Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Nitaficha wapi uso wangu? Rais Kikwete ameniumbua

Nikapata ushahidi wa haya kama ameyasema kweli Le Professeri JK, ndipo nitakapopata ari ya kuchangia hapa.
 
Wakati fulani tuseme na ukweli, wajerumani walitukuta hatuna hata nguo, tunauzwa sokoni kama mbuzi, je hilo jengo la ikulu kajenga nani kama sio wajerumani, reli ya kati kajenga nani kama sio wajerumani.ukweli mazuri ya wajerumani kwa miaka 35 waliyokaa hayawezi kulinganishwa na ya kwetu.
Ni kweli walifanya mema lakini yote ilikuwa kwa ajili ya kutunyonya. Motive haikuwa nzuri na hilo linanifanya niwaone kuwa ni wakoloni tu; na hawastahili shukurani yoyote. Hata mimi nimeumbuka sana kwa kauli za mkuu wa kaya. Nimeendelea kuthibitisha kuwa tuliingia choo kisicho. Tuwe makini zaidi ktk uchaguzi mkuu ujao.
 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama “HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA” katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za “The Dar es salaam School of thought” kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!
Mwafrika mweusi bado ana matatizo, hajitambui, huo ndiyo ukweli.Kwa vile Prof JK ametokana na sisi basi hiyo ni aibu yetu sote kama watanzania weusi na waafrika wengine weusi!
 
bila ukoloni tungekuwa ma bush man kama wa hazabe vile au masai hatuna dira,kila kitu kinatokea kwa sababu,elimu ya zamani ilikuwa jando tu na unyago sasa hivi mnapata elimu dunia.

Kikwete yuko sawa ila hakutakiwa kulopoka hivyo maana aibu
 
Wakati fulani tuseme na ukweli, wajerumani walitukuta hatuna hata nguo, tunauzwa sokoni kama mbuzi, je hilo jengo la ikulu kajenga nani kama sio wajerumani, reli ya kati kajenga nani kama sio wajerumani.ukweli mazuri ya wajerumani kwa miaka 35 waliyokaa hayawezi kulinganishwa na ya kwetu.

watu gani hao mlikutwa hamna nguo au historia uliyoisoma haiongelei ushonaji wa nguo za pamba, magome, ngozi n.k. kabla ya karne ya 19?
 
bila ukoloni tungekuwa ma bush man kama wa hazabe vile au masai hatuna dira,kila kitu kinatokea kwa sababu,elimu ya zamani ilikuwa jando tu na unyago sasa hivi mnapata elimu dunia.

Kikwete yuko sawa ila hakutakiwa kulopoka hivyo maana aibu

Tanzania ina zaidi ya 'makabila' 120 na kila moja ilikuwa na dira na maendeleo ya kiwango fulani, hatuwezi kuweka kila kitu kwenye kundi moja
 
nchi hii imekwisha kata tamaa hakuna matumaini yoyote. asipo sema hivyo hawezi pata misaada kwssababu fikra zake zote zimeengemea kwenye misaada.
 
Hapo itakuwa aliahidiwa suti ya dhahabu
 
Wakati fulani tuseme na ukweli, wajerumani walitukuta hatuna hata nguo, tunauzwa sokoni kama mbuzi, je hilo jengo la ikulu kajenga nani kama sio wajerumani, reli ya kati kajenga nani kama sio wajerumani.ukweli mazuri ya wajerumani kwa miaka 35 waliyokaa hayawezi kulinganishwa na ya kwetu.
Heri utawala wa kikoloni kuliko huu wa CCM!
 
Wakati fulani tuseme na ukweli, wajerumani walitukuta hatuna hata nguo, tunauzwa sokoni kama mbuzi, je hilo jengo la ikulu kajenga nani kama sio wajerumani, reli ya kati kajenga nani kama sio wajerumani.ukweli mazuri ya wajerumani kwa miaka 35 waliyokaa hayawezi kulinganishwa na ya kwetu.

Kwani yeye kakataa. Yeye kasema kaumburiwa
 
Mwafrika mweusi bado ana matatizo, hajitambui, huo ndiyo ukweli.Kwa vile Prof JK ametokana na sisi basi hiyo ni aibu yetu sote kama watanzania weusi na waafrika wengine weusi!
I always ask myself kwanini kivuli Ni cheusi?!
 
