Nipo njia panda wandugu

Habarini wana jf,
Naomba niende moja kwa moja kwenye point....

Usiku wa kuamka leo nimekosa amani totally na nimewaza sana lakini nakosa majibu nikaona ni bora niombe msaada kwenu.

Ni kwamba mimi ninaishi na binti mmoja ambaye mwanzoni tulikuwa na mahusiano mazuri tu lakini sasa hivi nipo dilemma kutokana na mwenendo wake jana nilimtia kibao kibao kimoja baada ya kunifyonza kiukweli hasira zilinipanda sana nikamnasa na siyo mara moja wala mara mbili kunifyonza na maneno mengine ya kejeli hasa anapokuwa na hasira.

Sasa baada ya tukio hilo alilia sana na kudai anataka aondoke kwamba hajawahi kupigwa na mwanaume yeyote ambaye atampiga hata kama ana makosa basi ni lazima amwache nilimbembeleza sana pasipo mafanikio baadae sana akakubali ingawa bado ana fundo moyoni.Shida ina kuja kwamba katika kupekua pekua simu yake nimeona namba fulani nadhani ndio inayompa kiburi ingawa sina uhakika maana huwa anafuta ushahidi na anapopigiwa hapokei ninapomuuliza kwa nini hapokei anadai hajisikii kupokea lakini nilipotazama zile call logs inaonyesha huwa anapokea mara kwa mara hiyo namba.

Shida nyingine dini zetu ni tofauti ingawa kweli nampenda kwa dhati kabisa nina mpango nae sasa mara kwa mara ninakuwa nina mashaka naye hasa anapokuwa anachart nimebaki najiuliza nifanye nini lakini nakosa cha kuamaua ...

Wazo jingine linaniambia nitemane naye na jingine linaniambia niwe na subira ...naombeni ushauri wenu hasa jinsi ya kuachana naye kwa amani zaidi pasipo mimi kuhisi maumivu kwani bado nampenda sna ila kuzungukwa ndiko kunakonifukuza
Shule zinafunguliwa lini wakuuu ...... acha utoto bhana kama amekushinda mwache aendeee lakin binti mpaka akusonye na blablaaa nyingine umesababisha mwenyewe jitasmini mkuu
 
Dah! watu mnajua kupenda kinoma,

Ningekuwa mm kitaambo nshammwaga, muhim kuliko yoote ni kujitathmini ww kwanza. Je wewe ndo umemuotea au yeye ndo amekuotea.
 
kumzalisha bado maana huwa nakimbia siku zake za hatari jambo ambalo litamcost yeye na mimi pia maana familia yake ina uwezo na wana hadhi fulani kidini hapa town
Ahaa kumbe tatizo huo uwezo na hadhi ya familia yake. Baadhi ya watoto toka ktk aina ya hizo familia hulelewa vibaya. She is probably a spoiled brat!
 
yupo mpaka sasa hivi ukweli ni kwamba hana hela ya kurudi hostel cuz ni mwanachuo chuo kimoja cha ualimu ...toka tuanze kuishi tuna mwaka mmoja now ina maana akipata hela anytime ni wa kuondoka huyo
kama anamwanaume ataondoka aidha umempa hella au hujampa,lakin jiangalie na wewe inawezekana ukawa chanzo cha hayo yote.maana kaa ukijuwa kama wewe nichanzo ata ukimuacha atakae fata nae itakuwa ivyo ivyo,mwanaume hasifiwi kwa kubadili wanawake,bali kwa kujenga familia imala kwa hekima aliyopewa na Mungu.mwanamke yko chini yako wewe ndio wakuijenga nyumba yako au kuibomoa,kama unampenda jion mtoe mkapate msosi sehem zungumza nae maisha yaendelee mbele,achana na mawazo yavijiweni.
 
ni kweli mkuu nimekuwa pia nikitafuta replacement yake ila bado sijaona ila ninamiini siku akipatikani nitampa uhuru achart mpaka wagalagale
watu wanakugongea bado tu unakomaa nae mwache aende utapata mwingine unamng'ang'ania kama mama yako mzazi
 
Mkuu demu akishajua umempenda ndio anapata pa kukuchezea sasa..Shida moja ulionesha udhaifu kwake kuwa 'umekufa na kuoza' ndio maana!!



BTW upo njia panda ya wapi??
 
Back
Top Bottom