Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama "HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA" katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za "The Dar es salaam School of thought" kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!

Huyu ndiye kikwete ninayemjua.
[h=2]MAZURI ya Kikwete ambayo hayajawahi kufanywa na marais waliomtangulia HAYA HAPA[/h]
Katika kipindi cha Kikwete masuala yafuatayo lazima tumpe Credit kwani baadhi yamefanywa na JK wa mwanzo tu na hayakufanywa na Mwinyi wala Mkapa.

1. Ujenzi wa Sekondari za Kata ni maamuzi sahihi ingawa yana changamoto zake zinazoweza kutatuliwa na watakaomfuatia, lakini hapa JK ametumia madaraka yake vizuri

2. Ameendelea na uendelezaji wa Miradi ya Barabara, suala lililoanza kujitokea wakati wa awamu ya 3, JK ameendelea nalo suala hilo kwa kasi kubwa na kwa kipindi chote

3. Daraja Kigamboni, Malagarasi na Kilombero ni miongoni mwa mambo yatakayokumbukwa forever

4. Ongezeko la Taasisi za Elimu ya Juu limefanyika vizuri sana katika awamu ya Kikwete, mbali na UDOM lakini taasisi na vyuo vingi vimeimarishwa, kupandishwa hadhi na vyuo vingi binafsi vimeanziswa. Kwa sasa Taifa haliko tena na dhana ya UDII, Mzumbe na SUA. Aidha ari na moyo wa watanzania kulipia huduma za elimu umeongezeka.

5. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ajira ukilinganisha na awamu mbili zilizomtangulia. Mkapa aliendesha Serikali nyembamba, suala ambalo ni zuri lakini lina changamoto zake kwa wale waliokuwepo wameliona hata akapewa sifa ya mzee wa "ukapa"

6. Mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa lengo la kutatua kero ya Umeme ni hatua nzuri ambayo haijawahi kufanywa katika awamu ya 2 na ya Tatu (Vyanzo vya Nishati)

7. Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Chuma (Kule Liganga?) ambao maandalizi ya ujenzi wake yamekamilika ni hatua nzuri ili kuvutia au kuanzisha uwekezaji wa zana za Chuma pamoja na Viwanda vikubwa.

8. Hatua ya Kujenga Bandari mpya eneo la Bagamoyo yenye hadhi ya 4th Generation ni tukio litakalokumbukwa na vizazi Dahri vijavyo.

9. Hatua ya Utekelezaji wa mradi wa DRT ambao ulikuwepo miaka mingi pia ni miongoni mwa mazuri yaliyotendeka katika awamu ya JK

10. Zoezi la kutambua na kuwarudisha kwao wahamiaji haramu pia ni zoezi zuri ambalo bila shaka halijawahi kufanywa katika uongozi wa awamu nyinginezo kwa kiwango na utashi wa namna hiyo

11. Kitendo cha utekelezaji wa mradi wa vitambulisho vya Taifa ni credit kubwa kwa JK ambao hakuna sababu za wazi kwanini nchi imekaa miaka 50 pasipo na vitambulisho vya uraia kwa wakazi wake na raia wake

12. Ameendelea kuiweka Tanzania kwenye mahusiano mazuri kimataifa hususan SADC, UN na nyanja nyingine za Kitaifa. Ukiacha EAC ambayo sababu za kuzorota kwake ziko wazi, lakini maeneo mengine ame-play well.
picha; maendeleo ya ujenzi wa daraja la kigamboni eneo la kurasini jijini dsm. ujenzi ulikuwa asilimia 47 mwezi july
1-+muonnekano+wa+daraja+la+kigamboni.JPG


images
 
...tabia ya wakwere si watu wapwani,hakuna kitu.....sisi huku Rorya tuliwatimua hao jermani vibaya...babu alikuwa anatusimlia.
 
katika mataifa yote wajerumani pekee ndiyo ambao angalau walituachia majengo na miundo mbinu kadhaa.

mwenyekiti wenu wa CCM amelitia aibu.
yeye ni mfano wa nyoe akili zenu zilizoganda.
 
Sitashangaa sana kama aliyonukuliwa ni ya kweli na aliyasema Ndugu Jakaya Kikwete katika ujio huu wa Rais wa Ujerumani. Historia ya performance yake kwenye press conference hapo Ikulu ina blunders kama hizi kadhaa.
 
huu ni upotoshaji mkubwa,,,,,,,,wengi tulisikiliza hotuba ya rais hakuyasema haya[/QUOT

Ama hukumulewa au umeamua kupotosha. Alisema Ujerumani na Tanzania (Tanganyika) zina historia ya UHUSIANO wa muda mrefu na jengo la ikulu linasimama kama kielelezo cha UHUSIANO huo. Nini tafsiri ya maneno hayo? Kwa mfano jengo hilo limejengwa lini? Lilijengwa wakati nchi hizi zina uhusiano wa aina gani? Je, uhusiano huu MZURI unajumuisha uhusiano wa wakati jengo la ikulu linajengwa (ukoloni)?
 
Sipati picha endapo hao wanafunzi wako wakitungiwa swali la Mock kuhusu ubaya wa wakoloni and at the same time wamemsikiliza mkuu wa kaya majibu yao yatakavyokua, kuna wengine watajibu sawa sawa na ulivyo fundisha while wengine watajibu sawa sawa na walivyo msikia mkuu, sasa sijui nani utamuwekea tick na nani utampa KOSA au X! Profesa ana mambo jamani, ukichukulia na mi nafanya kazi na makaburu halafu mkulu alikua anahutubia kwa kingereza so wamemsikia wenyewe, yaani mbona hata mi nina kazi kubwa huku!? Niliisha waambiaga nyie jamaa sio, mmewaua sana weusi wenzetu kule South Africa, naahidi kuanzia leo sitakunywa nao tena chai cause wataniuliza juu ya hili, siwezi kujitetea tena!
 
Mwenyekiti wa ccm na rais wa Tanzania.Kauli gani hii duh aibu ya mwaka
 
sisi tunawashukuru Wajerumani kutuletea Lutheran church,machame yote ni walutheri,ingekuwa siyo wakoloni inawezekana kilimanjaro yote ile ingekuwa kama Tanga vibaghashia kila kona,Thank you Jesus
FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Mleta mada pole. Kwanza ilikupasa kumpa somo huyo aliyewasifu hao wakoloni kwamba wanatakiwa watulipe. Hawa jamaa walinyonga wazee wetu wengi sana. Bila shaka alidhani akiwasifu itakuwa rahisi kupata msaada. Nadhani hawajui vizuri hawa jamaa. Hata na wao hakuna wasichokijua kuhusu rais wetu.
 
Nadhani kichwa chako ungeficha bafuni kwako maana hakina hata faida hata kidogo.
 
Ni wakati mwafaka kwa rais kikwete kutumia fursa hii kumwambia rais wa ujeruman kuwa wana Lindi na watanzania kwa ujumla wanahitaji kurejeshewa mjusi wao (dinosour) aliyeko berlin waliyemchukua miaka ya 1910's
 
Usisononeke, hiyo ni akili ya mbayu wayu, wanafunzi watakuelewa tu maana wanamfahamu Prof wa Kichina. hiyo ndo faida ya kuwa na prof wa kichina


Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama "HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA" katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za "The Dar es salaam School of thought" kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!
 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama "HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA" katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za "The Dar es salaam School of thought" kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!

Rais amesema ukweli!!!!!!!!!!!!! Wakoloni walituletea mambo mengi sana mazuri mfano, mashamba ya mikonge; Reli, Miundombinu ya maji, barabara nk. Pia walitutaka tufanye kazi kwa kutulazimisha........Yaani ni lazima ulime hekari tatu heka moja ya zao la biashara ya kwako, heka moja ya zao la biashara ya mkoloni na heka moja ya chakula ya kwako. Ni lazima kama minimu requirement.


Ukikutwa uko nyumbani kipindi cha kilimo ni lazima uwe na sababu za kutosha kwanini hukwenda shamba. Uwe na sababu kwa mfano u mgonjwa na cheti cha daktari uwe nacho. Huna unakula viboko!!!! Yaani walitulazimisha tufanye kazi kwa manufaa yetu na yao wao wenyewe.

Nini chanzo cha kudai mkoloni anatunyonya?
Ni Uvivu wetu......................!
Baada ya kuona tunalazimishwa utamaduni wa kuwa bize wakati wote na kwa kuwa sisi tumezoea kupiga domo muda mwingi na kukaa vibarazani kutwa nzima tukaona mkoloni kwa kutufanya tuwe bize anatunyanyasa.......Ule usiriaz wa mtawala anaostahili kuwa tukaona kero. (Siku hizi mtawala mzuri ni yule anayekwambia we kaa tu nitakuletea kila kitu; kuanzia mvua, mashamba, mazao, mashine ya kuvunia, ajira, vyandarua nk.)


Wanadai ujira aliokuwa anautoa mkoloni ulikuwa mdogo (ilikuwa minimum wage) lakini leo hii the so called minimum wage sijui hata kama inatosha. Ni heri kuwa fundi baiskeli utaziba pacha na kupata pesa nyingi kuliko mshara huo wa kima cha chini. Ndo wakaona anatunyonya! Wakaanzisha harakati za ukombozi.........
Lakini baada ya kupata uhuru hakuna hata barabara moja tuliyoianzisha zaidi ya zileziel alizozi "design" mkoloni. Reli hatuna mpya zaidi ya ile ya mkoloni (TAZARA labda) na hata hizo reli zimebakia historia tu.
Watu hawapendi kufanya kazi za mikono ama mitulinga. Wanataka kufanya kazi za kudanganya wenzao kisha wapate pesa. Ajira siku hizi inatafsriwa ni kuajiriwa ofisini na ukifika huko ni kupiga dili tu na wala si kufanya kazi.
Watawala wetu wanashindwa kutusimamia tupendekufanya kazi kwa sababu kuu mbili, kwanza wakisema hivyo watakuwa kama alivyofanya mkoloni hivyo kuogopa kuitwa na wao wakoloni, pili wanaogopa wakati wa uchaguzi watakosa kura maana watanzania tunapenda mtu anyesema nitajenga reli ama nitanunua ndege wakati hizo zilizopo hata ukarabati tu umeshindikana.


