Nisome vitabu gani vya coding? Nahitaji kujifunza kuhusu coding.

Nisome vitabu gani vya coding? Nahitaji kujifunza kuhusu coding.

Sokoro waito

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2014
Posts
2,201
Reaction score
2,602
Heko kwenu wadau wa CODING.

Nimekuwa nikitafakari mambo yajayo kuhusu maisha nikabaini kuwa lazima niwe na utaalamu au ujuzi kuhusu coding(programming).

Kwa kuwa sijawahi kuisoma elimu hii, ninaomba kwa moyo mweupe wale wadau na wajuzi wa mambo haya, waniwekee hapa vitabu vya kusoma kuhusu coding, tafadhali wekeni vitabu vya kuanzia yaani vitabu vyenye basics of coding na mengineyo.

Hakuna jinsi naweza kukwepa kusoma coding.

Karibuni wadau.
 
hapo nakushauri usome language ambazo ni nyepesi iliupate uzoefu kwa mfano JavaScript unaweza anzia apo
asante sana mkuu, kama una kitabu chochote kuhusu javascript niwekee hapa
 
Programming nakushauri anza kwa kusoma programming language achana kwanza scripting kama javascript.

Lugha nzuri ya kuanza ni C/C++, vitabu ambavyo ningekurecommend kuanza navyo ni vile Paul Daitel & Harvey Daite
amcho kinaitwa C How to Program. With an Introduction to C++
cc++.PNG

Ukikielewa hiko kitabu na ukafanya maswali ambayo yapo humo languages zingine kama javascript, java, php unateleza.

programming inahitaji uwe na commitment kuimaster.
 
Programming nakushauri anza kwa kusoma programming language achana kwanza scripting kama javascript.

Lugha nzuri ya kuanza ni C/C++, vitabu ambavyo ningekurecommend kuanza navyo ni vile Paul Daitel & Harvey Daite
amcho kinaitwa C How to Program. With an Introduction to C++
View attachment 884821
Ukikielewa hiko kitabu na ukafanya maswali ambayo yapo humo languages zingine kama javascript, java, php unateleza.

programming inahitaji uwe na commitment kuimaster.
Kitabu kizuri sana lakini cha muhimu ni hio part ya commitment,Mimi binafsi nimesom programming miaka 6 sasa na kiukweli nitakwambia zaidi ya kwamba naelewe basic concepts lakini siwezi kusema nitafika wakati nikae chini niandike program from scratch sana sna ujuzi wangu unanisaidi tu kuweza kucheza na existing programs na kuzisimamia.Na yote hiyo ni kutokana na ukweli kwamba programming lazima iwe hobby.Ila nimependa kwamba ameonesha nia,vingine taratibu.Jambo la muhimu pia ni atafuta programmer wazoefu awe anashare nao ideas ili apate challenge itamjenga
 
CODING ni about what you want to do kwanzia python to data structures na pia java so unachagua language unayotaka Kutumia so na suggest tumia website hizi.

Codecademy
Or
Helper22

Visit my new Tech forum on
Techz
 
Computer programming language ni:

1-C Language
2-C++
3-Objective C
4-Java
5-Javascript
6-Rubi
7-Python

Nakushauri anza na namba moja, uanze basics zake zote kisha uimalize yenyewe. Ukiweza kuimudu hizo nyingine utajifunza kirahisi
 
Computer programming language ni:

1-C Language
2-C++
3-Objective C
4-Java
5-Javascript
6-Rubi
7-Python

Nakushauri anza na namba moja, uanze basics zake zote kisha uimalize yenyewe. Ukiweza kuimudu hizo nyingine utajifunza kirahisi
Hata mimi hii fani huwa natamani sana kuijua ila kwa sasa nimeshajaa uvivu sana wa kusoma kwa maana ya shule sijui kwa nini
 
kaka nipo na cheza na java language huu mwaka wa pili lakin bado mambo sio fire kivile
 
Back
Top Bottom