Nini msimamo wa CHADEMA kuhusu Azimio la Arusha?

Nini msimamo wa CHADEMA kuhusu Azimio la Arusha?

Azimio la Arusha halikufanikiwa kwa sababu ya Psychplogical make-up ya Mtanzania. Watu wanaopata uongozi kwa bahati mbaya walikua kimwili lakini kuna Psycho-analytic factors fulani katika makuzi yao zilidumaa--au hata niseme zimedumaa.
Gia automatic katika akili ya binadamu ambayo inamfanya individual KUTII zaidi maitaji ya ID, na kuanza kutii Ego, na Baadaye Super-Ego, gia hii ina matatizo katika Mila na desturi zinazozaa Watanzania wanaopata uongozi.

Mtu anayetii zaidi Id au Ego yake ni mbinfsi wa kupindukia. Tafufa neno narcissism au selfishness kwenye net ujue nasema nini kama tatizo letu katika viongozi tulio nao. Hata ukirudisha Azimio la Arusha leo. Yale ni maandiko tu. Halitafanya kitu. Narcissist kila kitu anachokitazama mbele yake anakitizama kwa mawani yaliyoandikiwa MIMI. Ukitaka kujua mtizamo huu vizuri mtizame mtoto ambaye bado hajasikia mafundisho yanayosema watu wengine ni muhimu pia: Mpe kitu leo, au mpe nafasi ya kumwezesha kumiliki kitu kizuri--toy, chakula, anything. five seconds later ukimwomba ataficha mgongoni kwake chake peke yake. Hapa watu wanakuwa na midevu kabisa hata na wajukuu lakini kisaikolojia hawakugraduate kutoka Ngazi ya Id na Ego. We have a very serious cultural problem hapa. Na tatizo lenyewe ni Psychological. Taifa linaitaji nut cracker kulinyoosha. Ukishoot narcissit wawili watatu wengine wataanza kuogopa.

Kuna kitu kiliitwa Marshall Plan kuisaidia Ulaya baada ya vita kuu ya Pili ya Duniani kwa sababu uchumi na miundombinu yote iliharibiwa na vita ile. Marekani waliwahurumia ndugu zao wa damu kwenye eneo lile baada vita na kuanza kuwajenga upya. Ulaya ilijirudi katika hali yake ya kawaida kwa msaada ule wa mamilioni na fedha za msaada kutoka Marekani. In less than 10 years chumi za ulaya zilipona.

Tanzania nimepewa mabilioni ya dola na mataifa ya Ulaya, Urusi, Uchina, Marekani yenyewe. Pesa hizi zimekuwa kana zinatupwa chooni vile. Why? Psychological make-up ya watu wanaomanage fedha hizi haina sifa kuzifanya zikawa za taifa, zikaleta maendeleo. Kutokana na viongozi na watawala wao kuwa manarcissist wanarubuniwa na wageni, individually au collectively, vikampuni vya wageni vinawahonga vihela wakazalishie malaya dodoma na kwingineko. Pesa kubwa zinaondoka na kurudi zilikotoka.

Hili ni aina ya mambo yamaitaji kufikiri kwingi. Watanzania hawana Culture ya kufikiri kwingi. Back to pysychological problems. Tuna tatizo kubwa sana hapa. Kulinyoosha taifa unaitaji nut cracker. Mtu atayeinyoosha hii inchi atakuwa kama Hitler hivi--japo kwa miaka 10 tu. Atayefanya kazi naye ajue anafanya kazi na tyrant, watawaliwa wajue wanafanya kazi na tyrant. ubinafsi-binafsi upewe kichapo cha kutisha nchi itanyooka tu.

Kurudi ama kutokurudi Azimio la Arusha hakuna maana bila ku-address issue ya culture yetu hapa, ambayo kwa kweli inaumwa. Tena inaumwa sana.





Mi nafikiri wanaoisifia IMF na Benki ya dunia wangetutajia angalau nchi zilizoweza kujikwamua kiuchumi kutokana na kufata mapendekezo yao tumekuwa tukizungumzia nchi za asia ambazo miaka ya 60 tulikuwa kiwango kimoja cha uchumi lakini leo hii zina nguvu kubwa za kiuchumi zilitumia mbinu gani lakini kuna nchi kama Libya,Irak na venezuela au China ambazo wamepata mafanikio makubwa kiuchumi je walikopa au kufata masharti ya IMF kwa kifupi azimio la arusha na azimio la irak ni mojawapo ya mikakati mizuri ya kiuchumi duniani wakati Irak walifanikiwa Hugo Chavez siku zote alijisifu mafanikio yake kiuchumi yalitokana na kufata azimio la arusha tunapoudhuria kongamano la jtano tunapaswa kujiuliza pamoja na mambo mazuri ya azimio la arusha kwanini halikufanikiwa
 
Kwa kuwa Azimio la Arusha lilianzishwa na TANU iliyokuja kuzaa CCM,

Na kwa kuwa azimio la Arusha lilifanyika mwaka 1967,

Na kwa kuwa CHADEMA ilianzishwa mwaka 1992,,,

Nakushauri usiihusishe CHADEMA na hayo makitu ya CCM ni usanii mtupu. Hata katiba yao na ya nchi inaelezea habari za ujamaa na kujitegemea lakini hakuna anayetekeleza. Hata azimio la Arusha likirudi leo Chenge hawezi kurudisha mabilioni aliyoficha Jersey, Ridhiwani Kikwete hawezi kurudisha kampuni ya UDA aliyojiuzia na jamaa zake wa Simon Group kwa bei poa, Rostam Azizi hawezi kutusamehe deni la Dowans. Dawa sio azimio la Arusha, dawa ni kuiondoa CCM madarakani tuje na maazimio mengine na mipango yetu ya kimaendeleo inayoendana na mahitaji ya sasa ya kiuchumi na kitechnolojia. Usiwaingize CHADEMA kwenye maupuuzi ya CCM

Jenga hoja kaka usiuze mbuzi kwenye gunia kwa sababu za ushabiki tu (Naona unajaribu kuipigia debe Chadema bila vielelezo). Eleza azimio litakaloletwa na chadema kama lipo, kwa kukusaidia labda ujaribu kucheki reply ya Highlander. Hajaleta azimio la chadema lakini kajaribu kujenga hoja juu ya Azimio la Arusha (Azimio lililoletwa na CCM kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla). Kwa mtazamo wake kajaribu kuainisha mema na pia mapungufu ya Azimio hilo. Mwenye Busara siku zote hukosoa kwakutumia nguvu za hoja.
 
Nilikuwa natafuta ku-highlight mambo muhimu kwenye post hii nikakuta sina cha kuacha hapo. Ha ha ha ha.... Umefanya kazi nzuri kwa kweli Mkuu (na kwanini unajiita Jingalafalsafa?) una mawazo mazuri; ila nimeona unao ugomvi na mambo mawili hasa: Una ugomvi na Azimio la Zanzibar (AZ), una ugomvi na IMF. Na kama nimekuelewa vizuri, haya matatizo mawili yana uhusiano kama wa yai na kuku. Bila IMF, AZ isingekuwepo. Na AZ ndo jini lililoua Azimio La Arusha, ambalo wewe unasema lilikuwa na nia njema kwa taifa. Na wengi tunakubaliana kwa kiwango kikubwa kulikuwa na mazuri katika Azimio la Arusha, moja likiwa 'timing' yake kwa mazingira ya wakati ule kama unavyo suggest.

Natofautiana nawewe kidogo kwenye misimamo inayoashiria unataka Azimilo la Arusha lazima kutekelezwa jumla, na ule msimamo ya Kuilaumu IMF kwa matatizo yetu--ikiwapo Rushwa. Kwako nataka niseme hili: IMF inasaida nchi nyingi Duniani. Na hizo nchi nyingine hazina matatizo kama tuliyo nayo Tanzania. Tuna cultural handicap ambapo asilimia kubwa ya viongozi wanakuwa watu ambao hawakufanikiwa ku-graduate kutoka childish tendencies kuufikia cognitive maturity. Viongozi ni mitoto ina mvi! That is our problem. Nakubali AZ ni janga la Taifa, lakini naamini kwa moyo wangu wote si IMFwalioleta upuuzi huu. Ni ujinga, upumbavu na ukosefu wa analytical skills ndani ya chama kilichokuwa madarakani wakati ule ndo tatizo limetuletea upuuzi huu unaitwa Azimio la Zanzibar. Nimetafuta sana document ile hadi leo sijaiona. Wanaificha saaana kwa aibu. Kama Mkuu JingalaFalsafa unayo tafadhali iweke hapa hii AZ watu tuione na kuijadili.

Lakini si kweli pia kwamba Azimio la Arusha haliwezi kutekelezeka vipande vipande. Hakuna mtu katika CHADEMA, au hata chama kingine ambaye atakataa kwamba Kulikuwapo na mazuri katika Azimio la Arusha. Hayo tunaweza kuya identify tukayapa jina--hata tukiyaita Azimio la Kisarawe haina tatizo na tuyateleze kwa mustakabali wa taifa letu. Nililipenda sana eneo hili katika post yako:

1. Tunatambua na kuamini fika kuwa UADILIFU katika uongozi ni nguzo bora kabisa kwa ustawi wa taifa lolote! Lakini hatutaki kukubaliana na GHARAMA halisi za huo UADILIFU. Ndio maana wengi(wanafiki) watasema Uadilifu uliojengwa na AA ni SAWA, lakini kanuni/miiko ya AA ni marufuku! Tunathubutu kusema eti tuishi maudhui ya AA tu, tangu lini FANI na MAUDHUI vikatengwa? Hapa linaibuka jambo la pili.

2. Watz wengi Hatutambui mafungamano yaliyopo katika siasa, tamaduni na uchumi. Hili linatufanya TUSHINDWE KU-RELATE siasa zetu na uchumi wetu na tamaduni zetu! Yaani tunataka asali lakini hatutaki kufuga nyuki. Ni Ulimbukeni. Ni wazi kuwa kama sera za uchumi zinakinzana na za siasa ama utamaduni, hapo ni maumivu tu ni lazima kutokee mgongano utakaowaumiza raia, hasa wa kawaida.


Dawa ni kupata uongozi more mature psychologicaly, waendeshe hii nchi with an iron fist LAKINI KATIKA UKWELI NA HAKI. Tutavuka tu!
Kingine ni kurudisha mazuri ya AA au hata kuyaboresha kwa kutafanya "wheel alignment" ya malengo makuu tunayojiwekea yatekelezwe katika misingi ya Azimio la Arusha jipya, ambalo linaweka consideration ya mila na desturi zetu; hii ina maana kama kuna mila destructive, tunazikandamiza katika Azimio hili jipya, sawasawa kabisa na lile la Kwanza.




Kabla sijaigusia CDM na AA, binafsi naona mambo mawili ambayo watanzania yanatusumbua!
1. Tunatambua na kuamini fika kuwa UADILIFU katika uongozi ni nguzo bora kabisa kwa ustawi wa taifa lolote! Lakini hatutaki kukubaliana na GHARAMA halisi za huo UADILIFU. Ndio maana wengi(wanafiki) watasema Uadilifu uliojengwa na AA ni SAWA, lakini kanuni/miiko ya AA ni marufuku! Tunathubutu kusema eti tuishi maudhui ya AA tu, tangu lini FANI na MAUDHUI vikatengwa? Hapa linaibuka jambo la pili.
2. Watz wengi Hatutambui mafungamano yaliyopo katika siasa, tamaduni na uchumi. Hili linatufanya TUSHINDWE KU-RELATE siasa zetu na uchumi wetu na tamaduni zetu! Yaani tunataka asali lakini hatutaki kufuga nyuki. Ni Ulimbukeni. Ni wazi kuwa kama sera za uchumi zinakinzana na za siasa ama utamaduni, hapo ni maumivu tu ni lazima kutokee mgongano utakaowaumiza raia, hasa wa kawaida.
Hayo mambo mawili ni baadhi kati ya yaliyowakuta wale walioshadadia kuvunjwa kwa AA, na yananifanya niamini wazi kabisa kuwa, wote walioshiriki kuua AA hawakutumia akili zao binafsi, walikubali kushikiwa akili na nguruwe weupe! Ni kosa lao na Mungu atawalaani milele! Hawa walikubali kurubuniwa kwa maneno matamu ya HAKI, UHURU, DEMOKRASIA, nao wakasema NDIO, pasi kuangalia mazingira yetu, imani zetu, watu wetu, n.k wakakurupuka tu na kuanza kudai Soko huria! Leo wameshndwa wanataka kuturubuni eti ni RUSHWA. Swali, kwanini hamkuchunguza kuona aina ya watu ambao mlipanga kuwapa sera zenu mfu na kujua watazipokeaje na mjipange namna ya kuwakabili? Mwenye akili(foreseer) angekuwa ameshaona Rushwa kabla ya kutushinikiza. Kigezo cha kiwango cha elimu to our degree of political consciousness tu, kingetosha kuiona Rushwa ya leo miaka kenda nyuma, matokeo yake mkaburuzwa tu kisa IMF wamesema mkatuingiza shimoni. Pumbavu!
Walioandaa AA hawakuwa wapumbavu KUMFUNGA mtanzania, waliona wazi kabisa kuwa kulingana na viwango vyetu vya elimu, historia yetu, imani zetu, mazoe, hali yetu ya kiuchumi, mitazamo yetu, n.k. ni lazima TUFUNGWE kujenga UADILIFU si katika uongozi tu bali katika maisha yetu yote kwa ujumla(kwa raia wote). Nawalaumu wana AA kwa kulegeza baadhi za vifungo, vilivyotoa mianya ya usaliti wa wanafiki.
Mkuu Mchambuzi@ anasema IMF intervention ilikuja kihole sana, ni kweli. Lakini si bahati mbaya, WALIKUSUDIA HILO, ndio maana werevu(pro-AA) waliona hlo na walipinga. Wenzetu wakafumba macho wasione HILA ZA WAZI za IMF&World Bank. Matokeo yake ndio haya Masikini hana chake tena leo! Then wanajiita wakombozi.

CDM na AA:
Mimi naamini kabisa AZ ni uozo tupu, na chochote kitokacho humo! Ilikuwako AA, ikazaliwa AZ ikaua AA na miiko yake yote, AZ(uozo) ukatoa funye mkubwa anaitwa Demokrasia mama wa uvundo wote wa leo. Kusingekuwa na CCM hii wala CDM kama uozo huu usingekuwepo.

Kamwe mzoga hauwezi kutoa kimfaacho mtu kula. CDM kama ilivyo CCM inaongozwa na kufungwa na kanuni na taratibu za mzoga huo (AZ) Kilichokuwa ndani ya Azimio la Arusha ni IMANI thabiti.

Kamwe haiwezekani kuiishi nusunusu, kama moto moto ama baridi baridi. Adui wa kwanza wa imani hiyo, ndio msingi wa CDM na CCM ya leo!
a4afrika.
 
Mkuu Highlander naomba nichangie hapa kwanza!
Psychological make-up ya mtanzania ndio iliyoangusha AA. Ni sahihi kusema hivyo, japo. Japo umetumia istilahi ngumu za kisaikolojia, nimepata concept hapo. Kuto-advance kwa watz na kubaki katika ngazi ya ID, mimi naita HULKA (nisahihishe kama sijaelewa vyema) kusukumwa na HULKA without Reasoning-Logic-MANTIKI. Hulka ndio mama wa Ubinafsi, kila binadamu anazaliwa akiwa nazo (ni innate qualities). Hulka kuu ya binadamu ni KUJIKWEZA-kutafuta UKUU mbele ya wengine! Hapo ndipo unapozaliwa UMIMI KWANZA-UBINAFSI-KUJIFIKIRIA TU.
Binadamu huyu anapoachwa huru kufuata HULKA zake, kitakachotokea ni mikwaruzano kila siku. Utajipigania kuwa juu yangu, na nitajipigania kuwa juu yako. NITAJIFIKIRIA TU SITAJALI KAMA HUKU JUU NILIPO NIMEKANYAGA MABEGA YAKO NA UNAUMIA-MIMI KWANZA. Ndio kinachotokea leo, kila mtu anahangaika kutumia resources za mwenzake kujikweza na kudunisha wengine. Tunakuwa kama simba amuangaliavyo mwanaswala . Hiyo ni ID-HULKA. Si kwa raia wa kawaida wala kiongozi-"HAKUNA BINADAMU ATAKAYEACHWA HURU KUFUATA HULKA ZAKE NA ASIZIFUATE" akitokea ndio tuwaitao "ma-charismatic_exceptional". Hatuwezi kukaa tukasubiri muujiza wa kutokea watu hao. WE HAVE TO MAKE THEM. Hapo ndipo linapoibuka hitaji la KUMFUNGA mwanadamu, kamwe asiachwe huru kufuata HULKA zake. Ninaamini kwa zaidi ya 90% Azimio la Arusha lilizingatia hayo na lilikuwa na uwezo huo wa kufunga hulka zetu. Lengo lilikuwa kujenga FIKRA sahihi kwanza, zitakazojenga MAHUSIANO SAHIHI kati ya mtu na mtu na rasilimali zao, kufikia Ustawi wa jumuiya nzima.
UFU wa mentality yetu sio sababu ya moja kwa moja ya kuanguka AA. Jibu sahihi kwanini AA haikufanikiwa ni kwa sababu kuna wapumbavu waliliua mapema kwa ku-pioneer AZ, kwanini watu hawa waliua AA jibu ndio hili "ni kwa sababu walitumia HULKA zao katika kufikiri(ushahidi ni hiki kitokeacho leo)-hivyo ikawa rahisi kwao kurubuniwa na HILA ZA MAKUSUDI za nguruwe weupe(walitumika), wakahubiriwa na bigijii za utamu mfupi eti HAKI, UHURU, Demokrasia n.k. Leo tumo shimoni Unyonge umetuzunguka kila kona!
AA haikufa, kwani bado ilikuwa na waumini waliotaka kuishi, MANTIKI ikakiukwa HULKA za watu zikashika hatamu! Ni ni KILIO.
Mkuu Highlander umenena vyema kuhusu Marshal Plan kwa Ulaya, na mabilioni tuliyopewa aidha kwa kukopa ama msaada, iwe China au IMF. FIKRA zetu hazikuruhusu kupewa hizo hela, ndio maana tulipopewa tukazitumbua. Sasa mwerevu angezikataa, lakini waliotumia HULKA zao wakazikubali tena under harsh conditions, wakazileta watu wakazitumbua. Nani wa kulaumiwa? Madeni yamebaki tulichofanya hakuna. Je huo si ulimbukeni?
Sitaacha kumlaumu aliyeasisi AZ, japo kamwe siwezi kumchukia kwani nina amini Mtu mweusi yeyote ni ndugu yangu, hadi pale atakaponikana.
Nikipata muda nitakujibu post yako iliyofuata.
Mungu wetu anaita sasa.
 
Last edited by a moderator:
Nimefurahi kujifunza kiswahili cha hili neno ID kutoka kwako Mkuu JingalaFalsafa. Lakini pia nishukuru kwamba nimeeleweka vema machoni pako. Ulichokielewa ndicho hasa nilichokimaanisha katika bandiko hilo. Sisi Watanzania, kama taifa, nakumbuka tuliingia katika Structural Reforms na baadaye Economic Reforms kufuatia taifa kuishiwa fedha za kigeni kabisa baada ya vita vya Uganda na nchi yetu. Nina hakika utakuwa unakumbuka miaka ile ya kufua nguo kwa mapovu ya katani vijijini na foleni za sukari mijini. Watanzania tumekwenda kutafua wafadhali mbalimbali, ikiwapo IMF, tukiwa na 'force majeure'; force majeure ambayo ni wingu zito la economic depression.

Tume ya Bei (Price Commission) inapanga bei ya bidhaa katika Mashirika ya Umma ambayo hayana raw materials wala spea za mashine kutoka nje ili kuzalisha. Tuna SCOPO (Tume ya kupanga mishahara ya wafanyakazi katika Mashirika ya Umma) ambako kimsingi hakuna kazi inafanyika huko. Uchumi mfu unaendeshwa na Serikali. Serikali ilikuwa inafanya biashara--biashara ambayo haikuwepo in the first place! Nadiriki kusema Vita na Uganda ndiyo ilaumiwe katika kuja kwa Rushwa nchini--si IMF na World Bank!

Taaluma ya biashara na taaluma ya fedha zina principles zake. Wanaofuata kwa usahihi taratibu hizo mbili wanafanikiwa. Wanaoshindwa wanashindwa. Tumekwenda kukopa fedha IMF na World Bank, wanakupa masharti kulingana na taratibu za fedha ambazo zipo kila mahali duniani. Ni wajibu wako kupanga utafanya nini na hizo fedha uzalishe, ulipe deni. Umeshindwa kulipa deni, it is none of their problem. Wao watachotaka ni ulipe tu hela zao.

Swali: Je tulipokwenda IMF na World Bank tulikuwa na wataalam wa uchumi wakapima hizo pesa zitazalisha nini na kwa utaratibu gani, na kwa muda gani. I'd say NO!. Hatukuwa na wataalam kama hao. Wangekuwapo zingeleta tija. Ukisema Yes, nitasema tulituma wezi kuchukua mikopo. Ndiyo maana hizi fedha za mikopo na misaada hazijabadili hali ya maisha kwa walio wengi. Zimebadili maisha kwa wale walio na access na hizo hela--access kwa njia ya Rushwa. Hakuna njama yoyote ya IMF na World Bank kutusababishia Rushwa. Tuliwafuata sisi, wakatupatia masharti, tukaahidi kuyatuata. Baada ya fedha kufika, HULKA ika-take over reason. Azimio la Zanzibar ikawa nji tu ya Justication ya Wizi.

Ukilaumu wito wa HAKI, UHURU, Demokrasia n.k. kuwa kigezo cha mikopo unakosea kwa sababu IMF na World Bank wana uzoefu wa mikopo sehemu nyingi duniani. Sharti hili ni muhimu kwa sababu ya Uwajibikaji. Wanajua kabisa katika mataifa ambako hapakuwa na political checks and balances pesa hizo security ni dogo sana. Penye Haki, Uhuru na hiyo Demokrasia ingalau panakuwa na pressure kidogo hizo hela ziwafae wananchi. CHADEMA inajitahidi sana kufanya kazi hii kwa kudai uwajibikaji katika matumizi mabaya ya fedha za umma. Hata huu wito wa kupigana na Rushwa ni kwa sababu pana huu Uhuru na Demokrasia.

AZ ilikuwa kuhalalisha wizi na Rushwa. Hebu iweke hii document ya Azimio la Zanzibar hapa mkuu kama una access nayo tuijadili. This is our problem. Hakuna njama hapa. Kuna wizi tu!
 
jenga hoja kaka usiuze mbuzi kwenye gunia kwa sababu za ushabiki tu (naona unajaribu kuipigia debe chadema bila vielelezo). Eleza azimio litakaloletwa na chadema kama lipo, kwa kukusaidia labda ujaribu kucheki reply ya highlander. Hajaleta azimio la chadema lakini kajaribu kujenga hoja juu ya azimio la arusha (azimio lililoletwa na ccm kwa manufaa ya taifa kwa ujumla). Kwa mtazamo wake kajaribu kuainisha mema na pia mapungufu ya azimio hilo. mwenye busara siku zote hukosoa kwakutumia nguvu za hoja.

tanu 1967,ccm 1977,kwa hiyo azimio la arusha linazungumzia tanganyika inayotakiwa na cdm,je ccm mnaitaka tanganganyika?
 
Nimefuatilia kwa makini sana kuhusu mwenendo wa vyama viwili vikubwa na kugundua kuwa ili nchi hii isonge mbele, ni lazima ccm iondolewe madarakani. Na chama konachostahili kushika dola ni chadema ambaye ndiye changamoto kubwa kwa ccm.

Lakini kabla sijachukua kadi ya cdm, naomba kufahamishwa kuhusu msimamo wa cdm kuhusu Azimio la Arusha kwa sababu kilichopelekea nchi hii kukosa viongozi waadilifu ni kupuuza misingi ya uongozi iliyoanishwa katika azimio hilo.

Mimi nalihitaji azimio hilo sasa sijui msimamo wa chama ninachokipenda na kutaka kujiunga kama kina msimamo huo pia.
huwezi kupima chama kwa kuwa eti wanaunga mkono azimio la arusha au la, that is very low! hata ccm huwa nawasikia katika majukwaa ya kisiasa kuwa nao wanaunga mkono azimio la arusha..
and one more thing...... hebu tuache kuishi kwa kuangalia nyuma mambo yaliyopita?
ngoja nikuulize swali, umewahi kulisoma azimio la arusha (wewe mwenyewe personally) na kulielewa?
kama umewahi, utagundua kuna vitu kwa wakati tuklionao ni inappropriate, ndo maana nasema tuache kuishi kwa kutazama nyuma (hiyo ni dalili ya kukata tamaa).!
azimio la arusha liliwekwa na watu, hebu basi tukae chini ni kuweka misingi (au tunaweza kuliita azimio kama wengi mnavyopenda) ya uongozi thabiti ili ituvushe katika hali hii ya kukata tamaa..
 
Mara nyingi huwa naambiwa na jamaa zangu kuwa nina mawazo dhahania. Yanapingana na Falsafa ama misingi mikuu ya dunia! So mawazo yangu ni ya kusadikika-can NEVER LIVE. Hadi leo hii sijashawishika kuwaamini, lakini kwa vile wako wengi wanaodai falsafa hzo za dunia, ambazo mimi siziamini, basi ni wazi kuwa mimi ni mjinga/mfinyu wa maarifa juu ya falsafa hizo hadi pale nitakapowaamini ama wao kuniamini! Nimekubali kuwa mimi ni mjinga wa falsafa hzo, ninajiona hivyo kama jingalafalsafa, hadi pale itakapodhihirika tofauti. Mkuu Highlander lisikukwaze sana jina hilo.

