Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Sawa, kama ingekua zamani kabla ya hizi simu za kichina kuzagaa. Leo hamna haja vile, ila ni biashara upande wa vyombo vya matangazo. Unataka wakale polisi. Its busness bwana!
 
Oh samahani kwa ukali.

Watu wanatangaza vifo wakiwa katika hali ya uchungu na kuchanganyikiwa. Kwa watu wasio na mila ya kutangaza, huwa wana fanya vitu vingine. Kwa watu wenye mila hiyo, kukimbia radio one kutangaza ni moja ya njia ya kudumisha mila kwa ajili ya marehemu pamoja na kujifariji mwenyewe.

Ni complex kidogo, ndiyo maana nikasema waache watu wafanye vitu wanayoona ni muhimu kwao

Mila? Acha utani bro!
 
Hata mimi sioni maana yeyeote…Yaai wewe unapoteza mda wako kwa kutega sikio lako kubwa kusubiri matangazo ya kifo…kwa hiyo kama ktk matangazo hayuko ndugu au rafiki aliekufa ktk matangazo ya kifo utalalamika kwa kupoteza mda? kama sio kwa nini unasikiliza ???
Mbona msg za simu zinasambaa haraka zaidi kuliko simu…!!!!!

Issue sio kupoteza muda, matangazo ya kifo kwanza kusikia huwa ni by chance ila mara nyingi hata kama wewe hujasikia au hujawasha radio lazima kuna ambae atakuwa anakufahamu amesikia anakupa taarifa na kama sio wewe kuna ndugu yako mwingine na mnaanza kutafutana sasa, mara nyingi sie tuliobahatika kuwa na simu na uwezo wa kuingia humu mtandaoni huwa tunaona vitu kama kila Mtz ana access navyo kumbe kuna kundi kubwa zaidi ya wanaomilki simu na ku-access mitandao ya kijamii. Bado matangazo yapo valid ila ni nyongeza ya juhudi ya kuwatafuta ndugu kwa utaratibu mwingine kama wa simu na kule kwetu Itabagumba wa kurusha barua kwa kumpa mtu yoyote kwenye basi akifika eneo la tukio anairusha barua
 
Kuishi kwa mazoea, pia jina lako kutajwa radioni ni ufahari ukitangazwa wanajua kwa una hadhi ya kipekee so hata rambirambi utatoa ya kipekee
 
Unajua huku kaskazini huwa tunafukuzwa majumbani kurudi majaliwa mpaka mambo yanyooke, kuna watu wameondoka zaidi ya miaka mitano hawajulikani walipo. Kupitia redio mtu anaweza kupata habari za msiba husika.
Lakini wengine mbwembwe tu habari zimfikia mtoto mkubwa wa marehemu akiwa Havard university n.k
 
Jaalia kuna Mtanzania anae ishi marekani yupo Tanzania kwa matembezi...na akasikia Jina la mshkaji wake ambae yuko US limetajwa kwenye Matangazo ya kifo..upo uwezekano wa yeye kumpatia taarifa kwa namna anavyoweza...kwa io sio mbaya kumpelekea tangazo la kifo kwa mtu amabe yupo nje ya nchi...Tusiwe negative sana Jamani...Haya mambo wazee waliyaweka kwa Hikma...tusiliwe na wasap zetu hizi!
 
Ni muhimu maana unaweza kupata taarifa kuwa jamaa au rafiki yako kafiwa, sio lazima taarifa ikuhusu wewe moja kwa moja
 
Matangazo ya vifo yamekuwepo muda mrefu hasa wakati wa RTD wakati namna ya kupeana habari haikuwepo. Katika hali ya sasa ya teknolojia, je wapo wanaotegemea matangazo hayo au hata kusikiliza? Hakuna njia mbadala lazima radio zitumike kwa matangazo hayo?
 
Huwa naona TBC1 wanatangaza, lakini huwa nabadili channel, yaani kwa kifupi huwa siangalii
 
Matangazo ya vifo yamekuwepo muda mrefu hasa wakati wa rtd wakati namna ya kupeana habari haikuwepo. Katika hali ya sasa ya teknolojia, je wapo wanaotegemea matangazo hayo au hata kusikiliza? Hakuna njia mbadala lazima radio zitumike kwa matangazo hayo?

Akina Mushi bado wanatangaza haya matangazo kupitia Radio 1........!!!
 
Mengine mazoea tu. Mpaka mtu aende kituo cha Radio kutoa tangazo, tayari ujumbe unakuwa umeisha fika kwa walengwa kwa njia ya simu.

Radio Tanzania (sasa TCB) ilikuwa maarufu kwa watu wa Pwani. Radio One kwa watu wa Kilimanjaro!
 
Mbwembwe tu,"habari ziwafikie
1.Mtoto wa marehemu Prof ........ akiwa Glascow,Scotland
2.Mjukuu wamarehemu injinia ....... akiwa Frankfurt Ujerumani
3.Wafanyakazi wote wa Umoja wa Mataifa,New york Marikani!
 
Ni namna mojawapo ya vyombo vya habari kujipatia kipato, lakini ki-uhalisia na kwa teknolojia zilizopo kwa sasa almost hakuna mtu anayepokea taarifa ya msiba kupitia redioni tena. wangebadili wakafanya kama kumbukumbu/shukrani tu, zitolewe baada ya mazishi au muda mrefu kupita.
 
Mkuu Wacha tu hayo matangazo yaendelee kuwepo
Sio watu wote wenye kumiliki simu,si ajabu wakati wa tukio la kifo kuna wahusika ambao msiba huo unawahusu na wakati huo huenda Simu zao ni mbovu,zimeibiwa,zimepotea,hazina chaji,hazina vocha na mengineyo,

Lakini tangazo la kifo linaweza kukuta hata ndani ya daladala au chombo chochote cha usafiri na ukapata taarifa,au mtu wako wa karibu anaweza kusikia tangazo hilo na kukujulisha,


Ikumbukwe pia mtu huwezi kuwa na namba za simu za watu wote ambao ungependa kuwajulisha habari ya msiba,na kumjulisha mmoja mmoja kwa simu nafikiri gharama ni kubwa zaidi uki compare na gharama ya kutangaza redioni,


Hayo ni maoni yangu tu.
 
Mbwembwe tu,"habari ziwafikie
1.Mtoto wa marehemu Prof ........ akiwa Glascow,Scotland
2.Mjukuu wamarehemu injinia ....... akiwa Frankfurt Ujerumani
3.Wafanyakazi wote wa Umoja wa Mataifa,New york Marikani!
Natafuta kitufe cha like. Hii ni kweli tupu. Huyo mtoto huko Ujerumani anasikiliza radio one? Kazi kweli? Sielewi mtu anatoa Tangazo kwenye redio, ni kwa nia ya dhati kufikisha tangazo au kuna lingine. Na gharama yake kiasi gani?
 
Mbwembwe tu,"habari ziwafikie
1.Mtoto wa marehemu Prof ........ akiwa Glascow,Scotland
2.Mjukuu wamarehemu injinia ....... akiwa Frankfurt Ujerumani
3.Wafanyakazi wote wa Umoja wa Mataifa,New york Marikani!

Hahahahahaaaaaaaaaaaaa.... Chukua like mkuu
 
Back
Top Bottom