Maisha aliyokuwa akiishi mkoloni akiwa nchini kwetu akitutawala ndo yaleyale anayoishi hata kwake na maendeleo yake yamepaa.
Watakuja wanahistoria na wanasiasa waliopotoshwa na historia watasema mkoloni alikuwa mbaya maana alipora rasilmali zetu. Waulizeni ni rasilimali gani alizopora maana mkonge alipanda yeye na malighafi zingine. Muwaambie sasa hivi ndo tunaporwa rasilmali zetu maana hatuna hata mtambo mmoja uinaochimba madini kwa niaba ya serikali. Mitambo yote ni ya wageni na rasilmali zote zinazopatikana ni za kwao....Sisis twwambulia the so called ROYALTY ambayo haizidi asilimia tano. Uporaji mkubwa kushinda enzi za mkoloni……….


Watakuja wataalamu wa gesi na mafuta watasema serikali inachimba gesi kupitia shirika la petroli Tanzania (TPDC) waambieni PSA (Production Sharing Agreements) zina kasoro. Gharama za uchimbaji gesi na mapato wanagawana kama ifuiatavyo TPDC 20% na Mwekezaji 80% lakini mwisho wa siku kodi anayechanga asilimia 20 ndo analipa kodi. Pia gharama za uchimbaji zinapelekwa mbele (costs are capitalized and losses are carrief foraard indefinetelly) Maana yake ni kwamba makampuni yakianza uzalishaji gharama zilizotumika kutafiti mpaka kuzalisha gesi ama mafuta zitatolewa kwenye mapato baada ya kuanza kuuza gesi. Mrundikano wa gharama hizo mpaka uishe ndo kampuni ya gesi ianze kulipa kodi. Sisi wataalamu wa fedha uchumi na uhasibu tumepiga hesabu itachukua miaka hamsini kwa kampuni ya gesi kuanza kulipa kodi. Hayo maendeleo ya gesi yatawanufaisha wawekezaji sisi tutanufaika labda na gharama za nishati kushuka na bei za bidhaa kushuka viwandani maana vitatumia gesi. Napo pia tujiandae maana gesi inaweza kufanyiwa biashara na wakubwa mpaka tutachanganyikiwa!!!!! Kila mkubwa ataingiza vikampuni vyake kwa kisingizio cha kutoa huduma ama mkataba wa "kuhesabu gesi inayozalishwa........! .kisha akadai mamimilioni ya dola hatimaye yakasababisha bei za vitu kutoshuka maana inakuwa ni gharama kwa mwekezaji kuwalipa wakubwa gawio la mikataba ya "kuhesabu gesi iliyozalishwa......."


Angekuwapo mkoloni sasa hivi tungekuwa na barabara za ghorofa......
Faida za uhuru ni nyingi kubwa ni pale wananchi wanaweza kufanya jambo lolote bila kuchukuliwa hatua yoyote. Hayo ndo matunda ya uhuru.
Uhuru ulitokana na mawazo ya ku-"exercise practically the knowledge acquire in the class". kifupi uhuru ni theoretical ideas. Huwezi ukapata maendelo kwa kuchagua serikali kila baada ya miaka mitano na atakayekuja anakuja na mawazo yake binafsi na si sera ya taifa. Umaskini wa wananchi uwe ndo kigezo cha kuchagua Rais bora eti kwa matarajio ya kuja kuondosha umaskini wetu.......? hapana hiyo siyo sera na maendeleo kwa mtindo huo ni ndoto. Nawaambia hivi, kama kuna kijana kajiunga na mitandao ya kijamii akiwa na miaka ishirini nina hakika atafikisha umri wa kustaafu utumishi wa umma akiwa mchangiaji mzuri kwenye mitandao bila kuyaona haya maendeleo tunayoyataraji. Ni theoretical tu!!!!
Watanzania hawapendi viboko…wakadai uhuru bila ya kujua madhara yake…ambayo ni kuteswa na vyombo vya dola magerezani ama kulala na njaa kwa kutegemea mtu aliyeko madarakani akuletee chakula ama akupe kazi utakayoifanya ukipiga blabla tu kisha mshahara "burungutu…."
 
Did he said that!!! Maana huwa sisikilizagi hotuba zake. Alisema kwa ki- english au kwa kiswahili au kijerumani? Nahisi kuna shida hapa. Kwamba anawapongeza wakoloni kwa kututawala na kutuletea maendeleo! Kwa hiyo ndo maana kila siku yuko angani anatutafutia hawa wakoloni warudi kututawala ili watuletee maendeleo zaidi? Kwamba akina Nyerere na wenzake walifanya mapema sana harakati za kutafuta uhuru ili tuweze kujitegemea wenyewe? Kwamba Wa-Tz hatuwezi bila kuwezeshwa na wakoloni?




The sentence "Did he said that!", is grammatically wrong.
 
Back
Top Bottom