Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Mtafiti...
Nimeandika historia ya wazee wangu katika kukabiliana na ukoloni.

Vyanzo vyangu katika mwanzo wa kuunda African Association ni mswada alioandika Kleist Sykes kabla hajafariki.

Mswada huu upo Maktaba ya Chuo Kikuu Chs Dar es Salaam East Africana na uliwasilishwa na Daisy Sykes mjukuu wa Kleist kama seminar paper mwaka wa 1968.

Seminar paper ikawa katika kitabu kilichohaririwa na John Iliffe, "Modern Tanzanians," mwaka wa 1973.

Pamoja na mswada huo nilifunguliwa Sykes Papers zenye historia ya TAA na TANU kuanzia miaka ya 1920 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.

Pamoja na hao tena nilifanya mazungumzo marefu familia ya Sykes na wakanieleza yale waliyofanya wakati wa kuunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nilipita mikoani ambako nilizungumza na wazalendo waliokuwa hai na nilikusanya nyaraka na picha na kupata maelezo ya historia ya uhuru.


Unajua ipo hivi. Katika kuandika mambo kama haya unapaswa kuwa makini sana. Hapa unagusa hisia za watu. Pamoja ni jambo jema wewe kukiri kuwa unaandika historia ya babu/ndugu zako, hii si leseni ya wewe kuwa mkweli. Nimeona ukijinasibu mara kwa mara kuwa unaandika vya kwenu, hii inasabisha mtu yeyote critical awe makini kuangalia ujenzi wako wa hoja.

Aidha, haimaanishi eti kwakuwa wewe nasaba na hao wanaharakati basi usemacho ni kweli. Mtu asiye na nasaba anaweza kuandika ukweli zaidi kuliko wewe. Itategemea tu kila mmoja ana malengo gani.

Hata wanaokupinga hapa, haimaanishi wao ni wakweli kihivyo. Si ajabu wanatumia udhaifu wako wa kujenga hoja kukushambulia. Binafsi, kujigamba kuwa una undugu na hawa wapiganaji basi usikilizwe ninaona ni udhaifu. Shusha facts, wewe kaa kando.
 
Nguruvi..
Huyo ndiyo Abdul Sykes...

Kadri itakavyokuwa.

Ukimfuta kwenye historia ya TANU unafuta historia kubwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kivukoni wamejaribu na matokeo yake ndiyo haya.
kule kule, nani kasema Abdul Sykes afutwe katika historia?
Historia ina tabia moja, kwamba, huiandiki wala huifuti. Utamfutaje Hitler katika vita kuu ya dunia?
Likewise utamfutaje Kleist Sykes katibu wa AA au Mwalimu Matola Mwenyekiti wa AA au Abdul wa TAA
Tena tunamkosea Abdul, hatuelezi jitihada zake za kuwabambua makofi akiwa na wahuni ili watwae ofisi

Turudi kwenye mada hasa makabrasha uliyopata bahti ya kuyadurusu mwenzetu
Mwaka 1929, akiwa na AA , ipi namba ya kadi ya Kleist Abdallah Sykes ?
Naye Abdul akiwa na TAA baada ya kuwatia adabu wazee , kadi yake ya TAA ni ngapi?

Halafu, wanena TANU kuanzishwa 1929, iweje basi kadi ya mtoto wa miaka 7 wakati huo Mwalimu Nyerere iwe namba 1 na ile ya mwana wa familia ya Sykes Mh Abdul Sykes iwe namba 3.

Halafu tuendele..

Leo nipo Pongwe napata papa na ngogwe. Mashallah mashallah
 
Unajua ipo hivi. Katika kuandika mambo kama haya unapaswa kuwa makini sana. Hapa unagusa hisia za watu. Pamoja ni jambo jema wewe kukiri kuwa unaandika historia ya babu/ndugu zako, hii si leseni ya wewe kuwa mkweli. Nimeona ukijinasibu mara kwa mara kuwa unaandika vya kwenu, hii inasabisha mtu yeyote critical awe makini kuangalia ujenzi wako wa hoja.

Aidha, haimaanishi eti kwakuwa wewe nasaba na hao wanaharakati basi usemacho ni kweli. Mtu asiye na nasaba anaweza kuandika ukweli zaidi kuliko wewe. Itategemea tu kila mmoja ana malengo gani.

Hata wanaokupinga hapa, haimaanishi wao ni wakweli kihivyo. Si ajabu wanatumia udhaifu wako wa kujenga hoja kukushambulia. Binafsi, kujigamba kuwa una undugu na hawa wapiganaji basi usikilizwe ninaona ni udhaifu. Shusha facts, wewe kaa kando.
Mkuu Mtafiti77, mambo ni hivi...

Hawa mamluki, walowezi kutoka nje ya Tanganyika, walipewa upendeleo maalum na serikali za Kikoloni. Wakati Watanganyika wanaishi uswahilini kwenye mabanda ya makuti na wengine kwenye nyumba za mbavu za mbwa, hawa walowezi walitengewa sehemu maalum mjini Dar es Salaam na kujengewa zilizoitwa quarters. Hivyo Wazulu kutoka Afrika Kusini na Wamanyema kutoka Congo wakajikuta wanaishi pamoja kwenye hizo quarters kama mitaa ya Gerezani.

Wazulu, ambao wengi wao walikuwa Wakristo, walikuwa ni askari wa wakoloni na hivyo karibu wote hawakuwa na familia zao. Wamanyema walikuwa ni Waislaam na kwa kuwa walijikita zaidi na kueneza mambo ya kidini ilikuwa rahisi kwao kuleta familia zao. Kwa kuishi pamoja, Wazulu na Wamanyema walijikuta wakiingiliana kindoa na moja ya masharti kwa Wazulu kuoa mabinti wa Kimanyema ilikuwa ni kubadilisha dini na wengi walifanya hivyo.

Hivyo ndivyo ukoo wa Sykes, Wakristo, ulivyojikuta taratibu ukibadilisha imani na kuingia katika Uislaam na pia ndiyo moja ya sababu zao za kubaki Tanganyika. Hiki ndicho kiini cha mahusiano kati ya ukoo wa Mohamed Said na ukoo wa Sykes na kwa waliosoma historia ya Tanganyika wakati wa Ukoloni haya makabila mawili, wazulu na manyema, hawatajwi kwenye kitabu cha Watanganyika kilichoorodhesha makabila yote ya Tanganyika nyakati hizo.

Juhudi zote za Mohamed Said ni kuhakikisha kuwa anadumisha hii historia yake ya kuchonga ya wazee wake ili kusiwe na shaka kuhusu hawa walowezi kuingia kwenye historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika. Lakini natoa tahadhari...Tanganyika haikuwa koloni ya Mwingereza na kwa msingi huo hakukuwa na mapigano yoyote ya kudai uhuru. Uhuru wa Tanganyika tofauti na nchi zingine Afrika haukudaiwa kwa mtutu wa bunduki na mapigano, ulidaiwa kwa majadiliano.

Kilichotakiwa ni kutokea kwa Watanganyika wenye uwezo, sifa na elimu ya kukaa meza moja na kutoa hoja na sababu kwa nini muda umefika kwa Tanganyika kujitawala. Uingereza walipewa tu kuisimamia Tanganyika hadi iwapate watu kama hao na mwaka 1961, TANU iliweza kuuridhisha Umoja wa mataifa kwamba sasa inao hao watu wenye uwezo, sifa na elimu ya kutwaa madaraka na kujitawala wenyewe. Huu ndio ukweli, mengine ni porojo tu.
 
Unajua ipo hivi. Katika kuandika mambo kama haya unapaswa kuwa makini sana. Hapa unagusa hisia za watu. Pamoja ni jambo jema wewe kukiri kuwa unaandika historia ya babu/ndugu zako, hii si leseni ya wewe kuwa mkweli. Nimeona ukijinasibu mara kwa mara kuwa unaandika vya kwenu, hii inasabisha mtu yeyote critical awe makini kuangalia ujenzi wako wa hoja.

