Molleli
Senior Member
- Aug 29, 2020
- 178
- 160
Tandika mkeka wa buku ten nitumie namba ya kampuni nitalipia✌️Asante sana, uchambuzi maridhawa kabisa , Sasa naomba uchambue kuhusu gesi, tuliaminishwa hivyo hivyo.
Tandika mkeka wa buku ten nitumie namba ya kampuni nitalipia✌️Asante sana, uchambuzi maridhawa kabisa , Sasa naomba uchambue kuhusu gesi, tuliaminishwa hivyo hivyo.
Tuko pamojaStory tu hizo mpaka siku nitakapoanza kuhutumia ndio nitaamini
Acha tu jamaa yanguFuture impossible tense.
Sasa hivi tunanunua unit sh ngapi wakati tunatumia gas na maji.
$30bnIli kuweza kuibadili gas Yetu iwe katika kimiminika na kusafirishwa kwa njia ya mitungi, Project inaweza kugharimu kiasi gani cha fedha? Kwasababu hili likiwezekana ni hakika tutaifaidi Gas hii maradufu
Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Mbona unajua bill yako ya umeme unayolipa nyumbani kwako? Ni kipimo hicho hicho kinachotumiwa wakati wa kuuza huo umemeSasa naomba unieleweshe Kama tutauza hizo megawatts 500 ...tutajuaje Kama ni megawatts 500 zimeenda huko...je hawatakula nyingi tukajikuta tuko kwenye shida tena?
Hilo bwawa la Nyerere limetumia eneo la asilimia tatu tu la eneo lote 3% sionioni kwa nini watu wasemeseme kwa kaeneo kadogo hako.Tuwaamini wataalamu wetu wanaohusika na ujenzi wa Bwawa la Nyerere kwan kuzingatiwa athari na matokeo yake ya kijamii, kisiasa, mazingira na kiteknolojia (rejeeni EIA na SIA ya huo mradi).
Kwa mfano jenzi wa bwawa jipya na kubwa ni jibu la hoja ya Magimbi. Isitoshe juhudi na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya tabianchi imeonesha mafanikio mazuri jwani huu mwaka kumekuwa na mvua kubwa na nyingi.
Mwegeso..umeongea vyema kabisa. Lakini reserve ya maji itategemea na uwepo wa feed up channels..labda kuwepo na chemichemi ya kudumu ambazo pia msimu wa kiangazi hupungua uwezo wake wa kutoa maji. Unakumbuka kukauka kwa mabwawa miaka ya 2007-2008 ikaletelezea Richmond saga? Waswasi wangu uko hapo Mwegeso. HEP easy and cheap but very unreliable kutokana na kutegemea single sources of water resources hasa kwa sisi Tanzania. Mabadiliko ya tabia nchi na yenyewe hayatabiriki sana kutokana na population. Tuombe kama unasema kusitokee majanga ya mazingira. Lets hope all factors are constant then bwawa la Stigler gorge litadumu milele.Tuwaamini wataalamu wetu wanaohusika na ujenzi wa Bwawa la Nyerere kwan kuzingatiwa athari na matokeo yake ya kijamii, kisiasa, mazingira na kiteknolojia (rejeeni EIA na SIA ya huo mradi).
Kwa mfano jenzi wa bwawa jipya na kubwa ni jibu la hoja ya Magimbi. Isitoshe juhudi na mikakati ya kudhibiti mabadiliko ya tabianchi imeonesha mafanikio mazuri jwani huu mwaka kumekuwa na mvua kubwa na nyingi.
Mbaya zaidi, wengi wa wanaobishana humu jukwaani ni full siasa... unabaki unashangaa tu... mtu hata kwenye unit anaandi 2115m akimaanisha 2115mW... yaani ukiona mtu anaandika mw (millwatt) badala ya mW (Megawatt) ujuwe hajui units za power lakini ubishi unashika hatamu.. wataalamu hawapewi nafai... hasa kama TECHNICAL OPINION ya project husika ITAKWENDA TOFAUTI NA MATAKWA YA MTAWALA..Kukiwa na kiongozi dhaifu anayetoa maamuzi dhaifu, taaluma huwekwa pembeni na valaza hujitokeza kuwa washauri wa kiongozi na kwa bahati mbaya wanageuka kuwa wataalamu wa kuwafundisha hata wasomi. Kuhusu umeme wa Stiegler's Gorge ni kweli ulikuwa Mradi wa Mwalimu lakini si kweli kuwa alishindwa kutekeleza bali aliheshimu mikataba ya Kimataifa na kuiridhia badala yake akajenga Mtera kusaidia kuhifadhi maji kwa ajili ya Kidatu. Miaka mingi baadaye, Serikali ya Awamu nyingine ilijenga kwa ubabe Bwawa la umeme la Kihansi ingawa kulikuwa na upinzani mkali wa wanamazingira wa ndani na nje ya nchi mpaka Marekani ikajitolea kuhamisha na kuwahifadhi vyura ambao hawapatikani popote duniani. Vyura walirudishwa baada ya Bwawa kukamilika na kujazwa maji lakini wananchi hawaambiwi hali ya vyura wala Bwawa lenyewe halizungumzwi kabisa inawezekana lina matatizo. Mabwawa yote manne ya Kidatu, Mtera, Kihansi na linalojengwa la Nyerere yako kwenye mto mmoja na endapo mto utakosa maji ya kutosha nchi nzima itakosa umeme kabisa na ishara zinaanza kujitokeza kupungua kwa maji. Ruaha tawi muhimu la mto Rufiji linalotoa maji kwenye Bwawa la Mtera maji yameanza kupungua sana ingawa TANESCO hawasemi na Bwawa limeanza kujaa tope kutokana na kilimo cha umwagiliaji cha mpunga kwenye chanzo cha mto. Swali la kujiuliza ni, je hakuna vyanzo vingine vya kuzaliwa Umeme?
Kwani kuwa na nyukli maana yake mna umeme unaowatosha wakati wote..?Mkuu South Africa pamoja na umeme wa nyuklia lakini Wana power cut au mgawo mwaka huu wote yangu mwaka Jana.
Umeme huwaga hautoshagi. Na gharama za kupatikana kwa wananchi ndio shughuli pevu
ha ha haa aaaaaaaa, sasa ni wakati muafaka JF waongeze kitu kingine cha kubofya ili kuwapa notisi kwa watu wanaoposti upumbafu na ujinga uliopitiliza,utakuta Mtaalam Bingwa aliyebobea anabishana na watu wa "miliwatts"Mbaya zaidi, wengi wa wanaobishana humu jukwaani ni full siasa... unabaki unashangaa tu... mtu hata kwenye unit anaandi 2115m akimaanisha 2115mW... yaani ukiona mtu anaandika mw (millwatt) badala ya mW (Megawatt) ujuwe hajui units za power lakini ubishi unashika hatamu.. wataalamu hawapewi nafai... hasa kama TECHNICAL OPINION ya project husika ITAKWENDA TOFAUTI NA MATAKWA YA MTAWALA..
Tunajua wa mazingira almanusura yamkute na NO zake za kistigla
Hilo bwawa la Nyerere limetumia eneo la asilimia tatu tu la eneo lote 3% sionioni kwa nini watu wasemeseme kwa kaeneo kadogo hako.
Tujulishe pia kuhusu athari zake za muda mrefu kimazingira. Tulipopata umeme wa bwaws la mtera tuliambiwa tatizo la umeme lingeisha. Haikuchukua muda ukaja ukame wa msimu 97/98 bwawa likapungua maji tujaingia kwenye mgao uliotuingiza kwenye mkenge wa IPTL na DOWSNS. Tuna uhakika gani na uendelavu "sustainability" wa umeme huu hasa ukizingatia kwamba asilimia zaidi ya 90 ya maji yake yanategemea mito ya Ruaha mkuu na Kilombero anbayo maji yake yaneshaanza kupungua kwa kiasi kikubwa kutokana na uharibifu wa mazingira?..hoja yako ni nzuri sana na nimewahi kuisikia ikitolewa na Raisi.
..sasa moyo wa binadamu ni 0.69% ya uzito wa mwili wote.
..miguu ya binadamu ni 20.37% ya uzito wa mwili wote.
..sasa madaktari wakikwambia wachomoe moyo, au miguu, utachagua nini?
..hoja ya kutetea au kupinga bwawa la umeme haitakiwi ijikite kwenye ukubwa wa eneo la mradi peke yake.
..hoja inatakiwa iwe ni eneo la mradi lina umuhimu / athari kiasi gani kwa bonde zima la mto rufiji.
..kwasababu ujenzi umeshaanza, basi tunatakiwa tuwe na taarifa za kina za athari za kimazingira, na pia tupange mikakati ya kukabiliana na athari hizo. hakuna bwawa la umeme lisilo na athari kwa mazingira, cha msingi ni kiwango cha athari hizo, na mbinu za kupambana nazo.
cc Nguruvi3, Pascal Mayalla, Salary Slip
3% ya Tanzania nzima? Hivi unajuwa ukitaja kwa percentage watu wanaweza wasipate picha halisi ya eneo lililofyekwa... MWAMBIE MTU ENEO LILILOFYEKWA NI SAWA NA UKUBWA WA DAR ES SALAAM YOTE... sasa ukijumlisha na vilivyoondolewa (bearing in mind kuwa ni mbuga) ndo utapata picha kubwa ya kilichofanyika.. Viumbe hai wote wameswagwa mbalii na operations zitakazokuwepo during production ndo kabisaa..!!!Hilo bwawa la Nyerere limetumia eneo la asilimia tatu tu la eneo lote 3% sionioni kwa nini watu wasemeseme kwa kaeneo kadogo hako.
KIONGOZI...... Five years years to come, we will be back to square one...Tujulishe pia kuhusu athari zake za muda mrefu kimazingira. Tulipopata umeme wa bwaws la mtera tuliambiwa tatizo la umeme lingeisha. Haikuchukua muda ukaja ukame wa msimu 97/98 bwawa likapungua maji tujaingia kwenye mgao uliotuingiza kwenye mkenge wa IPTL na DOWSNS. Tuna uhakika gani na uendelavu "sustainability" wa umeme huu hasa ukizingatia kwamba asilimia zaidi ya 90 ya maji yake yanategemea mito ya Ruaha mkuu na Kilombero anbayo maji yake yaneshaanza kupungua kwa kiasi kikubwa kutokana na uharibifu wa mazingira?
Hawa ni wanachuo ndo wamekaririshwa, Aibu nimehisi mimi aseeKama wewe una elimu ya uhandisi umeme, nakushauri urudi chuo. Hesabu yako na huo mfano wako wa A/C ni ya kinadharia, maana ingekuwa uhalisia umeme unaozalishwa nchi ingekuwa gizani.
Nimesema eneo la Mbuga ya Selous3% ya Tanzania nzima? Hivi unajuwa ukitaja kwa percentage watu wanaweza wasipate picha halisi ya eneo lililofyekwa... MWAMBIE MTU ENEO LILILOFYEKWA NI SAWA NA UKUBWA WA DAR ES SALAAM YOTE... sasa ukijumlisha na vilivyoondolewa (bearing in mind kuwa ni mbuga) ndo utapata picha kubwa ya kilichofanyika.. Viumbe hai wote wameswagwa mbalii na operations zitakazokuwepo during production ndo kabisaa..!!!
Jaribu kuwaza pia.. Loriondo ni percentage ngapi kwenye ukubwa wa eneo la Tanzania? Je! kwa sababu ni kaeneo kadogo ka Tanzania, NI SAWA ILIVYOUZWA, KWA VILE NI KADOGO?