Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 59,021
- 132,763
Mkuu, kwanza asante kulichambua hili jambo kwa udani wake, mimi maoni yangu yatakuwa tofauti na wengi, ila huu ndio ukweli halisi!. Wakoloni walipotutawala sio tuu walijigawia maeneo yetu, bali pia walichukua na akili zetu na kuzitawala, kiasi kwanza hata baada ya kuisha kwa ukoloni, bado akili zetu nyingi zinatawaliwa na kitu kinachoitwa 'the colonial mentality', na nchi nyingi zilizokuwa colonized, hata baada ya kupata uhuru, zinaendelea kutawaliwa na the former colonial bosses kupitia neo colonialisim, na hii ndio basis ya msimamo wa UN kwenye suala na Western Sahara na AU is simply nothing but a puppet of UN ambayo imeshikwa na wale wale colonial masters!.Sahara Magharibi ilikuwa koloni la Hispania baada ya mataifa ya Ulaya kugawana makoloni kwenye ule mkutano wa Berlin wa mwaka 1884. Hispania walipoondoka Morocco iliikalia Sahara Magharibi kimabavu huku ikida kuwa eneo hilo ni sehemu ya himaya yake kwa sababu ukoo wa kifalme wa Morocco ulitokea eneo hilo kabla ya ukoloni. Hatua hiyo ilisababisha wananchi wa Sahara Magharibi kuingia katika harakati za ukombozi kwa kuanzisha kikundi cha Polisario cha kudai uhuru kwa njia ya mapambano.
cc kwa waliokwishafuatilia hili zuala huko nyuma Sheba, FJM, harbab, Mbopo, Raia Fulani, petrol, POLITIBURO, fige, andishile, KIM KARDASH, Kiona, NasDaz, SURUMA, Tumaini Makene, Halisi, Filipo, Kimbunga, JokaKuu, Kichuguu, Mag3, omujubi, Njaare, TUJITEGEMEE, MgonjwaUkimwi, Sangarara, mtotowamjini, MTAZAMO, Nguruvi3, mlagha, TUNTEMEKE, Phillemon Mikael, Kiranga, Tume ya Katiba, Pasco, Precise Pangolin, Njoka Ereguu, Abdillahjr, BAK, Jasusi, Ben saanane, OTIS, ocampo four, DSN, Ogah, Viol, Alinda, Ubongo Silaha, Tina, The Boss, Jagermaster, alles, bucho, Keil, Bongolander, Candid Scope, Sheba, Sniper, manucho, Mpui Lyazumbi, Synthesizer, Tiote, Mkandara, Iza, kalokolaVIII, Sikonge, mharakati, Ukwaju, Chakaza, Mzalendo, Ndahani , W. J. Malecela, JacksonMichael, Njoka Ereguu, TIMING, newazz, KIDUNDULIMA, Kiduku, Mtumishi Wetu, mpujufu, mkomatembo, Kizotaka
Ukweli ambao ni ukweli halisi, Western Sshara was part of Morroco before 1884 na wazungu washenzi hawa kuna nchi wamezigawa hata kati kati ya koo, na kuwafanya baadhi ya wana ukoo wako nchi moja na wanaukoo wengine wako nchi nyingine!. Sisi wa Afrika baada ya kila nchi kujitawala, tungepaswa tukae chini na kuifutilia mbali the colonial legacy ya washenzi hao waliotugawa na kufanya re patitioning ili zile koo zilizokatwa na colonia partitioning, zirejeshwe!. Eritrea irejeshwe Ethiopia na kufanyike consolidation ya himaya yote ya Abysinia. Baganda Kingdom irejeshewe maeneo yake ambayo Tanzania tungekubali kuwapoteza Wahaya na Wahangaza chini ya Bahima Kingdom, huku Warundi wangerudi kwetu!. Kule Arusha Wakenya wakubali kuwapoteza Wamasai na kulichukua eneo lote la Maasai Mara kulirudisha Tanzania, huku tukiwaachia Wajaluo wajirudie kwao!. Kule kusini tungepaswa kuwaachia Wamakonde waende kwao Msumbiji, na Wanyasa kuwa ni sehemu ya Malawi na hata Ziwa Nyasa kiukweli kabisa sio la kwetu!.
Wazungu hawa hawa waliotutawala kwa kupitia huko huko UN wanafanya double standard ya hali ya juu sana kupitia ujinga unaotwa Referendum, eti kisiwa cha Mayotte ni sehemu ya Ufaransa!. Leo unawapa masikini wa kutupwa option ya kupiga kura ya maoni kuchagua upande kati ya shida na heri!. Mfano umezaliwa kwenye familia masikini ya kutupwa, hohe hahe!, kisha Bill Gate aje na referendum upewe uhuru wa kuchagua unataka kulelewa familia gani kati ya familia yako ya asili, au assimileted family ya Bill Gates?!, nakuhakikishia kuna watu wata opt kuziacha familia zao za asili na kujiunga na Bill Gates huku wakijipongeza "to hell with umasikini"!. Hiki ndicho kinachofanyika kwenye hizo referendum za UN!. Leo ukiitisha referendum kwa Zanzibar kuhusu muungano, amini usiamini, wengi watasema no!, na ukiwa Zanzibar option ya kuchagua kama wanataka kuendelea kuwa part of URT na kujiunga na Ottoman Empire!, amini usiamini wata opt kujiunga na Oman!.
Mimi naunga mkono msimamo wa Morocco kuipa Sahara Magharibi mamlaka ya ndani kama ilivyokuwa kwa Palestina hapo mwanzo, lakini eneo hilo likabaki kuwa ni sehemu ya Morroco kama ilivyofanya kwa Taiwan, Hong Kong na Macau!. Kwenye vita vya Falkland mimi nilisimama na Argentina!.
Tena Waafrika ni watu wa ajabu sana!, Ghadafi alikuja na roadmap ya kuunda United States of Afrika na kushauri tuikate mizizi yote ya ukoloni kwa kuanzisha WB ya Afrika, IMF ya Afrika, mashirika ya mawasiliano na kila kitu kama ulaya kwa kupigia hesabu jumla ya rasilimali zetu zote za Afrika zikiwa consolidated, sisi ni matajiri mara 10 ya wazungu, why kila siku tubishe hodi kwenda kuwapigia magoti washenzi hawa?!. Wazungu walitishika na msimamo huu, kilichofuatia sote tunakijua!.
AU is just a barking dog! seldom bite!, ni toothless kabisa!.
Pasco