Nini tiba ya tatizo la kutokwa na damu puani?

machiaveli

JF-Expert Member
Jun 4, 2016
1,883
3,930
Rafiki yangu ana umri 35 ana tatizo la kutokwa na damu puani zaidi ya miaka 10,tatizo lilianza kipindi ameanza kazi ya fundi wa ujenzi!

Tatizo lake ni kwamba Kila aamkapo asubuhi wakati ana anawa uso damu zinatoka puani, wakati mwingine wakati amekaa tu damu zinatiririka!!

Naombeni msaada wenu madaktari
 
Mwambie achukue mwiba wa nungunugu awe anachoma ule moshi wake sasa uwe unaunusa au uwe uningia puani itakata fasta na kitendo hiki kifanyike mara baada ya damu kutoka au inaweza ikawa inatoka ukujipanguza ndo unafanya hicho kitendo itakuwa tiba yake hiyo.
 
Rafiki yangu ana umri 35 ana tatizo la kutokwa na damu puani zaidi ya miaka 10,tatizo lilianza kipindi ameanza kazi ya fundi wa ujenzi!

Tatizo lake ni kwamba Kila aamkapo asubuhi wakati ana anawa uso damu zinatoka puani, wakati mwingine wakati amekaa tu damu zinatiririka!!

Naombeni msaada wenu madaktari
Kama Tatizo lina Miaka 10,Mwambie aende Hospitali na Ikiwezekana Akacheck CT scan ya kichwa..

.Maana nina uhakika Tatizo huenda sio mishipa ya pua Huenda anaweza kuwa na Uvimbe kichwani au hata cancer aende apime CT Scan au MRI kuangalia Kichwa lakini pia ikiwezekana apime Carcinogenic properties
 
Mimi nilikuwa na tatizo hilo wakati niko mdogo,walikuwa wanasemaga ninadamu nyingi.

Na nilikuwa nasumbuliwa na kichwa kuuma sana,kwa sasa sina tatizo kabisa,na nina miaka mingi sana sijaumwa kichwa.
 
Kama Tatizo lina Miaka 10,Mwambie aende Hospitali na Ikiwezekana Akacheck CT scan ya kichwa..

.Maana nina uhakika Tatizo huenda sio mishipa ya pua Huenda anaweza kuwa na Uvimbe kichwani au hata cancer aende apime CT Scan au MRI kuangalia Kichwa lakini pia ikiwezekana apime Carcinogenic properties
Uvimbe ama cancer naweza nkaenda mbali kidogo na wewe boss.........kwasababu kama Kuna uvimbe why damu inatoka mda mmoja tuu?,na kama Kuna cancer(malignant)why damu inatoka mara moja tuuh (yaani akiwa ananawa uso)



Anyway Kwa kazi yake nahisi anakuwa anakuwa anakaa sana juani kipindi Cha mchana,so mishipa inakuwa inatanuka na damu inakuwa inapita Kwa kazi juu ya uso wa ngozi na muda wa kupumzika mishipa ya damu inakuwa imerelax sasa unapoweka maji unaishawishi mishipa iamke sasa Ile kuamka inapelekea baadhi ya capillaries kupasuka ndivyo damu unapoanza kutoka


Reason ya pili aangalie vyakula anavyokula kama ni vyachumvi nyingi ajitahidi kupunguza


Pia kitu Cha mwisho CT scan for head vessels kucheki kama kitakuwa na infections ama vipi lakini awe anakumbukumbu ya ajali alizozipata akiwa kazini kabla ya kwenda CT scan
 
Kuna watu wengne kutoka damu puani ni urithi nina friend pia yeye na bro wake wote damu huwa znatoka puan mda wowote....japo gambe tunapiga sanaa.....
 
Uvimbe ama cancer naweza nkaenda mbali kidogo na wewe boss.........kwasababu kama Kuna uvimbe why damu inatoka mda mmoja tuu?,na kama Kuna cancer(malignant)why damu inatoka mara moja tuuh (yaani akiwa ananawa uso)



Anyway Kwa kazi yake nahisi anakuwa anakuwa anakaa sana juani kipindi Cha mchana,so mishipa inakuwa inatanuka na damu inakuwa inapita Kwa kazi juu ya uso wa ngozi na muda wa kupumzika mishipa ya damu inakuwa imerelax sasa unapoweka maji unaishawishi mishipa iamke sasa Ile kuamka inapelekea baadhi ya capillaries kupasuka ndivyo damu unapoanza kutoka


Reason ya pili aangalie vyakula anavyokula kama ni vyachumvi nyingi ajitahidi kupunguza


Pia kitu Cha mwisho CT scan for head vessels kucheki kama kitakuwa na infections ama vipi lakini awe anakumbukumbu ya ajali alizozipata akiwa kazini kabla ya kwenda CT scan
Nimenda hii Sasa hawezi kuzuia hili tatizo kwa muda ama Moja kwa Moja mpaka aka CT scan
 
Rafiki yangu ana umri 35 ana tatizo la kutokwa na damu puani zaidi ya miaka 10,tatizo lilianza kipindi ameanza kazi ya fundi wa ujenzi!

