Wakuu
GAGL,
Mchambuzi,
Communist, na
Jethro , niwashukuru kwa mawazo mazuri yenye lengo la kujenga uelewa,na pengine kusaidia kuonesha njia ambayo taifa letu linatakiwa kuelekea kuanzia hapa tulipo.
Katika hoja ya msingi kwenye uzi huu, Mkuu GAGL anaonesha imani kuwa Chadema inao uwezekano wa kuleta uongozi mbadala, baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuonekana kukosa viongozi Waadilifu. Na wadau mmeonesha kukubaliana na msimamo huu, kwamba pana tatizo la Uadilifu katika namna nchi inavyoendeshwa.
Lakini Mkuu GAGL ameingiza suala la Azimo la Arusha katika hitimisho la hoja hii, kwa swali hili: "naomba kufahamishwa kuhusu msimamo wa CDM kuhusu Azimio la Arusha kwa sababu kilichopelekea nchi hii kukosa viongozi waadilifu ni kupuuza misingi ya uongozi [iliyoainishwa] katika azimio hilo. Mimi nalihitaji azimio hilo sasa sijui msimamo wa chama ninachokipenda na kutaka kujiunga kama kina msimamo huo pia. Mkuu
Mchambuzi amelaumu Breton Woods Institutions kwa kuzorota kwa uadilifu katika utendaji wa viongozi wa CCM na Serikali yake.
Nafurahi tunakubaliana kwamba tatizo kubwa la uongozi katika nchi yetu ni kukosekana kwa Uadilifu. Sidhani kama IFIs zina sababu ya kubeba lawama. Nakubaliana na Mkuu
Communist katika mtizamo wake huu: "IMF is just a Bank, haulazimishwi kukopa, Watafuta visingizio bana? Matajiri [wengi] wamepitia mikopo, hata makampuni ya China yalikopa. Issue kama ukakopa kuongeza mke hutaweza kulipa." Hili linaondoa hoja ya IFIs.
Tufanye nini kuleta uadilifu katika Serikali? Tutafute ufumbuzi tukijua kwa dhati kabisa kwamba tatizo ni internal--siyo external! Hili ndilo tunaitaji kulijadili. Mkuu
GAGL, anaamini suluhisho lipo katika kurejesha Azimio la Arusha, na angependa urudishwaji huo wa Azimio la Arusha ufanywe kupitia CHADEMA, chama ambacho amesema anakipnda.
Chadema haiwezi kurudisha Azimio la Arusha kwa sababu hii ilikuwa sera ya TANU. Lakini sioni ubaya wa kuchukua maudhui mazuri ya Sera ile na kuya integrate katika sera zake. Kwa bahati nzuri naona vijidalili kama tayari wanafanya hili--kitu ambacho kinanipa binafsi faraja sana. Na ninaomba kumpe Mkuu GAGL faraja pia. Nimalizie kwa kurudia maneno ambayo niliyasema awali. Ni kamkeka karefu kidogo, lakini naomba jipe nguvu usome hadi mwisho:
Mkuu GAGL kachukue kadi yako ya CHADEMA.
Kitu ambacho wengi wanakitamani katika Azimio na Arusha si jina la azimio lile, bali wanatamani maudhui yake fulani-fulani mazuri kwa taifa hili. Si kila kitu katika Azimio la Arusha kilikuwa sawa. Azimio la Arusha lilikuwa na Utopia nyingi sana mule, nikianzia na dhana kwamba mtu anaweza kuacha profit motive kabisa, kitu ambacho hakiwezekani. Kumbe kilichotakiwa kuonekana katika Azimio la Arusha ilikuwa dhamira ya ku-moderate profit motive. Mataifa yaliyoendelea yanafanya hivyo. Unaruhusu profit motive kushamiri, ila unai-moderate. Sera za CHADEMA zinatafuta kutumia profit motive kujenga uchumi wa taifa, lakini profit motive moderated.
Spirit ya kujikana reasonably, (narudhia: kujikana reasonably), ilikuwapo katika Azimio la Arusha. Kutaka wengine nao wapate faida katika yanayofanyika ndani ya taifa, hili lilikuwapo. Uadilifu katika utendaji ndani ya chama na serikali, hili pia lilikuwapo katika Azimio la Arusha. Na haya yanahubiriwa na wataalam wa mahubiri ya siasa katika CHADEMA.
Mi nionavyo, kikubwa katika Azimio la Arusha kinachostahili kukienzi ni Maudhui ya uadilifu katika kulinda maslahi ya kwako--wewe mtu binafsi--lakini kwa mtizamo kwamba wewe ni sehemu ya walio wengi, hivyo kwamba unafanya kazi unayoifanya kwa niaba ya wengi; yaani kwamba umepewa jukumu la kulinda maslahi makuu ya Taifa kwa ujumla wake, badala ya kulinda maslahi binafsi kwanza mtu anapokuwa katika nafasi yoyote ile ya uongozi. Chadema wanahubiri haya. Linda maslahi ya taifa kwanza. Mengine yafuate. Kwa hiyo hata kama hawatafufua Azimio la Arusha neno kwa neno kwa sababu lilikuwa na kasoro zake pia, maudhui katika Azimio la Arusha yenye nia njema kwa taifa tayari wanayahubiri.
Kwa maana hiyo, kama wewe ni mpenzi wa Azimio la Arusha, nina hakika utakuwa unalipenda Azimio lile kwa sababu ya maudhui yake mema. Maudhui ya uadilifu, maudhui ya kulinda masalahi makuu ya taifa kwa ujumla wake; kulinda maslahi ya Taifa kwanza kabla ya kulinda maslahi binafsi mtu anapokuwa katika nafasi yoyote ile ya uongozi. Haya Chadema inahubiri tayari na kwa kiasi kikubwa wanajitahidi kutekeleza mahubiri yao wao binafsi. Nilisikia John Mnyika anatembelea 'Vitz kobe' ndogo badala ya Prado. Niliipenda sana hii!
Wale unaosikia wamekiacha CHADEMA na kurudi CCM ni wale ambao walienda CHADEMA kutafuta ajira; wale ambao walienda kule kutafuta mianya ya utajirisho, wakidhani CHADEMA ni kama CCM. Walipokuta pale kuna kujitolea kwingi sana wakaona hapafai na kurudi kule ambako siasa malengo yake ni ajira ya utajirisho kwa hela halali na haramu. CHADEMA inatekeleza maudhui mema ya Azimio la Arusha nionavyo mimi. Hawawezi kutekeleza kila kilichokuwapo katika Azimio la Arusha kwa sababu si kila kitu kilikuwa sawa mule. Mengine hayakuwa sawa wakati ule, hayawezi kuwa sawa leo. Lakini pia Azimio la Arusha ilikuwa sera ya TANU. Chadema si TANU, japo inaweza ikawa KAMA TANU katika mambo fulanifulani. Huwezi kuzaa mtoto akafanana na wewe kwa kiiiiila kitu. Yapo mengine yatakuwa ya kwake yeye kama yeye.
Kachukue kadi mkuu. Ingia kwenye vita ya kurudisha heshima ya nchi yetu na utajiri wake mikononi mwetu. Go!