Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Nini Mantiki ya Matangazo ya Vifo Redioni?

Mtumishi Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2011
Posts
259
Reaction score
93
Ndugu wanajukwaaa, heshima kwenu! Kwa muda sasa nimekuwa ninajiuliza maana ya haya matangazo ya vifo kwenye radio haswa kwa nyakati hizi ambazo teknolojia ya mawasiliano imeboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Mtakubaliana name kwamba kwa sasa unapotokea msiba mahali, ndani ya nusu saa ndg wengi wa marehemu watakuwa wamepata taarifa hizo za msiba. Kilichonifanya niulize swali hili ni hapa majuzi kuna jirani yangu alifiwa na mama yake ambaye alikuwa anaishi nae hapa mjini.

Kesho yake msiba ule ukatangazwa na ndugu zake wakajulishwa kupitia tangazo redioni.

Nikashangazwa mdogo wake na huyu ndugu aliyetuma tangazo kuwajulisha ndugu zake nae akatangaza tena na kati ya waliotajwa kwenye tangazo ni yule ndg mkubwa ambaye msibwa umetokea nyumbani kwake, kwamba nae anapewa taarifa ya msiba!

Hii imekaaje wadau?
Ndugu Nyanshani Ngabire wa Nshamba muleba, anasikitika kutangaza kifo cha mjomba wake Samaki Kiruru kilichotokea ziwani kwa ajali ya mtumbwi. Habari ziwafikie;
-Ndg Mapuli Kandambili wa Marekani
-Ndg Lusato Malyatabu wa Afrika ya Kusini
-Bi Hawa Mwampambuli wa Naijeria

Hilo tangazo hao watu kweli watalisikia au wanaolengwa kusikia ni watu gani? Zamani wakati mawasiliano ya simu yalikuwa mtihani ilikuwa inaingia akilini, lakini ulimwengu wa sasa mimi sioni umuhimu wa Tangazo la kifo redioni, labda kama kuna sababu nyingine.
 
Ukweli ni huo uliouleza Hapo juu. Zamani njia za mawasiliano na upashanaji habari zilikuwa finyu sana. Simu za mikononi hazikuwepo, za kukoroga nazo zilikuwa mikoani, wilayani au baadhi ya miji midogo iliyo mashuhuri. Hata vituo vya Redio vilikuwa vichache sana labda 2 au vitatu, ukiacha vya nje ya nchi. Hata wenye kumiliki Redio nao walikuwa wachache sana. Kwenye kijiji unakuta wenye radio hawazidi 10 n.k.

Sasa kuna kila aina ya mawasiliano: radio, Tv , simu n.k. karibu kila familia INA mtu angalau 1 mwenye simu - hata vijijini. Kwa hiyo suala la tangazo la kifo laweza tangazwa katika simu- message, Facebook na mitandao mingine ya kijamii, n.k.

Kwa hiyo naona suala la kutangaza kifo ktk Redio limebaki kama kufanya kwa mazoea tu na tuendako umuhimu wake utapungua siku hadi siku.
 
Salamu zimfikie ndugu Chipumbu Kikubwa akiwa marekani!

Wakati hiyo redio hata huko Obamani haisikiki!

Halafu mbona matangazo mengi ya vifo katika Radio one yanatoka zile pande za juu
 
Niliwahi kuwaza hivi lakini baada ya kutafakari sana nimebaini kuwa taarifa hizi zina umuhimu zaidi kwa third party…..unapomtaja Fulani bin Fulani kafa na habari zimfikie Mtoto wa Marehemu Fulani bin Fulani akiwa TRA Mbeya ni obvious kuwa huyu jamaa wa TRA alikuwa na taarifa ya simu nk lkn sisi marafiki zake tuliosoma naye au aliotuacha mathalan TRA mwanza hatukuwa na taarifa kuwa jamaa yetu kafiwa na baba yake….Pia majirani/wanakijiji wenzake ambao kwa sasa tupo Mtwara tunapata taarifa kuwa baba yake Fulani tuliochezea vifuu kule Ngamiani kafariki.
 
Niliwahi kuwaza hivi lakini baada ya kutafakari sana nimebaini kuwa taarifa hizi zina umuhimu zaidi kwa third party…..unapomtaja Fulani bin Fulani kafa na habari zimfikie Mtoto wa Marehemu Fulani bin Fulani akiwa TRA Mbeya ni obvious kuwa huyu jamaa wa TRA alikuwa na taarifa ya simu nk lkn sisi marafiki zake tuliosoma naye au aliotuacha mathalan TRA mwanza hatukuwa na taarifa kuwa jamaa yetu kafiwa na baba yake….Pia majirani/wanakijiji wenzake ambao kwa sasa tupo Mtwara tunapata taarifa kuwa baba yake Fulani tuliochezea vifuu kula ngamiani kafariki.
Naona kama hii kidogo ina mantiki kwamba ni kwa ajili ya wale ambao sio walengwa wa moja kwa moja na msiba.
 
Salamu zimfikie ndugu Chipumbu Kikubwa akiwa marekani!

Wakati hiyo redio hata huko Obamani haisikiki!

Halafu mbona matangazo mengi ya vifo katika Radio one yanatoka zile pande za juu
Ni suala la mazoea na inategemea hao wenyeji huwa wanapendelea kusikiliza station gani ya radio mara kwa mara. Hebu jaribu kufanya na kauchunguzi uone matangazo mengi ya vifo Radio Free Africa yanawahusu watu wa pande zipi!
 
lengo la kutangaza ni kutoa taarifa kwa ndugu jamaa na marafiki sio ndugu wote tuna mawasilisano nao either facebook or twiter. Na redio inasikilizwa na watu wengi kuliko simu na mitandao kwa mfano kwenye gari kuna watu zaaidi ya 60 wote watasikia tangazo na labda kati yao mmoja atakua muhusika redio ndio njia rahisi na yenye tija kuliko simu ambayo inaweza ikaisha chaji na mkumbuko kijijini kwetu namtukuko umeme hakuna wala mtandao pia
 
Ndugu Nyanshani Ngabire wa Nshamba muleba, anasikitika kutangaza kifo cha mjomba wake Samaki Kiruru kilichotokea ziwani kwa ajali ya mtumbwi. Habari ziwafikie;
-Ndg Mapuli Kandambili wa Marekani
-Ndg Lusato Malyatabu wa Afrika ya Kusini
-Bi Hawa Mwampambuli wa Naijeria

Hilo tangazo hao watu kweli watalisikia au wanaolengwa kusikia ni watu gani? Zamani wakati mawasiliano ya simu yalikuwa mtihani ilikuwa inaingia akilini, lakini ulimwengu wa sasa mimi sioni umuhimu wa Tangazo la kifo redioni, labda kama kuna sababu nyingine.
 
Kuna faida nyingi sn na Wanatajwa wachache then HABARI ZIWAFIKÍE NDG,JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.
N.B.WACHAGA NJOONI KUNA JAMAA KAWABEEP.
 
Ndugu Nyanshani Ngabire wa Nshamba muleba, anasikitika kutangaza kifo cha mjomba wake Samaki Kiruru kilichotokea ziwani kwa ajali ya mtumbwi. Habari ziwafikie;
-Ndg Mapuli Kandambili wa Marekani
-Ndg Lusato Malyatabu wa Afrika ya Kusini
-Bi Hawa Mwampambuli wa Naijeria


Hilo tangazo hao watu kweli watalisikia au wanaolengwa kusikia ni watu gani? Zamani wakati mawasiliano ya simu yalikuwa mtihani ilikuwa inaingia akilini, lakini ulimwengu wa sasa mimi sioni umuhimu wa Tangazo la kifo redioni, labda kama kuna sababu nyingine.

Kuna wengine mbwembwe tu ila bado matangazo ya vifo yana umuhimu pia kwani kuna wengine wanategemea radio kama chombo cha mawasiliano, mpaka sasa tena mjini kuna watu kuwapata ni issue aisee yaani anakuwepo hewani leo baada ya mwezi hapatikani miezi mitatu na akija kupatikana anakuwa kabadilisha namba
 
bora umelina wewe mimi nilisha wahi kujiuliza nikakosaga majibu,redio one ndio wanaongoza kupokea matangazo ya vifo asilimia tisini na tisa ni kutoka mkoa wetu wa kilimanjaro,nikuonyesha wachaga tunapendaga sifa sana kusikika kwenye redio.
 
Si lazima hicho kitangazwacho redioni kisikike na wote waliotajwa, habari zinaweza kufikishwa na wengine wenye mawasiliano na waliotajwa...

Ukiacha hilo, matangazo ya vifo ni njia ya kuingiza pesa kwa makampuni ya media...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Waulize Wachaga na Wahaya ndiyo wanaoongoza kwenye matangazo ya vifo radioni
 
Halafu habari huwa zinatakiwa ziwafikie wa nchi za nje tuuuu.
 
Vijijini wengi nina uhakika wanasikiliza matangazo ya vifo, na hata wakiwa na simu hasa kwa watu wazima wengi wamekulia katika mazingira ya matangazo ya vifo, kwahiyo ishakuwa mazoea iwapo itakapofika muda wa matangazo ya vifo wenyewe wanafahamu ratiba na kuanza kufungulia hata kama walikuwa wanafanya shughuli nyingine
 
Acha watangaze wanqvojiskia na ujue vijijini watu wanasikuliza sana redio kuliko mijini ingawa kuna aimu kwahyo kutangaza wala haihusiana na sifa just to pass information basi
 
Hata mimi sioni maana yeyeote…Yaai wewe unapoteza mda wako kwa kutega sikio lako kubwa kusubiri matangazo ya kifo…kwa hiyo kama ktk matangazo hayuko ndugu au rafiki aliekufa ktk matangazo ya kifo utalalamika kwa kupoteza mda? kama sio kwa nini unasikiliza ???
Mbona msg za simu zinasambaa haraka zaidi kuliko simu…!!!!!
 
bado yanaumuhimu, unajua unaweza kuwa haupatikani kwa simu, ukapata habari, siku hizi kuna radio tunasikiliza hata tuliko Japan.
 
Back
Top Bottom