Kumekuwa na ujenzi wa hoja kwamba Chadema wanatekeleza elements fulani za azimio la arusha na kadhalika. Hii ni hoja nzuri na ya msingi sana, ingawa wanachama wengi wa chadema hawataki kabisa kusikia Chama chao kuhusishwa na TANU au azimio la Arusha; Mwaka jana nilianzisha mjadala kuhusiana na mfanano na utofauti baina ya TANU na Chadema; Hoja yangu ya msingi ilikuwa ni kwamba - Chadema kufananishwa na TANU is more of a political asset than a liability, huku mfananisho huo ni more of a political liability to CCM than political asset; uzi huo kama ifuatavyo:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/325723-chadema-na-tanu-mfanano-na-tofauti.html
Nikirudi kwenye hoja ya msingi, taifa letu kwa sasa linayumba kutokana na kukosa dira na mwelekeo ambao umekuwa digested, kueleweka na kukubalika na wananchi walio wengi; Marehemu Kolimba alijadili hili kwa kina na hoja yake inazidi kuwa na mashiko leo; Wakati wa ujamaa, kama taifa, tulikuja na maazimio kuhusiana na makubaliano juu ya nini tunataka, nini hatutaki, wapi tunataka kwenda na wapi hatutaki kwenda; Maazimio yote haya yakawekwa katika document moja ambayo ndio ilizaa azimio la arusha;jina Arusha ni kutokana na wapi kikao husika kilifanyika; maana yangu hapa ni kwamba - tusiogope neno azimio wala arusha kwani bado tunahitaji kuja na maazimio kama taifa juu ya wapi tunataka kwenda na tufiikaje katika safari tunayokudusia, na kikao juu ya hilo kinaweza fanyika Pwani, Tarime, Katavi, Simanjiro n.k; Kwa maana hii, kuna umuhimu wa kurudisha nchi katika mstari kwa kuja na azimio kwa mfano la Simanjiro iwapo tutaamua kufanyia vikao hivi muhimu huko; its as simple as that; sidhani kama kuna mwanachadema yoyote ambae anakataa kwamba nchi imekosa dira na inabidi tukae chini na kuja na maazimio na maamuzi magumu juu ya wapi tunataka kupeleka nchi yetu na njia za kufika huko tutakapochagua kwenda;
Kuna umuhimu wa watanzania kuacha kukubali propaganda kwamba mmiliki wa azimio la arusha ni TANU; Ukweli ni kwamba mmiliki huyo ni mtanzania ambae kwa wakati ule alikuja kubaliana na uamuzi kwamba tuanze na mfumo wa chama kimoja kwanza ili kujenga taifa kwa ufanisi zaidi, na hivyo mtanzania huyo alikubaliana na msimamo wa chama juu ya umuhimu wa azimio la arusha kwani ilikuwa ni njia pekee ya kutekeleza ahadi za uhuru; Mwalimu hakukurupuka kuja na azimio la arusha, the situation was so tense katika jamii, na alipoenda ziarani china kuangalia wenzetu wamefanya nini, ndipo akaja na wazo la azimio la arusha; Bottom line hapa ni kwamba mmiliki wa azimio la arusha alikuwa ni watanzania ambao leo hii baada ya mageuzi ya kisiasa, wengine ni wanachadema, wanaccm, CUF, NCCR, CCK, TLP, huku wengine wengi wakiwa hawana ushabiki wa chama chochote cha siasa; Kwahiyo hizi views kwamba Azimio la Arusha ni la TANU/CCM sio helpful, na kuna umuhimu wa kuweka mbele utaifa wetu katika hili; Iwapo Chadema mathalani wanataka kuja na manifesto ya kurudisha nchi kwenye mstari kwa mtindo wa maazimio Fulani, wajipange tu na kuchagua wapi wafanyie kikao hicho muhimu; Kikubwa ni waepuke kufanyia kikao hicho Kanda ya Kaskazini kwani Azimio la Kilimanjaro, Arusha, Manyara au Babati, hata kama litakuwa na manufaa makubwa kwa taifa, litashambuliwa kwa hoja nyingi za ovyo na wapinzani wa chadema, hasa wana CCM wasiokuwa na mapenzi na nchi yetu;