Mlishakaa mkazungumza kuhusu tatizo lenu? Je mlishirikisha familia na viongozi wa dini ikashindikana?
Talaka inatolewa pale mke na mume watakapotengana zaidi ya miaka miwili pasipo suluhu kupatikana
Kumaliza mwaka mmoja ktk kutengana kwenu hakumaanishi kuwa talaka itakubaliwa manake mke ametengana na wewe au mume ametengana na mke ili hasira zitulie kwanza. Hiyo kisheria inakubalika.
Talaka siyo nzuri, hata mahakama hawakubali kirahisi, labda iwe na sababu zenye mashiko kama mume au mke kufungwa gerezani kwa muda mrefu, maradhi yasiyotibika( cancer) unyanyasaji wa kijinsia, ukichaa baina ya wanandoa.
Jaribu kuongea na mwenza wako tena kabla hamjafikia huko kupeana talaka.
Sent using
Jamii Forums mobile app