Nionavyo Udhaifu wa Operesheni Sangara

Katiba haisababishi uongozi bora na uongozi wenyewe hausababishi katiba bora. Wananchi ndio huchagua uongozi na wakichagua uongozi mbaya matokeo yake yako wazi; wakichagua uongozi mzuri basi uongozi huo utaweza kusimamia kuandikwa kwa Katiba bora ambayo wao viongozi bora watakuwa tayari kuilinda na kuwa chini yake.

Hivyo, wananchi bora huleta viongozi bora na ambao huongoza kuandika Katiba bota itakayowafaa wote; na ikishaandikwa, wote wanakuwa chini ya Katiba hiyo bora.

Ndio maana Katiba yetu inasema "wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;".. kumbe msingi wa mamlaka yote siyo viongozi, katiba n.k bali ni wananchi! So.. kama wananchi wakiwa wazembe mamlaka zitakuwa zembe..

MKJJ,ni wazi vinategemeana lakini tunachotakiwa kufanya si comparisons as in this vs that.....Rather i think one is a step stone to the other,one MUST first be achieved as a step towards the other....Umesema kuwa uongozi bora hausababishi katiba bora lakini hapo hapo unadai kwamba wananchi wakichagua uongozi mzuri basi uongozi huo unaweza kusimamia kuandikwa kwa katiba bora.,whats the difference?
Turudi tu kwenye point sasa kwamba uongozi bora is a step stone towards achieving katiba bora?
 
Kishoka

Una mawazo mazuri lakini yamejikita kwenye nadharia zaidi ya vitendo, hayo unayoyasema si kuwa Chadema hawayajui wala hawayatendi ninachojua mimi wanayatenda hata zaidi ya unavyofikiri wanaenda kijiji kwa kijiji tena na data za kijiji, kwa mfano watasema zilitolewa kiasi kadhaa za kujenga madarasa matano lakini yamejengwa mawili kulikoni

tatizo hasa on the ground ni mbinu wanazotumia opponent wao CCM leo utaenda Maswa utawaambia wananchi bei ya pamba inatakiwa iwe sh 700 watakuitikia kwa makofi ukigeuza mgongo opponent wako ambaye ni chama tawala atakuja na kusema sisi ndio tuna serikali itanuua pamba kwa sh 400 kama hutaki kawauzie Chadema au CUF kesho ukirudi kuomba kura unafikiri watamupa nani ukiongeza na ukapa wa wananchi wenyewe

Nakubaliana na wewe kwa 100% lakini on the ground it is a different story, ukija upande wa wafanyakazi mambo ni yale yale mwajiri mkuu Tz ni serikali maana yake nini ina watu wengi wa karibu, wewe mfanyakazi ukionekana uko against nao kesho kibarua huna wakati hicho kibarua ndicho kinalisha familia yako utafanya nini. Ukisema kura ni siri utakipigia chama unachokipenda vilevile haisaidii unamtegemea nani akufanyie kampeni, wewe unajificha utamwachia Slaa pekee hadi lini kuna siku na yeye atachoka.

Kwa hiyo Kishoka orodha ni nzuri sana lakini wapokeaji si kama hawapo wapo lakini wamezongwa na matatizo yao mengi tu ni kama mzabibu uliomea kwenye miiba unataka kukua lakini hauwezi kwa vile umezingwa na miiba wapokeaji wachache waliopo achilia mbali matatizo yao vile vile wanatishwa na vyomba vya dola polisi, mahakama kubambikiziwa kesi nk
 
Kumbe mkuu ulidhani nataka CCM wabadili katiba? kwani Zanzibar Katiba wamebadioli CCM? mabadiliko ya katiba yanaletwa na nia, nguvu na mshikamano wa wananchi, hata siku moja CCM hawawezi kukubali hilo. Vyama vaya siasa should dedicate their resources in mabadiliko ya katiba. Ogaha tusitegemee zur5i lolote kutoka CCM! mabadiliko yanaletwa na wananchi kupitia vyama, bila mabadiliko CCM watatawala milele study zimeonyesha hivyo.

Sio rahisi ni nguvu na kujitoa vinatakiwa hapo ikiwa na kuwa tayari kudhalilishwa na kulazwa polisi, na hili hatulitaki! na hao wanaosema wapinzani hawataki hili!

Webby............sitegemei kuwa CCM wataleta mabadilikoya katiba.......kama nilivyokwishaeleza...............suala la Katiba nakuambia heri hata ya sisi hapa JF tulilipigia kelel wee mapka CCM wakakja na majibu kuwa.....eti tuwaeleze mapungufu yako wapi ili warekebishe..............hivi vyama vya upinzani ukiondoa juhudi binafsi za Mtikila.......sitegemei sana si kwa CHADEMA au CUF bara................

