Ninunue kipi gari au nijenge nyumba?

Ninunue kipi gari au nijenge nyumba?

mkuu kwani ushawahi Kulala nje kisa huna nyumba ya Kulala hapa jibu ni lazima hapana.

Ila ni mara ngapi ushatembea na miguu umbali mrefu kisa huna gari....ukicheki hapo utaona kabisa kuwa umeteseka mara nyingi kwa kutokuwa na gari kuliko kwa kutokuwa na nyumba.

Wakati ndio huu fanya maamuzi ya busara jenga heshima mjini.
 
Mkuu umetisha .....nimechukua ushaur
 
Km unamaanisha kweli kipato chako kitaongezeka mara mbili bas, nunua hio Gar, Ila kumbuka aset ya Gar na nyumb n vitu viwil tofaut sana, Binafsi siwez anza maisha kwa kununua Gar km Gharama za Gar na nyumba ni sawa,
 
Nenda kawekeze kwenye betting after 1 week utakuwa ushapata pesa zote za nyumba na gari kwa wakat mmoja
 
Habar VIP wakuu....najua ktk maisha ya vijana hua kuna mitazamo tofauti ya mfumo Wa maisha mtu atakavyo kuishi ...
Sina nyumba naish nimepanga hapa dar,lakini Nina kiwanja mbez..

Mpango wangu ninunue gar..MUNGU akisaidia mbeleni nitajenga tuu....sasa hili suala LA kutangulia kununua gar kabla ya kujenga,,baadh ya watu wameanza kuona et napotea njia,,wananiona sasa nimeanza kuchanganyikiwa....

Ushauli wenu wana JF......ninunue gar? Au nitangulie kujenga nyumba.
NB: endapo nitanunua gar ..kipato changu kitaongezeka Mara 2 ya nilichokua napata kwa mwez..
Panda mwendokasi, jenga nyumba, kama ni gari ya biashara na kweli kipato chako kitaobgezeka na kiwanja unacho basi hapa NUNUA GARI!
 
Nunua gari,,ndio nyenzo ya kazi vile vile,nyumba kwan sasa hiv unalala nje?? Halaf umenikera eti watu wanakuona utapotea kwan unaishi ili watu wakuone unachofanya? Au unaishi kwa kanuni zao,,au watakuchangia mafuta au bati ukijenga,,hela zako mwnyewe nunua gar utembee kwa kukaa hapa mjini,,nyumba utajenga tu maana anaenunua gar n mwepes kujenga kuliko anaejenga anunue gar..
 
"Ukiwa na gari utakuwa na kipato mara mbili zaidi ya kipato ulicho nacho kwa sasa" that's means kwamba gari unayotaka kuinunua siyo ya kuuzia sura kama wengi wetu ambavyo tumekuwa tukifanya, hata hao wanaokwambia unapotea hawaelewi mipango yako ndo maana wanasema unapotea. Wewe fanya kama ulivyo panga kufanya usirudishwe nyuma wala kukatishwa tamaa na ngonjera za watu wewe songa mbele fanya kile unachokiamini na si unacho ambiwa na watu, kwa sababu mustakabari wa maisha yako uko mikononi mwako na si kwa mtu mwingine.
 
Nunua gari,,ndio nyenzo ya kazi vile vile,nyumba kwan sasa hiv unalala nje?? Halaf umenikera eti watu wanakuona utapotea kwan unaishi ili watu wakuone unachofanya? Au unaishi kwa kanuni zao,,au watakuchangia mafuta au bati ukijenga,,hela zako mwnyewe nunua gar utembee kwa kukaa hapa mjini,,nyumba utajenga tu maana anaenunua gar n mwepes kujenga kuliko anaejenga anunue gar..
Nashukuru kwa ushaur mkuu
 
Mkuu umetisha .....nimechukua ushaur
Kitu nikionacho hapa ni umeleta uzi ila tayari uneshafanya maamuzi na tayari umeshachagua comments za kupenda na za kutokupenda, fata maamuzi yako mkuu!
Gari linahudumiwana ila nyumba inahudumia!
 
Kama hela ya gari inamaliza Nyumba uamie, jenga, ila kama hela ya gari inapeleka nyumba mpaka lenta, then nunua gari, halafu hela ambazo ungetumia kujenga kuanzia lenta utaanza msingi!
 
Nakushauri nunua gari la biashara au kama hela haitoshi nunua. Bajaji ili ile hela iwe inazunguka uweke kidogo kidogo mpaka utaweza kununua gari lingine na pia ukajenga nyumba. Ila ukikurpuka ukanunua gari ya starehe. Haina tofauti na kufuga mbwa wakati upo kwenye nyumba ya kupanga.
 
Sasa gari kama.hilo la kuanzia maisha litakuwa labda 10 mpaka 15m wakati nyumba itachukua labda 100m. Pia nyumba unajenga kwa muda mrefu wakati gari ni siku moja unanunua.

Ninao wafahamu wengi walinunua magari wakawa 'comfortble' na mizunguko yao ya kila siku kisha wakajenga miaka hata m3 au mi5 baadae. Hivi wahindi wanajengaga kweli ila wote wana magari mazuri lakini wamepanga nhc tu mpaka kesho.

Kama gari ni hitaji anza nalo hutojuta na hata wakati wa ujenzi inakuwa rahisi kufuatilia. Kujenga ni gharama kubwa tofauti na kununua gari.
 
"Ukiwa na gari utakuwa na kipato mara mbili zaidi ya kipato ulicho nacho kwa sasa" that's means kwamba gari unayotaka kuinunua siyo ya kuuzia sura kama wengi wetu ambavyo tumekuwa tukifanya, hata hao wanaokwambia unapotea hawaelewi mipango yako ndo maana wanasema unapotea. Wewe fanya kama ulivyo panga kufanya usirudishwe nyuma wala kukatishwa tamaa na ngonjera za watu wewe songa mbele fanya kile unachokiamini na si unacho ambiwa na watu, kwa sababu mustakabari wa maisha yako uko mikononi mwako na si kwa mtu mwingine.
Nimepokea ushaur wako
 
Km unamaanisha kweli kipato chako kitaongezeka mara mbili bas, nunua hio Gar, Ila kumbuka aset ya Gar na nyumb n vitu viwil tofaut sana, Binafsi siwez anza maisha kwa kununua Gar km Gharama za Gar na nyumba ni sawa,
Asante kwa ushaur
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom