Salamander
JF-Expert Member
- Dec 7, 2012
- 28,536
- 15,751
Ndugu Nyanshani Ngabire wa Nshamba muleba, anasikitika kutangaza kifo cha mjomba wake Samaki Kiruru kilichotokea ziwani kwa ajali ya mtumbwi. Habari ziwafikie;
-Ndg Mapuli Kandambili wa Marekani
-Ndg Lusato Malyatabu wa Afrika ya Kusini
-Bi Hawa Mwampambuli wa Naijeria
Hilo tangazo hao watu kweli watalisikia au wanaolengwa kusikia ni watu gani? Zamani wakati mawasiliano ya simu yalikuwa mtihani ilikuwa inaingia akilini, lakini ulimwengu wa sasa mimi sioni umuhimu wa Tangazo la kifo redioni, labda kama kuna sababu nyingine.
Hata watu waliotajwa kwenye tangazo wana habari ya msiba uliotokea lengo maana yake nyingine n kuwafahamisha watu wengine kuwa watajwa hapo wamepatwa na msiba. Ni jinsi ya kuwataarifu watu kuwa, marehemu alikuwa baba wa fulani a Afrika kusini,mjomba wa fulani Kibohehe na wengieneo wengi,na wala sio ujiko.