Kuhusu katiba mpya; msimamo wa CCM ni upi?

Kuhusu katiba mpya; msimamo wa CCM ni upi?

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
730
Reaction score
1,225
Katika siasa kuna kitu kinaitwa strategic ambiguity; mfano wake mkubwa ukiwa ni sera ya Marekani kuhusu Taiwan. Kwenye maandishi rasmi USA wanatambua One China policy, ila kila siku wanaendelea kuiuzia Taiwan silaha na kufadhili harakati zote za Taiwan kujitenga na China.

Hapa kwetu ni kama swala la Katiba mpya limeshafikia hatua hiyo. Wakati ilani ya CCM 2025-2030 iliahidi kuhuisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku mia moja za kwanza, hali sasa imeanza kuchukua mwelekeo tofauti.

Ingawa hoja ya kuwa na mchakato wa katiba mpya haikataliwi moja kwa moja, ukizitafakari kauli za Mh. Rais hususani wakati wa upisho wa makamu wa Rais na alipowahutubia wa wazee wa Dar es salaam, kauli ya waziri wa utumishi na utawala bora akiwahutubia wananchi Igunga na ya kauli ya mbunge wa jimbo la kibakwe hivi karibuni; ni wazi kuwa, hoja ya katiba mpya huenda siyo kipaumbele tena.

Changamoto kubwa ya maswala kama haya ambayo msimamo wa chama haupo bayana, ni kusababishiana ajali za kisiasa. Unaweza toka ukiwa na nia njema yakuisemea ilani ya chama kwa wananchi, wenzako nyuma wanaitisha vikao kukujadili.

Ni muhimu sana kwa chama, haswa kwa mambo yanayokuwa yamebeba uzito mkubwa kwenye siasa za nchi, kuwa na kauli thabiti, itakayotetewa na wanachama wote kwa pamoja.
 
Katika siasa kuna kitu kinaitwa strategic ambiguity; mfano wake mkubwa ukiwa ni sera ya Marekani kuhusu Taiwan. Kwenye maandishi rasmi USA wanatambua One China policy, ila kila siku wanaendelea kuiuzia Taiwan silaha na kufadhili harakati zote za Taiwan kujitenga na China.

Hapa kwetu ni kama swala la Katiba mpya limeshafikia hatua hiyo. Wakati ilani ya CCM 2025-2030 iliahidi kuhuisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku mia moja za kwanza, hali sasa imeanza kuchukua mwelekeo tofauti.

Ingawa hoja ya kuwa na mchakato wa katiba mpya haikataliwi moja kwa moja, ukizitafakari kauli za Mh. Rais hususani wakati wa upisho wa makamu wa Rais na alipowahutubia wa wazee wa Dar es salaam, kauli ya waziri wa utumishi na utawala bora akiwahutubia wananchi Igunga na ya kauli ya mbunge wa jimbo la kibakwe hivi karibuni; ni wazi kuwa, hoja ya katiba mpya huenda siyo kipaumbele tena.

Changamoto kubwa ya maswala kama haya ambayo msimamo wa chama haupo bayana, ni kusababishiana ajali za kisiasa. Unaweza toka ukiwa na nia njema yakuisemea ilani ya chama kwa wananchi, wenzako nyuma wanaitisha vikao kukujadili.

Ni muhimu sana kwa chama, haswa kwa mambo yanayokuwa yamebeba uzito mkubwa kwenye siasa za nchi, kuwa na kauli thabiti, itakayotetewa na wanachama wote kwa pamoja.
Ccm ni matapeli, huenda siku zote ulikuwa huijui.Nadhani sasa unaanza kuona mambo ambayo sisi tulio nje ya box tumekuwa tukiyaona siku zote. Ukishaona chama kinategemea mbeleko ya vyombo vya dola tu kuendelea kuwepo madarakani, basi ujue hilo ni genge la wahuni.
 
Hapa kwetu ni kama swala la Katiba mpya limeshafikia hatua hiyo. Wakati ilani ya CCM 2025-2030 iliahidi kuhuisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku mia moja za kwanza, hali sasa imeanza kuchukua mwelekeo tofauti.
Kwa mujibu wa utawala na chama , wanasema tumalize maridhiano kwanza , lakini kwa mwenendo unavyoenda , ni dhahiri imekua utapeli
 
Ccm ni matapeli, huenda siku zote ulikuwa huijui.Nadhani sasa unaanza kuona mambo ambayo sisi tulio nje ya box tumekuwa tukiyaona siku zote. Ukishaona chama kinategemea mbeleko ya vyombo vya dola tu kuendelea kuwepo madarakani, basi ujue hilo ni genge la wahuni.
Swadakta
 
Je msimamo wa Ilani ya CCM 2025 uliheshimiwa na wadau wengine kama wanaharakati na vyama vya siasa??
hudhani kuwa response ya wadau na wanaharakati ilikuwa ni matusi,kejeli na kujaribu kuipindua Serikali halali?
Kwa muktadha huu na ishara hizi unategemea CCM iendelee kuchimba kaburi lake yenyewe?
Siku wanaharakati na wapinzani watakapoacha kuitumia hitaji la katiba kama silaha yao ya kuchukua nchi ndio siku muafaka ya kuwa na katiba ya wananchi utafikiwa.
Kamwe isitokee na ni laana kuandaa katiba yenye lengo la kuifuta CCM na mrengo wa Ujamaa.
JE TUNATAKA KATIBA YA KUREJESHA MATAKWA YA WAKOLONI???
Katiba mpya na bora itatokana na CCM na itatoka ndani ya CCM...
Kama kweli unaitaka katiba mpya jenga hoja ukiwa ndani ya CCM na uoneshe namna ambavyo CCM inaweza kuishi madarakani au kuweza kuachia na kurudi madarakani....hii ndio itakuwa akili na sio kwa mwenendo wa sasa wa hooligans na vibaraka wa walami wanaolazimisha katiba mpya bila hata kutaja vipengele vinavyomgusa mwananchi asiye mwanasiasa.
 
Wanaweza kuamka na kusema hapajawahi kuwa na Bunge la katiba mpya hvy hawana taarifa za uwepo wa katiba mpya
 
Je msimamo wa Ilani ya CCM 2025 uliheshimiwa na wadau wengine kama wanaharakati na vyama vya siasa??
hudhani kuwa response ya wadau na wanaharakati ilikuwa ni matusi,kejeli na kujaribu kuipindua Serikali halali?
Kwa muktadha huu na ishara hizi unategemea CCM iendelee kuchimba kaburi lake yenyewe?
Siku wanaharakati na wapinzani watakapoacha kuitumia hitaji la katiba kama silaha yao ya kuchukua nchi ndio siku muafaka ya kuwa na katiba ya wananchi.
Kamwe isitokee na ni laana kuandaa katiba yenye lengo la kuifuta CCM na mrengo wa Ujamaa.
JE TUNATAKA KATIBA YA KUREJESHA MATAKWA YA WAKOLONI???
Mkuu habari za hapo Mchamba Wima
 
Je msimamo wa Ilani ya CCM 2025 uliheshimiwa na wadau wengine kama wanaharakati na vyama vya siasa??
hudhani kuwa response ya wadau na wanaharakati ilikuwa ni matusi,kejeli na kujaribu kuipindua Serikali halali?
Kwa muktadha huu na ishara hizi unategemea CCM iendelee kuchimba kaburi lake yenyewe?
Siku wanaharakati na wapinzani watakapoacha kuitumia hitaji la katiba kama silaha yao ya kuchukua nchi ndio siku muafaka ya kuwa na katiba ya wananchi.
Kamwe isitokee na ni laana kuandaa katiba yenye lengo la kuifuta CCM na mrengo wa Ujamaa.
JE TUNATAKA KATIBA YA KUREJESHA MATAKWA YA WAKOLONI???
Katiba mpya na bora itatokana na CCM na itatoka ndani ya CCM...
Kama kweli unaitaka katiba mpya jenga hoja ukiwa ndani ya CCM na uoneshe namna ambavyo CCM inaweza kuishi madarakani au kuweza kuachia na kurudi madarakani....hii ndio itakuwa akili na sio kwa mwenendo wa sasa wa hooligans na vibaraka wa walami wanaolazimisha katiba mpya bila hata kutaja vipengele vinavyomgusa mwananchi asiye mwanasiasa.
Changamoto kubwa sasa siyo tena kuwa au kutokuwa na mchakato wa katiba mpya, changamoto ni kuwa msimamo wa chama kati ya hayo mawili ni upi?
 
Katiba mpya ni tishio kwa. Vyama vya kitemi kama ccm..


Ninachotaka kukumbusha kua Kenya kabla ya kupata katiba mpya walimwaga damu ya kutosha 2007...

2010 wakapata katiba mpya
 
Katika siasa kuna kitu kinaitwa strategic ambiguity; mfano wake mkubwa ukiwa ni sera ya Marekani kuhusu Taiwan. Kwenye maandishi rasmi USA wanatambua One China policy, ila kila siku wanaendelea kuiuzia Taiwan silaha na kufadhili harakati zote za Taiwan kujitenga na China.

Hapa kwetu ni kama swala la Katiba mpya limeshafikia hatua hiyo. Wakati ilani ya CCM 2025-2030 iliahidi kuhuisha mchakato wa katiba mpya ndani ya siku mia moja za kwanza, hali sasa imeanza kuchukua mwelekeo tofauti.

Ingawa hoja ya kuwa na mchakato wa katiba mpya haikataliwi moja kwa moja, ukizitafakari kauli za Mh. Rais hususani wakati wa upisho wa makamu wa Rais na alipowahutubia wa wazee wa Dar es salaam, kauli ya waziri wa utumishi na utawala bora akiwahutubia wananchi Igunga na ya kauli ya mbunge wa jimbo la kibakwe hivi karibuni; ni wazi kuwa, hoja ya katiba mpya huenda siyo kipaumbele tena.

Changamoto kubwa ya maswala kama haya ambayo msimamo wa chama haupo bayana, ni kusababishiana ajali za kisiasa. Unaweza toka ukiwa na nia njema yakuisemea ilani ya chama kwa wananchi, wenzako nyuma wanaitisha vikao kukujadili.

Ni muhimu sana kwa chama, haswa kwa mambo yanayokuwa yamebeba uzito mkubwa kwenye siasa za nchi, kuwa na kauli thabiti, itakayotetewa na wanachama wote kwa pamoja.
 

Attachments

  • IMG-20260824-WA0073.jpg
    IMG-20260824-WA0073.jpg
    38.2 KB · Views: 4
Je msimamo wa Ilani ya CCM 2025 uliheshimiwa na wadau wengine kama wanaharakati na vyama vya siasa??
hudhani kuwa response ya wadau na wanaharakati ilikuwa ni matusi,kejeli na kujaribu kuipindua Serikali halali?
Kwa muktadha huu na ishara hizi unategemea CCM iendelee kuchimba kaburi lake yenyewe?
Siku wanaharakati na wapinzani watakapoacha kuitumia hitaji la katiba kama silaha yao ya kuchukua nchi ndio siku muafaka ya kuwa na katiba ya wananchi utafikiwa.
Kamwe isitokee na ni laana kuandaa katiba yenye lengo la kuifuta CCM na mrengo wa Ujamaa.
JE TUNATAKA KATIBA YA KUREJESHA MATAKWA YA WAKOLONI???
Katiba mpya na bora itatokana na CCM na itatoka ndani ya CCM...
Kama kweli unaitaka katiba mpya jenga hoja ukiwa ndani ya CCM na uoneshe namna ambavyo CCM inaweza kuishi madarakani au kuweza kuachia na kurudi madarakani....hii ndio itakuwa akili na sio kwa mwenendo wa sasa wa hooligans na vibaraka wa walami wanaolazimisha katiba mpya bila hata kutaja vipengele vinavyomgusa mwananchi asiye mwanasiasa.
Ile voters turn out ya juzi ndio ilidhihirisha ccm imefikia mwisho, na inajua ikiandikwa katiba mpya ccm itatoka madarakani. Lakini hata bila katiba mpya, ccm itatoka hata kwa umwagikaji mkubwa wa damu. Hiyo katiba mpya wangalau itawafanya wanaccm wengi wasifie jela. Lakini kwa uhalisia ulivyo katiba mpya itaandikwa penda msipende.
 
Wanaweza kuamka na kusema hapajawahi kuwa na Bunge la katiba mpya hvy hawana taarifa za uwepo wa katiba mpya
Hapo comrade unatusingizia, ni kweli kuna dalili za kutokuwepo muafaka wa kichama kuhusu kuanza kwa mchakato wa katiba mpya, ila kuna utashi usiobishaniwa kuwa ipo hoja na haja ya katiba mpya.
 
Msimamo wa CCM sio katiba mpya sio leo wala kesho, na sitarajii wala kuwaamini CCM wakiongelea katiba mpya.

Hamuwezi kukubali katiba mpya ambayo tutafunga majizi ya peaa za umma, majizi ya kura, mafisadi, watekaji na magenge yao , wauaji ambao sasa ndio wanaunda CCM.

Nguvu ya umma tu kama ile ya October 29 ikija na nguvu mara 2 yake ndio mtaamka usingizini na kukubali mambp mapya.
 
Changamoto kubwa sasa siyo tena kuwa au kutokuwa na mchakato wa katiba mpya, changamoto ni kuwa msimamo wa chama kati ya hayo mawili ni upi?
Msimamo wa CCM hauna ambuguity kama ulivyojaribu kushawishi lakini umeacha kuangazia mazingira ya ukwamishaji wa upendo na thubutu ya awamu ya sita kutaka kurejea kwenye mchakato wa katiba mpya kwa amani utulivu na suluhu ya pamoja.
Guestures za Samia kuhusu umoja wa kitaifa na hatimaye katiba mpya zilionekana wazi na mwanzoni mwa utawala wake lakini majibu aliyopewa hatosahau maishani...Hata kama ni mimi nisingetaka kuisikia tena hii kadhia ya kisiasa.
 
Kuna baadhi ya vyama vimeshapoteza uelekeo mpaka sasa. Havijui vipo pale kwa ajili gani, na vinafanya nini na kwamanufaa yapi, kiufupi tu Mambo Yameparanguka kilichobakia nani atakiludisha chama kwenye mstari ndo maana utakuta matamshi yanakinzana..Msimamo wa chama umebaki kwenye kuwawajibisha mwanachama tu..nasio katika utekelezaji.
 
Ile voters turn out ya juzi ndio ilidhihirisha ccm imefikia mwisho, na inajua ikiandikwa katiba mpya ccm itatoka madarakani. Lakini hata bila katiba mpya, ccm itatoka hata kwa umwagikaji mkubwa wa damu. Hiyo katiba mpya wangalau itawafanya wanaccm wengi wasifie jela. Lakini kwa uhalisia ulivyo katiba mpya itaandikwa penda msipende.
Mnaweza ku-opt njia hiyo ambayo mmeanza kuijaribu yaani kutaka damu imwagike lakini ni njia isiyowezekana kwa Tanzania..Hata wakati wa kudai uhuru TANU na ASP walikuwa na options hizo lakini kamwe zisingeweza kuleta uhuru wa kweli na kuliacha Taifa salama.
Nguvu hujibiwa kwa nguvu kinzani ...hoja hujibiwa kwa hoja.
 
Msimamo wa CCM hauna ambuguity kama ulivyojaribu kushawishi lakini umeacha kuangazia mazingira ya ukwamishaji wa upendo na thubutu ya awamu ya sita kutaka kurejea kwenye mchakato wa katiba mpya kwa amani utulivu na suluhu ya pamoja.
Guestures za Samia kuhusu umoja wa kitaifa na hatimaye katiba mpya zilionekana wazi na mwanzoni mwa utawala wake lakini majibu aliyopewa hatosahau maishani...Hata kama ni mimi nisingetaka kuisikia tena hii kadhia ya kisiasa.
Comrade ukiambiwa uandike msimamo wa chama chetu kuhusu katiba mpya kwa sentensi moja kwa sasa utaandika nini?
 
Back
Top Bottom