CCM Zanzibar wanalazima kufanya baadhi ya mambo kwa sababu ya upemba na uunguja....... period!.........otherwise visiwa havitawaliki idadi ya wawakilishi wa upinzani ni kubwa.............halafu kumbuka kwa wao zinapokuja issue za Muungano..........ukiangalia kwa undani (i.e. behind the curtain) utaona wako pamoja (CCM, CUF and the rest)...............kupatana kwa Seif na Karume wala si kitu kingine..............ni common interest ya Wazanzibari.........if you know what i mean..............
............and trust me kama kuna kosa la kiufundi CCM walifanya kuhusu Zanzibar ni kukataa ushauri wa JKN kuhusu serikali ya Mseto............ilikuwa ni mbaya kwa CCM......lakini ilikuwa ni nzuri kwa mageuzi...............kwani pressure yake umeiona na matokeo.........ndio hayo............

Kwa hiyo utaona kuwa Zenji........nguvu ya mabadiliko yao imetokana na mgawanyiko wa uongozi uliopo i.e. Pemba na Unguja..............hii kitu bara HAIPO.............labda mapinduzi yatokee..........otherwise it will take bara centuries..........kama mwendo wa upinzani ndio huu...........trust me...........
 
Webby............sitegemei kuwa CCM wataleta mabadilikoya katiba.......kama nilivyokwishaeleza...............suala la Katiba nakuambia heri hata ya sisi hapa JF tulilipigia kelel wee mapka CCM wakakja na majibu kuwa.....eti tuwaeleze mapungufu yako wapi ili warekebishe..............hivi vyama vya upinzani ukiondoa juhudi binafsi za Mtikila.......sitegemei sana si kwa CHADEMA au CUF bara................

CCM Zanzibar wanalazima kufanya baadhi ya mambo kwa sababu ya upemba na uunguja....... period!.........otherwise visiwa havitawaliki idadi ya wawakilishi wa upinzani ni kubwa.............halafu kumbuka kwa wao zinapokuja issue za Muungano..........ukiangalia kwa undani (i.e. behind the curtain) utaona wako pamoja (CCM, CUF and the rest)...............kupatana kwa Seif na Karume wala si kitu kingine..............ni common interest ya Wazanzibari.........if you know what i mean..............
............and trust me kama kuna kosa la kiufundi CCM walifanya kuhusu Zanzibar ni kukataa ushauri wa JKN kuhusu serikali ya Mseto............ilikuwa ni mbaya kwa CCM......lakini ilikuwa ni nzuri kwa mageuzi...............kwani pressure yake umeiona na matokeo.........ndio hayo............

Kwa hiyo utaona kuwa Zenji........nguvu ya mabadiliko yao imetokana na mgawanyiko wa uongozi uliopo i.e. Pemba na Unguja..............hii kitu bara HAIPO.............labda mapinduzi yatokee..........otherwise it will take bara centuries..........kama mwendo wa upinzani ndio huu...........trust me...........

Asante umeliona hilo na asante kwa kumtaja Mtikila, at least sasa baada ya mjadala huu tunaona jinsi gani kazi ilivyo nzito huko mbele ni kubwa kuliko kuandika hizi thread. Kazi wanayofanya Chadema ni kubwa na nzito, ni sawa na kusema saloon car ivute mabehewa ya treni na wayafikishe Kigoma. Hivyo basi, Chadema peke yake haitaweza, at least vyama vingine vya siasa kama vingekuwa ctive, lakini kazi kubwa sana, maana upepo wa Operation sangara ni mkali lakini unasahaulika haraka pia!

Ogah kwanza nikueleze leo na ukae ukijua kuwa siasa yetu ya siasa yetu ya sasa hivi haina tofauti na enzi za ukoloni na zinavunja haki za binadamu.Ebu nikupe ninatochokuwa ninatafakari:

Utanzania na Tanzania

Tanzania ni ya watanzania , wenye itikadi, imani, na mlengo tofauti, Tanzania inatakiwa kuongozwa na watanzania wote kama taifa na si kundi fulani la watu. Mathalani CCM wako milioni nne , haiwezekani hili kundi ndio likawa viongozi wa sisi wengine wote. Tanzania halisi inatakiwa kuongozwa na watanzania wote wakiwakilishwa na vyama vyao humo serikalini. Pamoja na itikadi zetu kuwa tofauti still kila mtanzania ana nia njema na taifa letu na itakuwa hivyo kwa sababu ya ni watanzania .

CCM

Kwa sababu CCM ni kundi dogo , linaloongozwa na wana CCM pekee, basi halina uhusiano na malengo na umoja wa watanzania wengine. I mean kama watanzania tumekubali hili ni taifa letu wote na tutaliongoza wote bila kujali itikadi zetu, then katika mkataba huu wa fikra CCM wako kinyume , kwanza wanakula rushwa na hakuna jema lolote nchi hii ambalo tunaweza kusema ni kwa sababu ya CCM! Kwa kifupi CCM ni wakoloni, wanaitawala Tanzania kibabe, HAKUNA MKATABA TULIOKUBALIANA KUWA CCM WALIONGOZE HILI TAIFA, MKATABA HUO NI KATIBA NA KATIBA HII NI ILE ILE YA CHAMA KIMOJA! CCM is leading this country without our consent!

HUMAN RIGHT

'All human beings are born free and equal in dignity and rights. They endowed with reasons and conscience and shouls act towards one another in a spirit of brotherhood' Artcile 1.

I regard class differences as contrary to justice and, in the last resort, based on force-Einstein

Hii siyo kitu kipya lakini ijulikane kuwa CCM wanaliendesha hili taifa kinyume na haki za binadamu. Taifa la Tanzania halipo, litazaliwa tu kama CCM ikikubali kutoa haki hii ya uhuru wa fikra kila mtu awe nao humu nchini, haki ya kuamini na kuongozwa na ninayempenda and the only means ni serikali ya mseto.



Privilege is the greatest enemy of right-Marie E.

Leo hii JK akikubalika na akapigiwa kura atapigiwa kura na wana CCM , lakini atatangazwa kuwa ameshindwa uchaguzi wa urais yaani kwa watanzania wote, I dont believe in this.

Nikitafakari hayo hapo juu naona giza mbele; wananchi wenyewe unaowaambia 'nyoka huyo' wanasema mbona hana sumu? mbona hatufi, shida tumeozea njia ya kuokoa HIKI KIZAZI NI KWENDA BEYOND THEIR THINKING CAPACITY kufanya kitru ambacho watakuelewa next 20yrs, na hicho kitu ni kivunja nguvu za CCM na mizizi yake kwa kuisafisaha katiba na kusema ...kila mmoja anauwezo wa kuongoza hili taifa kutokana na asilimia ya wanaowaamini! na ikiwezekana hivi ndiyo kuzaliwa kwa Tanzania.

Ndiyo ninavyowaza, tuko pamoja, na ninaunga mkono juhudi za vyama vyovyote , this is just another fairly way of looking!
 
Monoko Mushi,



Leo ukiwaambia Wananchi kuwa bajeti na fungu la bajeti iliyopaswa kuleta Hospitali au kujenga barabara, Uongozi wa Wilaya umezitumia visivyo, ni rahisi kwa wao kuelewa kuliko kuanza kuwaelezea kuhusu EPA.

Kwanza tukianza kuwaambia Wananchi kuhusu EPA na kusema pesa zimeibiwa, ni rahisi wao kutupuuzia maana kila siku kauli wanazozisikia kutoka kwa Viongozi ni kuwa Tanzania haina pesa na wameshawishika vizuri kuamini kuwa hakuna fedha.

Ndio maana unakuta wanashangilia pale mtu anapokuja na kudai ati ana Wafadhili au marafiki ulaya ambao watatuletea misaada. Hii ni kutokana na wao kuamini Tanzania haina uwezo na Serikali yao bado inajaribu kujikwamua tangu tamko la Mwalimu Nyerere baada ya vita vya kagera aliposema tujifunge mkanda!
Kwamba wananchi wameshawishika na kuaminishwa (wamedanganywa) kuwa nchi haina hela, isituzuie kuwaeleza ukweli. Kuwaeleza tu kuwa fedha zimetumika vibaya, na kuficha kuwaeleza kuwa EPA zimeibiwa fedha nyingi ambazo zingewaletea maendeleo, si jambo la busara sana.
Ukweli wa ufisadi na madhara yake uhubiriwe hadi wananchi waelewe, ndipo wataamka na kuchukua hatua.
Kuendelea kuwaeleza masuala ya misaada toka nje, hakutatofautisha CCM na Chadema - na kwa kweli ni kuwaficha ukweli wa nguvu na utajiri wa raslimali zao
 
Mheshimiwa Dr Slaa.Mimi naomba ugombee U-raisi wa nchi hii kwani unaonesha unaupeo wa hali ya juu katika kuchambua mambo, mfano mzuri ni huu mswada aliosaini raisi kikwete uwe sheria ilhali yeyebinafsi hajausoma, hii inaonesha hayuko serios na mambo na anaweza kulipeleka Taifa mahali pabaya, huu ni mwendelezo wa kusaini mikataba mibovu bila wao kuipitia na kujua kilichomo ndani. Nakuunga mkono na nategemea utatangaza nia yako mapema tujipange vizuri ushinde.
 
Monoko Mushi,

Mfumo bora ni mfumo shirikishi, mfumo huru wenye kutoa usawa na haki na zaidi kuwajenga wananchi kuwa huru na kuishi katika Demokrasi ya kweli.

Kilichofanyika Zanzibar 1992 ni mazingaombwe ambayo yaliishia kujaza maduka bidhaa za kuagiza na kuanzishwa kwa mfumo butu wa kisiasa.

Katiba haikubadilishwa, Sheri ahazikubadilishwa na bado CCM inaendelea kuongoza eti katika mfumo wa Vyama vingi lakini Katiba, Sheria na mengine mengi ni ya mfumo wa zamani uliokuwa ni wa Ki-TANU na CCM.

Ndio maana leo hii TISS wanahangaika kwa vitu vidogo visivyo na maana, lakini vile vya msingi hawavioni, tatizo ni mfumo tulionao.

Leo hii walioko CCM wanajifanyia wanachotaka, hakuna wa kuwashikisha adabu. Wakivunja sheria, wanaogopewa kwa kuwa Polisi na Mahakama bado zinatawaliwa na kuongozwa kutoka mfumo wa awali na katiba inayovifunga vyombo hivi.

Hata Bunge, linapaswa kuwa lenye nguvu huru, lakini kwa kuwa CCM haijiamini na wana wasiwasi kila siku, basi kudhibiti hata mapinduzi ndani ya Chama kutoka kwa Wabunge wake, wameendeleza mfumu butu ambao wabunge ni kama galasa kwenye karata!

Tukibadilisha mfumo tutapata nafasi mpya na kuvua zile nguvu za mabavu za CCM na wateule wake wanaojiona wako juu ya sheria.

Rev. Kishoka

Kwanza nikupongeze kwa hoja zako zenye nguvu na ambazo zinatuelekeza kwenye kutafuta kiini hasa cha tatizo linalotukabili. Mimi naamini kuwa kimsingi haupingi OS bali unalenga katika kuwawezesha CHADEMA wapanue wigo wa mapambano ili kwamba tuweze kujikita katika kiini cha tatizo na kukiondoa ili tupate mabadiliko ya kweli.

Naungana kinsingi na hoja yako kwamba mfumo wa kiutawala na kisiasa wa Tanzania bado ni wa chama kimoja. Kilichofanyika ni kiini macho cha kuweka vipengele vichache kuruhusu watu wachache waingie bungeni kama wapinzani.

Huwezi kupingana na chama ambacho:
  • Mwenyekiti wake ni rais wa nchi, ni sehemu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano na ni amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama - ikiwemo jeshi la polisi ambao wana kauli kubwa katika kuamua ni wakati gani vyama pinzani vifanye mikutano ama maandamano hata kama ni ya amani.
  • Rais na mwenyekiti wa chama tawala ana uwezo kikatiba wa kulivunja bunge pale ambapo watatofautiana katika masuala kadhaa - ndio maana bunge lilinywea katika mjadala wa Richmond baada ya kuonekana wazi kuwa mambo yaliyobaki yanamhusu Rais mwenyewe;
  • Rais anateua majaji wa mahakama kuu na mahakama ya rufaa na mwendesha mashitaka wa serikali;
  • Rais anateua Tume ya Uchaguzi - kumbuka kuwa tume imawatumia wakurugenzi wa halmashauri za wilaya kama wasimamizi wa uchaguzi - 'returning officers' na wakisha tangaza mshindi hakuna jinsi mpaka ufungue kesi mahakamani.
  • Rais anateua na kuwasimamia wakuu wa mikoa wote na wakuu wa wilaya zote ambao wote ni makada wakereketwa wa chama tawala na wenyeviti wa kamati za usalama za maeneo yao - kimsingi wao ndiyo wanatoa maelekezo kwa polisi na vyombo vingine vya usalama ya jinsi gani ya kuwadhibiti wapinzani.
  • Anateua na kuwasimamia hao maofisa wa usalama wa taifa ambao kimsingi kazi zao hapa Tanzania ni kumlinda rais na chama tawala na kuhakikisha kuwa hashindwi uchaguzi wowote.
  • Kama Rais ana uwezo wa kutumia resources zote za Serikali ama kihalali au kiharamu kuhakikisha kuwa chama chake kinashinda utawala.
Orodha ni ndefu lakini ninachojaribu kusema hapa kwa ufupi ni kuwa huwezi kupambana na kuing'oa CCM madarakani kwa kutumia mfumo huu uliosukwa kuhakikisha kuwa wanatawala milele. Na ndio maana baadhi yao wanasema CCM itatawala kwa miaka mia moja ijayo kwa sababu wanajua wanachosema.

