Niombe Talaka?

Niombe Talaka?

Wee bi dada kuwa kiakili acha kulalamika lalamika tuu
nilishawaaambia nyie mwali wadogo mnashida sana, huwaga mnataka kuwa rula kwa waume zenu mkasahau nao ni binadamu wana akili na uwezo wao wa kufikiri..................

toka siku ya kanza ulipokuwa unatakana ulishajua kwamba hapa naenda kuish na mtu ambaye si mama wala baba wla si kaka yangu huyu ni mume na kuna changamoto za kuish nae sasa unapoanza kulalamika nakushangaa.

ivi kwan wewe hukutarajia mumeo awe jeuri? ama awe mbinafsi? kwanz ubinafsi ni sifa ya kiume, ukitaka uliza mtu yyte. Umewah kuona mtoto akilia mwanaume akasema lete nimbebe zaid ya kukwambia mpe nyonyo?

afu sijui na wewe umekulia wapi eti unakwenda kushtak ukwen ili iweje? unategema ndugu zake wakutetee wewe badala ya kaka/mtt wao?

ndoa ni kujipanga kiakili zaid na si kimapenzi zaid.
wewe ulizidiwa na nguvu ya kupenda ukasahaua kwamba mumeo anawez akukosea na ukashindw akuvumilia. haudumii familia yake ana hudumia ndguze si wew umwendekeza ukitaka kumwonyesha kwamba anaweza kutunza familia??

ulishakosea approach toka siku ya kwanza................

ushauri wangu kwako ni huu
1. punguza mdomo wa kusema sema na kubishana na mwanaume, manake siku zote ubishan huleta hasira na ndo mwanzo wa kuchezea mbata

2. jifunze kutumia silaha ya kike kwa mumeo, usimfanye kuwa adui yako wala simba ndani mfanye kuwa rafiki ivi mara ya mwisho kumwambia nakupenda mume wangu ni lini?

3. usione msaada anaotoa mumeo kwa ndguze ni makosa, ila ona kama ni jambo la maana ila sasa mtrain kucontribute kwenye maswala ya ndani

4. Sali na omba Mungu zaid kama mwislam nenda kwa mashehe wakusomee dua utoe na sadaka, ili ndoa yako iwe na aman. kama mkristo pia nenda kwa kanisan sali na toa sadaka

5. acha hasira zisizokuwa na sabb kisa mumeo haamki kukusaidia mtt unaona kakosea, wengine tulienda kujifungua weneywe hosp, unapak gari nje unaingia leba na kusukuma, mtu kalala home anakoroma na ukirudi unamwambia laaziz zawadi ya baby boy hiyooo. tena kwa busu zitoo as if ndo alokuja kukuchukua hosp kumbe umekodisha dereva akuendeshe kurudi home

6. acha mawazo potofu na kuona kwamba wewe ndio rula ya kumbadili mumeo, kwan wewe Mungu? let him live his own life kwan lazima kila unachotaka akufanyie afanye.

7. jifunze kua kuna me time na us time. sasa ikiwa ni me time let him enjoy it to the fullest, sio unaanza kumbughudhi

8. jogoo halei eeeh bibie, wee uliona wapi jogoo kalea, ulishawah kuskia weye? ama ng'ombe dume hunyonyesha? sas akama hapana basi na wewe jua malezi ni jukumu lako as mama akifanya kakusaidia tu

9. acha kufananisha maisha yako na ya wenzio, ikiwa kuna mashost wanakusimulia maisha yao wewe usijikompee na yako ishi maisha yako halis

10. taka kuona kila siku unafurahia ndoa yako kuliko mtu baki kukufanya uifurahie, play your part effectively manake ukifanya ivyo basi wewe utakuwa na 50% na yeye akifanya kwa uvivu kabisa akikupa 20% basi tayari ni -B so uko pazuri iyo 30% sio kitu.

11. acha utoto wa kushtak na kuianika ndoa yako kwenye vikao vya ukoo ndiko unakochota haya manuksi namamikosi. adui zako wanapenyezea apo apo na wanafurah sana ukipigika manake wnajihesabia ushindi.

12. ndoa sio gereza bibie, iyo ni taasisi inayounganishwa na upendo kama ukiona humpendi basi achia ngazi bila kutangaza nia.

samahan kama nitakuudhi kwa maneno yangu. na hzi bia za j2 hizi God forbid

Umeolewa? Make nakuja pm soon...! Right woman kabisa.
 
Kamwe siwezi kuona mtoto analia masaa mawili nami nisitoe ushirikiano katika kujaribu kumbembeleza mtoto. Halafu lijanaume pumbavu on top of that mkewe kachanganyikiwa kwa mtoto kulia masaa mawili badala ya kumsaidia mkewe linaenda kumzaba vibao eti kwa kuulizwa tu mbona hujali mtoto kulia masaa yote haya? Si kila mwanaume anastahili kuwa mume/baba. Mianaume mingine ndivyo ilivyo!!!

Naungana na wewe 100%haiwezekani nini maana ya kuitwa baba?swala la malezi kwa mtoto/watoto ni jukum la wote baba na mama,iweje mwanao analia mflulizo masaa mawili wewe umelala tu,huo usingizi utakuwepo kweli?kwana kama kweli huyo ni mwanao utajiskia vibaya,pili ni kero mean kelele bila kuambembeleza hapalaliki.
 
Yeye kuhudumia watoto hakufanyii favor, NI WAJIBU WAKE. Yani ufanye maamuzi ya fasta kumshurutisha atoe hizo hela. Huko Ustawi ulisaidiwaje? kama itakubidi uende mahakamani, UENDE.

hizo hela unazotoa pekeyako sasahivi zingeweza kukusaidia kuendelea na maisha yako. mtu ameshakwambia uhusiano umeisha. hajapata mwingine huyo? huna kazi hapo. au unaogopa maneno ya watu ya "ameachika"? atakayeachika hapo ni yeye ukiondoka hapo.

bora hata kama uhusiano ndani umeisha lakini anahudumia watoto, ungejishikisha hapo.

mtu hata anakupiga makofi?? na wewe ndo umemuomba msamaha?? watakuja kukwambia mke huivunja ndo yake kwa mikono yake. watakwambia hukuvumilia vya kutosha. HAKUNAA.. ni mfumo kandamizaji. hustahili yote hayo....

najua ukifikiria kuanza maisha yako pekeyako na watoto wako unaogopa. sasa ukaeee ufikirie mwenyewe utafanyaje.

Sipati picha we ndio ungekuwa housegirl wake!!::
 
Huuu use.nge wa big secret unawafanya watu wengi wanaishi katika mateso eti kisa secret. Sijui uvumilivu my foot..
Koh koh koh!
Ikishindikana saga mjusi

Yule mweupe hapana namuogopa sana kwa kweli..
 
so the extra marrital affairs are due to feminism??? have the occurences of extramarital affairs actually increased or have people (especially women) just gotten the power to not put up with it anymore??

watu wanaona sifa kusema "ndoa ya miaka 50". doesnt matter huyo mwanamke alikuwa anachezea kipigo miaka 50. doesnt matter mumewe alikuwa **** nje miaka 50. all it matters ni ndoa imekaa miaka 50.

Mwenyewe mama yangu anaenda miaka 35 ya ndoa. maisha yangu yote nimeshuhudia mama akipigwa na kugombezwa na baba. amd shes a very polite woman by nature. ni kwamba hata simuonei huruma tena whether anapigwa au lah kwasababu nishamwambia hastahili yote hayo. excuse ya kuwa yuko pale kwaajili ya watoto is invalid.

miaka yoote kuinamisha kichwa tuu...kunyamaza tuu....kuwa mpole tuu...hudumia mwanaume tuu...mwanaume asiye na shukrani....halafu mbele za watu utafkiri sio wenyewe. NILIKUWA NAKEREKA.

sasa dawa yao ni kusubiri wazeeke, tuwatengahishe.

BULLSHIT. Me nasema, na zivunjwe tu, manake hakuna namna nyingine.

Mkuu unajua mimi nashindwa kuelewa binadam tumeumbwa vip hivi mtu kukuuliza kwa nini umelala mtoto analia mda mrefu hautoi ushirikiano ni sababu ya kumpiga?Then mtu hahudumii familia yake especially watoto wake,watu hum wanatoa povu kumtetea hiv inawezekana?lakini pia unajiskia vp unapomgeuza binadam mwenzako kama punda wa kubeba mizigo yako yote na kipigo juu?how do you feel?how can you enjoy love&sex with a person who always you makes her sad? Je ulisha jiuliza kuwa kwa yote unayomfanyia anaenjoy kufanya mapenzi na wewe?anafurahi na kuwa na amani wakati mnapokuwa faragha kama hamna basi hakuna mwanauma hapo ila na mbakaji.
 
Ahsante sana Mkuu kuna baadhi ya wanaume hawajitambui kabisa inapokuja kwenye haya maswala.

Naungana na wewe 100%haiwezekani nini maana ya kuitwa baba?swala la malezi kwa mtoto/watoto ni jukum la wote baba na mama,iweje mwanao analia mflulizo masaa mawili wewe umelala tu,huo usingizi utakuwepo kweli?kwana kama kweli huyo ni mwanao utajiskia vibaya,pili ni kero mean kelele bila kuambembeleza hapalaliki.
 
Hi,

Iam a mother of 2kids, usiku mmoja mtoto wetu mchanga alilia sana 4 2hrs, ajabu babae kaangalia 2, nikamuuliza kwanini hana huruma kiasi hicho? Mwanae analia hajali anamaanisha nini? hadi mtoto mkubwa(3yrs) aliamka, alinyanyuka kitandani, akaninyakua mtoto akamweka kitandani kisha akanizaba makofi nikaweweseka, nakulia sana, kwahasira nikamwambia naweza nikakuachia mtoto kitandani nikalale sebuleni.

Akaniambia ondoka uone kama sitaweza, roho iliniuma maana mtoto anahitaji msaada yeye analeta ugomvi, tukajibishana usiku huo, sasa ni 2weeks hakuna mawasiliano, nimemwomba anisamehe uenda mi ndio mkosaji, kaniambia tuendelee kulea tu watoto ila mahusiano yetu basi, nikishindwa niondoke.

Sio mlevi nimkorofi, mbinafsi nambishi, kibaya zaidi watoto nahudumia mwenyewe 90% yeye anahudumia nduguze tu, nikilalamika anadai nawachukia nduguze, nifanyeje? Nishamshitakia sana kwa Wakwe kwamambo mengi hadi naona nawakera siishi kumlalamikia kijana wao, Wakwe wanashauri nimvumilie tu eti nimkorofi, je nikae tu kama house keeper?


kwa waislamu hiyo inahesabika kama talaka moja kitendo cha mwanaume kutamka "uhusiano wetu umeisha" tu.


mtazamo wangu

katika biblia kuna sheria inasema "wanaume wapendeni wake zenu na wanawake watiini waume zenu" hili halina short cut.

kiukweli haiwezekani kwa mwanaume masaa mawili mtoto analia tu halafu asijiguse, lazima kuna kitu hapa kimefichwa kimetokea kabla ya mtoto Kuanza kulia, vinginevyo huyo mume ni kichaa.... ila pia pamoja na hayo angalia kauli iliyotumika muone imekaaje, "kwanini huna huruma kiasi hicho?"

kwa mwanamke "mtiifu" kauli nyepesi tu hapa ingemshughulisha huyo mwanaume mfano "mume wangu naomba nisaidie simuelewi mwanetu" simple! wallahi angekupiga hapa angekuwa chizi... lakini jiangalie umemfanya nini kabla halafu angalia na kauli uliyotumia.

siafiki hata kidogo suala la kudundana, ila sasa kuna wanaume hawawezi kujizuia kupiga, keshakuwa mumeo ushamjua, tumia maneno malaini hayo mengine yatajiseti yenyewe tu.

Mtii mumeo, atabadilika na atafanya kila kitu na utaona utamu wa ndoa In sha Allah.
 
Omba tuu haina shida. Mana ndo utashi wako ulipoishia nyie ndio mnaoingia kwenye ndoa mkengemkenge kwa kuhadithiwa na mashoga zenu, upande mmoja wa shilingi bila na ww kuongeza zako kujua upande mwingine. Nb ndoa ni zaidi shahada ya uzamivu au masters.
 
dah kiukweli hii taasisi ya ndoa inahitaji misuli ya imani....bila Mungu haiendi
 
mtoto alilia kwa masaa 4 how and why ??? wewe ulikuwa wapi
unaposema anaangalia unamaanisha nini????
kama unahudumia wanao kwa asilomia 90 huyu baba yao wa .nini au dushe tamu maana huna haja nae
sepa akaoe dada zake... maana anahisi wao ndo wamaana na wakat hata vitabu vitakatifu vinasema utaacha baba na mamako umfate mke au mumeo..... sasa yeye kwenye kundi hili hayupo chapa kandambili maee jipange
 
Utoto unahusika hapa mkae pamoja myazungumze na muweke bayana jinsi ya kutumia kipato chenu kwa manufaa ya familia. Nahisi mke umeongelea upande mmoja hata mwenzio anaona mapungufu yako. Sioni tatizo kwenye ndoa yenu zaidi ya utoto na mke kukurupuka badala ya ku solve matatizo ya ndani kwa busara
 
mtoto alilia kwa masaa 4 how and why ??? wewe ulikuwa wapi
unaposema anaangalia unamaanisha nini????
kama unahudumia wanao kwa asilomia 90 huyu baba yao wa .nini au dushe tamu maana huna haja nae
sepa akaoe dada zake... maana anahisi wao ndo wamaana na wakat hata vitabu vitakatifu vinasema utaacha baba na mamako umfate mke au mumeo..... sasa yeye kwenye kundi hili hayupo chapa kandambili maee jipange


umejuaje ana dada?
 
Ushauri wa JF huwa unachanganya Sana,wengine wanasema achana,wengine vumilia,Yale yale kati ya mvua na jua kipi bora....ushauri wa JF sometimes unachanganya mno.
 
Pole sana kwa masaibu yanayokukuta, mazingira yanaonyesha mume wako ana moyo mgumu, moyo baridi na kifuani amejaa visasi. Kuna uwezekano mkubwa yanayotokea na kuongea ni madogo kuliko chuki na uovu uliojaa kifuani pake.
 
Back
Top Bottom