Historia inajirudia;
1884 Carl Peters vs Chief Mangungu

2015 Germany President vs Tanzania President

Wakati ule Mangungu alipewa shanga akagawa nchi sijui mwaka huu tumepewa nini yarabi! Na hizo sifa zinazoanza kutolewa hivyo lazima kuna kitu. Tusije sikia Serengeti anayotembelea kesho inakuja kuitwa SERENGETI BUNDES PARK
 
Mr.Kikwete amelitia taifa aibu ya mwaka.
jamani huu ukilaza wa ccm kumbe unaanzia kwenye level ya mwenyekiti wao?
Nadhani unajua nini maana ya Profesa. Ni mtu ambaye baada ya kuwa mzamivu sasa amebobea na kuwa bingwa wa taaluma fulani. Huyu amefanya tafiti nyingi na kuzichapisha katika majarida mengi ya kitaaluma ya vyuo vikuu kadhaa. JK ni Profesa. Huo ni utafiti wake. Tuuheshimuni jamani!! Wajerumani walituletea maendeleo na labda wasingeshindwa vita na Waingereza, sasa nchi hii ingekuwa kama Ujerumani. Na CCM haijafanya mengi kwa muda wote waliotutawala kama wajerumani ambao walitutawala kwa muda mfupi na kufanya yote hayo. Hongera Prof. JK!!
 
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Profesa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete ameishukuru serikali ya Ujerumani kwa kututawala na kutuletea maendeleo wakati wa ukoloni.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari Ikulu jana, Rais Kikwete alimuambia Rais wa Ujerumani kwamba wakati wanatutawala walitufanyia mambo mengi sana mazuri ikiwemo kutujengea jengo la ikulu ambalo tunalitumia hadi sasa.

Rais ameniumbua. Sijui nitaficha wapi uso wangu.

Tangu mwaka 2008 nimekuwa nikiwafundisha wanafunzi wangu Historia nikiwaaminisha kwamba wakoloni hawakuwa na nia njema. Nimekua nikiwaambia wanafunzi wangu kuwa wakoloni walikuwa wakitunyonya, kutukandamiza na kutudhalilisha sana.

Niliwaambia hata elimu waliyoitoa na miundombinu waliyojenga ilikuwa ya kuendeleza unyonyaji.

Niliwaambia wanafunzi wangu kuwa watu waliowapinga ukoloni na kuwapiga vita kama kina Mkwawa, Mangi Meli, Mtemi Isike na Chifu Kimweri ndio mashujaa wetu. Niliwasema vibaya sana wakoloni huku nikitumia vitabu vya kina Walter Rodney kama "HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA" katika kujenga hoja. Pia nilitumia sehemu ya nukuu za "The Dar es salaam School of thought" kuaminisha wanafunzi wangu kwamba wakoloni walikuwa watu makatili na wasiotufaa.

Leo rais kaniumbua. Kawaambia Watanzania kuwa Wakoloni walikuwa watu wema sana na waliotuletea maendeleo. Rais akafika mbali zaidi na kukiri bila Ujerumani kututawala tusingekuwa na Ikulu ya Dar es Salaam.

Sasa najiuliza kama wanafunzi wangu wamemsikiliza Rais Kikwete nitakoma maana nitaumbuka. Na kama wamemsikiliza Lazima watamuamini kwa sababu Rais wetu ni Profesa.!!

Kwa heshima ya Malisa Godlisten naomba kushirikisha hii simanzi!

Kuna wakati Rais Kikwete aliwahi kusema hii nchi ina viwanda vya kutengeneza uongo...

Vyovyote vile mimi naamini utawala wa Mjerumani ulikuwa na manufaa maradufu ya Mwingereza.
 
Wakati fulani tuseme na ukweli, wajerumani walitukuta hatuna hata nguo, tunauzwa sokoni kama mbuzi, je hilo jengo la ikulu kajenga nani kama sio wajerumani, reli ya kati kajenga nani kama sio wajerumani.ukweli mazuri ya wajerumani kwa miaka 35 waliyokaa hayawezi kulinganishwa na ya kwetu.

Jirani akiwa azini na mkeo/mumeo na anampa fedha hilo ni jambo la kushangilia?
 
Back
Top Bottom