Nini jukumu la vyombo vya ulinzi na usalama kuwadhibiti wanasiasa wanahujumu nchi kwa ndimi mbili?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Naomba tujiulize vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimeshindwa kuingilia kati huu uchafuzi wakisiasa unaofanywa na viongozi waandamizi wakisiasa?

Hatuwezi kuwa na Taifa ambalo viongozi leo Wana msimamo huu kuhusu rasilimali na kesho wana msimamo ule kuhusu rasilimali zetu na hakuna anayewakemea.

Hatuwezi kuwa na Taifa ambalo kila wanachotaka wanasiasa ndicho kinatokea, kwanini dola isiwadhibiti baada ya chama dola kushindwa kuwadhibiti?

Tunasoma taarifa za wizi kila siku lakini hakuna wanasiasa wanaochukuliwa hatua kuhusu hasara wanayoisababishia serikali na vyombo vya dola vipo kimya.

Nchi inatunga sheria za zakiwawekea kinga wezi na wabadhirifu wa mali za umma, wahujumu Uhuru wa wengine na wakandamizaji wa haki za binadamu lakini hakuna chombo kinachokemea

Vyombo vyetu vinasubiri Rais aseme ndipo wachukue taarifa, wanakwama nini kuchukua hatua jinai inapotendeka?

Ni Siri gani wasizozijua kuhusu mikataba ya nchi? Hii mikataba mibovu inapotungwa wao wanakuwa wapi? Kwanini dola isiwe sehemu ya macho ya mikataba ya nchi? Kama wao ndio macho kwanini wanaruhusu watu wanapotosha taifa na kuuza rasilimali watakavyo just kwa sababu ni wanasiasa?

Vyombo vya dola mnalilindaje taifa na wizi huu wa rasilimali? Mnawafanya Nini majambazi ya kalamu?
 
Dadangu upende usipende hii ndiyo nadharia halisi ya katiba ya vyama vingi. Kama ni makosa yaliyo wazi, yenye ushahidi, vyombo vya dola ni wajibu wake kuwakamata wahusika na kuwafikidha mahakamani. Unayosema wewe ni matokeo ya sera mbovu, hata "kulindana" ni sera mbovu. Cha kufanya ni kuchukua Ilani ya tundulissu, na ya Membe,na ya Lipumba, na ya Mzee Kapunda je, ni ipi inakuridhisha? Jamaa alijizolea 84%. Ungekubali tu kiiutuuzima kuwa matusi yenu ndiyo yaliwaudhi wapiga kura.
 
Mbona hao hao (ulinzi na usalama)mbona nao wamefanya wizi mkubwa!ukuta pale merelani kulinda tanzanite na still tanzanite zinaibiwa kwa wingi tu,mipaka ya nchi imekuwa sehemu ya human trafficking ya kimataifa pamoja na drugs,60%ya illegally immigrate wanaokwenda SA wanapitia ardhi yetu na jeshi letu limelala
 
Kuna kitu kinaitwa kujiuzulu,

Wote wanaobadili misimamo yao hadharani kabisa, they are unfit for office they should come back to their senses and resign.

Kibinadamu na kidini sio sawa kabisa.
 
Back
Top Bottom