Nini tafsiri ya Megawatts 2,115 za umeme wa bwawa la Mwalimu Nyerere (Stiegler's Gorge)?

Tuwaamini wataalamu wetu wanaohusika na ujenzi wa Bwawa la Nyerere kwan kuzingatiwa athari na matokeo yake ya kijamii, kisiasa, mazingira na kiteknolojia (rejeeni EIA na SIA ya huo mradi).

Kwa mfano jenzi wa bwawa jipya na kubwa ni jibu la hoja ya Magimbi. Isitoshe juhudi na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya tabianchi imeonesha mafanikio mazuri jwani huu mwaka kumekuwa na mvua kubwa na nyingi.
Juhudi ipi ya kukabili Climate change imeonyesha mafanikio makubwa?? Una mifano??
 
Watu wavivu utawajua tuu, hivi huna habari kwamba watu tayari wana several schemes za irrigation kwa kutumia majenereta? Unadhani vitunguu, nyanya, hoho etc zinalimwaje kama siyo irrigation za kutumia water pumps??

Off-point.
 
Kuna porojo mbili umeongea:

1.Porojo ya kwanza ni kudai kuwa unit 565 zitabaki kwa hiyo zinapaswa kuuzwa.Hii ni porojo kwa sababu usichokijua ni kwamba huo umeme wote wa Stiglers Gorge bado ni mdogo sana kwa sababu kila mwaka idadi ya watu wanaongezeka na kuongezeka kwa idadi hiyo ya watu kunaambatana na kuongezeka kwa matumizi ya umeme majumbani,viwandani,madukani,mashuleni,kwenye vituo vya afya,etc

2.Porojo ya pili ni kudai kuwa mradi huo unatengenezwa kwa fedha zetu za ndani
 
Kwa mlinganisho na ufahamisho tu hadi mwaka 2018, Kenya walikuwa wanazalisha 2,700 MW za umeme na wana mpango wa kuzalisha 7,200 MW za umeme kufikia mwaka 2030.
 
Hata wewe ni muongo tuu maana haujatoa any proof to backup your argument.
Unajua Megawati moja ni watt ngapi? Kwa taarifa yako Mega watt moja ni Watts 1,000,000 sasa hilo jengo la Mkapa linaweza likatumia Watts Million we unaonekana jinga kabisa.
 
Umesahau SGR pekee itakula 700MWh itakapokamilika,
Na kwa sasa Dar - Moro imetengewa 30MWh
 
Mkishindwa kupangua hoja za Watanzania wenzenu kwa hoja mnakimbilia kuwaita mabeberu, ni ujuha tuu huo, pangua hoja kwa hoja siyo kurusha rungu, hoja haifi kwa kupigwa rungu (alisema JK).Mtu na akili zako unashindwa kuzima hoja kwa kujenga hoja nzito badala yake unakimbilia kumuita mara beberu, ooh siyo mzalendo, mara ooh shoga... Halafu unataka sisi wengine eti kutumaini na kukuona umeongea la maana kumbe pumba tupu.
HAPANA! Nazungumzia vihoja uchwara vilivyokuwa vikitolewa na mabeberu wakati wakipinga ujenzi wa hilo Bwawa; na vihoja hivyo hivyo ndivyo anakuja navyo Lissu na wewe leo! Ndiyo maana nasema nilishawahi kusikia vihoja kama hivi hapo zamani na majibu yake yalishatoka ikiwa na hiyo ya kusema kuwa sehemu ya huo mradi wa hilo Bwawa ni less than 2% ya eneo linalopigiwa kelele la hiyo mbuga ya Selous. Hiyo ni moja ya majibu ya vihoja hivyo dhidi ya hilo Bwawa and that is what I am trying to say hapo juu ndugu siyo matusi!
 
Na gesi ya kupikia (LNG) ambayo tuliambiwa mtungi wa elfu 50 tutanunua kwa elfu 10 imekuwaje???
Kama nilivyosema, kwa gas inachomwa kwenye majenereta, hivyo ikishachomwa ndo imeisha. Kupata gas kwa ajili ya LNG plant inatakiwa uwe na gas nyingine ujenge plant... Hiyo ya kujenga plant ndo haijafanyika hadi leo
 
Nikuongezee kanyama kengine,gas ikishachomwa sio kwamba matumizi yake yameisha, gas iliyochomwa hua inatumika tena kuzalisha umeme au kuchemsha maji kwa matumizi mengine itategemea na uhitaji wake, nenda tena pale kinyerezi 2 wanatumia gas turbine kufua umeme na hapo hapo gas iliyoungua inazalisha umeme wa mvuke (Stem turbine) tunaita combined cycle. Kijana punguza munkali wa siasa unapokuja kwenye utaalam na kama hujui jitahidi uchimbe kwanza na kuomba msaada kwa wajuvi wa haya mambo.
Hayo nayajuwa... nilitaka kuelezea kwamba huwezi ipata tena gas kama gas...
 