Hakika ugomvi wangu ni mkubwa sana dhidi ya hao wenye HILA. Ndio waliosimika misingi ya UNYONGE WETU. Siwezi kukilaumu chama moja kwa moja, kwani ndani ya chama walikuwepo waliopinga upuuzi huu wa AZ, Nyerere akiwemo. Nina hakika Nyerere asingeshindwa kuwadhibiti wanafiki(internal forces) walioshadadia AZ, lakini alishindwa mwishowe akaishia kutembea na nakala tu ya AA. Kipi kiliwapa kiburi hawa waasisi wa AZ, nani alikuwa nyuma yao aliyemzidi nguvu hata Nyerere? Kiburi cha hawa watu kulipinga AA na kusimika AZ kilitoka wapi kama sio mataifa makubwa under IMF? Sitamaliza ugomvi nao milele!

Kama nilivyosema katika post ya juu. Nina imani ya zaidi ya 90% kuwa AA lina uwezo wa kusimamia hulka zetu katika kuhakikisha tunajenga taifa na hatulibomoi. Kwa imani yangu, hatupaswi kuchagua yaliyo mema kutoka AA, bali tunachotakiwa ni KULIFANYIA MABORESHO TU sehemu chache kukidhi mazingira na nyakati zilizopo! Cha ajabu tukalitupa zima zima! Ni upunguani. HAKUKUWA NA HAKUNA HAJA YA KUWA NA AZIMIO JIPYA NJE YA MISINGI MIKUU YA AZIMIO LA ARUSHA. Wala hakuna haja ya kutekeleza vipandevipande, kwani linajitosheleza kwa kiasi kikubwa sana. Pia si kweli kuwa analytical skills zilikosekana ndani ya chama, zilikuwepo lakini zikazidiwa nguvu na HULKA za watu. Nguvu hiyo ilitoka wapi kama si IMF?
Kama miguu yetu ni michafu kuvaa viatu visafi, suluhisho si kuvitupa viatu ama kuvichafua navyo, bali ni kusafisha miguu yetu ili tuvae kiatu kisafi. AA ilitambua hilo, and it was going to handle it gradually! HILA zikakwamisha!
YES, dawa ni kupata viongozi ambao ni matured psychologically. Lakini ni lazima watengenezwe. Nani wa kuwatengeneza-ni MIMI NA WEWE=SISI. Uongozi bora si miujiza, ni HESABU naamini AA lilikuwa nazo. Tuanze kwanza na kuunganisha FIKRA zetu tupate IMANI kuu. Mengneyo yatafuata. MAENDELEO NI HESABU.
Mungu wetu anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Nikuombe ruksa yako Mkuu JingalaFalsafa, kutamka neno hili: kwamba wewe una mapenzi mema na taifa letu. Yapo mengi ambayo nakubaliana nawe katika bandiko lako lililopita. Baada ya hili niombe sasa kukujibu kwa mtindo tofauti kidogo kama ifuatavyo:

WEWE: ugomvi wangu ni mkubwa sana dhidi ya hao wenye HILA. Ndio waliosimika misingi ya UNYONGE WETU. Siwezi
kukilaumu chama moja kwa moja, kwani ndani ya chama walikuwepo waliopinga upuuzi huu wa AZ, Nyerere
akiwemo. Nina hakika Nyerere asingeshindwa kuwadhibiti wanafiki(internal forces) walioshadadia AZ, lakini
alishindwa mwishowe akaishia kutembea na nakala tu ya AA. Kipi kiliwapa kiburi hawa waasisi wa AZ, nani alikuwa
nyuma yao aliyemzidi nguvu hata Nyerere? Kiburi cha hawa watu kulipinga AA na kusimika AZ kilitoka wapi
kama sio mataifa makubwa under IMF?


MIMI: Naomba niruhusu kusema panapotokea tatizo katika nyumba, hata kama unao uhakika kabisa kuna mkono
wa mtu kutoka nje, swali zuri kujiuliza ni vizuri likawa nani kampa imani kwamba anaweza kufanikiwa
kutenda hilo hapa ndani ya nyumba yangu? Jibu lazima litakuwa kwamba ameona udhaifu unaomruhusu kufanya
hilo katika nyumba hiyo. Kwa hiyo hata kama ni mwizi kutoka nje kaweza kuingia nyumbani mwako na kukuibia,
jibu lililo sahihi katika picha hiyo ni kwamba wewe ndiye uliyejenga mazingira yaliyomwezesha mwizi yule
kufanikiwa kuingia na kuiba. Kwa hiyo tatizo si mwizi kutoka nje. Tatizo ni wewe uliyejenga mazingira ya
kumwezesha kuiba. Falsafa ya Kiswahili inayosema Kikulacho kii nguoni mwako ni mwafaka katika picha hii. Hata
kama mataifa makubwa yaliweka mashinikizo katika IMF kuweka maelekezo ya matumizi ya fedha za IMF, bado hili
haliwezei kuitwa HILA. Litaitwa Masharti. Hila ni kitu kinachofanyika kwa siri. Masharti ya IMF huwa siyo siri.
Unayakubali ama unayakataa. Tulikubali kwa hiari yetu wenyewe. Kwa hiyo hapakuwapo HILA katika hili.

Nikuelekeza sasa kwenye alimu ya mtaani; yaani kwenye uzoefu wa kipindi kile Azimio la Zanzibar lilipozaliwa.
Ali Hassan Mwinyi ndiye alikuwa rais wa Tanzania. Mshauri wake wa Uchumi alikuwa Ibrahim Haruna Lipumba.
Ali Hassan Mwinyi alikuwa ana tatizo moja. Serikali aliyokuwa akiiongoza ilikuwa ina allegiance kwa Nyerere bado.
Ninazo taarifa kwamba kuna mafaili fulani fulani ya Siri za Serikali watumishi wa Serikali walikuwa wanamuonesha
Nyerere kwanza kabla ya kumpa Ali Hassan Mwinyi--hasa watu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Mwinyi hakulipokea hili vizuri. Alihisi kama kwamba anafanya kazi na Parellel President. Ili kumwonesha Nyerere
kwamba yeye hasa ndiye alikwa Rais, kuna mambo fulani fulani Mwinyi aliyafanya kivyake, hili la AZ naamini
lilikuwa mojawapo. Kwa nini hili la kuflex muscle liwe ni Azimio la Zanzibar na si kitu Kinginge? Chini ya Ushauri
wa mtoto wa Kinyamwezi kutoka Uyui, Tabora, Ibrahim Haruna Lipumba, Mwinyi alitumia Monetary Theory ya
Milton Freedman kupandisha ujazi wa fedha katika uchumi iwe njia ya ku-stimulate uzalishaji, kustimulate
biashara. Sera hii ilileta tangazo la RUKSA. Katika nadharia za uchumi, hakuna ubaya kustimulate productivity
kwa kutumia ujazi wa fedha, ingawa hilo huambatana na mfumuko wa bei. Na hivyo ndivyo ilivyotokea kipindi
kile. Nakumbuka inflation rate ilikuwa inagonga hadi 40%. Matumaini huwa kwamba baadaye rate zitashuka iwapo
hizo biashara zilizoanzishwa zitaanza kuzalisha bidhaa za kutosha na kulazimisha inflation kushuka kwa sabu
bidhaa zinaongezeka.

Naamini kwamba Azimio la Zanzibar lilizuka, moja ikiwa njia ya Mwinyi kujitambulisha yeye ni rais na anaweza pia
akafanya kitu tofauti, lakini pili, kwa ajili ya kuwapa ruksa waliokuwa katika madarka kushiriki kuanzisha makapuni
na biashara mbalimbali.

Mimi binafsi sina ugomvi kabisa na dhana ya mfanya kazi wa Serikali kuendesha biashara. Tatizo lililokuja--na
ambalo ndiyo departure kubwa kutoka Azimio la Arusha ni Ruksa hii kutolewa pasipo kufanya sensa ya hawa
wafanyakazi waliingia serikalini na kitu gani? Ili wakijenga hoteli kubwa Ruaha mbuyuni au kununua hisa kwenye
mabasi ya Scandinavia tuhoji kama hizi ni pesa halali au haramu. Rushwa Serikalini iliruhusiwa, kukomazwa na
kupewa baraka na Azimio la Zanzibar kwa njia hiyo: yaani kutoa Ruksa ya wafanyakazi wa Serikali kujiingiza katika mambo ya biashara wakiwa bado wafanyakazi wa serikali pasipo kulazimishwa sensa ya kuhakiki waliingia na nini katika ajira ya Serikali. Kufikia miaka ya 1993, 94,na kuendelea, kila mwenye nafasi ya ajira serikalini alikuwa anaiba kwa urefu wa kamba yake akajenge mbezi, akafungue kisteshenari karibu na Club Bilcanas, au kujenga jumba la fahari Segerea.

Azimio la Zanzibar tatizo lake kubwa lilikuwa ni kule kutangazwa kabla ya sensa ya utajiri wa wafanyakazi wa
serikali. Basi. Hiki ndo kiini hasa cha Rushwa serikalini.

WEWE: Nina imani ya zaidi ya 90% kuwa AA lina uwezo wa kusimamia hulka zetu katika kuhakikisha tunajenga taifa na
hatulibomoi. Kwa imani yangu, hatupaswi kuchagua yaliyo mema kutoka AA, bali tunachotakiwa ni KULIFANYIA
MABORESHO TU sehemu chache kukidhi mazingira na nyakati zilizopo! Cha ajabu tukalitupa zima zima! Ni
upunguani. HAKUKUWA NA HAKUNA HAJA YA KUWA NA AZIMIO JIPYA NJE YA MISINGI MIKUU YA AZIMIO LA
ARUSHA. Wala hakuna haja ya kutekeleza vipandevipande, kwani linajitosheleza kwa kiasi kikubwa sana. Pia si
kweli kuwa analytical skills zilikosekana ndani ya chama, zilikuwepo lakini zikazidiwa nguvu na HULKA za watu.

MIMI: Kule marekani kuna msemo huu: "there is more than one way to skin a cat." Azimio la Arusha lilikuwa na vionjo
vya kusimamia uchumi ambao unaongozwa ha Serikali. Sehemu kubwa ya dunia imefutilia mbali dhana ya Serikali
kufanya biashara. Tanzania imekwisha achana kabisa na upuuzi wa Serikali kufanya biashara, na mimi ni mmoja
kati ya watanzania wanaounga mkono mtizamo huu mpya. Dhamira ya Kuidhibiti HULKA naiunga mkono. Tatizo la
HULKA linasumbua mifumo yote ya uendeshaji wa serikali na hata uendeshaji wa biashara, kwa kuna haja ya
kutengeza utaratibu wa kudhibiti HULKA. Kule Marekeni walilazimika kupitisha sheria zilizoitwa Anti-rust na
anti-oligapoly kwa sababu hiyo. Kwa hiyo usifungwe na Azimio La Arusha. Fungwa na dhana ya udhibiti wa
HULKA, hata kama itaitwa jina jingine.

WEWE: Kama miguu yetu ni michafu kuvaa viatu visafi, suluhisho si kuvitupa viatu ama kuvichafua navyo, bali ni
kusafisha miguu yetu ili tuvae kiatu kisafi. AA ilitambua hilo, and it was going to handle it gradually! HILA
zikakwamisha! YES, dawa ni kupata viongozi ambao ni matured psychologically. Lakini ni lazima watengenezwe.
Nani wa kuwatengeneza-ni MIMI NA WEWE=SISI. Uongozi bora si miujiza, ni HESABU naamini AA lilikuwa nazo.
Tuanze kwanza na kuunganisha FIKRA zetu tupate IMANI kuu. Mengneyo yatafuata. MAENDELEO NI HESABU.
Mungu wetu anaita sasa!

MIMI: Mawazo haya nayaunga mkono kwa moyo wangu wote. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika!
 
Nimeombwa na WanaCDM kadhaa nijibu thread iliyoanzishwa na MwanaJF "Gagl" anayeuliza ni nini Msimamo wa CHADEMA kuhusu Azimio la Arusha.

Niseme kwanza kwamba nimebahatika kuwa Muasisi na Mwenyekiti (Taifa) wa kwanza wa Chadema. Pili, licha ya kwamba naendelea kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama, sijaweza kujadili maudhui ya mada hii na viongozi wenzangu.

Tatu, nafarijika kuona kuwa MwanaJF Gagl anapenda misimamo ya chama na anaweza kujiunga nasi katika harakati zetu za kuchukua dola ili misimamo na sera zetu zitekelezwe kuhudumia umma.

Nne, nieleze kwamba nilibahatika kukaribishwa kuhudhuria Mkutano wa N.E.C. ya TANU wakati Azimio la Arusha likijadiliwa mwanzoni mwa Februari, 1967. Nilikuwa mwanachama wa TANU (tangu nikiwa Chuo Kikuu, 1956), lakini kualikwa kwangu kulitokana na kuwa Gavana wa BoT ambayo ilikuwa imeanza tu mashughuli yake kikamilifu Juni,1966.

Wakati wa majadiliano Mwenyekiti, Mwalimu Nyerere, aliniruhusu nichangie; na mchango wangu ulihusu jinsi watu wenye fedha Tanzania walivyokuwa wameanza kutorosha fedha zao toka nchini. Nilisisitisha kuwa matajiri walikuwa wamekosa imani na Tanzania kutokana na taarifa zilizokuwa zinatolewa toka mkutanoni Arusha.

Benki Kuu ilikuwa inalazimika kuzibadilisha kwa forex, hizo fedha za Tanzania zilizotoroshwa; na kwa hiyo akiba yetu ya fedha za kigeni ingepungua kiasi cha kuathiri uwezo wetu wa kuagiza bidhaa muhimu toka nje. Nilisisitiza kuwa wakati wa kutekeleza maazimio itatupasa tulipe fidia kwa mali zitakazotaifishwa. Kutokana na maelezo yangu, Rais Nyerere aliagiza Waziri wa Fedha (wakati huo akiwa Amir Jamal) na mimi tushirikiane kuweka udhibiti wa malipo (Exchange Control) kati yetu na nchi zote, pamoja na Kenya na Uganda zilizokuwa katika Soko la Pamoja.

Inavyokumbukwa, sio tu tulitaifisha mabenki na makampuni yote makubwa ya viwanda na biashara na mashamba makubwa, bali chini ya taratibu na mikakati hii, Serikali ilianzisha mashirika mengi ya kibiashara. Mengi ya haya mashirika ya umma yalianza kudorora miaka michache baadae kutokana na ufinyu wa mitaji, teknolojia zisizokidhi hali halisi, ukosefu wa wataalam wa kuyaendesha, ukosefu wa uadilifu, wizi na mara nyingine kuingiliwa na wanasiasa waliokazania maslahi binafsi. Ukosefu wa malighafi toka ng'ambo na vipuri wakati tulipopungukiwa na fedha za kigeni sana, vililazimisha kufungwa au kufilisika kwa viwanda. Uchumi wetu uliathirika sana miaka ya 1980/85 kutokana na ung'ang'anizi wa utekelezaji wa sera hizi; ukame na athari za ongezeko kubwa la bei za mafuta ya petroli, vikichangia.

Naweza kusema kwamba Tanzania tulijikongoja na kupiga hatua, tukisifika kuwa nchi ya amani na utulivu. Hii hasa ilitokana na uongozi wa Mwalimu Nyerere ambaye alisifika kimataifa kwa uadilifu wake na kwa misimamo yake ya kutetea wanyonge ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Fursa ya kuanzisha vyama vingi vya siasa ilitufanya sisi tuliyoona na kuonja athari za ung'ang'anizi wa sera zisizotekelezeka, kuasisitiza umuhimu wa demokrasia na maendeleo. WanaChadema tumejaribu kuboresha misimamo yetu tangu chama kisajiliwe, na hasa kuanzia 2004, uongozi umesisitiza umuhimu wa michango ya vijana na wanazuoni; tukihakikisha tunazingatia uongozi wenye uadilifu.

Mimi binafsi naamini na ninasisitiza kwa wanaChadema viongozi wenzangu kwamba mtiririko wa muda mrefu wa mitaji mikubwa mikubwa ni muhimu kwa kuchapuza na kuharakisha kukua kwa uchumi wetu. Maliasili zetu ni nyingi na zinasubiri uwekezaji. Pia miundombinu ni aghali na inahitaji mikopo ya muda mrefu kama ya Benki ya Dunia au ruzuku toka kwa wahisani. Ni ujinga kuogopa mikopo.

Ubia baina ya Wazawa na vyama vyao vya ushirika kwa upande mmoja, na Wawekezaji wakubwa toka ng'ambo kwa upande mwingine uhimizwe, tukihakikisha wazawa wana hisa miliki. Papo hapo utaalamu na teknolojia za kisasa vihimizwe kwa vijana wetu. Hakuna Kulala.

Nifafanue na kusisitiza kwamba, kama demokrasia ya kweli itatumika kupata uongozi wetu, basi umma utaongoza na kudhibiti Serikali na maslahi ya wengi (yaani kuondoa unyonge na umaskini) vitazingatiwa.









 
Nimeombwa na WanaCDM kadhaa nijibu thread iliyoanzishwa na MwanaJF "Gagl" anayeuliza ni nini Msimamo wa CHADEMA kuhusu Azimio la Arusha.

Niseme kwanza kwamba nimebahatika kuwa Muasisi na Mwenyekiti (Taifa) wa kwanza wa Chadema. Pili, licha ya kwamba naendelea kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama, sijaweza kujadili maudhui ya mada hii na viongozi wenzangu.

