Nini tafsiri ya Serikali inapoogopa kuangushwa kwa maandamano?

Criterion

JF-Expert Member
Jan 8, 2008
11,798
11,881
Ninaomba tujadiliane kwa hoja na umakini mkubwa.

Serikail yetu imejibainishwa kupendwa na kuungwa mkono na Watanzania asiliamia kubwa kama siyo wote. Serikali hii inaundwa na chama kinachopendwa na kukubalika kila mahala ndani na nje ya nchi kiasi kwamba katika kila chaguzi, chama hiki kimekuwa kikishinda kwa asilimia za juu kwa wastani wa 80%.

Kwa nini sasa inakuwa na hofu ya kuangushwa na watu wachache tu wasioichagua ambao hata si zaidi ya 20%? Ninasema hivi kwa mshangao kwa nini nguvu kubwa mno zitumike kuwazuia hawa wachache wasiokuwa hata na silaha wala influence kufanya mikutano yao?

Zaidi sana kumekuwa na sintofahamu kubwa inayoonyeshwa na hofu za viongozi wa hii serikali pale wanaposikia kuna watu wanataka kuandamana kwa amani ili kufikisha ujumbe wao kwa masuala wanayohitaji yafanyiwe kazi. Hii hofu na taharuki inatoka wapi? Kwa nini serikali isitumie jehsi la polisi kusimamia usalama wa hayo maandamano ili yafanyikie kwa amani ? Hizo nguvu za kuua waandamanaji, zisingezaa matunda mema na ya amani kama zingelitumika kulinda usalama wa hao waandamanaji na wadau wengine pasipo kufanya mauaji?

Inakuwaje serikali pendwa inaogopa maandamano na mikutano ya hao 20% ambao wala hawawezi kufanya hatari yoyote?

Zaidi sana ninaomba tujadiliane hii dhana ya kutafsiri kwamba maandamano ya amani ni mapinduzi, inatoka wapi? Kuna kivuli kibaya kinacholeta ndoto mbaya zinazoopelekea watu wakimbie usingizini pasipo sababu?

Ninatamani viongozi wa nchi yangu, wangekubali kuongoza kwa kufuata katiba ya nchi, kuwaruhusu wanaotaka kuandamana waandamane ili mradi hawafanyi fujo, iwaruhusu watu wakusanyike kwenye mikutano ya siasa kama chama kilichopo madarakani kinavyofanya ili mradi hawavunji sheria. Serikai iendelee na kufanya maendeleo ya taifa bila matusi, ubaguzi, na kitu kinatiwa unyanyasi wa ki itikadi na kuimarisha uhusiano wa viongozi na watu wa kawaida.


Nini maoni yako?
 
Serikali ambayo kila kukicha madiwani wa upinzani wanajiuzulu ili kuunga mkono Mwenyekiti wa ccm , hofu iko wapi ?

Hilo ndilo swali kubwa. Nchi nzima, kuanzia watu binafsi, vyombo vyote vya habari, vionogzi wote na watu wa vyama mbali mbali na serikali kila kukichwa wanaonyesha mioyo ya dhati ya kuunga mkono serikali na chama chake. Hakuna anayelalamika, maisha ni bora, uongozi safi, demokrasia iko juu, Hofu hiyo inaatokana na nini?

Kuna ugumu gani wa kuwasikiliza hao wachache wasiofika hata 20%, na kuwpa haki zao za kikatiba za kuwalinda na kuwapa uhuru wa kusema, kisha wakajibiwa tu kistaarabu badala ya kuwaua?

Tunahitaji kuelekezana. Yawezekana kuna kitu hakijaeleweka.
 
Hilo ndilo swali kubwa. Nchi nzima, kuanzia watu binafsi, vyombo vyote vya habari, vionogzi wote na watu wa vyama mbali mbali na serikali kila kukichwa wanaonyesha mioyo ya dhati ya kuunga mkono serikali na chama chake. Hakuna anayelalamika, maisha ni bora, uongozi safi, demokrasia iko juu, Hofu hiyo inaatokana na nini?

Kuna ugumu gani wa kuwasikiliza hao wachache wasiofika hata 20%, na kuwpa haki zao za kikatiba za kuwalinda na kuwapa uhuru wa kusema, kisha wakajibiwa tu kistaarabu badala ya kuwaua?

Tunahitaji kuelekezana. Yawezekana kuna kitu hakijaeleweka.
Bila Polisi ccm ni wepesi kuliko pamba .
 
Nadhani ni zile figisu za NEC na wizi wa kura kuna mfanya mtawala wetu asijismini sana.
Tofauti kati yake na mshindani wake kwa hesabu za NEC ni million mbili tuu hivyo anajua kuna watu zaidi ya million sita hawa mtaki ndio sababu ya woga na hofu yake na wafuasi wake.
 
Ninaomba tujadiliane kwa hoja na umakini mkubwa.

Serikail yetu imejibainishwa kupendwa na kuungwa mkono na Watanzania asiliamia kubwa kama siyo wote. Serikali hii inaundwa na chama kinachopendwa na kukubalika kila mahala ndani na nje ya nchi kiasi kwamba katika kila chaguzi, chama hiki kimekuwa kikishinda kwa asilimia za juu kwa wastani wa 80%.

Kwa nini sasa inakuwa na hofu ya kuangushwa na watu wachache tu wasioichagua ambao hata si zaidi ya 20%? Ninasema hivi kwa mshangao kwa nini nguvu kubwa mno zitumike kuwazuia hawa wachache wasiokuwa hata na silaha wala influence kufanya mikutano yao?

Zaidi sana kumekuwa na sintofahamu kubwa inayoonyeshwa na hofu za viongozi wa hii serikali pale wanaposikia kuna watu wanataka kuandamana kwa amani ili kufikisha ujumbe wao kwa masuala wanayohitaji yafanyiwe kazi. Hii hofu na taharuki inatoka wapi? Kwa nini serikali isitumie jehsi la polisi kusimamia usalama wa hayo maandamano ili yafanyikie kwa amani ? Hizo nguvu za kuua waandamanaji, zisingezaa matunda mema na ya amani kama zingelitumika kulinda usalama wa hao waandamanaji na wadau wengine pasipo kufanya mauaji?

Inakuwaje serikali pendwa inaogopa maandamano na mikutano ya hao 20% ambao wala hawawezi kufanya hatari yoyote?

Zaidi sana ninaomba tujadiliane hii dhana ya kutafsiri kwamba maandamano ya amani ni mapinduzi, inatoka wapi? Kuna kivuli kibaya kinacholeta ndoto mbaya zinazoopelekea watu wakimbie usingizini pasipo sababu?

Ninatamani viongozi wa nchi yangu, wangekubali kuongoza kwa kufuata katiba ya nchi, kuwaruhusu wanaotaka kuandamana waandamane ili mradi hawafanyi fujo, iwaruhusu watu wakusanyike kwenye mikutano ya siasa kama chama kilichopo madarakani kinavyofanya ili mradi hawavunji sheria. Serikai iendelee na kufanya maendeleo ya taifa bila matusi, ubaguzi, na kitu kinatiwa unyanyasi wa ki itikadi na kuimarisha uhusiano wa viongozi na watu wa kawaida.


Nini maoni yako?
Zile CD na DVD za mikutano ya kampeni za mwaka 2015 bado wanaziangalia kila wakati kila siku. Midomoni hakuna upinzani mioyoni upinzani upo wa kutisha.
 
Nadhani ni zile figisu za NEC na wizi wa kura kuna mfanya mtawala wetu asijismini sana.
Tofauti kati yake na mshindani wake kwa hesabu za NEC ni million mbili tuu hivyo anajua kuna watu zaidi ya million sita hawa mtaki ndio sababu ya woga na hofu yake na wafuasi wake.

Ni sahihi kiongozi. Lakini juhudi zake za kuonyesha umahili katika kazi zimethibitika ndiyo sababu sasa mwaka wa tatu huu, ameweza kuua upinzani na kufanya wapinzani wengi waache vyeo na vyama vyao ili kumuunga mkono. Baada ya kuua kabaisa upinzani kama vila chama chake kinajibainisha, bado kuna hofu ya nini tena? Waliomnyima kura sasa maeflu kwa maelfu wanakimbillia kwake na chama chake. Nini tena kinaleta hofu hii?
 
Zile CD na DVD za mikutano ya kampeni za mwaka 2015 bado wanaziangalia kila wakati kila siku. Midomoni hakuna upinzani mioyoni upinzani upo wa kutisha.

Ni wakati muafaka wa kuwashauri, waache kuangalia CD za nyuma. Waangalie CD za sasa ambapo wameweza kushinda chaguzi zote katika majimbo ya uchaguzi mdogo wa wabunge na madiwani tena kwa kura nyingi zinazokaribia 100%.

Wanashindwa nini kuamini ushindi huu mnono ili uwaondolee taswiira za kutisha za nyuma?
 
Ni wakati muafaka wa kuwashauri, waache kuangalia CD za nyuma. Waangalie CD za sasa ambapo wameweza kushinda chaguzi zote katika majimbo ya uchaguzi mdogo wa wabunge na madiwani tena kwa kura nyingi zinazokaribia 100%.

Wanashindwa nini kuamini ushindi huu mnono ili uwaondolee taswiira za kutisha za nyuma?
Wanajua walivyoshinda changuzi ndogo
 
Heh, kumbe haya maandamano ni kwa ajiri ya kuingo'a serikali? Acha kumbe watu wapigwe tu
 
Hii ndiyo serikali ya kwanza kusikia inataka kuangushwa kwa maandamano katika Tanganyika kama ni kweli basi serikali yenyewe ijitafakari upya
 
Ni sahihi kiongozi. Lakini juhudi zake za kuonyesha umahili katika kazi zimethibitika ndiyo sababu sasa mwaka wa tatu huu, ameweza kuua upinzani na kufanya wapinzani wengi waache vyeo na vyama vyao ili kumuunga mkono. Baada ya kuua kabaisa upinzani kama vila chama chake kinajibainisha, bado kuna hofu ya nini tena? Waliomnyima kura sasa maeflu kwa maelfu wanakimbillia kwake na chama chake. Nini tena kinaleta hofu hii?
Anayajua maigizo anayoyafanya. Wachawi hawakaukiwi wasiwasi.
 
Eti maandamano yanaongozwa na mange,let be serious!! Kweli tunampa umaarufu asiostahili.
 
Eti maandamano yanaongozwa na mange,let be serious!! Kweli tunampa umaarufu asiostahili.

Macho yako tu. Lakini Mange hahitaji umaarufu hata kidogo. Wanaotafuta umaarufu ni wasanii wa bongo movie. Mange ni reality show!.

Kama ndivyo, asingewatetemesha wakuu kiasi cha kupanic kwa ngazi hiyo. Ama wewe huoni ambavvyo hawaoni hadi wanaanza kurambana chenga wenyewe na karibu wanajifunga bao wao wenyewe kwa kudhani wanashambuliwa adui wakati mchezo uko gorini kwao?
 
Intelligensia inajua uhalisia on the ground.Zimbabwe juzi kila mtu alishangaa Mgabe alikuwaje anapata kura nyingi.Hata Libya Ghadafi alikuwa anapata 99%!Lakini hofu haikuisha moyoni mwake.
 
hawa watu ni wa ajabu sana .wanafikia kisema ati kunawatu wanatumiwa na watu wasiolitakia mema taifa .taifa hili la Tanzania? kuna yule mshamba anayetumia vyeti vya watu bwana bashite ati anasema mpaka yye aondoke ndo mandamano yafanyike.hivi huu umungu mtu wanaupata wapi hawa washamba
 
Hakuna kitu kibaya kama kujindanganya kama hii awamu ya tano wanaona wanakubalika wanatumia Nguvu nyingi waonekane wanakubalika kumbe amna kitu wanajidanganya wenyewe
 
Back
Top Bottom