Nini hutoa baada ya mtu kuzikwa

Siyo kweli. Mtu akishafukiwa kule chini hakuna hewa na hakuna mdudu anaweza kuishi. Hivyo mwili ukauka na kubaki ulivyo. Uliza wanaifukua makaburi!
 
Nimepigiwa simu asubuhi na wazee wa kwenye kilabu Cha ulanzi ninaokunywaga nao kuwa wamenimiss siku nyingi sijaenda kuwahabarisha habari mbalimbali .

Sasa nilisoma uzi mmoja walisema usiwe available Sana ili ukuze thamani yako ,basi nilikuwa siendi siku hizi ili thamani na brand yangu ikue hata walivyopiga simu nimewaambia kwasasa niko bize na kazi za serikali kumbe hata ubize huo haupo nipo tu nacheza na vimbwa vyangu na paka getini kwangu ,ila kwa haya maneno nimeogopa Sana ,wacha nitoke job niende tu maana kumbe mwisho wa yote wadudu watanila tu .

Nashukuru Kaka ,wacha niende kwenye jukwaa la siasa nipate walau maneno na Mambo mapya ili nikienda nikawape ubuyu wa kutosha
 
Siyo kweli. Mtu akishafukiwa kule chini hakuna hewa na hakuna mdudu anaweza kuishi. Hivyo mwili ukauka na kubaki ulivyo. Uliza
Mwili wako una wadudu ambao wapo tumboni ukifa tu wanaanza kushambulia
 
Nashukuru sana, pole pia....
Nilishafiwa hadi na mzazi ila hii ya sahivi mmh haiponi. 😢
 
Inashangaza kuona manzi anamwambia mwanaume aliyemtongoza kuwa sio type yake

Jamaa anavunja sheria halafu anatamba akisema unanijua mimi ni nani

Hiyo ni mifano michache tu ya aina ya watu wenye kiburi na majivuno

Acheni usenge nyinyi wenye majivuno mwisho wetu sote ni huu hapa:

 
Kwamba ana nywele? Kama alitolewa mochwari mkaenda kumzika huenda waliomba apuliziwe dawa ili achelewe kuoza lkn ukweli ni kwampa hio melanin pigment na keratin zinakuwa not secreted out kwaio au niishie hapo tu
Hata km ila ndo tulimkuta hivyoo.
 
Me naomba kuchomwa moto, kufunikwa plus kulaliwa na udongo mzito huwa nikiwa msibani nafikiria sana hilo,

Japo watu wa Imani nao hawapo mbali, sijui usiku wa kwanza kaburini una mambo yake,

Mara Kuna kufufuka, ngachoka mimi
 
Hata km ila ndo tulimkuta hivyoo.
Ulichoandika yawezekana ni kweli, maana nimewahusikia kua mtu akifa kucha huendekea kukua,nilisikiaga kuna utafiti ulifanyikaga na Prof.Sarungi.
 
Siyo kweli. Mtu akishafukiwa kule chini hakuna hewa na hakuna mdudu anaweza kuishi. Hivyo mwili ukauka na kubaki ulivyo. Uliza wanaifukua makaburi!
Mie nimesema pia, tulishawahi kufukua maiti iliyozikwa, na kwenda kuzika sehemu ingine,
Tulikuta maiti iko safii badoo. Na hapo ni 13 yrs after 1St buried.
 
duuh afu kuna member anasema eti miaka kumi 13 na bado hajaoza 😁
 
Ulichoandika yawezekana ni kweli, maana nimewahusikia kua mtu akifa kucha huendekea kukua,nilisikiaga kuna utafiti ulifanyikaga na Prof.Sarungi.
Mie sio nimesikia, hii ilitokea kwetu, ni baba angu mkubwa, kizazi ki1 na baba angu mzazi,

Baba mkubwa alizikwa wilaya nyingine, sasa ule usumbufu wa kwenda kufagilia na kuombea, ilibidi afukuliwe kule na aletwe kuzikwa ktk makaburi waliyozikwa ndugu wengi, ili iwe rahisi ktk kuzingatia kufagilia na kuombea.

Alizikwa 2008 na tulifukua 2021, tulimkuta yuko safi, ila maeneo ya tumboni ndo paliharibika, ila kwingine yuko safi kabisa,
Kucha ndefu, nywele ndefu, ila kakauka sana yuko kau kau.

Na hii hufanyika hadi kupata kibali cha polisi.
Sasa nashangaa hapa huyu anayo yaeleza inakuajee. Khaaah
 
Kwamba miaka 13?? 🤣🤣🤣 uongo wa level z phd
Sasa km ni uongo bas haya, sina la zaidi kukuhakikishia.

Labda useme kwa waislamu, ila wakristo na haya majeneza, wallah anachelewa sana kuharibika, nimeshuhudia, sio kwamba nimesikia au kusimuliwa.
Hivyoo yaan.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…