Tatizo lake ni kwamba Kila aamkapo asubuhi wakati ana anawa uso damu zinatoka puani, wakati mwingine wakati amekaa tu damu zinatiririka!!

Naombeni msaada wenu madaktari
Nilizaliwa na Tatizo la kutoka na damu puani ila sasa halipo tena tangu 2009/2010 -2023.
1. Nikitembea kwenye jua kali nilikuwa lazima nitoke damu puani
2. Nikiumwa lazima nitoke damu puani au nikianza kupona, damu ilikuwa inatoka puani tena inatoka nyingi sana mpk unalowanisha kitambaa, unaweka kwenye paji la uso huku umelala chali. Ilinitesa sana maana shuka, nguo zilichafuka damu.
Nakumbuka mwaka 2009 au 2010 sina kumbukumbu vizuri ila mwaka mojawapo.
Kulikuwa kuna mahubiri ya walokole, wanahubiri. Sasa baada ya mahubiri, wakasema walio na shida mbalimbali waje mbele. Yesu kristo wa nazaleti aliye hai yupo hapa, atatenda miujiza. Nikapita mbele, nikaombewa tena nakumbuka alinishika mkono kichwani huku kimoyomoyo nami nakemea kuhusu tatizo la kutoka damu puani.
Nilivyotoka pale kwenye mahubiri 2009/2010 tangu sasa hivi 2023 sijawahi kutokwa na damu puani. Natembea juani, naumwa lkn sijawahi tena kutoka damu puani.
 
Uvimbe ama cancer naweza nkaenda mbali kidogo na wewe boss.........kwasababu kama Kuna uvimbe why damu inatoka mda mmoja tuu?,na kama Kuna cancer(malignant)why damu inatoka mara moja tuuh (yaani akiwa ananawa uso)
Chief umesoma Hx yake vizuri kuna vipengele ulitakiwa kuviangalia sana..Nahisi umevi-over look check hapa chini...
Rafiki yangu ana umri 35 ana tatizo la kutokwa na damu puani zaidi ya miaka 10,tatizo lilianza kipindi ameanza kazi ya fundi wa ujenzi!

Tatizo lake ni kwamba Kila aamkapo asubuhi wakati ana anawa uso damu zinatoka puani, wakati mwingine wakati amekaa tu damu zinatiririka!!
  • Ntaanza na Damu puani Zaidi ya miaka 10
Chief huoni kwamba this Chronic Epistaxis no matter which aetiology mgonjwa atakayosema unatakiwa kuichukulia Kama red flag kutokana n duration yake..

Na kwa maelezo yake kuwa damu damu inatoka akinawa na pia akiwa amekaa tu huoni kama kuwa uwezekano mkubwa kuna pressure inaongezeka kwenye
Kiesselbach’s plexus ndo inayofnya Damu itoke nje ya nasal septum..

Na pressure hiyo huenda inaweza kusababishwa na kazi yake kama ulivyosema lakini hata uvimbe iwe ni malignant au ni benign kama Polyp (Nasal polyp) also other neoplastic kama hemangioma, hemangiopericytoma, nasal papilloma, pyogenic granuloma, angiofibroma na hata carcinoma kama nilivyosema awali yote hiyo imetokana na duration ya Epistaxis

Na aliposema alipoanza kazi ya Ujenzi maybe it was caused by chemical irritant but haiwez kudumu kwa zaidi ya miaka kumi unless its recurent Irritation from chemical

Nimemuona RO7 ZA MGOS Alivyocomments hapo naomba kusema pia kasema kweli kabisa kuna matatizo ya kutoka damu husababishwa na kiukoo pia na kitaalamu huitwa Hereditary hemorrhagic telangiectasias "HHT" ambayo pia unaweza ukaita Osler-Weber-Rendu syndrome..

lakini kuna vitu vingi ukiacha nilivyotaja hapo juu vinaweza kusababisha Damu puani...
kama irritant chemical,Platelets disorder na pia hata mazingira kama jua,Homa ambavyo vingine husababisha kupanda kwa pressure ya ndani ya pua etc..

na ndo maana nikashauri aende hospital wakampime mpaka viashiria vya Cancer (carcinogenic properties) ila pia Afanye CT sinus Na ikiwezekana hata MRI Sinus...(Japo Ct scan for Head vessel sijawahi kuiona)

Na vipimo not always kucomfirm the Dx (Diagnosis) but hata ku "rul out" the Thought aetiology..
Tuwe na safe side katika Kutibu ili isije ikwa Multidx na tukam-miss Mgonjw

na kama atafanya examination ya nasal endoscopy wanaweza wakajua kipi ni shida...
 
Back
Top Bottom