Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,833
Ugomvi wa baba na mama umekuwa ukiongezeka siku hadi siku. Nipo kijijini kwa mapumziko ya likizo ya siku 28. Hali hii imekuwa ikinikera sana hivyo nikaona kwasababu mimi ni mtu mzima nikae chini na Mzee Wangu tuyaongee, kwani shida ni nini?
Basi, kwa kuwa Mzee Wangu ni mtu wa kupenda maji machungu, nikaenda mnadani, nikanunua mbuzi dume, beberu kubwa, nikalipeleka nyumbani, nikawahuma vijana wamchinje tumchome.
Nikatoka kidogo nikaenda mjini nikanunua vinywaji mbalimbali, pombe za aina kwa aina, soda na maji na vyakula.
Nikarudi kijiiini na mzigo wangu wa mapochopocho. Basi baada ya mlo mida ya saa moja moja nimekaa chobingo na baba, mtu mbili tu, pambano la kiutu uzima, tunapiga story huku tukijitafuna na kusonsomola huku yeye akigida maji yake machungu.
Ndipo nikamuuliza, baba inakuwaje mara kwa mara unagombana na mpenzi wako, mchumba wako, mke wako ambaye pia ni mama watoto wako? Kwanini hali hiyo imekuwepo?
Mzee akanijibu, asante sana mwanangu kwa swali lako zuri, naona kwa kweli umekuwa mtu mzima hadi kiwango cha kujua mambo yangu ya ndani, mimi na mke wangu. Basi nakutuma kamuulize mama yako, kwanini ananinyima unyumba?
Nikajikuta nimeishiwa nguvu, nikaanguka miguuni, nikaanza kulia huku nikiomba msamaha, baba nisamehe, baba unisamehe, nimekosa mimi. Nikalia sana hadi alipo niinua kutoka ardhini.
Dah, nikajifunza somo kubwa sana.
Basi, kwa kuwa Mzee Wangu ni mtu wa kupenda maji machungu, nikaenda mnadani, nikanunua mbuzi dume, beberu kubwa, nikalipeleka nyumbani, nikawahuma vijana wamchinje tumchome.
Nikatoka kidogo nikaenda mjini nikanunua vinywaji mbalimbali, pombe za aina kwa aina, soda na maji na vyakula.
Nikarudi kijiiini na mzigo wangu wa mapochopocho. Basi baada ya mlo mida ya saa moja moja nimekaa chobingo na baba, mtu mbili tu, pambano la kiutu uzima, tunapiga story huku tukijitafuna na kusonsomola huku yeye akigida maji yake machungu.
Ndipo nikamuuliza, baba inakuwaje mara kwa mara unagombana na mpenzi wako, mchumba wako, mke wako ambaye pia ni mama watoto wako? Kwanini hali hiyo imekuwepo?
Mzee akanijibu, asante sana mwanangu kwa swali lako zuri, naona kwa kweli umekuwa mtu mzima hadi kiwango cha kujua mambo yangu ya ndani, mimi na mke wangu. Basi nakutuma kamuulize mama yako, kwanini ananinyima unyumba?
Nikajikuta nimeishiwa nguvu, nikaanguka miguuni, nikaanza kulia huku nikiomba msamaha, baba nisamehe, baba unisamehe, nimekosa mimi. Nikalia sana hadi alipo niinua kutoka ardhini.
Dah, nikajifunza somo kubwa sana.