EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,347
Sahara Magharibi ilikuwa koloni la Hispania baada ya mataifa ya Ulaya kugawana makoloni kwenye ule mkutano wa Berlin wa mwaka 1884. Hispania walipoondoka Morocco iliikalia Sahara Magharibi kimabavu huku ikida kuwa eneo hilo ni sehemu ya himaya yake kwa sababu ukoo wa kifalme wa Morocco ulitokea eneo hilo kabla ya ukoloni. Hatua hiyo ilisababisha wananchi wa Sahara Magharibi kuingia katika harakati za ukombozi kwa kuanzisha kikundi cha Polisario cha kudai uhuru kwa njia ya mapambano.
Kati ya mwaka 1966 hadi 1973, Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha maazimio kama saba hivi yaliyotambua umuhimu wa Sahara Magharibu kujiamulia mambo yake. Aidha mnamo mwaka 1975, Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice), katika hukumu yake, ilitupilia mbali kuwa Sahara Magharibi ilikuwa sehemu ya Morocco.
Mapambano yalisitishwa mwaka 1991 na Umoja wa Mataifa ulitaka ifanyike kura ya maoni ili kuamua hatma ya taifa hili. Hata hivyo, mpaka sasa kura ya maoni yaijafanyika kutokana na mgogoro wa kutambua wanaostahili kupiga kura. Mfano, Morocco inataka wavamizi wake kwenye eneo hilo nao waruhusiwe kupiga kura. Jitihada za kusuluhisha mgogoro wa Sahara Magharibi kwa njia wa amani bado zinaendelea.
Kwa muda mrefu Tanzania imekuwa katika mtari wa mbele kidiplomasia katika kudai uhuru wa Sahara Magharibi. Tanzania haina uhasama na Morocco, lakini kwa muda mrefu imekuwa ikipinga kitendo cha Morocco kuendelea kuikalia Sahara Magharibi kimabavu. Pia Tanzania imekuwa ikiishauri Morocco kurejea kwenye Umoja wa Afrika (ambao Sahara Magharibi ni mwanachama) na kukubali kura ya maoni ili wananachi wa Sahara Magharibi waamue hatima yao wenyewe.
Hata hivyo, hivi karibuni kumekuwa na ziara za viongozi wa Tanzania nchini Morocco na habari zitokanazo na ziara hizo aidha zinaleta utata juu ya msimamo wa sasa wa Tanzania kuhusu Sahara Magharibi au labda hatuambiwi kwa uwazi dhamira yetu na nini hasa kinachozungumziwa na kukubaliwa na serikali ya Morocco kila viongozi wetu wanapoenda huko. Pia huwa huwa wanaenda tuu Morocco au wanaenda kujadiliana pia na viongozi wa Sahara Magharibi?
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana akiwa na Spika wa Bunge la Morocco, Rachid Talbi Alami, juzi Jumatatu nchini Morocco.
Habari zilizoripotiwa na tovuti ya lugha ya Kifaransa ya Le360 zinadai kuwa Tanzania inasonga mbele na majadiliano yake na Morocco kutoitambua tena Sahara Magharibi (Sahrawi Arab Democratic Republic) kama nchi inayotakiwa kujitawala yenyewe. Tovuti inadai kuwa jana Jumatatu, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alifanya mazungumzo na spika wa Bunge la Morocco Rachid Talbi Alami jijini Rabat, Morocco.
Vyanzo vya habari vya Le360 kutoka Bunge la Morocco ambavyo havikutaka kutajwa majina yao vimedai kuwa majadiliano yanaendelea vizuri kati ya Tanzania na Morocco kutoitambua tena Sahara Magharibi kama nchi inayotawaliwa kimabavu na Morocco. Aidha Le360 inadai Tanzania inataka kuboresha uhusiano wake na Morocco kwa kutambua pendekezo la Morocco la kuipa Sahara Magharibi mamlaka ya utawala wa ndani tuu wa eneo hilo.
Chama cha Ukombozi wa Sahara ya Magharibi, Polisario, kimekuwa kinalitaka jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa, MINUSRO, kuandaa kura ya maoni ili kuamua kuhusu mustakabali wa himaya hiyo yenye utajiri mkubwa wa mafuta. Morocco inakubali tuu kuwepo kwa mamlaka ya utawala wa ndani eneo hilo. Morocco inadai kuwa kujitawala eneo hilo la Sahara Magharibi si suluhisho la kudumu la mgogoro wa eneo hilo. Inadai kuwa Sahara Magharibi inapaswa kuacha mapambano ya kupigania uhuru wa eneo hilo.
Lowassa na kamati yake ya Bunge walipozuru Morocco mwaka 2012.
Itakumbukwa kuwa Mwaka 2012, Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ikiwa chini ya Mwenyekiti Edward Lowassa ilifanya ziara nchini Morocco ambapo vyombo vya huko viliripoti kuwa aliunga mkono pendekezo la Morocco la kuipa Western Sahara mamlaka ya ndani bila kuwa nchi huru. "Tanzania hopes to see a settlement of the Sahara issue and welcomes Morocco's autonomy proposal," anadaiwa kusema Lowassa alipokutana na Naibu Spika wa Bunge la Morocco Deputy Speaker Mohamed Yatim.
Vyombo vya habari Morroco vilidai kumnukuu Lowassa akisema, "Tanzania is satisfied with the autonomy proposal to the southern provinces put forward by Morocco as a solution to the Sahara issue" and "The Moroccan autonomy plan must be supported by all African countries and we will defend the proposal and convey the reality of this issue to our partners, because our goal is to see the Sahara in good hands as part of a united Africa."
Lakini aporejea nchni na kuongea na waandishi wa habari Dodoma Lowassa alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa "Sisi kama Bunge la Tanzania tunaunga mkono msimamo wa Morocco wa kuitisha kura ya maoni, ambao ni msimamo wa Umoja wa Mataifa". Hata hivyo, nukuu hii ina utata kwa sababu, tofauti na Sahara Magharibi, Morocco haitaki kuwe na kura ya maoni kwa sababu tayari inajua matokeo yatakuwaje. Labda Manyerere Jackton atafafanua walikuwa na maana gani walivyoripiti vile.
Chombo kingine cha habari cha ndani kilidai kuwa Kamati hiyo ya Bunge kamati_ya_bunge_yalikoroga inadaiwa "kukubaliana" na utawala wa Morocco juu ya kuinyima Sahara Magharibi uhuru kamili. Inadaiwa wajumbe wa kamati waliombwa na serikali ya Morocco kuipigia chapuo katika vikao vya Umoja wa Afrika (AU) ili Sahara isipate uhuru kamili. Kamati ya bunge iliombwa na serikali ya Morocco kushawishi serikali ya Tanzania na baadaye serikali kushawishi nchi za Kusini mwa Afrika na baadaye Umoja wa Afrika (AU) kukubaliana na Morocco kuwa Sahara ni sehemu yake.[/URL]
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (MB), akitoa msimamo wa Tanzania kuhusu suala la Sahara Magharibi na Morocco, wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Baada ya Lowassa kuyasema hayo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alitoa msimamo wa serikali ya juu ya mgogoro baina ya nchi za Morocco na Sahara Magharibi kwamba haiko upande wa Morocco kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari vya nchi za Magharibi. Alisema msimamo wa serikali umeafikiana na Umoja wa nchi za Afrika (AU) kwamba Sahara Magharibi inafaa kujitawala yenyewe hivyo yaitishwe makubaliano na watu waweze kupiga kura ili ijulikane kama inajitawala yenyewe au inakuwa pamoja na Morocco.
Membe aliongeza kuwa, Tanzania itaheshimu maamuzi yoyote ya wananchi wa Sahara Magharibi kwa vile "tunaamini wataamua kujitawala wenyewe na siyo kuwa kama kile Kisiwa cha Mayote nchini Comoro". Wananchi wa Kisiwa hicho waliamua kuwa sehemu ya nchi ya Ufaransa, ingawa kipo Afrika.
Rais Kikwete akihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa
Akihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa mwaka 2011, Rais Kikwete alisema kuwa uhuru wa Sahara Magharibi ni "outstanding" issue na kutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua kuwawezesha watu wa Sahara Magharibi kupata haki yao ya kujitawala wenyewe kama nchi huru.
Rais Kikwete alisema "It is heart-warming indeed, to see our efforts, sacrifices and contributions having been rewarded so handsomely with the independence of all African countries and apartheid having been dismantled in South Africa. Only Western Sahara remains outstanding. I hope the United Nations will expedite the process so that people of Saharawi can determine their future peacefully."
Wakati wa kuadhimisha miaka 50 tokea Tanzania ipate uhuru wake, Rais wa Sahara Magharibi ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama cha Polisario Mohamed Abdelaziz, alimtumia Rais Kikwete salamu zake. Salamu hizo zilisema "As our brothers in Tanzania celebrate- with deserved pride- the 50th Anniversary of their independence, it is a great honour for me to express to you and through your Excellency to the people of Tanzania, our warmest congratulations on behalf of the Saharawi people, the government of the Saharawi Arab Democratic Republic and on my own behalf as well as our best wishes for success".
Abdelaziz aliongeza "Since its independence, Tanzania became a shrine for all Liberation Movement and Freedom Fighters of Africa" huku akinukuu maneno ya Mwalimu Nyerere kuwa "For, the right to freedom either exists throughout Africa, or it does not exist anywhere in Africa". Alimalizia salamu zake kwa ku-reiterate "our high appreciation and profound gratitude for the support and solidarity constantly extended by Tanzania to the just struggle of the Saharawi people for freedom and independence".
cc kwa waliokwishafuatilia hili zuala huko nyuma Sheba, FJM, harbab, Mbopo, Raia Fulani, petrol, POLITIBURO, fige, andishile, KIM KARDASH, Kiona, NasDaz, SURUMA, Tumaini Makene, Halisi, Filipo, Kimbunga, JokaKuu, Kichuguu, Mag3, omujubi, Njaare, TUJITEGEMEE, MgonjwaUkimwi, Sangarara, mtotowamjini, MTAZAMO, Nguruvi3, mlagha, TUNTEMEKE, Phillemon Mikael, Kiranga, Tume ya Katiba, Pasco, Precise Pangolin, Njoka Ereguu, Abdillahjr, BAK, Jasusi, Ben saanane, OTIS, ocampo four, DSN, Ogah, Viol, Alinda, Ubongo Silaha, Tina, The Boss, Jagermaster, alles, bucho, Keil, Bongolander, Candid Scope, Sheba, Sniper, manucho, Mpui Lyazumbi, Synthesizer, Tiote, Mkandara, Iza, kalokolaVIII, Sikonge, mharakati, Ukwaju, Chakaza, Mzalendo, Ndahani , W. J. Malecela, JacksonMichael, Njoka Ereguu, TIMING, newazz, KIDUNDULIMA, Kiduku, Mtumishi Wetu, mpujufu, mkomatembo, Kizotaka
Kati ya mwaka 1966 hadi 1973, Baraza la Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha maazimio kama saba hivi yaliyotambua umuhimu wa Sahara Magharibu kujiamulia mambo yake. Aidha mnamo mwaka 1975, Mahakama ya Kimataifa ya Haki (International Court of Justice), katika hukumu yake, ilitupilia mbali kuwa Sahara Magharibi ilikuwa sehemu ya Morocco.
Mapambano yalisitishwa mwaka 1991 na Umoja wa Mataifa ulitaka ifanyike kura ya maoni ili kuamua hatma ya taifa hili. Hata hivyo, mpaka sasa kura ya maoni yaijafanyika kutokana na mgogoro wa kutambua wanaostahili kupiga kura. Mfano, Morocco inataka wavamizi wake kwenye eneo hilo nao waruhusiwe kupiga kura. Jitihada za kusuluhisha mgogoro wa Sahara Magharibi kwa njia wa amani bado zinaendelea.
Kwa muda mrefu Tanzania imekuwa katika mtari wa mbele kidiplomasia katika kudai uhuru wa Sahara Magharibi. Tanzania haina uhasama na Morocco, lakini kwa muda mrefu imekuwa ikipinga kitendo cha Morocco kuendelea kuikalia Sahara Magharibi kimabavu. Pia Tanzania imekuwa ikiishauri Morocco kurejea kwenye Umoja wa Afrika (ambao Sahara Magharibi ni mwanachama) na kukubali kura ya maoni ili wananachi wa Sahara Magharibi waamue hatima yao wenyewe.
Hata hivyo, hivi karibuni kumekuwa na ziara za viongozi wa Tanzania nchini Morocco na habari zitokanazo na ziara hizo aidha zinaleta utata juu ya msimamo wa sasa wa Tanzania kuhusu Sahara Magharibi au labda hatuambiwi kwa uwazi dhamira yetu na nini hasa kinachozungumziwa na kukubaliwa na serikali ya Morocco kila viongozi wetu wanapoenda huko. Pia huwa huwa wanaenda tuu Morocco au wanaenda kujadiliana pia na viongozi wa Sahara Magharibi?
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana akiwa na Spika wa Bunge la Morocco, Rachid Talbi Alami, juzi Jumatatu nchini Morocco.
Habari zilizoripotiwa na tovuti ya lugha ya Kifaransa ya Le360 zinadai kuwa Tanzania inasonga mbele na majadiliano yake na Morocco kutoitambua tena Sahara Magharibi (Sahrawi Arab Democratic Republic) kama nchi inayotakiwa kujitawala yenyewe. Tovuti inadai kuwa jana Jumatatu, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, alifanya mazungumzo na spika wa Bunge la Morocco Rachid Talbi Alami jijini Rabat, Morocco.
Vyanzo vya habari vya Le360 kutoka Bunge la Morocco ambavyo havikutaka kutajwa majina yao vimedai kuwa majadiliano yanaendelea vizuri kati ya Tanzania na Morocco kutoitambua tena Sahara Magharibi kama nchi inayotawaliwa kimabavu na Morocco. Aidha Le360 inadai Tanzania inataka kuboresha uhusiano wake na Morocco kwa kutambua pendekezo la Morocco la kuipa Sahara Magharibi mamlaka ya utawala wa ndani tuu wa eneo hilo.
Chama cha Ukombozi wa Sahara ya Magharibi, Polisario, kimekuwa kinalitaka jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa, MINUSRO, kuandaa kura ya maoni ili kuamua kuhusu mustakabali wa himaya hiyo yenye utajiri mkubwa wa mafuta. Morocco inakubali tuu kuwepo kwa mamlaka ya utawala wa ndani eneo hilo. Morocco inadai kuwa kujitawala eneo hilo la Sahara Magharibi si suluhisho la kudumu la mgogoro wa eneo hilo. Inadai kuwa Sahara Magharibi inapaswa kuacha mapambano ya kupigania uhuru wa eneo hilo.
Lowassa na kamati yake ya Bunge walipozuru Morocco mwaka 2012.
Itakumbukwa kuwa Mwaka 2012, Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ikiwa chini ya Mwenyekiti Edward Lowassa ilifanya ziara nchini Morocco ambapo vyombo vya huko viliripoti kuwa aliunga mkono pendekezo la Morocco la kuipa Western Sahara mamlaka ya ndani bila kuwa nchi huru. "Tanzania hopes to see a settlement of the Sahara issue and welcomes Morocco's autonomy proposal," anadaiwa kusema Lowassa alipokutana na Naibu Spika wa Bunge la Morocco Deputy Speaker Mohamed Yatim.
Vyombo vya habari Morroco vilidai kumnukuu Lowassa akisema, "Tanzania is satisfied with the autonomy proposal to the southern provinces put forward by Morocco as a solution to the Sahara issue" and "The Moroccan autonomy plan must be supported by all African countries and we will defend the proposal and convey the reality of this issue to our partners, because our goal is to see the Sahara in good hands as part of a united Africa."
Lakini aporejea nchni na kuongea na waandishi wa habari Dodoma Lowassa alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa "Sisi kama Bunge la Tanzania tunaunga mkono msimamo wa Morocco wa kuitisha kura ya maoni, ambao ni msimamo wa Umoja wa Mataifa". Hata hivyo, nukuu hii ina utata kwa sababu, tofauti na Sahara Magharibi, Morocco haitaki kuwe na kura ya maoni kwa sababu tayari inajua matokeo yatakuwaje. Labda Manyerere Jackton atafafanua walikuwa na maana gani walivyoripiti vile.
Chombo kingine cha habari cha ndani kilidai kuwa Kamati hiyo ya Bunge kamati_ya_bunge_yalikoroga inadaiwa "kukubaliana" na utawala wa Morocco juu ya kuinyima Sahara Magharibi uhuru kamili. Inadaiwa wajumbe wa kamati waliombwa na serikali ya Morocco kuipigia chapuo katika vikao vya Umoja wa Afrika (AU) ili Sahara isipate uhuru kamili. Kamati ya bunge iliombwa na serikali ya Morocco kushawishi serikali ya Tanzania na baadaye serikali kushawishi nchi za Kusini mwa Afrika na baadaye Umoja wa Afrika (AU) kukubaliana na Morocco kuwa Sahara ni sehemu yake.[/URL]
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard K. Membe (MB), akitoa msimamo wa Tanzania kuhusu suala la Sahara Magharibi na Morocco, wakati akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Baada ya Lowassa kuyasema hayo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alitoa msimamo wa serikali ya juu ya mgogoro baina ya nchi za Morocco na Sahara Magharibi kwamba haiko upande wa Morocco kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari vya nchi za Magharibi. Alisema msimamo wa serikali umeafikiana na Umoja wa nchi za Afrika (AU) kwamba Sahara Magharibi inafaa kujitawala yenyewe hivyo yaitishwe makubaliano na watu waweze kupiga kura ili ijulikane kama inajitawala yenyewe au inakuwa pamoja na Morocco.
Membe aliongeza kuwa, Tanzania itaheshimu maamuzi yoyote ya wananchi wa Sahara Magharibi kwa vile "tunaamini wataamua kujitawala wenyewe na siyo kuwa kama kile Kisiwa cha Mayote nchini Comoro". Wananchi wa Kisiwa hicho waliamua kuwa sehemu ya nchi ya Ufaransa, ingawa kipo Afrika.
Rais Kikwete akihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa
Akihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa mwaka 2011, Rais Kikwete alisema kuwa uhuru wa Sahara Magharibi ni "outstanding" issue na kutaka Umoja wa Mataifa kuchukua hatua kuwawezesha watu wa Sahara Magharibi kupata haki yao ya kujitawala wenyewe kama nchi huru.
Rais Kikwete alisema "It is heart-warming indeed, to see our efforts, sacrifices and contributions having been rewarded so handsomely with the independence of all African countries and apartheid having been dismantled in South Africa. Only Western Sahara remains outstanding. I hope the United Nations will expedite the process so that people of Saharawi can determine their future peacefully."
Wakati wa kuadhimisha miaka 50 tokea Tanzania ipate uhuru wake, Rais wa Sahara Magharibi ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama cha Polisario Mohamed Abdelaziz, alimtumia Rais Kikwete salamu zake. Salamu hizo zilisema "As our brothers in Tanzania celebrate- with deserved pride- the 50th Anniversary of their independence, it is a great honour for me to express to you and through your Excellency to the people of Tanzania, our warmest congratulations on behalf of the Saharawi people, the government of the Saharawi Arab Democratic Republic and on my own behalf as well as our best wishes for success".
Abdelaziz aliongeza "Since its independence, Tanzania became a shrine for all Liberation Movement and Freedom Fighters of Africa" huku akinukuu maneno ya Mwalimu Nyerere kuwa "For, the right to freedom either exists throughout Africa, or it does not exist anywhere in Africa". Alimalizia salamu zake kwa ku-reiterate "our high appreciation and profound gratitude for the support and solidarity constantly extended by Tanzania to the just struggle of the Saharawi people for freedom and independence".
cc kwa waliokwishafuatilia hili zuala huko nyuma Sheba, FJM, harbab, Mbopo, Raia Fulani, petrol, POLITIBURO, fige, andishile, KIM KARDASH, Kiona, NasDaz, SURUMA, Tumaini Makene, Halisi, Filipo, Kimbunga, JokaKuu, Kichuguu, Mag3, omujubi, Njaare, TUJITEGEMEE, MgonjwaUkimwi, Sangarara, mtotowamjini, MTAZAMO, Nguruvi3, mlagha, TUNTEMEKE, Phillemon Mikael, Kiranga, Tume ya Katiba, Pasco, Precise Pangolin, Njoka Ereguu, Abdillahjr, BAK, Jasusi, Ben saanane, OTIS, ocampo four, DSN, Ogah, Viol, Alinda, Ubongo Silaha, Tina, The Boss, Jagermaster, alles, bucho, Keil, Bongolander, Candid Scope, Sheba, Sniper, manucho, Mpui Lyazumbi, Synthesizer, Tiote, Mkandara, Iza, kalokolaVIII, Sikonge, mharakati, Ukwaju, Chakaza, Mzalendo, Ndahani , W. J. Malecela, JacksonMichael, Njoka Ereguu, TIMING, newazz, KIDUNDULIMA, Kiduku, Mtumishi Wetu, mpujufu, mkomatembo, Kizotaka
Last edited by a moderator: