Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,920
- 30,263
Picha zilizopo katika makala haya nilipiga Ukumbi wa Arnautoglo 1993 wakati chama cha National Emancipation Movement (NEMA) kinahakiki wanachama wake 1993 ili kupata usajili wa kudumu.
April 1953 katika ukumbi huu palifanyika Uchaguzi wa Mwaka Abdul Sykes na Nyerere waligombea nafasi ya President wa TAA.
Nyerere alikuwa anaomba kura kwa watu mfano wa hawa katika picha ambao yeye hawajui na wao hawamjui.
Nyerere alishinda uchaguzi ule kwa kura chache sana.
Alishindaje mtu mgeni Julius Nyerere dhidi ya mwanamji Abdulwahid Sykes?
Kisa ndani ya historia ya uchaguzi huu kinasisimua sana.
Nimekieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Kuna mengi ya kuzingatia katika historia hii na mafunzo muhimu sana.
Fungua kitabu chochote cha historia hukuti mahali imeelezwa uchaguzi huu au kueleza kuwa Nyerere alipokea uongozi wa TAA 1953 kutoka mikononi kwa Abdul Sykes.
Nyerere mwenyewe katika hotuba maarufu ya Diamond Jubilee Hall alimtaja Abdul na TAA akasema kuwa anadhani Abdul alikuwa Secretary wa TAA.
Maana yake hana hakika na nafasi ya uongozi wa Abdul Sykes katika TAA.
Kidogo inastaajabisha.
Baada ya uchaguzi ule wa March, ilipofika June, makao makuu ya TAA, New Street yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere (Rais), Abdulwahid Sykes, (Makamu wa Rais); J. P. Kasella Bantu (Katibu Mkuu); Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, (Makatibu wa muhtasari); Wajumbe wa Kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko (Tanganyika Standard, 19 th June 1953).
Alipofariki Abdul Sykes magazeti ya TANU The Nationalist na Uhuru hayakuandika chochote kuhusu Abdul Sykes ukitoa kueleza kuwa Julius Nyerere kuhudhuria maziko yake.
Tanganyika Standard kupitia Sunday News 13 October, 1968 wakachapa taazia iliyomweleza Abdul Sykes kama chanzo cha kuundwa kwa chama cha TANU 1954.
April 1953 katika ukumbi huu palifanyika Uchaguzi wa Mwaka Abdul Sykes na Nyerere waligombea nafasi ya President wa TAA.
Nyerere alikuwa anaomba kura kwa watu mfano wa hawa katika picha ambao yeye hawajui na wao hawamjui.
Nyerere alishinda uchaguzi ule kwa kura chache sana.
Alishindaje mtu mgeni Julius Nyerere dhidi ya mwanamji Abdulwahid Sykes?
Kisa ndani ya historia ya uchaguzi huu kinasisimua sana.
Nimekieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Kuna mengi ya kuzingatia katika historia hii na mafunzo muhimu sana.
Fungua kitabu chochote cha historia hukuti mahali imeelezwa uchaguzi huu au kueleza kuwa Nyerere alipokea uongozi wa TAA 1953 kutoka mikononi kwa Abdul Sykes.
Nyerere mwenyewe katika hotuba maarufu ya Diamond Jubilee Hall alimtaja Abdul na TAA akasema kuwa anadhani Abdul alikuwa Secretary wa TAA.
Maana yake hana hakika na nafasi ya uongozi wa Abdul Sykes katika TAA.
Kidogo inastaajabisha.
Baada ya uchaguzi ule wa March, ilipofika June, makao makuu ya TAA, New Street yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere (Rais), Abdulwahid Sykes, (Makamu wa Rais); J. P. Kasella Bantu (Katibu Mkuu); Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, (Makatibu wa muhtasari); Wajumbe wa Kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko (Tanganyika Standard, 19 th June 1953).
Alipofariki Abdul Sykes magazeti ya TANU The Nationalist na Uhuru hayakuandika chochote kuhusu Abdul Sykes ukitoa kueleza kuwa Julius Nyerere kuhudhuria maziko yake.
Tanganyika Standard kupitia Sunday News 13 October, 1968 wakachapa taazia iliyomweleza Abdul Sykes kama chanzo cha kuundwa kwa chama cha TANU 1954.