Nipo Njia Panda Naomba Mnishauri

Nipo Njia Panda Naomba Mnishauri

Miaka mitatu ni mingi sana washasahauliana na hawawezi kurudiana tena, ww piga mzigo haraka sana kabla ujapoteza hiyo nafasi,
 
Huyo mchizi wako kama akaimaindi atakuwa boya....na wewe acha uboya kula huyo demu...nakumbuka nilikuwa na mchizi wangu very close friend kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari mpaka mtaani ....mi nikila demu na yeye anamvizia anagonga..na yeye akila demu nafanya hivyo hivyo....na wote tunakua tunajua....hakuna anaye mind...siku nyingine tukiamua tulikuwa tunapiga collabo(mtungo) hasa tukishamlewesha demu...na mambo yalikuwa yanaenda...mpaka nilkuja kuoa demu ambae pia alimkosa kosa kidogo...kwa hiyo nyie wote nawaona ni maboya kama mnamaind vitu vidogo namna hii,hao viumbe hawahitaji staha yeyote
 
Mimi kwakweli kuwa na mahusiano na mtu aliyekuwa na mahusiano na rafiki angu naona ni usaliti.

Mimi mwenyewe rafiki angu akitembea na aliyekuwa mpenzi wangu, sitakaa nimtazame vizuri.
Kweli mkuu ndio maana mimi nafsi inanisuta hata kabla sijachukua uamuzi
 
Hii hali ishanitokea, in fact inaniathiri hadi leo wakati nilifanya hivo zaidi ya miaka minne ilopita.
Well, mi nilifanya hivo kama kulipiza kisasi kwa ex wangu...nahisi na huyo dada atakuwa anajaribu kukutumia wewe kama mimi nilivofanya...nikuhakikishie kuwa athari ni nyingi kuliko faida, na kumbuka undugu ni hazina...hivi umefikiria siku mkiachana na huyo dada??!
Usiruhusu kutumika kama chambo, kama kweli unampenda huyo rafiki ako hii kitu itakuathiri maana nikuhakikishie kuwa urafiki wenu ndo utakuwa umefika mwisho.

Hakuna lolote...hautakiwi kuweka rohoni hivi vitu....mimi nina best yangu tulikuwa tunapokezana mademu sana tu,tena wengine tulikwa tunawapenda sana tu...wengine mpaka mtungo tulishawahi kupiga.....na mpaka leo mimi na jamaa ni marafiki wakubwa ila mademu tumewatosa wengi sana......inategemea na kiasi cha uboya wenu
 
Huyo mchizi wako kama akaimaindi atakuwa boya....na wewe acha uboya kula huyo demu...nakumbuka nilikuwa na mchizi wangu very close friend kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari mpaka mtaani ....mi nikila demu na yeye anamvizia anagonga..na yeye akila demu nafanya hivyo hivyo....na wote tunakua tunajua....hakuna anaye mind...siku nyingine tukiamua tulikuwa tunapiga collabo(mtungo) hasa tukishamlewesha demu...na mambo yalikuwa yanaenda...mpaka nilkuja kuoa demu ambae pia alimkosa kosa kidogo...kwa hiyo nyie wote nawaona ni maboya kama mnamaind vitu vidogo namna hii,hao viumbe hawahitaji staha yeyote
Duh mkuu kwa historia hiyo basi huyo mkeo jamaa sio kwamba alimkosakosa bali alishampitia. Au atakuja mpitia tu huko mbeleni.
 
Wakuu habari za mda huu. Kwanza kabisa TGIF.

Naomba niende kwenye mada moja kwa moja bila kupoteza wakati. Mimi ni kijana bado yanki kidogo nimehitimu chuo kikuu mwaka juzi. Sasa tatizo langu lipo kuwa kuna mdada ambaye tulisoma nae chuo ambaye wakati tukiwa chuoni alikuwa mpenzi wa rafiki yangu wa karibu sana.

Yani rafiki wa karibu kiasi cha kutosha maana tullikuwa tuna share mambo yetu na hata kusaidiana kwa hali na mali. Huyu shemeji wameachana kwa mda sasa tokea tukiwa chuoni lakini juzi hapa amenitafuta akaniambia amenimiss anaomba tuonane.

Kweli tumeonana na katika kukaa kwetu akaanza vijitabia ambavyo sikuvielewa elewa (kurembua rembua na mikonyezo mingi) ila nikajiongeza kusingizia dharura nikaondoka. Baadae usiku akanitumia sms kuwa kwanini namfanyia makusudi sitaki kukaa nae sijui anaumia moyo, nikashtuka sana. Kiukweli kwangu mimi naona kama jambo la ajabu ukizingatia alishawahi kuwa mpenzi wa rafiki yangu japo ni miaka kama mitatu imepita tokea walipoachana.

Naona kama kitendo cha kuwa nae ni kama usaliti kwa msela wangu japo sijui kama yeye atachukulia vipi au jamii mnachukuliaje swala kama hilo. Huyu binti ananitafuta kila wakati sio asubuhi mchana wala jioni, kisingizio ni kuwa anasema najali na alinipenda mda tokea chuoni ila ni baada ya kuwa alishakuwa na rafiki yangu.

Anadai alipenda jinsi nilivyokuwa mcheshi, ninaejali na nimaejituma kwenye masomo kuanzia ngazi ya mimi mwenyewe hadi kwenye group ambalo tulikuwa nae group moja na mara nyingi nilikuwa namsaidia assignments hata kama hakuwepo chuoni nilimfanyia na mwisho akapata na yeye GPA nzuri tu.

Tatizo kubwa jingine linakuja kuwa anajiamini kuwa ataninasa kutokana na hali mbaya ya ajira na maisha kuwa magumu na yeye kwao ulimbo upo na hata hiyo degree alisoma tu ili apate kujua masuala ya usimamizi wa biashara za nyumbani kwao, hivyo anatumia nguvu ya ulimbo kuninasa maana mpaka sasa nipo mtaani natangatanga sina hata shilingi.

Wakuu hali hii kusema kweli imenifanya nizidiwe na msongo wa mawazo ukizingatia kuwa mimi naona kama nitakuwa nimemsaliti mwana alafu kwa upande mwingine naona kama ndio sehemu ya kujifariji maana sina hata demu kila ninaemtaka anaringa kisa sina hela. Wakati hapa mbele yangu naona kabisa kuna faraja lakini nikimfikiria msela nakosa kabisa la kufanya.

Naombeni ushauri wenu wakuu nifanyeje.
Kuwa makini sana. Ukiendekeza ujinga na umaskini utakuwa kulia maisha yako yote.
 
Hii dunia ya ubepari mzee baba wewe kwanza yule baadae.

mm nilikuwa na rafiki yangu damu damu halafu family yao iko vizuri alinipeleka kwao nikakutana na mdogo wake nikakata, kipindi hiko nimechoka mbaya.

Jamaa alipojua alimind lakin dogo ndo hivyo alining'ang'ania ikabidi awe mpole akabaki na kinyongo moyoni

Mpaka muda huu nimemuoa dogo na family yake imenipa cha kufanya, nakula vyuku kwa mrija.

Kuwa na sera kama za mmareka maslahi kwanza urafiki baadae.
 
Kweli mkuu ndio maana mimi nafsi inanisuta hata kabla sijachukua uamuzi

Don't do that.

Swala la pesa, pambana kiume...yaani nakushangaa wataka kuwa mariooo?? Au utapewa ajira kwenye miradi yao??

Unafikiri utajisikia uko huru?? Mwanaume kupewa pesa na ke ni kuishushia hadhi uanaume. Pambana uwe na vyako bana, umpe mke pesa.
 
Hakuna lolote...hautakiwi kuweka rohoni hivi vitu....mimi nina best yangu tulikuwa tunapokezana mademu sana tu,tena wengine tulikwa tunawapenda sana tu...wengine mpaka mtungo tulishawahi kupiga.....na mpaka leo mimi na jamaa ni marafiki wakubwa ila mademu tumewatosa wengi sana......inategemea na kiasi cha uboya wenu

Ni kweli nyie ni maboya...na hao madada ni maboya wahead
 
Hii dunia ya ubepari mzee baba wewe kwanza yule baadae.

mm nilikuwa na rafiki yangu damu damu halafu family yao iko vizuri alinipeleka kwao nikakutana na mdogo wake nikakata, kipindi hiko nimechoka mbaya.

Jamaa alipojua alimind lakin dogo ndo hivyo alining'ang'ania ikabidi awe mpole akabaki na kinyongo moyoni

Mpaka muda huu nimemuoa dogo na family yake imenipa cha kufanya, nakula vyuku kwa mrija.

Kuwa na sera kama za mmareka maslahi kwanza urafiki baadae.
Hahaha mkuu wewe ni nyoko
 
Mkuu for the sake of your friendship na mwana. Jikatae mbaba usile huyo shem wa kale.
Ila kama huna option kill the friendship beba huyo mtoto.
 
Sababu ya yeye kuachana nae uliijua?
Kulala na ex wa rafiki yako ni tabia mbaya.. yaani wewe ni utakuwa bomu usiyejiheshimu. Kichefuchefu kuwa hata unafikiria kufanya hivyo..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom