Mimi kwangu hela sio ishu kihivyo nimeridhika, naishi Upanga kwenye nyumba ya msajili ambayo ni kwangu, kila mahali ninaweza kwenda kwa miguu kama nikitaka hata kwenye harusi zenu za ma-low IQs diamond huwa natembea tu, kariakoo natembea nikitaka, baharini kupunga upepo kwa miguu tu, huduma zote za kibenki na kiserikali nakwenda kwa miguu tuu sijui foleni, na hapo hapo kama mchango wangu najitolea kuwafundisha watoto washule za sekondari wanaotoka familia masikini, Hisabati na Fizikia bila kipato chochote na furaha yangu ni pale matokeo yanapotoka nakuona wamefaulu sana hasa ukichukulia wengine walikuja kwangu wakiwa wana ufahamu mdogo sana wa Fizikia na Hisabati, hivyo nina maisha mazuri sana tu!
Isitoshe ningetaka utajiri nimeshafwatwa na watu wanataka wanipe mpaka milioni 600 niwaachie nyumba ya Msajili Upanga nimekataa, hivyo pesa sio kila kitu!