Nini kimempeleka Mbowe huko South Africa?

Nini kimempeleka Mbowe huko South Africa?

Tatizo humu jukwaani watu huwa wanachukulia vitu kwa msimamo mkali utasema dini, ukienda against tu unaonekana upo upande wa pili kiitikadi wakati kinachotakiwa ni kuangalia kwa jicho la kawaida na umuhimu wa safari ya mheshimiwa nje ya nchi maana kama alitangaza ingekuwa vyema na yeye akawepo na kwa vyovyote hiyo safari sio dharula hivyo kulikuwa na possibility ya kuangalia kufanya maandamano kwa siku za usoni baada ya yeye kurudi. (akingefanya hivyo ingewapa hamasa zaidi wananchi na wafuasi wake, hasa wale waliojitokeza bila kuitwa juzi kati wakati anakwenda kuhojiwa mpaka ikapelekea wakapigwa pamoja na waandishi wa habari)

Sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana. Wewe unakandia, kisha wakati huohuo unashauri na kujaribu kuelekeza. kwani wafuasi wa Mbowe na Chadema ni lazima wafurahi au kufanya vile unataka wewe? Sometimes kujifanya unajua kwa mambo yasiyokuhusu ni "UMALAYA WA MDOMO" Mbowe kusafiri au kutosafiri, kushitiki au kutoshiriki maandamano ni isue ya Wanachadema wenyewe, wewe inakuhusu nini?
 
KUNA MKUTANO WA WAMILIKI WA CLUB ZA USIKU DUNIANI UNAFANYIKA S.AFRIKA,KAENDA KUHUDHURIA.MWAKA JANA ILIKUWA MACAU CHINA.Si munajua kamanda mjasiria mali.

kwa hiyo kahudhuria mkutano wa wamiliki wa madanguro?
 
Unaishi dunia gani wewe mpaka useme hujawahi kuona JK akikosolewa? By the way, siyo kila anayekosoa CDM ni CCM.

... Wanaokosoa Utalii Wa Jk Ni Cdm Lakn Ccm Wanapongeza Sana Kwamba Tumekuwa Tukipata Misaada
 
> Hii iwe onyo kwako na kwa wengine wenye tabia za malezi mabaya kama wewe, usirudie tena kumtaja mama yangu kwa matusi we humjui mama tena ukome na jifunze kuwa na adabu tena ujieshimu ili ueshimika na jamii inayokuzunguka. Usifikiri matusi yako yana tija kwangu au kwako ila unaonekana mpumbavu kwa kunajisi mdomo wako. USIRUDIE KUNITUSI TENA JIFUNZE UTU na kueshimu mawazo ya watu.

Unatafuta heshima kwa watu unaowaona na kuwaita majuha, misukule, mazwazwa, na majina mengi ya aina hiyo? Ungetaka kuheshimiwa wewe pamoja na mama yako ungejiepusha na uropokaji unaoufanya dhidi ya wenzako.
 
kwa hiyo kahudhuria mkutano wa wamiliki wa madanguro?

> Haya mengine ni matusi tena hayana tija sisi kama vijana jifunzeni kujieshimu na wala post yangu haina matusi ina swali kama huwezi kujibu swali acha UTU wako ni wa thamani sana jieshimu vijana tumieni akiri zenu vyema ili tusaidie maelfu ya watu wengi ambao hawana hata ufahamu wa kile tunachojua.
 
Maandamano hayataleta katiba wala hayatasimamisha au kuahirisha bunge. Ni kutaka kujenga utamaduni wa nchi kutotawalika. Ila hilo halitafanikiwa kwa sababu watakaoathirika kwa mabomu au risasi au kushtakiwa mahakamani ni watu masikini watakaokuwa wamedanganywa tu. Kwani walichokubaliana na Rais ni nini na wanachofanya ni nini na ili iweje. Halafu ndio hawa waje kuongoza nchi baada ya jambo rahisi kuwashinda kulitekeleza au kuvuta subira na kuona?
 
... Kuna Jamaa Aliwah Kusema Kwamba Wauza Unga Anawaju Pamoja Na Majangiri, Tena Ni Mtu Mkubwa Kabsa Hapa Tz
 
Watanzania wengine watu wa ajabu sana hawalalamiki wakati kajambazi kanakolalala Magogoni kakitembea kama malaya kwa pesa za walipa kodi, wanaweweseka na mtu anayetumia mpunga wake, ndio ajabu hiyo ... ... .
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Unatafuta heshima kwa watu unaowaona na kuwaita majuha, misukule, mazwazwa, na majina mengi ya aina hiyo? Ungetaka kuheshimiwa wewe pamoja na mama yako ungejiepusha na uropokaji unaoufanya dhidi ya wenzako.

> Hayo maneno ni yako wala sijasema mimi unanilisha maneno wewe. Narudia tena tumia vyema mdomo wake tena uwe na adabu jiangalie jitathini maneno yako machafu.
 
> Hayo maneno ni yako wala sijasema mimi unanilisha maneno wewe. Narudia tena tumia vyema mdomo wake tena uwe na adabu jiangalie jitathini maneno yako machafu.


Mi sioni sababu ya kujibishana na mazwazwa wakati we ni mtu unaejitambua.
 
KUNA MKUTANO WA WAMILIKI WA CLUB ZA USIKU DUNIANI UNAFANYIKA S.AFRIKA,KAENDA KUHUDHURIA.MWAKA JANA ILIKUWA MACAU CHINA.Si munajua kamanda mjasiria mali.

Kwa hiyo kuna mastripers wa kumwaga
 
Sisi Watanzania ni watu wa ajabu sana. Wewe unakandia, kisha wakati huohuo unashauri na kujaribu kuelekeza. kwani wafuasi wa Mbowe na Chadema ni lazima wafurahi au kufanya vile unataka wewe? Sometimes kujifanya unajua kwa mambo yasiyokuhusu ni "UMALAYA WA MDOMO" Mbowe kusafiri au kutosafiri, kushitiki au kutoshiriki maandamano ni isue ya Wanachadema wenyewe, wewe inakuhusu nini?

Mkuu CDM au CCM kama ni wanachama wenyewe wasingekuwa na idadi ya wabunge hao, kuna watu wengine ambao ni wafuasi na washabiki ambao ni wa muhimu pia na ndio wamevifanya mpaka dakika hii vimesimama na ndio vyama vyenye wapenzi wengi, kama una akili siku nyingine usirudie kusema mambo ya CDM ni ya wanachama wenyewe kwa kuwa ukichukua idadi ya wanachama wa CDM katika majimbo walioshinda utagundua ni wachache kuliko kura walizopata wagomembea in this case mambo ya CDM sio wanachama pekee hata wafuasi na washabiki pia, ukikomaa na wanachama peke yake mkuu kama ni kiongozi wa CDM inabidi upigwe chini maana huna strategy, usichukulie siasa kama dini sometime inabidi tujifunze kuji-challenge wenyewe kwa faida ya taifa (hujalazimishwa kukubali mawazo ya mtu ila ni sehemu tu ya kufanya brainstorming, soma signature yangu ndio utajijua wewe upo kwenye nafasi gani kwenye jamii hii, approach unayotumia ni kama ya CCM ya mtu akitoa mawazo tofauti na wewe unaibuka na matusi mara umetumwa mara sijui nini, naona na wewe umekuja na msamiati mpya wa UMALAYA WA MDOMO, inabidi uje na mkakati mpya wa kujibu hoja sio unatoa hoja za kunyamazisha watu kwa lugha za kejeli kama wanavyofanya CCM)


Rudia kusoma vizuri ile comment yangu yangu ya awali na nilikuwa nimemjibu mtu mwingine based na comment yake wala sikukandia mtu, nimetoa observation yangu based na comment ya Ndibalema kisha nikatoa comment yangu (hapo kuna vitu viwili). Tatizo umesoma kwa ajili ya kujibu na si kwa ajili ya kuelewa
 
Leo dunia ni zaidi mtaa mmoja kwa Teknolojia. Mhe.Mbowe na Kikwete wanaweza kuongoza vyama vyao popote walipo duniani !
 
Mbowe as mwenyekiti wa chama na MB pia kiongozi wa kambi rasimi ya upinzani (KUB) anamajukumu mengi,so kusafiri ni moja ya taratibu zake za kazi

Majukumu ya chama yataendelezwa na walio chini yake

Kumbe wanaotakiwa kuandamana ni wale wasio na majukumu mengi....
 
Mbowe kweli kausaliti uma alio utangazia maandamano, hata kama yamejaribu kufanyika je, yamefanyika kama ilivyo tarajiwa.
 
Maandamano yetu yanawahusu nini? na kinachofanyika hamkijui siku zote tunasema akili ndogo haiwezi kutawala akili kubwa.
 
Tuambieni kwanza Mwenyekiti wenu atatulia lini asome hata kaukurasa kamoja ka nyaraka nyeti ya serikali. Mkapa hata speech alikuwa anaandika mwenyewe na ikitungwa sheria au Sera anaisona na kutoa maoni. Kiguu na njia.
 
Back
Top Bottom