Tatu, nafarijika kuona kuwa MwanaJF Gagl anapenda misimamo ya chama na anaweza kujiunga nasi katika harakati zetu za kuchukua dola ili misimamo na sera zetu zitekelezwe kuhudumia umma.

Nne, nieleze kwamba nilibahatika kukaribishwa kuhudhuria Mkutano wa N.E.C. ya TANU wakati Azimio la Arusha likijadiliwa mwanzoni mwa Februari, 1967. Nilikuwa mwanachama wa TANU (tangu nikiwa Chuo Kikuu, 1956), lakini kualikwa kwangu kulitokana na kuwa Gavana wa BoT ambayo ilikuwa imeanza tu mashughuli yake kikamilifu Juni,1966










Heshima kwako mzee Mtei....hongera sana kwa kujitokeza kujibu hii hoja.....Labda nikuulize....Huoni sasa kwa vile falsafa ya azimio la Arusha ilitupwa na ccm nyie CDM mnaweza kui re-adopt na kuifanyia kazi???...kwasababu ni falsafa ambayo ilifanya kazi na kuonyesha matokeo...

..Lingine labda ombi muhimu kwako: Huoni ni muhimu kwako sasa kama muasisi wa CDM...kutafta muda na vijana wa CDM ukaongea nao wote namna ya kuimarisha chama?....nasema hivi nikirejea matukio mabaya ambayo yamekua yanaashiria michafuko ndani ya vijana wa CDM....huoni ni muhimu sasa kwa wewe kuwaandaa hawa vijana...maana mwisho wa siku nao watashika hatamu za chama!.....Ni hayo tu mzee....ningeshukuru kama ungeyatolea ufafanuzi.....
 
Heshima kwako mzee Mtei....hongera sana kwa kujitokeza kujibu hii hoja.....Labda nikuulize....Huoni sasa kwa vile falsafa ya azimio la Arusha ilitupwa na ccm nyie CDM mnaweza kui re-adopt na kuifanyia kazi???...kwasababu ni falsafa ambayo ilifanya kazi na kuonyesha matokeo...

..Lingine labda ombi muhimu kwako: Huoni ni muhimu kwako sasa kama muasisi wa CDM...kutafta muda na vijana wa CDM ukaongea nao wote namna ya kuimarisha chama?....nasema hivi nikirejea matukio mabaya ambayo yamekua yanaashiria michafuko ndani ya vijana wa CDM....huoni ni muhimu sasa kwa wewe kuwaandaa hawa vijana...maana mwisho wa siku nao watashika hatamu za chama!.....Ni hayo tu mzee....ningeshukuru kama ungeyatolea ufafanuzi.....


Mkuu Nderingosha, mimi nina ombi maalum kwako. Tuna bahati kubwa kupata uwepo wa Mzee Edwin Mtei kwenye uzi huu.
Ombi langu ni hili: Tafadhali ondoa sehemu ya pili ya swali lako ili kutokuhamisha focus ya Uzi. Tumekuwa tunajadili Azimio la Arusha na kwa kiasi fulani Mchango wa IMF na World Bank katika dispensetion ya siasa za uchumi wa Tanzania.

Umeingiza mambo ya CHADEMA NA VIJANA kuondoa focus ya Uzi tafadhali. Tumuombe Mzee ajadili Azimio la Arusha na mchango wa IFIs (au niseme Bretton Woods Institutions) kwenye mazingira ambayo tunayo sasa: hasa tatizo la Rushwa.


Naomba kuwasilisha kwako Mkuu.
 
Mkuu Highlander, binafsi cjapata kuliona AZ zaidi kulisoma tu hapa na pale! Huwa napenda kutafakari na kuchambua jambo lolote kwa kutumia ile Core Value yake, kwani humo kila kitu kitajitokeza! Pia utaniwia radhi, umri wangu hahukurusu kuliishi Azimio la Arusha! Sina experience yoyote, japo tafakari zangu zinanifanya nijione huko.
Mkuu Highlander nakiri kutokupata vyema hapa unapoilaumu Vita ya Uganda na Rushwa! Ni hivi, si kwamba kipindi cha AA hakukuwa na Rushwa, wahujumu uchumi walikuwepo na rushwa ndio ilikuwa nguzo yao kuu. Tunacholisifu AA ni kuwa lilikuwa na Taratibu za kuibana mianya hiyo ya rushwa. Si kwa kutunga sheria tu, bali ni total ways of life zilimjenga Mtz kuichukia Rushwa. Taratibu hizo hazikuvunjwa na Vita ya Kagera, bali ni AZ kwa vigezo vya HAKI ZA BINADAMU, DEMOKRASIA, Free Economy n.k!
Ni kweli taaluma ya biashara na taaluma ya fedha zina kanuni zake! Lakini kanuni hizo haziwezi kuwa sawa duniani kote kwani kanuni hizo hutakiwa kusadifu Mazingira na Nyakati za eneo husika. Zinapokiuka tu, ni MIGONGANO. Hapo ndipo ninapoilaumu IMF na kanuni zao BATILI walizotushinikiza kuzifuata! Matokeo yake ni haya, ya kiongozi mchaguliwa na wananchi kusafirisha nyara zetu nje, na bado akaendelea kutukenulia meno.
Mkuu Highlander kuwa na wataalamu wa uchumi ama kutokuwa nao siko kunako halalisha ama kubatilisha mikopo under IMF conditions. Muhimu hapa Je, tulistahili kuchukua mikopo hiyo under conditions zao? Je, conditions zao ni relevant kwa Mazingira na Nyakati zetu? Mkuu wangu Highlander, naamini unaweza kutafakari vizuri maneno haya mawili HAKI na UHURU kwa misingi ya Demokrasia husianisha na mazingira na nyakati zetu halisi. Utaona kilichojificha humo!
Mkuu Highlander:
1. Si mimi mkuu niliyejenga mazingira ya usaliti wa watoto wangu! Kwanza wao ni watu wazima, walipaswa kuwa reasonable. Cha kushangaza wakatumia muda ambao nilikuwa naugulia kitandani maumivu yangu niliyopata gerezani, waka-side na adui zangu. Nakiri kuwa sikupata muda wa kuwaandaa vyema wanangu, kwani tangu wanazaliwa nipo kifungoni.
2. Mkuu wangu, tunaposema Njama/HILA za IMF hatuangalii masharti yao! Ni wazi masharti yao yanavutia machoni. Lakini yepi ni matokeo ya kufuata masharti yao kulingana na Mazingra na Nyakati zetu? Nitakupa mfano: Tumeshinikizwa kutumia njia ya wengi wape katika kufanya maamuzi yoyote(demokrasia-uhuru wa kuchagua). Embu mfikirie bibi yangu aliyeenda kupiga kura 2010 aking'ang'ania aoneshwe sehemu ya Nyerere ampigie kura! Mfikirie mama yangu aliyetembea aliyepiga kura kwa kuhongwa kitenge. Mfikirie na dada na kaka zangu waliopiga kura kwa mahaba yao ya vidole viwili juu tu, ama ngangari tu, ama waliobebwa kwenye rori tu. Matokeo yake ni nini? Si kupata viongozi walioenda kusaini mikataba nyeti ughaibuni? Kiongoza under Demokrasia kwa sehemu ambayo ni relevant, huchaguliwa kwa uzito wa sera zake. Je, political conciousness yetu inaruhusu hilo? Kama laa, kipi kinachosimika viongozi wetu kama si HULKA/MAHABA yetu? Unadhani IMF hawakuona hilo?
3. Naomba nikujibu baadae kuhusu State Control Economy. Ila niseme tu ndio relevant economy kwa nchi nyingi za Afrika, lakini gharama yake ni AFRIKAMOJA, kama hatuwezi ni ndoto kuwaza maziwa na asali.
(Natumia simu Mkuu wangu, inanisumbua kidogo) Tumsikilize Mzee wetu nadhani atatusaidia sana, tunashukuru kwa ujio wake!
Mungu wetu anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Wakati tukimsubiri Mzee wetu kuweka mchango wake wa ziada hapa, nikiri kwamba haya mambo yanayoitwa HAKI ZA BINADAMU, DEMOKRASIA, Free Economy n.k! ni kweli kwamba yanayo mapungufu yake.

Demokarasia kwa mfano, huu ni utaratibu ambao nakubaliana nawe unaleta shida unapotumika katika mazingira yenye ufinyu wa elimu; hasa ufinyu wa elimu! Tatizo linakuja kwa sababu ili demokrasia ifanye kazi vizuri, unahitaji watu wajadili Issues (nadhani tafsiri yake sahihi itakuwa ni kujadili masuala ya msingi).Ufinyu wa elimu unapunguza faida ya demokrasia kwa sababu vigezo vya uchaguzi vinavyotumika si lazima viwe vya uelewa wa issues. Migongano unayoizungumzia inaweza kuja kwa namna hiyo.

Lakini je, upande wa pili wa shilingi hii umekaaje? Tunapata nini pasipokuwapo demokrasia? Je matatizo yanayokuwapo katika kutumia demokrasia ni mengi kuzidi matatizo yanayokuwapo pasipotumika demokrasia? Mimi nimeishi katika Tanzania yenye sura zote mbili. Nimeishi katika chama kimoja, nimeishi katika vyama vingi. Ningesema Demokrasia, pamoja na madhaifu yake, imepanua Ushirikishaji wa wananchi katika maamuzi ya mwelekeo wa nchi yetu. Kitabu cha Megatrends kinaita siasa za namna hii kwa jina la Participatory Democrasy, na huu ndio mtindo wa kisasa wa kuendesha taifa. Ukosefu wa Demokrasia unaleta mwanya ya utawala wa kidikteta, na hili si zuri. Matatizo ya wananchi yanakuwa hayajulikani kwa sabu wanakuwa hawashirikishwi ipasavyo.

Kwa hiyo noamba tufute wazo la kuiponda demokrasia; pengine tuzungumzie njia za kuiboresha ili iweze kuwa na tija katika mazingira tuliyo nayo. Baada ya melezo haya kuhusu Demokrasia, naomba nijibu hoja nyingie kwa ule mtindo wa maswali na majibu:

WEWE:
nakiri kutokupata vyema hapa unapoilaumu Vita ya Uganda na Rushwa! Ni hivi, si kwamba kipindi cha AA hakukuwa na Rushwa, wahujumu uchumi walikuwepo na rushwa ndio ilikuwa nguzo yao kuu. Tunacholisifu AA ni kuwa lilikuwa na Taratibu za kuibana mianya hiyo ya rushwa. Si kwa kutunga sheria tu, bali ni total ways of life zilimjenga Mtz kuichukia Rushwa. Taratibu hizo hazikuvunjwa na Vita ya Kagera, bali ni AZ kwa vigezo vya HAKI ZA BINADAMU, DEMOKRASIA, Free Economy n.k!

MIMI:
Kwa nini nahusisha vita vya Kagera na kushamiri kwa rushwa? Kuna mahali umetamka umri wako kuwa mdogo. Mimi nina umri wa zaidi ya miaka 50. Miaka ya 1960 na Miaka ya 1970 hali ya uchumi ilikuwa nzuri kiasi--relatively. Nilikuwa nasafiri umbali wa kilometa karibia 2000 kwenda sekondari, shilingi mia moja (100/-) ilikuwa inabaki chenji. Nikisimulia uzuri wa miaka ile nafasi hii itakua haitoshi. Kwa hiyo naomba ujue tu kwamba hali ilikuja kugeuka kuwa mbaya hasa hasa baada ya Vita ya Kagera. Foreign exhange reserves zetu zilipukutika kwa vita ile, ingawa redio mbao zilikuwa zinasema mataifa fulani ya nje yalitupa taf katika vita ile, lakini hatukuweza kuokoa foreign reserves. Mwalimu Nyerere alitangaza hali ngumu ya Uchumi kwa muda wa Miezi 18. Hii ilikuwa kauli ya kututia moyo. Mimi nilikuwa mwalimu wakati ule. Hali mbaya ya Uchumi ilidumu kwa muda mrefu kuzidi miezi ile 18 tuliyoambiwa tukaze mikanda. Tulisahau kunywa Cocacola. Nakumbuka mtu mmoja aligundua soda fulani zikiitwa Potelo.

Hali mbaya ilidumu miaka yote ya 1980 huku serikali ikibuni mipango ya kurekebisha uchumi kwa majina mbalimbali. Mara Structural Reforms I, mara Structural Reform II Mara Economic Reform Commission, na baadaye Economic Recovery Plan.
Wakati wa hizi dhiki Watanzania walijifunza utapeli wa aina mbalimbali, ambapo wafanyakazi kwenye maofisi mbalimbali walianza kutumia nafasi zao kujinufaisha. Mafundi simu wa TTCL walianza kulangua laini za simu, Hospitalini dawa zikawa zinaibwa. Mimi nilikuwa naishi na mfanya kazi wa bandarini. Kila wiki alikuja na vitu kaiba kazini akawa anauza. Yote haya katika kukabiliana na hali ngumu iliyokuja baada ya vita ya Kagera.

Kuna msemo fulani niliwahi kupewa na Mwalimu wangu mahali: Alisema ukitaka kujua chanzo cha tatizo, tumia fomula hii: The cause of the cause is the cause of caused. Rushwa ilikuwapo kabla ya sasa. Ilishamiri zaidi baada ya vita vya Kagera. Mwinyi alichukua urais wakati Tanzania ipo katika jitihada za kujikwamua kutoka katika hali mbaya ya Uchumi ambayo ililetwa kwa kiasi kikubwa na ile vita. So hapo syquence ya mambo ipo hivi: Vita - hali mbaya ya uchumi - rushwa - Azimio la Zanzibar - Rushwa. Rushwa ilikuzwa na hali mbaya ya uchumi, na chanzo chake kwa mujibu wa maon yangu ilkuwa Vita.

Tulishindwa vipi kuidhibiti hiyo rushwa? Hilo sasa ndo ambalo tumetoka nalo tangu mwanzo wa uzi. Wewe unaona tatizo kutoka nje kwa sura ya HILA ya IMF, mi naona matatizo ya uongozi. Kama kuna hila basi iwe ni hila ya Kupukutisha foreign exchange reserves zetu kwa njia ya vita. Kama tuliingia vitani kwa sababu ya IMF na World Bank, nitakubali hoja yako. Kama tuliingia katika vita kwa sababu zingine, sitakubali hoja yako.


WEWE: Ni kweli taaluma ya biashara na taaluma ya fedha zina kanuni zake! Lakini kanuni hizo haziwezi kuwa sawa duniani kote kwani kanuni hizo hutakiwa kusadifu Mazingira na Nyakati za eneo husika.

MIMI: Maelezo hayo si kweli.
 
Highlander na wadau wengine, nitarejea;niwieni radhi kwa kutorudi kwa wakati for counter arguments;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Nakubaliana nawe Mkuu @Higlander kuhusu kushamiri kwa rushwa baada ya vita! Pia ni lazma tutambue kuwa serikali under AA haikubweteka kimya, kulikuwa na jitihada za kutunusuru na makovu ya vita! Nani alizikatisha kama si IMF kupitia AZ? Ipi faida ya AZ leo?
Mkuu wangu, itathimini Demokrasia vizuri na utagundua ni zaidi ya 90% ni majanga, na labda 5% ni faida. Kumbuka kuwa Demokrasia is more than politics, ni pamoja na tamaduni na uchumi. Zingatia principles zake, zitafakari kisha relate them with Nyakati na Mazingira yetu, utaona!
Mkuu wangu unaamini kuna kanuni za dunia nzima za biashara na fedha, labda ungezitaja hizo kanuni. Maana zile nizifikiriazo mimi kamwe haziwezi kuishi Ulaya na Afrika na kuzaa matunda sawa, labda sizo!
Mungu wetu anaita sasa!
 
Kwa kuwa Azimio la Arusha lilianzishwa na TANU iliyokuja kuzaa CCM,

Na kwa kuwa azimio la Arusha lilifanyika mwaka 1967,

Na kwa kuwa CHADEMA ilianzishwa mwaka 1992,,,

Nakushauri usiihusishe CHADEMA na hayo makitu ya CCM ni usanii mtupu. Hata katiba yao na ya nchi inaelezea habari za ujamaa na kujitegemea lakini hakuna anayetekeleza. Hata azimio la Arusha likirudi leo Chenge hawezi kurudisha mabilioni aliyoficha Jersey, Ridhiwani Kikwete hawezi kurudisha kampuni ya UDA aliyojiuzia na jamaa zake wa Simon Group kwa bei poa, Rostam Azizi hawezi kutusamehe deni la Dowans. Dawa sio azimio la Arusha, dawa ni kuiondoa CCM madarakani tuje na maazimio mengine na mipango yetu ya kimaendeleo inayoendana na mahitaji ya sasa ya kiuchumi na kitechnolojia. Usiwaingize CHADEMA kwenye maupuuzi ya CCM

azimio la arusha sio makitu ya ccm wewe.,soma historia..usikurupuke kiushabiki...unafkirì huku jf cdm n wewe tu??! Chadema tuko wengi ila cdm co kuropoka ni kuongea point,,uctuharibie chama,.kama umechoka hama.,
 
Naamini tunakwenda vizuri Wakuu Mchambuzi na JingalaFalsafa. Kwa kweli nchi yetu Tanzania ni mahali pazuri kuishi. Tumuombe Mungu wetu atupe uelewa sahihi wa matatizo yanayotaka kuiharibu nchi yetu, ili miaka 100 ijayo, tuwe na kizazi kinachosema tulikabidhiwa nchi njema; tulikabidhiwa nchi yenye upendo, nchi yenye amani na utulivu, lakini pia nchi isiyokuwa na njaa. Mambo haya mema yatapatikana kwa mijadala kama huu tunaofanya katika hili bunge letu la hewani.

Karibu tena Mkuu Mchambuzi. Tumekumiss kwa karibia siku nzima nadhani. Ukiwa haupo tumepata bahati ya kutembelewa na Mzee Mtei kwenye huu uzi jana. Mkuu JingalaFalsafa, naomba nisijadili lile unalolikubali kwa kuwa tunakuwa tumefikia mwafaka. Bandiko lako la mwisho limebakiza hoja kama mbili tatu hivi. Naomba kuzijibu ifuatavyo:

1. Umesema "tutambue kuwa serikali under AA haikubweteka kimya, kulikuwa na jitihada za kutunusuru na makovu ya vita! Nani alizikatisha kama si IMF kupitia AZ? Ipi faida ya AZ leo?"

Jibu: Jitihada kubwa sana zilifanyika na Serikali kulitoa taifa shimoni. Tulikuwa kama mfa maji anatapatapa. Tulitafuta kila upenyo ulioonekana kujinasua. Ni hapo ndipo tulipojikuta tunakwenda IMF na World Bank katika jitihada za kutafuta ufumbuzi. Nafasi ya hizi taasisi mbili ilikuwa ni nafasi ya mganga katika maisha ya mgonjwa. Waliweka dawa pamoja na masharti yake: Binafsisha mashirika ya umma, punguza ukubwa wa ajira serikalini, vunja vitengo fulani vya serikali au viunganishe. Ni kipind hiki pia tulianza kusikia Jeshi lipunzwe ukubwa wake libakie kuwa professional army. Makada wa CCM waliokuwa jeshini wakijifanya wanajeshi wakapewa nafasi kuchagua ama kurudi uraiani, ama kubaki jeshini. Wengi walichagua kurudi uraiani. Ndo hawa akina Kinana, akina Ditopile Mzuzuri, akina Makamba, nadhani hata Kikwete alikuwa katika kundi hili. Nadhani sharti la kuleta vyama vingi lilikuwa mojawapo ya maelekezo ya IMF na World bank, ingawa upepo wa siasa za "participatory democracy" ulikuwa unavuma kila kona ya dunia.

Serikali ilitii masharti hayo na kufikia miaka ya mwanzoni mwa 1990, zilianza kuonekana dalili za uchumi kufufuka. Maduka yakaanza kujaa vitu. Nguo za mitumba zikaleta unafuu wa mavazi. Naamini kwa moyo wangu wote kwamba dalili za kupona huyu mgonjwa zilianza kuonesha "opportunity" ya biashara na ustawi mzuri kwa watanzania.

Azimio la Zanzibar lilikuja kama tendo la Watu waliokuwa katika nafasi za uongozi na utawala kurukia "opportunity" ambazo walikuwa wanaziona. Nitumie neno lako hapa. Hii ilikuwa HULKA ya ulafi hapa. Kwa hivyo
pamoja na kwamba kimsingi sipingani na utaratibu wa mfanyakazi wa Serikali kuendesha biashara wakati akiwa bado yupo katika ajira ya Serikali, ni kwamba katika Azimio la Zanzibar palikosekana kipengele cha kumbana mfanyakazi ajulikane anapokuwa kapata mtaji wa biashara zake kwa hila ya wizi wa mali ya umma au rushwa.

Nasema AZ lililetwa kwa HULKA ya ulafi. Tiba ya IMF ilipoanza kuonesha dalili za kuleta afueni, walio katika madaraka wakaona nafasi ya utajirisho binafsi. Kwa hiyo hapa IMF na World Bank wapokelewe kama mkombozi, na Wale waliokuwa katika madaraka wakati AZ linazaliwa wapokelewe kama walafi wakubwa sana na waroho, wezi! Hicho ndo kilicholeta Azimio la Zanzibar.

2. Umesema "
itathimini Demokrasia vizuri na utagundua ni zaidi ya 90% ni majanga, na labda 5% ni faida. Kumbuka kuwa Demokrasia is more than politics, ni pamoja na tamaduni na uchumi. Zingatia principles zake, zitafakari kisha relate them with Nyakati na Mazingira yetu, utaona!"

Jibu: Tumechakachua neno hili Demokrasia kutoka neno la Kigiriki la
Dēmokritos, neno ambalo tafsiri yake ya kiingereza ni "chosen of the people")--yaani chaguo la watu. Utaonekana mtu wa ajabu sana kama utaendesha nchi pasipo kushirikisha wananchi katika miaka ya sasa. Nilikuambia awali kwamba Participatory Democrasy ndiyo mtindo wa kisasa wa kuendesha taifa lolote. Na hakuna njia sahihi zaidi ya hiyo kwa karne tuliyo nayo. Ukitaka kurudisha udikteta kwa kisingizio cha ukosefu wa elimu miongoni wa electorate, watu watakushangaa kwa nini usifanye jitihada kutoa elimu huko kwenye electorate wakajitambua wana haki ya kuchagua mtu atayewafaa.

Lakini kikubwa ni kwamba leo tuna ushahidi kwamba hao unaosema ni mbumbumbu hawawezi kuitumia demokrasia vizuri, tayari wanaitumia demokrasia vizuri. Kama kuna mtu wanamtaka kuwaongoza ukiwalazimishia mwingine wanapiga kura ya chuki wanahamia chama kingine. Demokrasia ni jibu sahihi kwa utawala bora. Nimeshuhudia hili kwenye maeneo kadhaa nchini. Demokrasia haina tatizo kabisa, ingawa itakuwa bora zaidi viwango vya elimu vitapoongezeka huko mbele.

Hili la kanuni za biashara na fedha naomba nisirudie maelezo. Ni kitu scientific ambacho kinaongozwa na hitaji la kupata faida tu. Hakuna kanuni nyingine inayo guide kanuni za biashara na fedha nje ya kitu faida. Nenda kokote duniani, kanuni ni hiyo tu.



 
Kwa kuwa Azimio la Arusha lilianzishwa na TANU iliyokuja kuzaa CCM,

Na kwa kuwa azimio la Arusha lilifanyika mwaka 1967,

Na kwa kuwa CHADEMA ilianzishwa mwaka 1992,,,

Nakushauri usiihusishe CHADEMA na hayo makitu ya CCM ni usanii mtupu. Hata katiba yao na ya nchi inaelezea habari za ujamaa na kujitegemea lakini hakuna anayetekeleza. Hata azimio la Arusha likirudi leo Chenge hawezi kurudisha mabilioni aliyoficha Jersey, Ridhiwani Kikwete hawezi kurudisha kampuni ya UDA aliyojiuzia na jamaa zake wa Simon Group kwa bei poa, Rostam Azizi hawezi kutusamehe deni la Dowans. Dawa sio azimio la Arusha, dawa ni kuiondoa CCM madarakani tuje na maazimio mengine na mipango yetu ya kimaendeleo inayoendana na mahitaji ya sasa ya kiuchumi na kitechnolojia. Usiwaingize CHADEMA kwenye maupuuzi ya CCM
UMEMJIBU VIZURI SANA HUYU JAMAA SHABIKI WA azimio la arusha. au ungesema hivi, the sky is not falling but CCM's credibility is.
 
Nimefuatilia kwa makini sana kuhusu mwenendo wa vyama viwili vikubwa na kugundua kuwa ili nchi hii isonge mbele, ni lazima ccm iondolewe madarakani. Na chama konachostahili kushika dola ni chadema ambaye ndiye changamoto kubwa kwa ccm.

Lakini kabla sijachukua kadi ya cdm, naomba kufahamishwa kuhusu msimamo wa cdm kuhusu Azimio la Arusha kwa sababu kilichopelekea nchi hii kukosa viongozi waadilifu ni kupuuza misingi ya uongozi iliyoanishwa katika azimio hilo.

Mimi nalihitaji azimio hilo sasa sijui msimamo wa chama ninachokipenda na kutaka kujiunga kama kina msimamo huo pia.

Kilichotufikisha hapa kama taifa siyo kuondoshwa kwa Azimio la Arusha na miiko ya viongozi ambayo ilikuwa sehemu ya Azimio hilo.

Kimsingi, baada ya kuondoshwa kwa Azimio la Arusha, kumekuwepo Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kama replacement of miiko ya viongozi wa umma.

Tukumbuke, sheria ina nguvu zaidi ya sera, ingawa sera ndiyo msingi wa sheria.
Azimio la Arusha ilikuwa ni Sera, kwa maana ingine "was a policy document committing Tanzania to socialism and self-reliance"

Tumefika hapa kutokana na waliopewa dhamana ya kutuongoza kushindwa kusimamia Sheria( Sheria ya maadili ya Viongozi wa Umma na nyinginezo)
 
Back
Top Bottom