binadamu aliletwa duniani kwa sababu alikiuka sharti alilopewa na Mungu (Mwanzo; 1:16-17), kwahiyo, adhabu mojawapo ilikua ni kumfukuza bustani ya Eden ili asije kula matunda ya mti wa uzima akaishi milele ( Mwanzo; 3:22).
Akili aliyotupatia ni kwasababu alitaka mwanadamu akatawale viumbe wengine wote na ndio maana alisema tumuumbe mwanadamu kwa mfano wetu, it means unakuwa na uwezo wa kufikiri tofauti na viumbe wengine, ndio maana ata hapo unajiuliza uwepo wa Mungu;... nyani, tembo, nzi au ata mende hawawezi fikiria uwepo wa Mungu. (Mwanzo; 1:26-28)
Of course hauwezi kumpenda Mungu usiyemuona wakati unamchukia jirani yako unayemuona, kwasababu kadili unavyompenda na kumtendea wema yule unayemuona ndio hivyo hivyo unavyompendeza Mungu pia (Luka; 10; 27-37)
Hayo maswali mengine nitasaidiwa na wakuu humu.
Waroma (9; 20-21)
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: "Kwa nini umenitengeneza namna hii? " Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matukizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.