Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama “HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA” katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za “The Dar es salaam School of thought” kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!

Anaeweza kukuumbuwa ni yule aliyekuumba tu.

Wacha ushirikina kudhani kuwa binaadam mwenzio anaweza kukuumbuwa.
 
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.
 
Kuna wakati Rais Kikwete aliwahi kusema hii nchi ina viwanda vya kutengeneza uongo...

Vyovyote vile mimi naamini utawala wa Mjerumani ulikuwa na manufaa maradufu ya Mwingereza.
kwani mleta mada kasemaje?
 
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.

Kwa nini CCM wanashindwa kuendesha nchi Kama walivyoiendesha Wajerumani?
 
bado naona ww mawlm ndo una matatizo...... katika kufundishabkwako koooote hujaaahi kuona swali la "colonial rule was brea and butter to Africans discuss "........we unadhan hapo utabishana na swali.....


nenda kasome tena
 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama “HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA” katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za “The Dar es salaam School of thought” kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!
Kama JK amesema hivyo basi mwacheni Mugabe aitwe Mugabe. Hiyo ni aibu kwetu sote na ndo maana tunahitaji Raisi mwenye macho ya tofauti kuwafundisha watanzania kuwa wanaweza na wajiamini waondokane na mtazamo wa kutembeza bakuli dunia nzima
 
Ninawasiwasi na baadh ya wachangia thread kama kwel ni great thinkers kwa wanavyofagilia ukolon.
Da! Mleta mada mi nahis kuna wajeruman humu jf.
 
Huyu ndiye kikwete ninayemjua.
[h=2]MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA[/h]
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.

1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri

2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote

3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever

4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.

5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"

6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)

7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.

8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.

9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK

10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo

11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake

12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july
1-+muonnekano+wa+daraja+la+kigamboni.JPG


images

Sometimes huwa nawashangaa sana watu wanaosema shule za kata na chuo kikuu DODOMA kimejengwa na JK.

Ninavokumbuka hizi shule zilianza kujengwa 2004 wakati Benja M akiwa bado madarakani. UDOM pia kilianza kujengwa kipindi cha MKAPA.

Ifike mahali watu tuwe wakweli na sio kuleta propaganda mfu ambazo hazijengi???
 
Siamini kuwa alisema hivyo, hataaa haiingii akilini kwa Rais tena Prof. APONGEZE WATU WALIOTULETEA ADHABU YA KIFO
 
sisi tunawashukuru Wajerumani kutuletea Lutheran church,machame yote ni walutheri,ingekuwa siyo wakoloni inawezekana kilimanjaro yote ile ingekuwa kama Tanga vibaghashia kila kona,Thank you Jesus

So your the best human because of your belief? Mental slavery
 
Haa haa, kikwete haishi vituko! Si angewaomba waje tena kututawala angalau kwa miezi 8 kuanzia sasa?
 
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.
Waarabu walileta Utumwa na kujitoa muhanga tuu
 
Kama tumeshindwa kujenga IKULU yetu huko Chamwino Dodoma, hata baada ya miaka ya 54 ya uhuru, kwanini asiwapongeza Wajerumani walioweza kujenga hiyo Ikulu ya Magogoni zaidi ya miaka 100 iliyopita!

Pia angeendelea kuwasifu Wajerumani, kwani tangu walipotuletea meli ya MV Liemba, Sisi hata baada ya miaka 54 ya Uhuru tumeshindwa kuweka meli ya kiwango hicho ziwa Tanganyika.

Hatujashindwa kujenga ikulu yetu, ninadhani ni suala la maamuzi tu, majengo mangapi ya thamani ya hali ya juu yamejengwa including nyumba ya J.K Nyerere, makumbusho ya Nyerere kule Musoma, na Nyumba za marais wastaafu kama ya Mwinyi, Mkapa, na hata ile ya Kikwete pale Msoga zote zinajengwa kwa pesa ya watanzania. Nadhani pesa ya kujenga ikulu pale Dodoma ipo tatizo hawataki kuhamia kule sababu ya per diem huo ndio ukweli.
 
Siamini leo watu wanashukuru wajerumani jamani someni Historia najua maisha magumu yamewachanganya ndugu zangu watanganyika hamna cha kuwashukuru mali zetu ndio zimeijenga berlin!!! Wao ndio watushukuruu dah
 
Wewe kachukue buku saba ukapumzike,kwamba babu zako walibebeshwa mataruma ya reli begani na wengi kufa kwa mateso bado unasema walikuachia miundo mbinu?????hivi ikulu inatengewa bajeti ya shilingi ngapi kila mwaka toka 2005???? hizo pekee hazitoshi kujenga IKULU nyingine DODOMA,acheni akili mgando kama za CHINESE PROFESSOR
katika mataifa yote wajerumani pekee ndiyo ambao angalau walituachia majengo na miundo mbinu kadhaa.
 
Haya ndiyo matokeo ya kuendekeza njaa,kayasema haya Ili asinyimwe kibaba,hizi zote ni mbinu za kuombea kibaba maana serekali ya chama cha kina fulani inapenda sana kuomba na bila kuomba kibaba serekali haipo,imekuwa serekali ya kuendeshwa kwa kutegemea vibaba vya kuomba,siku mwenye vibaba akikataa kutoa vibaba watanzania ndiyo watakufa kwa njaa.

Ni kweli wakoloni walifanya mambo mengi mazuri tena kwa uadilifu mkubwa pengine hata kushinda watawala wetu wa sasa,kitu kinachoitwa ufisadi kwao hakikuwepo kwao,pamoja na mazuri waliyoyafanya,Je ni vitu vingapi walichukua kwetu?,Je hayo mazuri waliyo yafanya tena kwa kutumia kodi ya wananchi wa ujerumani waliyafanya kwa hasara pasipo kupata faida yoyote?

Hapa ndipo ninapo mkumbuka mzee wa uzanaki angewasema kwanza tena kwa maneno makali yaliyojaa maudhi lakini mwisho angemalizia kwa kuwaomba msaada na kuwaambia kuwa hivi vitu mnavyotusaidia ni mali zetu mlizotupora kwa hiyo mnaturudishia mali zetu.
 
Faiza nadhani mababu zetu waliotangilia mbele ya haki wangeisikia kauli hii wangekuchuna ngozi,sema wewe na serikali yako ndo hamuwezi lolote hivyo basi wapisheni wanaoweza kazi hapo magogoni msaidiwe maana imeshawashinda!!!!Kwamba unasifia ukoloni kwamba wametujengea barabara na kutupangia mji wa Tanga hii mishahara mnaowalipa TOWN PLANNERS ni za nini???? haya mabilioni mnayoyatafuna hapo BOT yangetosha kujenga barabara ngapi zetu kama watanzania???Unyama uliofanya na kila TOM VON PRINCE na wengineo unausifia,historia tunaijua nashauri mkawadanganye huko vijijini wasiojua historia ya unyama wa wajerumani
Tena licha ya Ikulu, Mjerumani kafanya kweli, reli ya kati mpaka leo.

Barabara karibu zote unazotumia leo ni zile zile za Mjerumani, sanasana tumezipanuwa na kuweka lami.

Nenda Tanga, moja katika miji ambayo imepangika vizuri na hiyo ni toka Mjerumani, si leo.

Ukweli ubaki kuwa ukweli. Natamani tungebaki kutawaliwa na Wajerumani hadi leo hii. Hatuwezi lolote.
 
Back
Top Bottom