Nipo KIA, si kawaida

Nipo KIA, si kawaida

zomba

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2007
Posts
17,240
Reaction score
3,935
Katika jumla jamala ya kutimiza krismasi, nimejishtukia nikialikwa kwenda kusherehekea krismasi Arusha. Kwa bahati nzuri (au mbaya?), mwenyeji wangu aliyenialika, kwao ni uso kwa uso na KIA na hapa kwao panaitwa KIA. Duh!

Cha kustaajabisha na ambacho "si kawaida", wenyeji wangu wamenitoa "outing".

Wenyeji wangu wamenileta kwenye "kumbi ya starehe" kwa jina panaitwa "kwa godi". Toka tumefika hapa saa moja kamili ya usiku huu mpaka nnapoandika haya, tunastareheshwa kwa nyimbo za taarabu. Si maajabu hayo? KIA na taarab wapi na wapi? Hususan Wameru! Amma kweli Kikwete ana shani yake na asifiwe. Nakumbuka "baniani mbaya kiatu chake dawa".
 
Kikwete apewe shani kwa Wameru kusikiliza Taarab!!!? Lini alifanya kampeni ya kuwahamasisha Wameru wasikilize Taarab? Taarab ilikuwepo kabla ya Kikwete kuingia madarakani. Tembea Zomba uione Tanzania yetu na ukibahatika kufika sehemu nyingi ndio utagundua kwamba pamoja na tofauti za kikabila, kidini, kiitikadi Watanzania tunashabihiana sana katika mambo mbali mbali. Hivyo mimi sishangai kabisa hapo kwa Godi kufungulia muziki wa Taarab ili kuwatumbuiza wateja wake.

Happy New Year Zomba.
 
Nasoma hii thread kwa mara ya 3 sasa, na bado sijaelewa mantiki ya kulinganisha JK na taarabu.
Labda ndiyo hasa maana ya starehe ya kunywa BALIMI EXTRA LAGER. Agiza zingine mbili, na mwambie mhudumu afungue zote- bili kwangu.
 
Nasoma hii thread kwa mara ya 3 sasa, na bado sijaelewa mantiki ya kulinganisha JK na taarabu.
Labda ndiyo hasa maana ya starehe ya kunywa BALIMI EXTRA LAGER. Agiza zingine mbili, na mwambie mhudumu afungue zote- bili kwangu.

hahahaha nahisi wewe umeelewa
 
Zungukia Kominite, Line Police, Kileleni, n.k.,
Na Ukimaliza hapo nenda pale Njia Panda, pamechangamka sana mkuu. Utakuta kuna Kwa Rose, Maonga, Sasco-J n.k.

Mpaka umalize hizo sehemu basi sikukuu yako itakua murua kabisa.
 
Wenyeji wangu wamenileta kwenye "kumbi ya starehe" kwa jina panaitwa "kwa godi". Toka tumefika hapa saa moja kamili ya usiku huu mpaka nnapoandika haya, tunastareheshwa kwa nyimbo za taarabu. Si maajabu hayo? KIA na taarab wapi na wapi? Hususan Wameru! Amma kweli Kikwete ana shani yake na asifiwe. Nakumbuka "baniani mbaya kiatu chake dawa".

Muziki wa taarab siku hizi umekubalika sana ukilinganisha na zamani. Kote Tanzania nilikozunguka mimi nyimbo za taarab hupigwa nimezisikia sana. Hivyo si jambo la kushangaza kusikia taarab KIA.
 
kwani mmelazimishwa hapo kwa god?hamieni sehemu nyingine tu!!
 
mie ndo najuta kufungua huu uzi......thread nyingine bana...



Nasoma hii thread kwa mara ya 3 sasa, na bado sijaelewa mantiki ya kulinganisha JK na taarabu.
Labda ndiyo hasa maana ya starehe ya kunywa BALIMI EXTRA LAGER. Agiza zingine mbili, na mwambie mhudumu afungue zote- bili kwangu.
 
Nasoma hii thread kwa mara ya 3 sasa, na bado sijaelewa mantiki ya kulinganisha JK na taarabu.
Labda ndiyo hasa maana ya starehe ya kunywa BALIMI EXTRA LAGER. Agiza zingine mbili, na mwambie mhudumu afungue zote- bili kwangu.

haa haaa haaaa, hata mimi nimechoka kabisa

taarab vs kikwete

dah
 
Yani thread nyingine hazina kichwa wala miguu.

Kwahiyo maendeleo kwako wewe ni kukuta taarabu zinapigwa mpaka KIA???

Ndio maana Kikwete huwa anatimkia nje kwenda kula bata tu maana mambo mengine mnayomuunganisha nayo hata hayaeleweki.
 
Kumbe kuenea kwa taarabu ni sehem ya mafanikio ya JK na ccm?..ccm wanunue kipindi tbc kutangaza haya mafanikio.
 
Muelekezeni mahali pa kupata vyangudoa hapo arusha maana na hiyo ni mojawapo ya maendeleo ya jk
 
Mafanikio kumbe tunayapima kwa namna nyingi aisee?nadhani na hiyo ya taarabu kusikika ilikuwa ni ndani ya ilani au ahadi binafsi za rais
 
haa haaa haa

ukifika moshi mjini ilizia Onyonya Okunonze wanapiga taarabu nzuri sana
 
"Kanunua simu kampa demu, walipoachana, kampokonya... cheza kidogo cheza kidogo... haishikiki eeh haishikiki, pembe ya ng´ombe..."
 
Ni bora kulisha mbuzi utamla nyama.Jamaa amepata rafiki wa kumkarimu xmass kwa chakula na kinywaji ameshiba badala ya kushukuru ameanza kukosoa.Akirudi kwao ataenda kusema mwenyeji wake alilala chumbani na mke wake yeye wakamwacha alale mwenyewe.
 
Kama vp waambie wenyeji wako wakulete mitaa fulani inaiwa KIDIRE hapo utatukuta wanajf maarufu pia utakutana na banana baridi, gongo baridi ,na muziki wa kijanja wa kimeru na kimasai.
 
"kanunua simu kampa demu, walipoachana, kampokonya... Cheza kidogo cheza kidogo... Haishikiki eeh haishikiki, pembe ya ng´ombe..."

halishikiki kwa asili yake halishikiki ..............pembe la ng'ombe, cheza kidogo cheza kidogo................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom