Ninunue kipi gari au nijenge nyumba?

Ninunue kipi gari au nijenge nyumba?

Habari vipi wakuu,

Najua katika maisha ya vijana hua kuna mitazamo tofauti ya mfumo wa maisha mtu atakavyo kuishi sina nyumba naishi nimepanga hapa Dar, lakini nina kiwanja Mbezi.

Mpango wangu ninunue gari MUNGU akisaidia mbeleni nitajenga tuu sasa hili suala la kutangulia kununua gari kabla ya kujenga, baadhi ya watu wameanza kuona eti napotea njia, wananiona sasa nimeanza kuchanganyikiwa.

Ushauri wenu wana JF ninunue gari au nitangulie kujenga nyumba.

NB: Endapo nitanunua gari kipato changu kitaongezeka Mara 2 ya nilichokua napata kwa mwezi
 
Mimi huwa naamini kwenye kuongeza thamani, kama kwel ukinunua gari kipato chako kitaongezeka basi nunua gari after 2yrs utajenga nyumba nzuri zaid ya uliotaka kujenga now.
 
Una familia au uko single.Kama una familia inabidi uanze na nyumba gari baadae.Kama uko single unaweza kuanza na usafiri nyumba baadae.Gari siyo asset gari ni liability lazima uilipie mafuta,vipuri,tochi za trafiki nk.Nyumba >Gari.
 
Una familia au uko single.Kama una familia inabidi uanze na nyumba gari baadae.Kama uko single unaweza kuanza na usafiri nyumba baadae.Gari siyo asset gari ni liability lazima uilipie mafuta,vipuri,tochi za trafiki nk.Nyumba >Gari.
Naishi singo sijaoa mkuu
 
Mimi huwa naamini kwenye kuongeza thamani, kama kwel ukinunua gari kipato chako kitaongezeka basi nunua gari after 2yrs utajenga nyumba nzuri zaid ya uliotaka kujenga now.
Sankc bro
 
nunua ka vitz tu mana nalo ni gari, jenga nyumba then baadae uje ununue gari la maana.
 
Mtu hajasema ana shilingi ngapi...mnaanzaje kumshauri ajenge Nyumba? Kujenga ''Nyumba'' mpaka iishe si mchezo, unless unataka kujenga ''kibanda'' tu.

Kwa kuwa amesema akinunua gari kipato chake kinaongezeka twice as much, assumptions hapa ni kwamba hataki kununua gari la starehe, bali ananunua la kufanyia biashara (bus, tipper, canter, etc). Nigekuwa ni mimi ningenunua Gari kwanza then ile additional income ningeanza kuichanga mdogomdogo na kuanza kujenga Nyumba taratibu
 
Nilikopa bank nikanunua gari...nikakaa nikaona gari inanipoteza service si mchezo ingawaje gari ina heshima yake.

Baadae nikakaa nikapiga hesabu, naishi nyumba ya kupanga, gari nalaza barazani (nyumba haina fence).

Nikaona ni vema na busara kuwa na nyumba kwanza. Nikauza gari, nikanunua kiwanja ndani ya mwezi mmoja nikahamia kwangu.

Though nyumba bado haina umeme but maisha ya nyumba yako mwenyewe ni mazuri sana.
Ukizingatia nimeoa, nakushauri jenga achana na magari.

Utanunua gari kwa bahati mbaya siku unaingia barabarani tu inagongwa. Sina maana nyumba hazina risk lahasha
 
Nilikopa bank nikanunua gari...nikakaa nikaona gari inanipoteza service si mchezo ingawaje gari ina heshima yake.

Baadae nikakaa nikapiga hesabu, naishi nyumba ya kupanga, gari nalaza barazani (nyumba haina fence).

Nikaona ni vema na busara kuwa na nyumba kwanza. Nikauza gari, nikanunua kiwanja ndani ya mwezi mmoja nikahamia kwangu.

Though nyumba bado haina umeme but maisha ya nyumba yako mwenyewe ni mazuri sana.
Ukizingatia nimeoa, nakushauri jenga achana na magari.

Utanunua gari kwa bahati mbaya siku unaingia barabarani tu inagongwa. Sina maana nyumba hazina risk lahasha
Asante mkuu
 
15 million unapata gari, kujenga hiyo same amount utapata kiwanja , say 7million plus materials kama mchanga , kokoto na tofali. So ujenzi wa nyumba unahitaji mara mbili au tatu ya pesa ya gari.vinginevyo itakuchukua mila Madhya kukamilisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom