Nioe au nijenge kwanza?!

Nioe au nijenge kwanza?!

Usithubutu kujenga Wala kuoa, kwanza nakushauri uuze hicho kiwanja uende kitambaa Cheupe ukale Bata maisha mafupi haya.

Unasema story za kujenga vipi Kama ukienda kununua bati afu kwa bahati mbaya zikakukata ukaumia utamlaumu Nani? Achana na hizo mambo we kula Bata life is too short.
Daah umenifany nicheke kweeeel yaaan!
 
Umri wako huo kibongobongo ukiingia kwenye NDOA Kuna changamoto utazipata, Fanya maendeleo Kwanza mf Jenga Kwanza utaona tu NDOA hiyo hapo

Achana na Hao wazushi wanasema eti oa Kwanza na milango ya baraka itafunguliwa, baraka zipi hizo zinatokana na NDOA?

Wakupe mifano ya watu walipooa tu basi wakajenga majumba ya kifahari na sio kupanga tofali,

Baada ya kuoa tu, basi wakaweza Kununua mandinga Kama ma BMW na Mercedes Benz brand new kutokana na baraka za NDOA
Aminaaa,,,ntalifanyia kazi mkuu maana kweli ukijenga Uhuru unakuwepo
 
Jenga kwanza Ili mke aje akute una nyumba,mkizinguana anasepa peke yake.Lakini ukisema uoe halafu uje kujenga,mkizinguana atadai mlijenga wote na nyumba ipigwe bei mgawane pesa.Ndio ishu ambayo imenikuta Mimi,inanitesa mbaya sana.
Umenifumbua macho aisee
 
Unaishi peke yako ila unataka kujenga coz unapata uchungu kwa kuona kua kodi unayolipa unamfaidisha mwenye Nyumba tu,

Halafu unatuuliza Ujenge au uoe kwanza? Serious? Kwani ukioa huo uchungu wa kodi unayolipa utaisha?

Jenga kwanza ili umalize uchungu wa kulipa kodi,ama sivyo utajikuta una uchungu wa mambo mawili kwa pamoja,uchungu wa ndoa na uchungu wa kulipa kodi.
 
Wapendwa Habari za wakati huu!!
MUNGU ni mwema anazidi kutupigania siku zote.
Sifa na utukufu vimrudie yeye

Kuna kitu naomba ushauri wenu wapendwa katika hili, nipo na umri miaka 27 sijaoa na wala sina mchumba nipo nimepanga ,, MUNGU kanisaidia katika kupambana katika kazi huku na kule nimefanikiwa kupata kiwanja japo ni kidogo lakini cha kuanzia maisha,
Niliwaza saana kuhusu kodi ninazo mpa mwenye nyumba nikapata uchungu hapa namfaidisha mwenye nyumba japo naishi kwake,,Basi ndo hivyo MUNGU akanijalia kwa mapenzi yake.

MSAADA:
Nimewaza na kuwazua kati ya haya mawili lipi litangulie,,japo sina kipato kikubwa saaana cha kusema naweza kufanya kati ya kimoja wapo kwa mkupuo hapana bali ni kujichanga taratibu maaana ni mimi kama mimi najitagemea.
Na mnavyojua ujenzi ni taratibu na hasa kama kipato ni cha kuunga

Je, wakuu niendelee kupambana tu ili nijenge hata chumba kimoja cha kuanzia ama nioe kabla sijajenga?

Ushauri wenu wakuu ili nifanye maamuzi sahihi kwanza.
MUNGU awabariki!
Sijasoma content.
Ila kwa kutumia title ya bandiko lako, nakushauri Kama unaweza kujenga kwanza fanya hivyo.
 
YANI JENGAA UMALIZEEE MKUUU... ila ubaya siku mkiachana na mkeo kugawana mali ndo rohoo itaumaaa balaaa
 
Back
Top Bottom