Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Mbwembwe tu,"habari ziwafikie
1.Mtoto wa marehemu Prof ........ akiwa Glascow,Scotland
2.Mjukuu wamarehemu injinia ....... akiwa Frankfurt Ujerumani
3.Wafanyakazi wote wa Umoja wa Mataifa,New york Marikani!
ha haha ha sasa hutaki
 
Haina tatizo, kizuri ni kwamba watu hawalazimishwi wanalipia wenyewe na wote wanaopeleka matangazo ya vifo redioni ni watu wenye uelewa hivyo, nchi yetu watu huwa watafanya baadhi ya mambo kama sifa na ili waonekane na wao wako juu.
 
Mbwembwe tu,"habari ziwafikie
1.Mtoto wa marehemu Prof ........ akiwa Glascow,Scotland
2.Mjukuu wamarehemu injinia ....... akiwa Frankfurt Ujerumani
3.Wafanyakazi wote wa Umoja wa Mataifa,New york Marikani!

4. Bibi wa marehemu Balozi ....akiwa Hong Kong, China.
5.Mjomba wa mrehemu Daktari....akiwa Havanna , Cuba.
6.Rafiki wa marehemu Jaji .....akiwa The Heague, Swaziland.
7. Shangazi wa marehemu Mheshimiwa.... akiwa Paris, Ufansa.
8.Baba mdogo wa marehemu Brigedia ....akiwa Damascus, Syria.
9.Mke wa marehemu Muhazini mkuu wa B.o.T.... akiwa Majengo pacha pale Posta.
10. Jirani wa marehemu Inpector General wa ....akiwa Bombay India kwa matibabu.
 
4. Bibi wa marehemu Balozi ....akiwa Hong Kong, China.
5.Mjomba wa mrehemu Daktari....akiwa Havanna , Cuba.
6.Rafiki wa marehemu Jaji .....akiwa The Heague, Swaziland.
7. Shangazi wa marehemu Mheshimiwa.... akiwa Paris, Ufansa.
8.Baba mdogo wa marehemu Brigedia ....akiwa Damascus, Syria.
9.Mke wa marehemu Muhazini mkuu wa B.o.T.... akiwa Majengo pacha pale Posta.
10. Jirani wa marehemu Inpector General wa ....akiwa Bombay India kwa matibabu.
Nimeipenda the Heague Swaziland. Lakini huu ni upotevu mwingine wa pesa
 
Natafuta kitufe cha like. Hii ni kweli tupu. Huyo mtoto huko Ujerumani anasikiliza radio one? Kazi kweli? Sielewi mtu anatoa Tangazo kwenye redio, ni kwa nia ya dhati kufikisha tangazo au kuna lingine. Na gharama yake kiasi gani?

Amini nakwambia kwa zamani yalisaidia sana tulipata msiba wa babu yetu miaka ya 2000 kuna kaka yetu alikuwa ghana likatolewa tangazo kama ivo kumbe washkaj zake wanaomfaham wakasikia wakampigia simu bila hata sisi kujua, alikuja ktk msiba japo hakuwahi kuzika. . . tulishangaa kwa kweli.
 
Amini nakwambia kwa zamani yalisaidia sana tulipata msiba wa babu yetu miaka ya 2000 kuna kaka yetu alikuwa ghana likatolewa tangazo kama ivo kumbe washkaj zake wanaomfaham wakasikia wakampigia simu bila hata sisi kujua, alikuja ktk msiba japo hakuwahi kuzika. . . tulishangaa kwa kweli.
Kwa zamani yalikuwa msaada mkubwa saana. Nikiwa mtoto nilifiwa na mzazi wangu sasa watu wazima wakawa wanaficha lakini nilisikia kwenye radio.
Lakini umuhim ule upo mpaka sasa?
 
Amini nakwambia kwa zamani yalisaidia sana tulipata msiba wa babu yetu miaka ya 2000 kuna kaka yetu alikuwa ghana likatolewa tangazo kama ivo kumbe washkaj zake wanaomfaham wakasikia wakampigia simu bila hata sisi kujua, alikuja ktk msiba japo hakuwahi kuzika. . . tulishangaa kwa kweli.

Sahihi kabisa kuna watu wamesoma na marehemu,wamefanyakazi na marehemu nk sio wote familia ya marehemu yanaweza kuwapigia simu, kupitia tangazo LA kifo watu wengi wanaleta taarifa na itamwezesha mwingine kumpigia simu rafiki wa marehemu "una taarifa? nimesikia kwenye radio furani kafa" vitu kama hivyo.
 
matangazo ya vifo yanasaidia hasa kwa wale waliombali na hawana mawasiliano ya moja kwa moja, unaweza kuwa kwenye gari na ukapata taarifa za kifo cha rafiki yako wa siku nyingi mliyepozana zamani!
 
Matangazo ya vifo yamekuwepo muda mrefu hasa wakati wa RTD wakati namna ya kupeana habari haikuwepo. Katika hali ya sasa ya teknolojia, je wapo wanaotegemea matangazo hayo au hata kusikiliza? Hakuna njia mbadala lazima radio zitumike kwa matangazo hayo?

Hili jambo nilikuwa nalifikiria muda si mrefu,mimi naona hayana faida katka ulimwengu huu wa teknologia
 
Sahihi kabisa kuna watu wamesoma na marehemu,wamefanyakazi na marehemu nk sio wote familia ya marehemu yanaweza kuwapigia simu, kupitia tangazo LA kifo watu wengi wanaleta taarifa na itamwezesha mwingine kumpigia simu rafiki wa marehemu "una taarifa? nimesikia kwenye radio furani kafa" vitu kama hivyo.

matangazo ya vifo yanasaidia hasa kwa wale waliombali na hawana mawasiliano ya moja kwa moja, unaweza kuwa kwenye gari na ukapata taarifa za kifo cha rafiki yako wa siku nyingi mliyepozana zamani!
Hapo hiyo taarifa itakuwa imekusaidia nini? Na kama ni rafiki kweli, unahitaji radio?
Ni watu gani waliopo mbali wasio na mawasiliano mbadala hadi wategemee radio tu? Wakati ule ilikuwa RTD tu, sasa hivi unasikiliza radio gani ili ufahamu waliofariki?
 
Mkuu Wacha tu hayo matangazo yaendelee kuwepo
Sio watu wote wenye kumiliki simu,si ajabu wakati wa tukio la kifo kuna wahusika ambao msiba huo unawahusu na wakati huo huenda Simu zao ni mbovu,zimeibiwa,zimepotea,hazina chaji,hazina vocha na mengineyo,

Lakini tangazo la kifo linaweza kukuta hata ndani ya daladala au chombo chochote cha usafiri na ukapata taarifa,au mtu wako wa karibu anaweza kusikia tangazo hilo na kukujulisha,


Ikumbukwe pia mtu huwezi kuwa na namba za simu za watu wote ambao ungependa kuwajulisha habari ya msiba,na kumjulisha mmoja mmoja kwa simu nafikiri gharama ni kubwa zaidi uki compare na gharama ya kutangaza redioni,


Hayo ni maoni yangu tu.
Kimsingi kutangaza kupitia vyombo vya habari km redio,magazeti, TV n.k. ni tofauti na kutaarifu kupitia simu,e-mail,sms n.k na kila mfumo una walengwa wake
 
Nimeipenda the Heague Swaziland. Lakini huu ni upotevu mwingine wa pesa

Hahahaaaaa!! Mimi nilifikiri bado Ipo Holland kumbe walisha ihamishia Swaziland!!😅😅😆😆😆😆
 
Hapo hiyo taarifa itakuwa imekusaidia nini? Na kama ni rafiki kweli, unahitaji radio?
Ni watu gani waliopo mbali wasio na mawasiliano mbadala hadi wategemee radio tu? Wakati ule ilikuwa RTD tu, sasa hivi unasikiliza radio gani ili ufahamu waliofariki?
Ufinyu wa kufikiri unakiangamiza kizazi cha watanzania! Nadhani tatizo liko kwenye elimu! Tangazo la kifo kwenye redio bado ni muhimu sana: Msiba ukitokea HAIWEZEKANI muwe na mawasialiano ya ndugu jamaa na marafiki wa marehemu wote ili muwape taarifa. Na hata kama mna mawasialiano inaweza kutokea mkasahau! Hivyo basi tangazo kwenye redio ndio njia rahisi ya kuweza kuwafikia walengwa wote. Chukulia mfano wa mtu aliyesoma sehemu mbali mbali mpaka akahitimu chuo kikuu na sasa anafanya kazi. Sehemu zote alizopitia kusoma, sehemu zote alizopitia kufanya kazi, sehemu zote alizoishi atakuwa ameacha marafiki na watu anaojuana nao kwa sababu moja ama nyingine. Je, kama akifariki ndugu zake watakuwa wanawajua wahusika wote na wana mawasiliano yao yote? Kwa vyovyote jibu ni hapana na radio ni njia nzuri ya kuweza kuwahabarisha watu wengi kwa wakati mmoja.
 
Ufinyu wa kufikiri unakiangamiza kizazi cha watanzania! Nadhani tatizo liko kwenye elimu! Tangazo la kifo kwenye redio bado ni muhimu sana: Msiba ukitokea HAIWEZEKANI muwe na mawasialiano ya ndugu jamaa na marafiki wa marehemu wote ili muwape taarifa. Na hata kama mna mawasialiano inaweza kutokea mkasahau! Hivyo basi tangazo kwenye redio ndio njia rahisi ya kuweza kuwafikia walengwa wote. Chukulia mfano wa mtu aliyesoma sehemu mbali mbali mpaka akahitimu chuo kikuu na sasa anafanya kazi. Sehemu zote alizopitia kusoma, sehemu zote alizopitia kufanya kazi, sehemu zote alizoishi atakuwa ameacha marafiki na watu anaojuana nao kwa sababu moja ama nyingine. Je, kama akifariki ndugu zake watakuwa wanawajua wahusika wote na wana mawasiliano yao yote? Kwa vyovyote jibu ni hapana na radio ni njia nzuri ya kuweza kuwahabarisha watu wengi kwa wakati mmoja.
chukua like mkuu!
 
Km Masika tunatumia noti kuchemsha majı, kwa ninı tusitumie vıjisentı vyetu kujulishana vifo vya wapendwa wetu?Heko the Chaga.
 
Hahahaaaaa!! Mimi nilifikiri bado Ipo Holland kumbe walisha ihamishia Swaziland!!

Siku hizi ipo Belgium,wanaihamisha kila baada ya miaka mitano
 
Hili jambo nilikuwa nalifikiria muda si mrefu,mimi naona hayana faida katka ulimwengu huu wa teknologia
Yana faida sana. wewe unadhani watu wote wanaofika misibani au hata kujua tu juu ya msiba fulani wanapata taarifa kupitia simu tu.It is way to make the sad event more public and not remain private issue.
 
Huu wote huwa ni ulimbukeni tu. Mtu yuko HK china au Nevada sijui kama ni kweli, viredio vya bongo vinasikika huko??
 
Back
Top Bottom