Aidha, haimaanishi eti kwakuwa wewe nasaba na hao wanaharakati basi usemacho ni kweli. Mtu asiye na nasaba anaweza kuandika ukweli zaidi kuliko wewe. Itategemea tu kila mmoja ana malengo gani.

Hata wanaokupinga hapa, haimaanishi wao ni wakweli kihivyo. Si ajabu wanatumia udhaifu wako wa kujenga hoja kukushambulia. Binafsi, kujigamba kuwa una undugu na hawa wapiganaji basi usikilizwe ninaona ni udhaifu. Shusha facts, wewe kaa kando.
Mtafiti...
Hayo hayanihusu mie.

Iliandikwa historia ya TANU ya Chuo.Cha CCM Kivukoni yote mnayosoma hapa hayakuwemo yamefutwa.

Labda kwa kukosa kujua nyie mkadhani ile ndiyo historia ya TANU.

Nimeandika historia ya kweli.

Hebu waulizeni maswali Kivukoni.
Ilikuwaje?

Ndiyo hivyo hivvyo magazeti ya TANU nayo hayakumwandika Abdul Sykes alipofariki.
 
Mkuu Mtafiti77, mambo ni hivi...

Hawa mamluki, walowezi kutoka nje ya Tanganyika, walipewa upendeleo maalum na serikali za Kikoloni. Wakati Watanganyika wanaishi uswahilini kwenye mabanda ya makuti na wengine kwenye nyumba za mbavu za mbwa, hawa walowezi walitengewa sehemu maalum mjini Dar es Salaam na kujengewa zilizoitwa quarters. Hivyo Wazulu kutoka Afrika Kusini na Wamanyema kutoka Congo wakajikuta wanaishi pamoja kwenye hizo quarters kama mitaa ya Gerezani.

Wazulu, ambao wengi wao walikuwa Wakristo, walikuwa ni askari wa wakoloni na hivyo karibu wote hawakuwa na familia zao. Wamanyema walikuwa ni Waislaam na kwa kuwa walijikita zaidi na kueneza mambo ya kidini ilikuwa rahisi kwao kuleta familia zao. Kwa kuishi pamoja, Wazulu na Wamanyema walijikuta wakiingiliana kindoa na moja ya masharti kwa Wazulu kuoa mabinti wa Kimanyema ilikuwa ni kubadilisha dini na wengi walifanya hivyo.

Hivyo ndivyo ukoo wa Sykes, Wakristo, ulivyojikuta taratibu ukibadilisha imani na kuingia katika Uislaam na pia ndiyo moja ya sababu zao za kubaki Tanganyika. Hiki ndicho kiini cha mahusiano kati ya ukoo wa Mohamed Said na ukoo wa Sykes na kwa waliosoma historia ya Tanganyika wakati wa Ukoloni haya makabila mawili, wazulu na manyema, hawatajwi kwenye kitabu cha Watanganyika kilichoorodhesha makabila yote ya Tanganyika nyakati hizo.

Juhudi zote za Mohamed Said ni kuhakikisha kuwa anadumisha hii historia yake ya kuchonga ya wazee wake ili kusiwe na shaka kuhusu hawa walowezi kuingia kwenye historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika. Lakini natoa tahadhari...Tanganyika haikuwa koloni ya Mwingereza na kwa msingi huo hakukuwa na mapigano yoyote ya kudai uhuru. Uhuru wa Tanganyika tofauti na nchi zingine Afrika haukudaiwa kwa mtutu wa bunduki na mapigano, ulidaiwa kwa majadiliano.

Kilichotakiwa ni kutokea kwa Watanganyika wenye uwezo, sifa na elimu ya kukaa meza moja na kutoa hoja na sababu kwa nini muda umefika kwa Tanganyika kujitawala. Uingereza walipewa tu kuisimamia Tanganyika hadi iwapate watu kama hao na mwaka 1961, TANU iliweza kuuridhisha Umoja wa mataifa kwamba sasa inao hao watu wenye uwezo, sifa na elimu ya kutwaa madaraka na kujitawala wenyewe. Huu ndio ukweli, mengine ni porojo tu.
Mag3,
Karibu ndugu yangu.

Hii ndiyo raha ya kuandika.
Ukishaandika watu wanasoma na kutoa fikra zao.

Ukipenda kuita porojo nani wa kukuzuia?
 
kule kule, nani kasema Abdul Sykes afutwe katika historia?
Historia ina tabia moja, kwamba, huiandiki wala huifuti. Utamfutaje Hitler katika vita kuu ya dunia?
Likewise utamfutaje Kleist Sykes katibu wa AA au Mwalimu Matola Mwenyekiti wa AA au Abdul wa TAA
Tena tunamkosea Abdul, hatuelezi jitihada zake za kuwabambua makofi akiwa na wahuni ili watwae ofisi

Turudi kwenye mada hasa makabrasha uliyopata bahti ya kuyadurusu mwenzetu
Mwaka 1929, akiwa na AA , ipi namba ya kadi ya Kleist Abdallah Sykes ?
Naye Abdul akiwa na TAA baada ya kuwatia adabu wazee , kadi yake ya TAA ni ngapi?

Halafu, wanena TANU kuanzishwa 1929, iweje basi kadi ya mtoto wa miaka 7 wakati huo Mwalimu Nyerere iwe namba 1 na ile ya mwana wa familia ya Sykes Mh Abdul Sykes iwe namba 3.

Halafu tuendele..

Leo nipo Pongwe napata papa na ngogwe. Mashallah mashallah
Unaandika vitu vizito na adimu kuliko pumba na uzushi za huyu mfia dini aliyejaa uongo.
 
Mtafiti...
Hayo hayanihusu mie.

Iliandikwa historia ya TANU ya Chuo.Cha CCM Kivukoni yote mnayosoma hapa hayakuwemo yamefutwa.

Labda kwa kukosa kujua nyie mkadhani ile ndiyi historia ya TANU.

Nimeandika historia ya kweli.

Hebu waulizeni maswali Kivukoni.
Ilikuwaje?

Ndiyo hivyo hivvyo magazeti ya TANU nayo hayakumwandika Abdul Sykes alipofariki.
Eti hayakuhusu wewe, unaandika mipasho kama mwanamke muimba taarab, hii historia yako ya kulazimishia ni Uongo mtupu ndio maana hapa unaaibishwa tu ila kwakuwa kichwa ngumu kimejaa ubishi unagangamala na kutapatapa.
 
Mohamed Said
Wamekwisha elekea kwa Manani wote hao.
Acha porojo zako bali ; waombee kwa Muumba walale kwa amani. Ukiandika zaidi inakuwa ni uzandiki tu na siyo tija tena kwa waja wote.

Tanzania ni moja nasi tu wamoja.
 
Mohamed Said ,

Habari zako hizi ni sawa na pepo tusiyoijua kwa wewe kuyaleta haya leo hizi.

Waache hao waja wapumzike kwa amani huko walikotangulia kwa Manani.

Kwa kheri.
 
First generation Zulu colonial army mercenaries and Manyemas masquarading as patriotic, indigenous sons of Tanganyika. Mzee Muddy jibu hoja: how far back does the Sykes family and your own family have roots in Tanganyika?
 
Wahamiaji wazulu na wamanyema leo hii wawafanya wazalendo mashujaa! Wee mzee muddy ukoo wako una generations ngapi Tanganyika? Achilia mbali hao Miungu watu wako kina Sykes ambao hata generations 3 hawana nchi hii.
 
Mohamed Said ,

Habari zako hizi ni sawa na pepo tusiyoijua kwa wewe kuyaleta haya leo hizi.

Waache hao waja wapumzike kwa amani huko walikotangulia kwa Manani.

Kwa kheri.
Poise,
Maiti hazitaabiki kwa kufanyiwa tabaruku.

Somo la historia ni somo linalovutia sana.

Nimepongezwa na watu wengi sana kwa video hiyo.

Bahati mbaya sana wewe inakutaabisha.
 
Mzee Muddy baada ya kupingwa sana sasa naona kapiga 90 degrees kama siyo 180 degrees turn na kudai yeye amejikita kwenye kuandika historia ya wazee wake enzi za harakati za kudai uhuru. Lakini hapo hapo anapinga kwa nguvu zake zote historia inayotambulika kitaifa ya harakati za uhuru. Sasa hapo kuna ukinzani mkubwa. Kwa mantiki yake , mzee muddy ana imply kila mtu ni rukhsa kuandika historia za wazee wake lkn hapohapo nia na malengo yake ni ku challenge official narratives za harakati za kudai uhuru. Sasa kama kila mdau Tanzania nzima angekuja na private histories za wazee wake enzi za kudai uhuru, na kuwaweka mstari wa mbele kama mashujaa na wazalendo nambari one si ingekuwa fujo tu? Hawa walowezi na askari wa kukodi wa kikoloni Wazulu kutoka south africa ghafla wageuke kuwa national heroes kwa nguvu ya dini yao amnayo waliakisi baada ya kuoa wanawake wa Kimanyema?
 
Wanajamvi

1. Tunaelewa Abdul hakumpokea Nyerere Dar es Salaam

2. Katiba ya TANU imeandikwa na Mwalimu Nyerere. Hakuna ushahidi Abdul alishiriki

3. Kadi ya TANU ya Nyerere ni namba 1 na Abdul Sykes ni namba 3. Hili linaeleza kitu kuhusu kuundwa kwa Chama
4. Hakuna kadi ya uanachama wala KATIBA ya Kleist au Abdul wakiwa na AA na TAA.

5. Abdul Sykes hakuwahi kufanya mkutano wa hadhara popote pale nje ya Tandamti na kidongo chekundu

6. Nyerere alibadili siasa za vyama ni kuvifanya viwe organization, viwe na katiba, vijuwe wanancham na hata kadi kama sehemu ya kuwatambua wanachama

7. Nyerere alisambaza chama mikoani. Mohamed anathibitisha hili, rejea mwaliko wa Chambera kwenda Lindi

8. Hawa Wazulu hawakuwa Waislam walipofika. Kama ingalikuwa iweje basi Waislam hao wawapige vita Waislam wenzao kama akina Abushiri na Mkwawa?

9. Kwamba Wamanyema na Wazulu walikuja kwa ukombozi si kweli. Hawa ni wahamiaji tu waliokuwa 'opportunists''
Mohamed anathibitisha pale anaposema, wenyeji wa Dar es Salaam waliwaita ''Wakuja''
Na mwaka 1960 Wenyeji wa Dar walisusia maulidi yaliyoandaliwa na Sykes.

Wanajamvi tunapoita historia ya Mohamed NGANO hatufanyi dhihaka. Katika video hiyo Mohamed anasema Wazungu wakija tayari watu walikuwa na ustaraabu wao wa kuandika tenzi na Ngano.
Kuna ubaya gani utamaduni wa tenzi na ngao kuendelezwa? Hata hivyo si kubadili ngano kuwa historia

Hizi ni kumbu kumbu kila hatua tutaangali neno kwa neno, kwenye uongo, uzushi au upotoshaji tutasema

Tuendelea na Ngano
 
Kwanza, hilo jina la ukoo “Sykes” ni la kabila gani la kizawa Tanganyika na hata visiwani? Halafu jina “Said” ni ukoo na kabila gani haswa la Kitanganyika? Au ni pseudonym tu? Unajificha nyuma ya kalamu??
 
Walikuwa Manyapara wa Kizulu walioletwa na Wazungu kuja kutuchapa bakora. Baadaye ema walichungulia fursa au Waingereza walitaka kuweka mapandikizi yao
Mtchoro,
Ndiyo faida ya kuandika.

Umepata na wewe nafasi ya kuchangia histori ya nchi yetu.

Hebu soma hii hapo chini:

GEREZANI FAMILY DAY

Ahsanteni sana Wanagerezani kwa siku nzuri ya hii Jumapili khasa kwa ile biriani ya kumwaga.

Allah atuzidishie mapenzi na mshikamano.

Leo kwa mara yangu ya kwanza nimehudhuria Gerezani Day.

Kwa hakika ni siku ya kupendeza sana ingawa kwa namna fulani kuna majonzi kidogo yanakuja pale unapowafikiria wale ambao ulikuwanao udogoni mkicheza mpira Kidongo Chekundu na wao wametangulia mbele ya haki.

Kidongo Chekundu leo haipo lakini pamejengwa viwanja vya michezo.

Kwangu mimi ni mara yangu ya kwanza kuhudhuria siku hii na In Shaa Allah naomba iwe narejea na kurejea kila mwaka hadi mwish wa umri wangu.

Laiti kama si kwa kuwa nipo katika Group hakuna ambae angenijua kwa sura ila watu wachache sana pengine wasiozidi hata watano.

Kutoka mwaka wa 1952 nilipozaliwa mimi Mtaa wa Kipata hadi leo miaka mingi imepita.

Kuna baadhi ya watu umri wangu na wengine chini kidogo nimeweza kuwatambua kwa sura zao kuwa zinakuja akilini lakini majina hayaji.

Ngoja nikuchukueni safari yangu ya Gerezani ilivyokuwa na nataka In Shaa Allah niifungamanishe na Dar es Salaam ile ya 1950/60 ambayo naamini wanagerezani wachache sana wanaijua kwani leo pale wengi niliowaona ni vijana sana.

Huenda wengine mimi nimecheza na baba zao.

Nimetokea nyumbani kwangu Magomeni Mapipa nyumba ya kwanza ambayo ina kumbukumbu kubwa kwangu ni pale nilipopinda kona kulia kuingia Mtaa wa Kipata (Sasa Mtaa wa Sykes).

Nimeacha kuitaja ofisi ya CCM ambayo pale ilikuwa ofisi ya African Association iliyojengwa kwa kujitolea kila siku ya Jumapili kuanzia mwaka wa 1929 – 1933.

Nyumba ya kwanza yenye kumbukumbu kubwa kwangu iko mkono wa kulia yaweza kuwa ni nyumba ya tatu hivi kutoka Lumumba Avenue na Mtaa wa Sykes.

Leo hapo kuna kituo cha kuuza petroli.

Hii ilikuwa nyumba ya Liwali Abdallah Simba wa Songea ambae nyumba yake nyingine ilikuwa Mtaa wa Somali (Sasa Omari Londo).

Babu yangu aliishi nyumba hii miaka wa ya 1920 ingawa yeye alikuwa na nyumba yake Mtaa wa Mbaruku na Congo jirani na nyumba ya Aziz Ali.

Nyumba hiyo ndipo alipokulia baba yangu.

Umuhimu wa nyumba hii ni kuwa baba yangu kayaona yote ya harakati za uhuru akiwa pale na kanieleza mengi.

Mkabala na nyumba hii ni nyumba ya Kleist Sykes ambae katika video aliyotengeneza Mohamed Ghassani kampa jina, ‘’Mbuyu wa Mzizima.’’

Video hiyo nimekuwekeeni hapa kwenye Group toka jana usiku.

Mtakumbuka kuwa mliponikaribisha kuzungumza nilikuelezeni kuwa harakati za kuiokomboa Tanganyika kutoka ukoloni wa Waingereza zilianza nyumba hii.

Kleist alikuwa katibu muasisi wa African Association na aliishi nyumba hii na wanae wote walizaliwa hapo.

Ndani ya nyumba hiyo wakati wa TAA Ally Sykes mwaka wa 1953 alificha mashine ya kudurufu ambayo ndiyo aliyokuwa akichapa makaratasi ambayo Waingereza waliita ya ‘’uchochezi,’’ akawa anayatawanya kwa wananchi wajiunge na TAA ili TANU itakapokuja kuundwa mwaka wa 1954 iwe na wanachama wa kutosha.

Historia ya Ally Sykes sote tunaijua.

Katika nyumba hii ndipo siku chache baada ya kuundwa kwa TANU Ally Sykes na kaka yake Abdul walikaa mchana mmoja kumsubiri Mwalimu Nyerere aje kuwapa habari za usajili wa chama cha TANU.

Alipofika pale Nyerere aliwapa habari mbaya kuwa TANU imekataliwa usajili.
Nyumba ile haipo na badala yake kuna gorofa ndefu.

Jengo hili hili linahitaji kuwekewa kumbukumbu.
Nimeswali Msikiti wa Kipata na ukanikumbusha ule msikiti mdogo wa zamani.

Mkabala wa nyumba hii NO. 18 alikuwa akiishi mama yangu Mkubwa Bi. Mwanaisha Bint Mohamed ambako Nakioze alikuwa na genge lake akiuza mboga na matunda.

Hili jina "Naikioze," alipewa kwa kuwa wateja wake walikuwa wakilalamika kwa ughali wa bei za vitu vyake yeye akiwaambia, ‘’Acha usinunue nakioze.’’

Nyumba hii ilikuwa ya Bi. Mkubwa mmoja akiitwa Bint Salum.

Nakumbuka mwaka wa 1956 wakati Princess Margaret alipokuja Tanganyika.

Siku ile nilikuwa hapa kwa mama yangu mkubwa na kwa kuwa mtaa wa nyuma ni Mtaa wa Kitchwelle alikokuwa anapitishwa akitokea uwanja wa ndege nakumbuka sana kuwa mimi nilisimama mbele ya duka la Toti pamoja na umma mkubwa wa watu na wanafunzi wa shule kumpungia Princes Margaret tukiwa tumeshika, ‘’Union Jack,’’ bendera ya Uingereza.

Naingia Mtaa wa Sikukuu nakata kushoto kutokea Mtaa wa Sykes kulia kwenye kona ndipo ilipokuwapo nyumba ya Mzee Clement Mohamed Mtamila mmoja wa viongozi wa African Association aliyekuwa katika ya TAA na baadae Mwenyekiti wa TANU 1955.

Siku zile TANU ilikuwa na Rais na Mwenyekiti ambae alifanya kazi zaidi kama mwenyekiti wa Halmashauri ya TANU.

Mwalimu Nyerere alipoandikiwa barua ya achague mawili siasa au ualimu, barua ile ilijadiliwa kwenye kikao kwenye nyumba hii na mmoja wa wajumbe alikuwa Bi. Tatu bint Mzee ambae alikuwa anaishi Gerezani Mtaa wa Kirk Street sasa Mtaa wa Lindi.

Jengo hili linastahili kuwekea kumbukumbu.

Nimepita Mtaa wa Lindi kwenye kona kulikuwa na kinyozi Muingereza na pale palikuwa barza kubwa ya wana TANU wakikaa kuzungumza.

Hii ni sehemu muhimu ya kuwekewa kumbukumbu na hivi sasa kuna ujenzi pale wa kujenga ofisi ya CCM.

Ukiwa hapo nyumba ya Bi. Mruguru bint Mussa mama yake Abdul Syks unaiona ile pale na watu wengi wa Gerezani wanakumbuka kumuona Nyerere akipita pale kwa Muingereza kaongozana na Abdul Sykes wanakwenda kumsalimia Bi. Mruguru.

Wazalendo hawa wawili mara nyingine walikuwa wanasiamama hapo kutupiana maneno na wana TANU wenzao na ilipoanza Congress watatupiana makombora na wafuasi wa Zuberi Mtemvu aliyekuwa President wa Congress, kisha hao watapita.

Mtemvu alikuwa akiishi Mtaa wa Somali ambao sasa ni Mtaa wa Omari Londo.

Gereza ni ina kumbukumbu nyingi na ni muhimu sana kumbukumbu hizi zihifadhiwe kwa kizazi kijacho vinginevyo historia ya Gerezani yote itapotea.
 
Walikuwa Manyapara wa Kizulu walioletwa na Wazungu kuja kutuchapa bakora. Baadaye ema walichungulia fursa au Waingereza walitaka kuweka mapandikizi yao
Leo Wazulu, walioletwa na Wakoloni kutoka South Africa kama askari vibaraka bado wanatumia jina la ukoo la “Sykes” kwa kuficha uasili wao na hapo hapo wanadai wao ni Watanganyika damudamu na “mashujaa”, “wapigania uhuru” namba moja?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom