Nini kilimsibu Haruna Moshi?

phenomena

Member
Jul 12, 2010
20
0
Hatimaye mchezaji Mtanzania aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini Sweden Haruna Moshi amerejea nchini na kusema hana mpango wa kurejea tena nchini sweden.

Tunaomba Agent wake aongee ukweli na si kuficha. Kwani kuna wanaosema alikuwa akipokea fedha kidogo kutokana na makato makubwa ya kodi, kuna wanaosema aliingizwa mjini na wakala wake katika swala la mkataba na wengine wanasema hakufurahishwa na namba aliyokuwa akipangwa kwa kuchezeshwa kama kiungo mkabaji.

Ni hayo tuuu
 
Hujui mpira bila marijuana kwa wachezaji wa kibongo haupigiki?
 
Haruna Moshi a.k.a Boban kakatisha mkataba wake na klabu moja huko Sweden.

Kutokana na maelezo yake, yeye hataki sifa kwamba anacheza Ulaya bali anachotaka ni mkwanja(fedha)!! Kwamba pesa anayopata huko ni kiduchu. Wakala wa FIFA, Bwana Ndumbaru amemuasa Boban aseme ukweli kv Sweden analipwa vizuri kuliko Simba(may be kuliko TZ pay)!!! Which is which?!

Kutokana na maelezo ya Ndumbaru, Boban analipwa takriban USD 5000! Ofcoz, kwa kuitamka inaonekana ni nyingi as compared to hapa TZ! Likewise, Ndumbaru anasema kwamba Boban ametafutiwa nyumba "yenye kila kitu ndani!!" lakini ni Boban mwenyewe ndie yupo responsible pango la nyumba hiyo (unless kama sikumsikia vizuri Ndumbaru).

Mie ni mtu wa mswazi; hebu wadau nielewesheni!! Hivi nyumba yenye kila kitu ndani si ile inayoitwa FULL FURNISHED?!! For what i knw, nyumba iliyo full furnished hata hapa Dar haipungui USD 1000!!! wadau nikosoeni!!! Kama hivyo ndivyo; kumbe Boban atajikuta mwisho wa mwezi na kiasi kisichozidi USD 4000 (kama accomodation ni USD 1000 kwa mwezi). Aidha, Boban hataki kukatwa kodi!!!!!! Kodi ni lazima! Sasa tuseme Sweden PAYE ni 10%. this means, kodi yake kwa mwezi ni USD 500! Kwa ujumla wake, baada ya kodi na pango, Boban atabaki na USD 3500!! Wenyewe wanaoishi Sweden ndio wanaofahamu gharama za maisha! Tofauti na Dar ambako anaweza kuingia restaurant au bar na kununuliwa msosi na kilaji; Boban kakuta favor kama hiyo haipati uzunguni!!! Sasa tuseme chakula na vitu vingine vidogo vidogo vinamgharimu USD 1500 pm; this means atajikuta anabaki na USD 2000!

Na kuna uwezekano mkubwa kwamba anabaki na pesa chini ya hapo kwa kuzingatia maisha ya huko na matarajio waliyonayo ndugu zake ka ile tu kucheza Ulaya!! Hivyo basi, endapo Boban si mtu wa kuangalia career yake, i hope yupo right kv hicho kiwango anaweza kubaki nacho hata hapa Dar endapo anaweza kuwa mbunifu kwa kile kidogo anachopata!

Hata hivyo, hili ni somo kwa wa-Tz wote, na si wanasoka pekee!!! Siku nilipoajiriwa, nilikuwa na mshikaji mmoja. Kwenye mkataba waliandika salary ni TZS 275,000/=; abt 20% PAYE; 10% PPF. Mshikaji wangu hakuangalia hayo mambo! Siku anapata mshahara wake wa kwanza, akajikuta anapata pesa ndogo kuliko vile alivyotarajia! Na hii wengi tunayo achilia mbali Boban ambae si ajabu shule yenyewe ni ya kuunga unga! We're not analytical! Je, kuna mtu alimwelewesha Boban kwamba, out of USD 5000, at the end of story utabaki si zaidi na USD 2000?

Mawakala mnawaelimisha watu wenu ambao wengi wao si analytica?
 
Ni yeye tu ndo anakatwa hiyo kodi kubwa???
Akina Drogba vipi??? au wao walianziaga mishara mikubwa..
By the way ni maisha yake..
 
Mibangi tuu, jana huyo ndumbaro kasema jamaa alikuwa analipwa dolaa 5000 kwa mwezi (5000X1450)=7,250,000 haya kodi kubwa walikuwa wanachukua mshahara wote au? halafu nimesikia leo asubuhi CLOUDZ fm hiyo timu ya jamaa imeingia Champions league na watapambana na Liverpool sasa jamaa kachemsha KINOOOOMA
 
Bobani ni mvuta Bangi tu, mtu asie mvumilivu, mtu asiejua thamani ya mpira, hapa kafuata mademu na baghi,
Ndumbaro kila siku anaeleza sababu za Boban kurudi hapa, eti analalamikia Kodi, mjinga huyu
 
Mibangi tuu, jana huyo ndumbaro kasema jamaa alikuwa analipwa dolaa 5000 kwa mwezi (5000X1450)=7,250,000 haya kodi kubwa walikuwa wanachukua mshahara wote au? halafu nimesikia leo asubuhi CLOUDZ fm hiyo timu ya jamaa imeingia Champions league na watapambana na Liverpool sasa jamaa kachemsha KINOOOOMA

Liverpool aichezi Champions League waache na wao uongo wao waeleze ukweli!!
 
Hivi wabongo tunakosaagaa kulaumuuuu...nani katulogaaa sisi watanzaniaaa????????
 
naomba anyone who knows,aniambie nimchezaji gani tanzania,amewahi cheza proffessional football nje na akawa a success-maana naona local press zetu uwa zina wa big up and in the end it always ends up in tears.Hao waliocheza arabuni hatuwahesabu maana a player past his prime in europe ndio huenda cheza mpira arabuni
 
Habari wana JF, kama kuna mwana JF anayefahamu sababu za msingi zilizosababisha HARUNA ''BOBAN'' kurejea nyumbani TZ aziweke hapa niweze kufahamu.
 
Habari wana JF, kama kuna mwana JF anayefahamu sababu za msingi zilizosababisha HARUNA ''BOBAN'' kurejea nyumbani TZ aziweke hapa niweze kufahamu.
...Kwa mujibu wa maelezo ya wakala wake Damas Ndumbaro, Haruna alikatisha mkataba wake na hiyo timu aliyokuwa akichezea huko Sweden kwa sabau kubwa mbili 1. Haoni kama kuna maslahi kuendelea kuichezea hiyo timu kwa nikipato apatacho kwa mtazamo wake ni kidogo 2. Kiwangi cha soka sweden haoni kama ni cha ushindani ingawa kuna maelezo kuwa hiyo timu ime-qualify kucheza kombe la ulaya????!!!!

Lakini kwa maoni yangu nilichoona kwa upande wa Haruna ni upeo mdogo wa kujua mambo na pia kukosa dhamira ya kucheza soka la ushindani. Haruna yeye hataki kukatwa kodi kwenye mshahara wake (pay as you earn), alitafutiwa nyumba lakini akatakiwa alipie kodi mwenyewe.

Nimegundua wachezaji wetu wengi wa soka wana akili finyu sana (sitaki kuzungumzia elimu hapa) maana kama ni elimu akina George Weah walipiga soka ulaya na hawakuwa na elimu sana au akina Kanu, Toure. isipokuwa wanakosa dhamira ya kweli kutaka kucheza soka ulaya na pia kukosa malengo. Hivi kwa timu kuweza kupata tiketi ya kucheza ubingwa wa ulaya si ndio ilikuwa njia ya yeye kuonyesha umahili wake ili aonekane na hatimaye kupata timu kubwa zaidi na hatimaye kupata mkataba wenye maslahi zaidi??

Kwa hiyo Haruna ameona bora kurudi simba...Kweli akilini nywele!!!:A S 39::A S 39::frusty::frusty:
 
naomba anyone who knows,aniambie nimchezaji gani tanzania,amewahi cheza proffessional football nje na akawa a success-maana naona local press zetu uwa zina wa big up and in the end it always ends up in tears.hao waliocheza arabuni hatuwahesabu maana a player past his prime in europe ndio huenda cheza mpira arabuni
sunday manara
 
...Kwa mujibu wa maelezo ya wakala wake Damas Ndumbaro, Haruna alikatisha mkataba wake na hiyo timu aliyokuwa akichezea huko Sweden kwa sabau kubwa mbili 1. Haoni kama kuna maslahi kuendelea kuichezea hiyo timu kwa nikipato apatacho kwa mtazamo wake ni kidogo 2. Kiwangi cha soka sweden haoni kama ni cha ushindani ingawa kuna maelezo kuwa hiyo timu ime-qualify kucheza kombe la ulaya????!!!!

Lakini kwa maoni yangu nilichoona kwa upande wa Haruna ni upeo mdogo wa kujua mambo na pia kukosa dhamira ya kucheza soka la ushindani. Haruna yeye hataki kukatwa kodi kwenye mshahara wake (pay as you earn), alitafutiwa nyumba lakini akatakiwa alipie kodi mwenyewe.

Nimegundua wachezaji wetu wengi wa soka wana akili finyu sana (sitaki kuzungumzia elimu hapa) maana kama ni elimu akina George Weah walipiga soka ulaya na hawakuwa na elimu sana au akina Kanu, Toure. isipokuwa wanakosa dhamira ya kweli kutaka kucheza soka ulaya na pia kukosa malengo. Hivi kwa timu kuweza kupata tiketi ya kucheza ubingwa wa ulaya si ndio ilikuwa njia ya yeye kuonyesha umahili wake ili aonekane na hatimaye kupata timu kubwa zaidi na hatimaye kupata mkataba wenye maslahi zaidi??

Kwa hiyo Haruna ameona bora kurudi simba...Kweli akilini nywele!!!
A%20S%2039.gif
A%20S%2039.gif
:frusty::frusty:

Heshima kwako Sajenti,

Nakubaliana na maelezo yako,leo asubuhi nilikuwa natazama TBC1 wakala wake Bwana Ndumbaro aliainisha kila kitu.Ukweli ni kwamba Haruna Moshi akili yake imekaa kibangi bangi,wakati alipokuwa akisaini mkataba inaelekea alishavuta mibangi ndiyo maana akakubali kusaini mkataba bila kuangalia maslahi.Eti anataka geti collection apewe, asikatwe kodi sijui anafikiri bado yuko Bongo mahali ambapo kodi inaweza kukwepwa?

Nadhani Haruna Moshi hana maono ya mbali, inaelekea ni aina ya watu wanaodhani mafanikio yanadondoka tu bila kutia juhudi. Mpira wa Simba na Yanga kamwe haujawahi mchezaji kimaslahi mara nyingi tumeshuhudia wachezaji wenye majina makubwa wakiishi maisha magumu sana mara wanapotundika madaruga yao.
 
Liverpool aichezi Champions League waache na wao uongo wao waeleze ukweli!!
hiyo timu yake boban inaitwa gefle if,imeshika nafasi ya 10,haimo ktk michuano yoyote ya ulaya,labda friend mechi ndio wacheze na liverpool
 
Habari wana JF, kama kuna mwana JF anayefahamu sababu za msingi zilizosababisha HARUNA ''BOBAN'' kurejea nyumbani TZ aziweke hapa niweze kufahamu.

Mkuu, majuu hakuna chance ya kuvuta bangi kisha ukaingia uwanjani kucheza mpira. Uwezo wake kimchezo unatokana na bangi na huko ameminywa havuti hiyo kitu. Hapa bongo ni tambarare players wengi ni bangi kwa mbele.
 
Mibangi tuu, jana huyo ndumbaro kasema jamaa alikuwa analipwa dolaa 5000 kwa mwezi (5000X1450)=7,250,000 haya kodi kubwa walikuwa wanachukua mshahara wote au? halafu nimesikia leo asubuhi CLOUDZ fm hiyo timu ya jamaa imeingia Champions league na watapambana na Liverpool sasa jamaa kachemsha KINOOOOMA

hiyo timu yake boban inaitwa gefle if,imeshika nafasi ya 10,haimo ktk michuano yoyote ya ulaya,labda friend mechi ndio wacheze na liverpool
 
Back
Top Bottom