Nini maoni yako kuhusu maslahi ya Wabunge?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Ben aliacha kiinua mgongo cha Mbunge kikiwa 35M. JK awamu ya kwanza akakitoa 35M to 90M na awamu ya pili akapandisha kutoka 90M hadi 240M. Bila shaka hapo ndipo ubunge ulipoacha kuwa utumishi ukageuka fursa ya kiuchumi.

Yohana hajaongeza hata mia. Ameacha kama alivyokuta. Lakini kumekuwa na mjadala kuwa maslahi ya wabunge yapunguzwe kikiwemo kiinua mgongo ili kufanya ubunge kuwa utumishi. Hapo ni nje ya mshahara wa 12M kwa mwezi, mkopo wa gari 90M, bima ya afya inayoweza kumpatia matibabu hadi ya 250M yeye na familia yake, pasi ya kusafiria ya kidiplomasia, mafuta ya gari lita 1,000 kila mwezi etc.

Nini maoni yako? Maslahi ya wabunge yapunguzwe, yaongezwe au yaachwe yalivyo?

Malisa GJ
 
Kwa hii mitano tena, BUNGE lifutiliwe mbali, kama mitano tena itaisha,tutakaa kikao cha nchi nzima kuona jinsi gani nzuri ya kulirudisha tena bunge kwa maridhiano ya wadanganyika wote.

Kwenye kikao hicho, watakaohisiwa kuwa wakorofi, wapiga VIBAO wazee hawataruhusiwa.

Kwa sasa hata wakuu wa mikoa na wilaya tufute tu, wakurugenzi, sijui RAS na DAS kama wanatosha tu.

Mi mwenyewe sielewi.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Leo umekuja na thread yenye akili, sio zile za maaskofu wako feki mara wameota nini unakimbilia kuanzisha uzi.
 
Huyo anayejiita mzalendo namba moja ina maana hizo pesa hazioni zilivyo nyingi, tena huku wafanyakazi wengine wa serikali wakilalamika hawajapandishwa mishahara miaka mitano?

Ndio maana huwa nna doubt huu uzalendo wake wa kuchagua, wengine anawaambia wazi mishahara yenu mikubwa sana lazima ipunguzwe, kwa wale wabunge kimya, au kwasababu hilo bunge lipo kwa ajili ya kumsifia ndio maana anawalea tu.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Huyo anayejiita mzalendo namba moja ina maana hizo pesa hazioni zilivyo nyingi, tena huku wafanyakazi wengine wa serikali wakilalamika hawajapandishwa mishahara miaka mitano?...
Sio yeye tu, hata wale waliokuwa kambi rasmi ya upinzani bungeni ni wanyonyanyi tu kama wenzao wakijani. Sijawahi sikia hata siku moja wakisema kwa uzalendo wao, minoti ile waitumie jimboni angalau hata kwa kununua vitabu kwenye shule za kata...naaam, miaka 5 unapata kiinua mgongo 240m!!! 12m kama mshahara ambao hauko taxed.

Utumishi wa umma uliotukuka wa miaka 36, bila posho wala nauli wala n.k, unapewa kiinua mgongo 52m

Ila wabunge wote kwa pamoja waliungana kugomea namna gani zao kipindi kile na juzi wamelalamika pesa ya kununulia ndinga haitoshi, 90m hiyo ambayo mtumishi wa 36yrs haipati.

SIASA na hasa hii yaTZ, ni kama BWAWA la maji taka, chochote kitakachotokea humo, ni TAKA
 
Back
Top Bottom