NINI TAFSIRI YA MEGAWATTS 2,115 ZA UMEME WA BWAWA LA MWALIMU NYERERE (Stiglers Gorge)?

Kuzielewa Megawatts 2115 na ukubwa wake ni rahisi ukipitia na kujua matumizi ya umeme na mahitaji ya umeme kwa taifa letu. Mfano mwepesi tu ni kwamba mahitaji halisi ya umeme kwa mikoa kama ya Mtwara na Lindi ili umeme usikatike hata sekunde ni Megawatts 22 hadi 30 tu, ina maana katika zile Megawatts 2,1
Ngoja nikuulize!

Assume kiasi ambacho mtu anatakiwa kula ni 1kg ya mchele na 1 kg ya nyama, ambazo total ni TSh 10K! Lakini kwa kuwa hana uwezo wa Sh.10K, anaamua kula 1/2 kg ya mchele na 1/kg ya nyama ambayo total ni TShs. 5K

Je, unaweza kusema mahitaji ya huyo mtu ni TSh. 5K?!
Tanzania ina Mikoa 31, hivyo ukifanya kila mkoa upate Megawatts 50 tu kama makadirio ya juu kabisa hata kwa mikoa isiyozidi matumizi hayo maana yake ni sawa na kupeleka bahari ya umeme kila mkoa na bado matumizi tutaishia Megawatts 1,550 na bado zitabaki Megawatts 565 kama akiba ya umeme tuliyoiweka kibindoni. Bado hiyo Megawatts 50 kiwastani hata ukijumlisha mikoa yenye viwanda vingi na vikubwa kama Pwani, Dar es Salaam, Arusha, Tanga na Mwanza bado ni kubwa sana. Nimeweka kwa kiwango cha Juu saana usisahau matumizi ya Mtwara na Lindi ni Megawatts 22- 30 tu.

Ina maana hapo tunaenda kuua kabisa stori za mgao wa umeme na mambo ya umeme kukatikakatika. Hapo wenye viwanda vikubwa, vya kati na vidogo kabisa watazalisha bidhaa zao bila tatizo na zaidi kwa gharama nafuu kutegemea na urahisi wa gharama kwa umeme wa maji.
Hapa napo unatakiwa kujiuliza suali la hapo juu!!!!

Anyway, wacha nikujuze!!!

Mahitaji ya Lindi na Mtwara sio hizo 22MW to 30MW ulizotaja bali umaskini ndio unakufanya udhani mahitaji yao ni 22-30MW!!

Bei kubwa ya umeme inawafanya watu wasiwe wanatumia vifaa vya umeme vinavyotumia umeme mwingi kama vile majiko na pasi!

Umaskini unawafanya watu wa Lindi na Tanzania kwa ujumla wasiwe na uwezo wa kununua vifaa vya nyumbani vinavyotumia umeme kama vile majiko, majokofu, mashine za kufulia nguo, redio n.k!!!

Kwahiyo hicho unachoona kama matumizi yetu Tanzania ni 1550 MW inatokana na watu ku-opt kula mchele 1/2 kilo na nyama 1/2 kilo wakati mahitaji yao ni 1kg ya nyama na 1kg ya mchele kwa sababu hawana uwezo wa kununua 1kg ya nyama na mchele!!!

Leo hii ikitokea situation kwamba 50% TU ya watu wanaoishi Dar es salaam peke yake wawe na uwezo wa kununua na kutumia majiko ya umeme, pasi, majokofu, mashine za kufulia nguo; hata bila ya kungalia mikoa mingine, hapo hapo utagundua hizo 2114MW si lolote si chochote!!

And remember, hivyo vifaa nilivyotaja hapo juu ni basic home appliances!!

That's one but two, umeonesha mapungufu makubwa ya kiuchambuzi pale unapodai:-
Umeme wa Kinyerezi ambao ndiyo tunaojivunia kwa sasa kuwa ni mradi mkubwa wa umeme kiwango chake cha mwisho cha kuzalisha umeme ni Megawatts 1,560 tu ina maana Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee yake linaenda kutupa umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni rahisi zaidi kuliko aina yoyote ile ya umeme duniani ukiachana na wa jua, upepo, nyukl
Hapo umedanganya, ama kwa makusudi au kwa kutojua!!!

Kiwango chake cha mwisho kinachoweza kuzalishwa pale Kinyerezi kitategemeana na kiwango cha gesi kitakacholetwa pale relative to capacity ya bomba linalosafirisha gas husika!

Hapo kabla iliwahi kutangazwa kwamba Bomba la Gesi linaloenda Kinyerezi linasafirisha ONLY 6% ya uwezo wake!! Kwa sasa labda itakuwa imefikia 15-20%, au kama imezidi sana labda 25%!!!

Hii maana yake ni kwamba si kweli eti uwezo wake wa kuzalisha pale Kinyerezi ni Megawatts 1560 tu bali hizo Megawatts 1560 zinatokana na gas ambayo inaenda pale!!! Kwa maana nyingine, hata bila ya kujenga bomba lingine, pale Kinyerezi tunaweza kuzalisha zaidi 6000MW za umeme!!

Na hata bomba likielemewa, bado unaweza kujenga bomba lingine na terminal kuwa at the same Kinyerezi Power Plant or elsewhere provided gas bado ipo!!

Lakini kwa upande mwingine, labda kwa sababu umeamua kuleta ushabiki wa kisiasa au kwa kutojua, umeshindwa kuelezea multiplier effect inayoweza kupatikana kwenye uwekezaji kupitia gas as compared na umeme wa maji!

Wakati kinachoweza kupatikana kwenye uwekezaji wa Bwawa la Nyerere ni umeme pekee (na faida zake), uwekezaji kwenye gas ungeleta huo umeme ambao utapatikana kupitia Bwawa la Nyerere, na pia ingepatikana nishati mbadala ambayo ni gas yenyewe!!

On top of that, unapofanya gas processing kunakuwa na byproducts zinazoweza kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya mbolea na plastic, na ndio maana Dangote alitaka kuanzisha kiwanda kikubwa sana cha mbolea kule Mtwara!!!

Kwa kujiongeza zaidi, pitia hapa chini:
Associated hydrocarbons, known as 'natural gas liquids' (NGLs) can be very valuable by-products of natural gas processing. NGLs include ethane, propane, butane, isobutane, and natural gasoline. These NGLs are sold separately and have a variety of different uses; including enhancing oil recovery in oil wells, providing raw materials for oil refineries or petrochemical plants, and as sources of energy. The actual practice of processing natural gas to pipeline dry gas quality levels can be quite complex, but usually involves four main processes to remove the various impurities:
Multiplier effect (economic multiplier effect) nyingine ambayo ni kubwa sana ni ile ya kwenye ajira zinazokuwa generated kutoka kwenye gas extraction, gas processing, gas distribution and transportation, and many more!!

Yote hayo hayawezi kupatikana kwenye mradi wenu mnaotuaminisha kwamba ndo mwisho wa matatizo!!!
 
..wachumi wana msemo wao wanasema, " CETERIS PARIBUS. "

..maana yake ni all other FACTORS remaining constant.

..sasa ni kweli kwamba gharama umeme wa maji, ceteris paribus, ni ndongo kuliko umeme wa vyanzo vingine.

..lakini kwa hapa Tz siyo kweli kwamba factors zote zitakuwa constant.

..Kwa mfano kama tumechukua MKOPO WA KIFISADI kwa ajili ya ujenzi wa mradi basi umeme utakaozalishw utakuwa wa gharama zaidi.

..Kama hatukuzingatia taarifa za mazingira kabla hatujaanza ujenzi basi tutaingia gharama wakati wa uendeshaji wa mradi.

..Kama tukishindwa kutunza mazingira ktk VYANZO VYA MAJI ktk mradi huo gharama zitaongezeka.

..Kama tuna miradi mingine mibaya isiyo na ufanisi ya kuzalisha umeme, then bei ya umeme kwa ujumla itaathirika.

..Stieglers gorge sio mradi wa kwanza wa umeme wa maji hapa nchini. Tayari tuna miradi kama Kidatu, Mtera, Pangani, etc etc lakini nayo ina changamoto zake.
Ahsante sana for ceteris paribus manake hata hizo 2115MW anazodai ni nyingi kweli kweli, zitaendelea kuwa nyingi endapo tu kiwango cha uchumi wa Tanzania kitabaki kama kilivyo, lakini leo hii ikitokea 5% ya Watanzania wakanunua majiko ya umeme na kuyatumia, in no time atajua 2115MW ni umeme kidogo sana!!!
 
Ngoja nikuulize!

Assume kiasi ambacho mtu anatakiwa kula ni 1kg ya mchele na 1 kg ya nyama, ambazo total ni TSh 10K! Lakini kwa kuwa hana uwezo wa Sh.10K, anaamua kula 1/2 kg ya mchele na 1/kg ya nyama ambayo total ni TShs. 5K

Je, unaweza kusema mahitaji ya huyo mtu ni TSh. 5K?!

Hapa napo unatakiwa kujiuliza suali la hapo juu!!!!

Anyway, wacha nikujuze!!!

Mahitaji ya Lindi na Mtwara sio hizo 22MW to 30MW ulizotaja bali umaskini ndio unakufanya udhani mahitaji yao ni 22-30MW!!

Bei kubwa ya umeme inawafanya watu wasiwe wanatumia vifaa vya umeme vinavyotumia umeme mwingi kama vile majiko na pasi!

Umaskini unawafanya watu wa Lindi na Tanzania kwa ujumla wasiwe na uwezo wa kununua vifaa vya nyumbani vinavyotumia umeme kama vile majiko, majokofu, mashine za kufulia nguo, redio n.k!!!

Kwahiyo hicho unachoona kama matumizi yetu Tanzania ni 1550 MW inatokana na watu ku-opt kula mchele 1/2 kilo na nyama 1/2 kilo wakati mahitaji yao ni 1kg ya nyama na 1kg ya mchele kwa sababu hawana uwezo wa kununua 1kg ya nyama na mchele!!!

Leo hii ikitokea situation kwamba 50% TU ya watu wanaoishi Dar es salaam peke yake wawe na uwezo wa kununua na kutumia majiko ya umeme, pasi, majokofu, mashine za kufulia nguo; hata bila ya kungalia mikoa mingine, hapo hapo utagundua hizo 2114MW si lolote si chochote!!

And remember, hivyo vifaa nilivyotaja hapo juu ni basic home appliances!!

That's one but two, umeonesha mapungufu makubwa ya kiuchambuzi pale unapodai:-

Hapo umedanganya, ama kwa makusudi au kwa kutojua!!!

Kiwango chake cha mwisho kinachoweza kuzalishwa pale Kinyerezi kitategemeana na kiwango cha gesi kitakacholetwa pale relative to capacity ya bomba linalosafirisha gas husika!

Hapo kabla iliwahi kutangazwa kwamba Bomba la Gesi linaloenda Kinyerezi linasafirisha ONLY 6% ya uwezo wake!! Kwa sasa labda itakuwa imefikia 15-20%, au kama imezidi sana labda 25%!!!

Hii maana yake ni kwamba si kweli eti uwezo wake wa kuzalisha pale Kinyerezi ni Megawatts 1560 tu bali hizo Megawatts 1560 zinatokana na gas ambayo inaenda pale!!! Kwa maana nyingine, hata bila ya kujenga bomba lingine, pale Kinyerezi tunaweza kuzalisha zaidi 6000MW za umeme!!

Na hata bomba likielemewa, bado unaweza kujenga bomba lingine na terminal kuwa at the same Kinyerezi Power Plant or elsewhere provided gas bado ipo!!

Lakini kwa upande mwingine, labda kwa sababu umeamua kuleta ushabiki wa kisiasa au kwa kutojua, umeshindwa kuelezea multiplier effect inayoweza kupatikana kwenye uwekezaji kupitia gas as compared na umeme wa maji!

Wakati kinachoweza kupatikana kwenye uwekezaji wa Bwawa la Nyerere ni umeme pekee (na faida zake), uwekezaji kwenye gas ungeleta huo umeme ambao utapatikana kupitia Bwawa la Nyerere, na pia ingepatikana nishati mbadala ambayo ni gas yenyewe!!

On top of that, unapofanya gas processing kunakuwa na byproducts zinazoweza kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya mbolea na plastic, na ndio maana Dangote alitaka kuanzisha kiwanda kikubwa sana cha mbolea kule Mtwara!!!

Kwa kujiongeza zaidi, pitia hapa chini:

Multiplier effect (economic multiplier effect) nyingine ambayo ni kubwa sana ni ile ya kwenye ajira zinazokuwa generated kutoka kwenye gas extraction, gas processing, gas distribution and transportation, and many more!!

Yote hayo hayawezi kupatikana kwenye mradi wenu mnaotuaminisha kwamba ndo mwisho wa matatizo!!!
Kinyerezi I inatoa MW185 na Kinyerezi II inatoa MW 240 umeme mwingine unatoka katika vyanzo vingine mzee usidanganye na kujitia unajua sana angalia document hiyo
 

Attachments

  • Kinyrezi Project.pdf
    6.1 MB · Views: 6
NINI TAFSIRI YA MEGAWATTS 2,115 ZA UMEME WA BWAWA LA MWALIMU NYERERE (Stiglers Gorge)?

Wengi tunaona na kusikia kuhusu habari ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa uzalishaji umeme wa maji wa Megawatts 2115 kutoka kwenye Mto Rufiji, mradi uliobuniwa na Mwalimu Nyerere toka mwaka 1975 na sasa unatekelezwa na Rais wa awamu ya 5 Dkt John Pombe Magufuli.

Tumesikia habari ya ukubwa wake huo mradi, gharama ya utekelezaji wa mradi wenyewe, umeme unaoenda kuzalishwa na mambo mengine mengi sana kuuhusu mradi huo wa Stieglers Gorge (Bwawa la Mwalimu Nyerere). Sasa leo ngoja tuumulike kidogo mradi huu wa umeme, tujue idadi ya namba zilizoko za gharama na Megawatts zinazoenda kuzalishwa hapo na tafsili yake kwa Watanzania na uchumi wetu.

Kwanza kuingia kwa Serikali ya awamu ya 5 kulifungua ukurasa mpya wa utekelezaji wa maono ya Baba wa Taifa ya toka mwaka 1975 ya kutaka kuzalisha umeme kwenye bonde la Mto Rufiji kupitia mradi huo mkubwa kabisa namba 4 wa uzalishaji wa umeme barani Afrika unaoenda kuzalisha Megawatts 2115 kwa gharama ya Trillion 6.5 tena kwa fedha zetu za ndani.

Adhima ya utekelezaji wa mradi huo inakuja wakati nchi ikiwa kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda ambao kwa kiwango kikubwa unategemea sana nishati umeme ya kuwezesha viwanda kupata nishati ya kutosha ili iweze kuzalisha vya kutosha na muhimu kwa gharama nafuu. Viwanda ni umeme na umeme ni viwanda.

Lakini licha ya yote ni wangapi tunaelewa tafsiri halisi ya Megawatts 2,115 za umeme zinazoenda kuzalishwa pale Mto Rufiji? kwa sisi watu wa kawaida ambao si wataalamu wala wahandisi tunaelewa nini kuhusu Megawatts 2115? twende sawa hapo chini.

Kuzielewa Megawatts 2115 na ukubwa wake ni rahisi ukipitia na kujua matumizi ya umeme na mahitaji ya umeme kwa taifa letu. Mfano mwepesi tu ni kwamba mahitaji halisi ya umeme kwa mikoa kama ya Mtwara na Lindi ili umeme usikatike hata sekunde ni Megawatts 22 hadi 30 tu, ina maana katika zile Megawatts 2,115 tunakuwa na chenji kama ya Megawatts 2,085.

Tanzania ina Mikoa 31, hivyo ukifanya kila mkoa upate Megawatts 50 tu kama makadirio ya juu kabisa hata kwa mikoa isiyozidi matumizi hayo maana yake ni sawa na kupeleka bahari ya umeme kila mkoa na bado matumizi tutaishia Megawatts 1,550 na bado zitabaki Megawatts 565 kama akiba ya umeme tuliyoiweka kibindoni. Bado hiyo Megawatts 50 kiwastani hata ukijumlisha mikoa yenye viwanda vingi na vikubwa kama Pwani, Dar es Salaam, Arusha, Tanga na Mwanza bado ni kubwa sana. Nimeweka kwa kiwango cha Juu saana usisahau matumizi ya Mtwara na Lindi ni Megawatts 22- 30 tu.

Ina maana hapo tunaenda kuua kabisa stori za mgao wa umeme na mambo ya umeme kukatikakatika. Hapo wenye viwanda vikubwa, vya kati na vidogo kabisa watazalisha bidhaa zao bila tatizo na zaidi kwa gharama nafuu kutegemea na urahisi wa gharama kwa umeme wa maji.

Umeme wa Kinyerezi ambao ndiyo tunaojivunia kwa sasa kuwa ni mradi mkubwa wa umeme kiwango chake cha mwisho cha kuzalisha umeme ni Megawatts 1,560 tu ina maana Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee yake linaenda kutupa umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni rahisi zaidi kuliko aina yoyote ile ya umeme duniani ukiachana na wa jua, upepo, nyuklia, makaa ya mawe, mafuta na gesi.

Tukumbuke umeme unaozalishwa na maji ndio umeme wa gharama nafuu na rahisi zaidi kuliko umeme wowote ule duniani. Kumbuka uniti 1 inayozalishwa na maji ni shilingi 36 tu wakati umeme wa nyuklia ni shilingi 65 kwa uniti, umeme wa jua shilingi 103.05, upepo 103.05, makaa ya mawe 118, gesi asilia 147 na mafuta ni 426. Hivyo tunaenda kushusha maradufu bei ya umeme kwa watumiaji hivyo kuhimili mfumuko wa bei wa bidhaa za viwandani.

Hii tafsili yake kukamilika tu kwa Bwawa la uzalishaji wa umeme la Mwalimu Nyerere kutashusha kwa kiwango kikubwa sana gharama ya umeme mpaka shilingi 36 tu kwa uniti hivyo kutoa nafasi kwa bidhaa zetu za viwanda nazo kushuka sana. Hapo mpaka kwenye matumizi ya kawaida nyumbani yatashuka na hata kwa watanzania watakaofungua viwanda vidogo kwa vikubwa watanufaika sana na gharama ndogo ya uzalishaji wa bidhaa itakayoleta neema na nafuu mpaka kwa sisi watu wa hali ya chini kabisa, machinga, mama nitilie, wajasiriamali na makundi mengine.

Unapokuwa na umeme wa uhakika, lakini sio wa uhakika tu tena na wa gharama nafuu ya bei tayali unavutia wawekezaji wengi zaidi kuja kujenga viwanda hapahapa. Suala la uhakika wa umeme na nafuu yake ni mambo ya msingi sana kwa mwekezaji anayefikiri kwenda kuwekeza sehemu yoyote ile kwasababu kiwanda ni nishati.

Vipi umefikilia hizo Megawatts zingine zaidi ya 565 ambazo tunakuwa tumezitia kibindoni baada kujihakikishia uhakika wa umeme nchi nzima? hapo tunaweza kuamua kuuza kwa majirani zetu hapo Kenya, Malawi, Uganda au Msumbiji ambako tunajua bado hawana uhakika wa umeme. Hapo unazungumza kuhusu umeme wa Rufiji tu, hujaenda Kinyerezi, Kidatu, Mtera, Nyumba ya Mungu na kwingine ambako umeme unaendelea kuzalishwa.

Rais Magufuli na Serikali yake baada ya kugundua hatuna umeme wa kutosha na wenye bei nafuu kwa wananchi wake ndiyo ikaja na suluhisho hilo la Bwawa la Mwalimu Nyerere. Nini tena sasa? Tusiposema sisi kwa haya yanayofanyika basi hata mawe yatapiga kelele siku moja.View attachment 1597580
Kwa nini 2,115? Kwani ukitoa 3,000 shida iko wapi? Yaani ikifika 2,200 au 2,120 kuna shida gani? Si maji yapo?
 
Kinyerezi I inatoa MW185 na Kinyerezi II inatoa MW 240 umeme mwingine unatoka katika vyanzo vingine mzee usidanganye na kujitia unajua sana angalia document hiyo
We Juha kweli!!

Mimi na wewe nani anayejifanya kujua au anayedanganya watu?!

Wapi nimesema Kinyerezi inazalisha kiwango fulani cha umeme zaidi ya maelezo yangu kuegemea na kile kilichoandikwa na mleta mada kwamba:-
Umeme wa Kinyerezi ambao ndiyo tunaojivunia kwa sasa kuwa ni mradi mkubwa wa umeme kiwango chake cha mwisho cha kuzalisha umeme ni Megawatts 1,560 tu ina maana Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee yake linaenda kutupa umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni rahisi zaidi kuliko aina yoyote ile ya umeme duniani ukiachana na wa jua, upepo, nyuklia, makaa ya mawe, mafuta na gesi.
Nyie Misukule ya Lumumba kichwani bure kabisa ndo maana mmebaki kushangilia mambo ya kijinga!
 
Back
Top Bottom