Hivyo nakubaliana na Rev. Kishoka anapojenga hoja kuwa pamoja na OS na mapambano (cosmetic) dhidi ya ufisadi tunapaswa tujielekeze vilevile katika kubomoa huu mfumo uliopo wa kikatiba na kisheria kwa lengo la kuleta 'checks and balances' zinazotakiwa ili kuuruhusu upinzani uweze kustawi na kukua nchini.

Eneo moja ambalo nadhani wapinzania na hasa watanzania wote tungejielekeza ni kudai kwa nguvu zote kuandikwa upya kwa katiba na sheria zinazotawala uchaguzi na uongozi ili tuanze vizuri.

Hatuwezi kupambana na kuushinda ufisadi kwa kutumia sheria hizi hizi ambazo ndicho kiini hasa cha ufisadi wenyewe.
 
Operesheni Sangara ni mkakati mzuri sana wa kuwazindua wananchi..Asikudanganye mtu unamanufaa sana kuliko wengi wanavyodhani na kujifariji..Sisi tunaiongia filed tunafahamu hili ukiwa nje sio rahisi kuona..
 
Nimewauliza nyote, je kma OS ni nzuri sana, je matunda yake yameonekana wapi? Ukiondoa Tarime ambayo ilikuwa ni given, je Wananchi wa sehemu gani wameipokea OS na kuifanyia kazi na kuikataa CCM?

Mkishindwa kunipa kijiji, kata, tarafa, wilaya hata mkoa basi mjue wazi kuwa OS haifanyi kazi, bali inapoteza muda kama si kutumia mbinu butu au ni dhahiri Watanzania wanaenda shangilia na ni fuata upepo kama Jakaya aliyotuambia!
 
Rev Kishoka,
Op Sangara ilianza baada ya CHADEMA kushinda uchaguzi mdogo uliofuatia kifo cha Wangwe. Mafanikio yake yanaweza kupimwa kwa kuangalia chama hicho kilivuna nini kwenye chaguzi ndogo zilizofatia Op hiyo za Busanda na Biharamulo. Hapa JF tunaweza tusijue mafanikio ya Op hiyo, lakini watawala wanayafahamu sana na yanawatisha kwelikweli!
 
Rev Kishoka,
Op Sangara ilianza baada ya CHADEMA kushinda uchaguzi mdogo uliofuatia kifo cha Wangwe. Mafanikio yake yanaweza kupimwa kwa kuangalia chama hicho kilivuna nini kwenye chaguzi ndogo zilizofatia Op hiyo za Busanda na Biharamulo. Hapa JF tunaweza tusijue mafanikio ya Op hiyo, lakini watawala wanayafahamu sana na yanawatisha kwelikweli!

Gag,

Kama OS ingekuwa effective, TAMISEMI 2009 ingemeguka japo kwa 45% na kwenda Upinzani! Lakini almost 98% ya TAMISEMI imerudi CCM, utasemaje Watawala wametishika?
 
Gag,

Kama OS ingekuwa effective, TAMISEMI 2009 ingemeguka japo kwa 45% na kwenda Upinzani! Lakini almost 98% ya TAMISEMI imerudi CCM, utasemaje Watawala wametishika?

Ukitazama kwa undani utaona kuwa hizi chaguzi za mitaa ni moja ya mbinu kali ya CCM ku divert resource za wapinzani kwa kuuweka mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu. Chadema wangekuwa na resources za kuwekeza kwenye huu uchaguzi nakuambia kuwa wangeshinda kwa asilimia kubwa tu. lakini waliangalia kama wangeweza kufund saa hizi wangekuwa choka mbaya sana kifedha na chama cha wenyewe kingekuwa kinatesa tu. hata mimi mwanzo niliwalaumu sana pale nilipokuwa namsaidia dogo mmoja aweze kuwa mwenyekiti lakini tukakosa kabisa reource pamoja kuwa nilitoa karibu laki tatu zangu. Lakini nilipopata maelezo na khali ya reource nikaona wamefanya jambo nzuri tu. Kwa CCM pamoja na ruzuku zao za mabilioni lakini hawakutumia na wenyewe fedha nyingi ila wanachofanya ni kutangaza kuwa ukishinda cheo hiki basi utakuwa tajiri na mafisadi wanatumia fedha zao kuwekeza pale ili waje wapate fedha baadaye.
 
Gag,

Kama OS ingekuwa effective, TAMISEMI 2009 ingemeguka japo kwa 45% na kwenda Upinzani! Lakini almost 98% ya TAMISEMI imerudi CCM, utasemaje Watawala wametishika?
Rev.Kishoka usipime ufanisi wa OS kwa kutumia kigezo kimoja tu cha matokeo ya TAMISEMI jaribu kuangalia na vigezo vingine hiyo ni kasumba ya wengi kwamba mwanafunzi kushinda mtihani ni hadi afaulu mtihani wa mwisho, mtihani wa mwisho si kipimo tosha cha uelewa wa mwanafunzi

hata hivyo kwa kutumia kigezo chako chunguza ni vijiji vingapi na mitaa mingapi Chadema imepata ukilinganisha na ile ya mwaka 2004
 
Luteni na Shalom,

Mtazamo wenu uko kwenye sehemu finyu ambayo ni Ubunge na Urais.

Serikali bora na siasa mbadala hujengwa kwanzia vijijini kwenda juu na si kutoka juu kwenda chini. Kosa la Upinzani mpaka leo hii ni kukimbilia ngazi za juu na si ngazi za chini ambako ujumbe wao utashika moto na kusambaa kwenda juu.

Sasa kama CHADEMA waliona hakuna maana ya TAMISEMI je wamejiuliza kilichotoke 2004 kwenye TAMISEMI na kukiwezesha CCM kushinda kwa kishindo 2005?

Hao wa TAMISEMI ndio wakala wa uchaguzi, wahamasishaji, watafuta wapiga kura, wanakata mbuga kutoka kijiji, kata, tarafa mpaka wilayani kuhamasisha. Hii ndio mbinu tulitumia kudai Uhuru wetu na kufanikiwa kumng'oa mkoloni. Hoo ni mbinu CCM wanaitumia mpaka leo hii kuendelea kuchaguliwa na kutawala.

Kosa lenu ni kufikiri kinachohitajika ni kushika Ikulu na Bunge pekee. Tanzania ya leo kubadilika ni kuanzia mitaani, vijijini, kwenye kata hadi tarafa na huko watu wakishaelimika, basi huku juu ni kazi rahisi.

Labda niwaulize moja la mwisho, kama ilikuwa ni gharama sana, mbona hata kwenye miji mikubwa ambako vyama ya upinzani inafahamika hakuna hata iti ya kutosa iliyoenda kwao kwenye TAMISEMI 2009 pamoja na watu wa mijini kuwa ndio wenye redio, magazeti, luninga na mifumo kebekebe ya kupashwa habari?
 
Luteni na Shalom,

Mtazamo wenu uko kwenye sehemu finyu ambayo ni Ubunge na Urais.

Serikali bora na siasa mbadala hujengwa kwanzia vijijini kwenda juu na si kutoka juu kwenda chini. Kosa la Upinzani mpaka leo hii ni kukimbilia ngazi za juu na si ngazi za chini ambako ujumbe wao utashika moto na kusambaa kwenda juu.

Sasa kama CHADEMA waliona hakuna maana ya TAMISEMI je wamejiuliza kilichotoke 2004 kwenye TAMISEMI na kukiwezesha CCM kushinda kwa kishindo 2005?

Hao wa TAMISEMI ndio wakala wa uchaguzi, wahamasishaji, watafuta wapiga kura, wanakata mbuga kutoka kijiji, kata, tarafa mpaka wilayani kuhamasisha. Hii ndio mbinu tulitumia kudai Uhuru wetu na kufanikiwa kumng'oa mkoloni. Hoo ni mbinu CCM wanaitumia mpaka leo hii kuendelea kuchaguliwa na kutawala.

Kosa lenu ni kufikiri kinachohitajika ni kushika Ikulu na Bunge pekee. Tanzania ya leo kubadilika ni kuanzia mitaani, vijijini, kwenye kata hadi tarafa na huko watu wakishaelimika, basi huku juu ni kazi rahisi.

Labda niwaulize moja la mwisho, kama ilikuwa ni gharama sana, mbona hata kwenye miji mikubwa ambako vyama ya upinzani inafahamika hakuna hata iti ya kutosa iliyoenda kwao kwenye TAMISEMI 2009 pamoja na watu wa mijini kuwa ndio wenye redio, magazeti, luninga na mifumo kebekebe ya kupashwa habari?

Unataka kusema kuwa ni bora kama wangepata ushindi wa TAMISEMI na kukosa kabisa wabunge? hapo ndipo tofauti ilipo. Nilishiriki uchanguzi wa Tamisemi na siwalaumu kabisa Chadema hawa CCM sijui wanasaidiwa na nani lakini ni lazima huyo mtu ni powerful sana and Evil!
 
Luteni na Shalom,

Mtazamo wenu uko kwenye sehemu finyu ambayo ni Ubunge na Urais.

Serikali bora na siasa mbadala hujengwa kwanzia vijijini kwenda juu na si kutoka juu kwenda chini. Kosa la Upinzani mpaka leo hii ni kukimbilia ngazi za juu na si ngazi za chini ambako ujumbe wao utashika moto na kusambaa kwenda juu.

Sasa kama CHADEMA waliona hakuna maana ya TAMISEMI je wamejiuliza kilichotoke 2004 kwenye TAMISEMI na kukiwezesha CCM kushinda kwa kishindo 2005?

Hao wa TAMISEMI ndio wakala wa uchaguzi, wahamasishaji, watafuta wapiga kura, wanakata mbuga kutoka kijiji, kata, tarafa mpaka wilayani kuhamasisha. Hii ndio mbinu tulitumia kudai Uhuru wetu na kufanikiwa kumng'oa mkoloni. Hoo ni mbinu CCM wanaitumia mpaka leo hii kuendelea kuchaguliwa na kutawala.

Kosa lenu ni kufikiri kinachohitajika ni kushika Ikulu na Bunge pekee. Tanzania ya leo kubadilika ni kuanzia mitaani, vijijini, kwenye kata hadi tarafa na huko watu wakishaelimika, basi huku juu ni kazi rahisi.

Labda niwaulize moja la mwisho, kama ilikuwa ni gharama sana, mbona hata kwenye miji mikubwa ambako vyama ya upinzani inafahamika hakuna hata iti ya kutosa iliyoenda kwao kwenye TAMISEMI 2009 pamoja na watu wa mijini kuwa ndio wenye redio, magazeti, luninga na mifumo kebekebe ya kupashwa habari?
Kishoka
Ukitaka mafanikio ya haraka haraka jaribu wizi,
Lengo la chama cha siasa si kushinda uchaguzi peke yake lengo ni kuona yale unayoyataka yanatokea au kutekelezwa hata kabla ya kushinda uchaguzi, unaweza kushinda na kuingia madarakani ukashindwa ku deliver

CCM wako madarakani kwa muda mrefu wana resources nyingi wanamtandao mkubwa hadi vijijini kutaka kuilinganisha na Chadema ya juzi eti kwanini haikushinda TAMISEMI ni ufinyu wa kufikiria kutegemea kesho tu Chadema itande nchi nzima ni ndoto za alinacha kwa hiyo kupima matokeo ya TAMISEMI kati ya CCM na Chadema bila kuangalia hali halisi(reality) ni umasikini wa utafiti

Kishoka unaweza kuniambia mwaka 1994 Chadema ilikuwa inaongoza vijiji/mitaa na Halimashauri ngapi nafikiri ilikuwa haina hata kijiji, Halimashauri zote zilikuwa chini ya CCM tuambie hizo Halimashauri za Chadema na hiyo mitaa ya CUF imetoka wapi Kenya au ilikuwa ya ODM Kenya, sometimes tujifunze ku appreciate what opps parties are doing hata kama si kwa speed unayotaka wewe mipango huendeshwa kwa ustaarabu na taratibu ndiyo maana hapo juu nilisema ukitaka mafanikio ya haraka haraka jaribu kuwa mwizi hata wizi wa kura ni wizi kitu ambacho vyama vya upinzani ikiwemo Chadema hawakifanyi
 
Luteni, Shalom,

CCM have seen teh bigger picture and it requires them to have full control of local government network and that is why they invest hevily on TAMISEMI to guarantee at least 60% seats on parliament!

Mmeshajiuliza kwa nini Mzee Malecela alizunguka nchi nzima 2004 kuirudisha iti ya TAMISEMI CCM? Jibu lake ni matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2005, kitu CCM wanachotambia kuwa ni ushindi wa Tsunami. Ni mvuto na ufuasi uliojijenga kwa wana CCM na Watanzania kwa ujumla kuona kuwa hakuna Chama chenye uwezo wala sera bali ni CCM.

Nikirudi kwa CHADEMA, wao wamekosa strategty waliofanya CUF ambayo ni kuhakikisha total dominance kwenye eneo fulani na kisha kuelekea maeneo yote. Mfano, CHADEMA ingejipanga vyema 2005, ingekuwa na 50% ya viti vya Ubunge kwa mikoa ya Dar, Tanga, Pwani, Kilimanjaro, Arusha, Mara na hata kudokoa 25% huko Mwanza, Shinyanga, Tabora na Morogoro.

CHADEMA ingekuwa na uhakika wa kuwa na Wabunge wa kuchaguliwa si chini ya 30 na si namba za sasa hivi ambapo ni finyu na kuwategemea kina KOmu wa viti maalum.

It is all about strategy and strong grass roots. CHADEMA kimekuwa in existance karibu miaka 20 sasa.

TANU hata kama mtasema ilikuwa TAA, bado iliweza kujijenga na kuchukua nchi katika kipindi cha chini ya miaka mitano kwa kuwa Wananchi walikuwa wamechoka kunyanyaswa.

Sasa kama leo hii bado tumechoshwa na unyongo, lakini hatuna imani na CHADEMA mtasemaje kuwa ni lazima CHADEMA kipewe miaka 50 ili kiweze kuaminika na ku[ewa dhamana ya kuongoza Tanzania?
 
Kishoka
If you dont see any change or development which has been done by opps parties since the introduction of multipartism in Tanzania then what is your opinion, should the existing parties quit and give up because they are useless OR.......
 
Kishoka
Ukitaka mafanikio ya haraka haraka jaribu wizi,
Lengo la chama cha siasa si kushinda uchaguzi peke yake lengo ni kuona yale unayoyataka yanatokea au kutekelezwa hata kabla ya kushinda uchaguzi, unaweza kushinda na kuingia madarakani ukashindwa ku deliver

CCM wako madarakani kwa muda mrefu wana resources nyingi wanamtandao mkubwa hadi vijijini kutaka kuilinganisha na Chadema ya juzi eti kwanini haikushinda TAMISEMI ni ufinyu wa kufikiria kutegemea kesho tu Chadema itande nchi nzima ni ndoto za alinacha kwa hiyo kupima matokeo ya TAMISEMI kati ya CCM na Chadema bila kuangalia hali halisi(reality) ni umasikini wa utafiti

Kishoka unaweza kuniambia mwaka 1994 Chadema ilikuwa inaongoza vijiji/mitaa na Halimashauri ngapi nafikiri ilikuwa haina hata kijiji, Halimashauri zote zilikuwa chini ya CCM tuambie hizo Halimashauri za Chadema na hiyo mitaa ya CUF imetoka wapi Kenya au ilikuwa ya ODM Kenya, sometimes tujifunze ku appreciate what opps parties are doing hata kama si kwa speed unayotaka wewe mipango huendeshwa kwa ustaarabu na taratibu ndiyo maana hapo juu nilisema ukitaka mafanikio ya haraka haraka jaribu kuwa mwizi hata wizi wa kura ni wizi kitu ambacho vyama vya upinzani ikiwemo Chadema hawakifanyi

Luteni,

NI ajabu njinsi ulivyoweza kuandika niliyotaka kuyaandika lakini nikashindwa kupangilia maneno kama ulivyo fanya. Labda kama Rev naye yupo kwenye kundi la watu wanaoamini kuwa ili CCJ ifanikiwe basi lazima wailipue Chadema lakini kama ni myu ambaye anataka maendeleo ya Chadema ni lazima amepata picture ya khali halisi.

Nikiwa ni mt niliyeshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa najua kuwa chadema walijitahidi sana kuweza kushinda na walikuwa busy sana lakini ni lazima tukubariane kuwa CCM imeinvest sana kwenye nnchi hii kiasi cha kuwa unapojipanga zaidi ndiyo unashindwa zaidi. CCM imeinvest kwenye ujinga wa watanzania kwa asilimia 100% wewe jaribu kufanya majadiriano na watu kuhusu siasa hata kwenye dala dala au basi la mkoa ndipo utakapo wavulia kofia Chadema kwa haya waliyoweza kuyafanya ukiwa Utah ama Leeds utabaki kusema tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom