi mwisho Mungu atakutoa bila ya wewe kujielewa, nilimpa moyo. Shija nitajitahidi kufanya hivyo .
Tuliongozana na Helena kurudi kijijini, njiani tulizungumza mengi yakiwemo yale tuliyoyafanya wakati tukiwa marafiki. Tulipofika kijijini tuliagana na kila mmoja alienda kwao. Nilipofika nyumbani nilijikuta nikijawa na mawazo mengi juu ya maneno ya Helena ya kuniomba msamaha.
Japo nilikuwa na wasiwasi kwa maneno yake na kuyaona kama kweli yalipandikizwa ili kuniteka kimawazo na kunifanyia kitu kibaya. Lakini moyo wangu ulijaa ujasiri kwa kuamini kile nilichomueleza Sabina amsamehe Helena, kuwa adui wa jana anaweza kuwa rafiki mwema wa leo.
Nilijikuta nikimuamini Helena kwa kauli yake kwamba kutaka kuniua kulitokana na shinikizo la kutolewa yeye kafara. Nilijikuta nikimuonea huruma, siku zote pamoja na ubaya aliotaka kunifanyia lakini bado niliyakumbuka mema aliyonifanyia pale alipojitolea kwa hali na mali kumtorosha marehemu kaka yangu.
Badala ya kujionea huruma mimi nilijikuta nikimuonea huruma Helena kwa masaibu yote aliyopata mpaka kuponea tundu la sindano kuuawa na Sabina. Kumbe hata angemuua angekufa na siri nzito moyoni ambayo ilionesha mimi ndiye mhusika mkuu.
Niliamua kusahau yote yaliyopita na kuganga yajayo , nikamchukulia Sabina kama rafiki yangu mwema aliyetaka kujiokoa kwa kuutoa uhai wangu. Siku zote niliamini mwenye uwezo wa kuuchukua uhai wa mwanadamu ni Mungu pekee na si nguvu za giza wala mashetani.
Siku zilikatika, niliendelea na masomo yangu vyema huku nikionekana zile nguvu nilizokuwa nazo shule ya msingi nimezihamishia sekondari, Nilikuwa mmoja ya wanafunzi tegemezi kutokana na uwezo wangu niliouonesha darasani ambao ulinifanya niwe maarufu shuleni.
Wakati wa likizo kubwa mama alinieleza kwamba mjomba ananiita mjini. Nilikwenda kwa mjomba ambako nilijua muda wangu nitautumia kusoma. Jioni ya siku niliyofika , mjomba aliniita pembeni na kutaka kujua niliyomueleza kuhusu kumleta marehemu kaka akiwa hai yaliishia wapi? Anko mbona kimya, harakati zako za kumleta kaka yako ziliishia wapi?
Swali lilikuwa zito, nilijikuta nimebakia kimya nikiwa sijui niseme nini. Sikuwa na cha kumueleza kwa kuamini kila nitakachomueleza atazidi kuniona muongo. Shija si nakuuliza? Ulisema kaka yako hakufa yupo hai, si ndiyo?
Kuna mtu alinihakikishia lakini mwisho wa siku alisema alikuwa akinidanganya, nilitengeneza uongo ili kuficha siri nzito ya kifo cha kaka nilichokishuhudia kwa macho yangu.
Kwa hiyo hayupo hai? Ndiyo. Lakini si ulituhakikishia kuwa ulimuona akiwa hai? Niliwadanganya kwa vile kuna mtu alinihakikishia kamuoa akiwa hai na kuniahidi atamtoa nije kwako nimtafutie nafasi.
Yeye alinijuaje? Aliniuliza kama kuna mtu aliye mbali na kijiji ili akimtoa tumlete, nilimueleza upo wewe mjomba ndipo aliponieleza nije nikuambie kwa kunihakikishia kumtoa, hata nilipokuja hapa nilikuwa najiamini kutokana na kauli zake. Mmh! Tulijua huo ni uongo, tulikukubalia ili kukuridhisha lakini hakuna kitu kama hicho.
Kaka yako alikufa na tukamzika, hata wewe ulishuhudia. Sikuwa na jibu zaidi ya kukubali kosa huku nikiendelea kuificha siri nzito moyoni mwangu. Niliamini kama ningemueleza ukweli kuwa kaka yangu hakufa ila ameliwa nyama wakati wa kumtorosha bado asingeniamini. Baada ya likizo nilirudi kijijini kujiandaa na msimu mpya wa kuingia kidato cha pili.
Kama kawaida nilikutana na Helena ambaye alionesha ushirikiano wa karibu sana, muda wote nilipokuwa nyumbani tulikuwa pamoja. Huwezi kuamini kila nilipotoka shuleni nilimkuta njiani akinisubiri na kurudi naye mpaka kijijini.
Siku zilikatika huku nikiendelea kufanya vizuri katika masomo yangu kiasi cha kila mmoja kunibashiria kufanya vizuri katika mtihani wa mwisho kwa kupata division one.
Nilipofika kidato cha nne katika mwezi wa saba, miezi mitatu kabla kufanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne nilitokewa na jambo jingine la kutisha.
Naikumbuka siku hiyo, wakati natoka shule nikiwa katikati ya mashamba sehemu iliyokuwa haina nyumba, wingu zito lilitanda kuonesha muda wowote ingeshuka mvua kubwa.
Nilijikuta njia panda kwani kurudi shuleni ilikuwa mbali na kwenda nyumbani ilikuwa mbali. Lakini kwa vile nilikuwa nakwenda nyumbani, nilikaza mwendo kuwahi kabla mvua haijateremka. Sikufika mbali mvua iliyoambatana na upepo mkali ikaanza kunyesha.
Nilianza kukimbia lakini upepo mkali ulioambatana na mvua ulinifanya nisione mbele. Niliangalia mti wa karibu ambao niliamini kabisa utanisaidia kupunguza kasi ya upepo japo kwa mvua ningeendelea kunyeshewa .
Nilisogea chini ya mti wa mwembe mkubwa na kujibanza na upepo mkali lakini mvua iliendelea kuninyeshea. Mfuko wa madaftari wote ulilowa pamoja na madaftali yote yaliyokuwemo . Kwa muda mfupi giza zito lilitanda
kama usiku wa manane.
Nilijikuta nikijiuliza kile ni kitu gani? Sikuamini muda wa saa tisa alasiri niliotoka shule mpaka kufika eneo mvua iliponikutia si muda mrefu kisasi cha kuwa na giza zito kama lile.
Nikiwa bado nipo chini ya mtu nikimuomba Mungu aniokoe na janga lile, nilishtushwa na sauti za watu waliokuwa wakicheka mfululizo. Nilitetemeka na woga ulinitawala na kukumbuka mambo niliyoyasahau ya kusumbuliwa na wachawi .
Inaendelea....
Helena lolote utakalonieleza nitakuelewa. Nikikueleza kuwa nimeacha uchawi nitakudanganya ila kwa asilimia kubwa sitashiriki kwenye kazi za kichawi, muda wangu mwingi nitautumia kuhakikisha usalama wako japo kwa sasa najua huna tatizo lolote kutokana mzee Manoni kukusimamia.
Najua una kazi nzito ya kuibadili tabia uliyoizoea lakini kila kitu kina mwisho wake, uchukie uchawi mwisho Mungu atakutoa bila ya wewe kujielewa, nilimpa moyo. Shija nitajitahidi kufanya hivyo .
Tuliongozana na Helena kurudi kijijini, njiani tulizungumza mengi yakiwemo yale tuliyoyafanya wakati tukiwa marafiki. Tulipofika kijijini tuliagana na kila mmoja alienda kwao. Nilipofika nyumbani nilijikuta nikijawa na mawazo mengi juu ya maneno ya Helena ya kuniomba msamaha.
Japo nilikuwa na wasiwasi kwa maneno yake na kuyaona kama kweli yalipandikizwa ili kuniteka kimawazo na kunifanyia kitu kibaya. Lakini moyo wangu ulijaa ujasiri kwa kuamini kile nilichomueleza Sabina amsamehe Helena, kuwa adui wa jana anaweza kuwa rafiki mwema wa leo.
Nilijikuta nikimuamini Helena kwa kauli yake kwamba kutaka kuniua kulitokana na shinikizo la kutolewa yeye kafara. Nilijikuta nikimuonea huruma, siku zote pamoja na ubaya aliotaka kunifanyia lakini bado niliyakumbuka mema aliyonifanyia pale alipojitolea kwa hali na mali kumtorosha marehemu kaka yangu.
Badala ya kujionea huruma mimi nilijikuta nikimuonea huruma Helena kwa masaibu yote aliyopata mpaka kuponea tundu la sindano kuuawa na Sabina. Kumbe hata angemuua angekufa na siri nzito moyoni ambayo ilionesha mimi ndiye mhusika mkuu.
Niliamua kusahau yote yaliyopita na kuganga yajayo , nikamchukulia Sabina kama rafiki yangu mwema aliyetaka kujiokoa kwa kuutoa uhai wangu. Siku zote niliamini mwenye uwezo wa kuuchukua uhai wa mwanadamu ni Mungu pekee na si nguvu za giza wala mashetani.
Siku zilikatika, niliendelea na masomo yangu vyema huku nikionekana zile nguvu nilizokuwa nazo shule ya msingi nimezihamishia sekondari, Nilikuwa mmoja ya wanafunzi tegemezi kutokana na uwezo wangu niliouonesha darasani ambao ulinifanya niwe maarufu shuleni.
Wakati wa likizo kubwa mama alinieleza kwamba mjomba ananiita mjini. Nilikwenda kwa mjomba ambako nilijua muda wangu nitautumia kusoma. Jioni ya siku niliyofika , mjomba aliniita pembeni na kutaka kujua niliyomueleza kuhusu kumleta marehemu kaka akiwa hai yaliishia wapi? Anko mbona kimya, harakati zako za kumleta kaka yako ziliishia wapi?
Swali lilikuwa zito, nilijikuta nimebakia kimya nikiwa sijui niseme nini. Sikuwa na cha kumueleza kwa kuamini kila nitakachomueleza atazidi kuniona muongo. Shija si nakuuliza? Ulisema kaka yako hakufa yupo hai, si ndiyo?
Kuna mtu alinihakikishia lakini mwisho wa siku alisema alikuwa akinidanganya, nilitengeneza uongo ili kuficha siri nzito ya kifo cha kaka nilichokishuhudia kwa macho yangu.
Kwa hiyo hayupo hai? Ndiyo. Lakini si ulituhakikishia kuwa ulimuona akiwa hai? Niliwadanganya kwa vile kuna mtu alinihakikishia kamuoa akiwa hai na kuniahidi atamtoa nije kwako nimtafutie nafasi.
Yeye alinijuaje? Aliniuliza kama kuna mtu aliye mbali na kijiji ili akimtoa tumlete, nilimueleza upo wewe mjomba ndipo aliponieleza nije nikuambie kwa kunihakikishia kumtoa, hata nilipokuja hapa nilikuwa najiamini kutokana na kauli zake. Mmh! Tulijua huo ni uongo, tulikukubalia ili kukuridhisha lakini hakuna kitu kama hicho.
Kaka yako alikufa na tukamzika, hata wewe ulishuhudia. Sikuwa na jibu zaidi ya kukubali kosa huku nikiendelea kuificha siri nzito moyoni mwangu. Niliamini kama ningemueleza ukweli kuwa kaka yangu hakufa ila ameliwa nyama wakati wa kumtorosha bado asingeniamini. Baada ya likizo nilirudi kijijini kujiandaa na msimu mpya wa kuingia kidato cha pili.
Kama kawaida nilikutana na Helena ambaye alionesha ushirikiano wa karibu sana, muda wote nilipokuwa nyumbani tulikuwa pamoja. Huwezi kuamini kila nilipotoka shuleni nilimkuta njiani akinisubiri na kurudi naye mpaka kijijini.
Siku zilikatika huku nikiendelea kufanya vizuri katika masomo yangu kiasi cha kila mmoja kunibashiria kufanya vizuri katika mtihani wa mwisho kwa kupata division one.
Nilipofika kidato cha nne katika mwezi wa saba, miezi mitatu kabla kufanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne nilitokewa na jambo jingine la kutisha.
Naikumbuka siku hiyo, wakati natoka shule nikiwa katikati ya mashamba sehemu iliyokuwa haina nyumba, wingu zito lilitanda kuonesha muda wowote ingeshuka mvua kubwa.
Nilijikuta njia panda kwani kurudi shuleni ilikuwa mbali na kwenda nyumbani ilikuwa mbali. Lakini kwa vile nilikuwa nakwenda nyumbani, nilikaza mwendo kuwahi kabla mvua haijateremka. Sikufika mbali mvua iliyoambatana na upepo mkali ikaanza kunyesha.
Nilianza kukimbia lakini upepo mkali ulioambatana na mvua ulinifanya nisione mbele. Niliangalia mti wa karibu ambao niliamini kabisa utanisaidia kupunguza kasi ya upepo japo kwa mvua ningeendelea kunyeshewa .
Nilisogea chini ya mti wa mwembe mkubwa na kujibanza na upepo mkali lakini mvua iliendelea kuninyeshea. Mfuko wa madaftari wote ulilowa pamoja na madaftali yote yaliyokuwemo . Kwa muda mfupi giza zito lilitanda
kama usiku wa manane.
Nilijikuta nikijiuliza kile ni kitu gani? Sikuamini muda wa saa tisa alasiri niliotoka shule mpaka kufika eneo mvua iliponikutia si muda mrefu kisasi cha kuwa na giza zito kama lile.
Nikiwa bado nipo chini ya mtu nikimuomba Mungu aniokoe na janga lile, nilishtushwa na sauti za watu waliokuwa wakicheka mfululizo. Nilitetemeka na woga ulinitawala na kukumbuka mambo niliyoyasahau ya kusumbuliwa na wachawi .
Inaendelea....